picha

Magonjwa ya zinaa

Posti hii inahusu magonjwa ya zinaa, ni magonjwa yanayosambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya kujamiiana pasipo kutumia kinga au kwa lugha nyingine tunaita ngono zembe.

Mambo yanayochangia kuwepo au kuenea kwa magonjwa ya zinaa.

1. Pamoja na kuwepo kwa magonjwa haya ya zinaa Kunaa mambo yanayochangia zaidi kuwepo na kuenea kwa magonjwa haya kutoka kizazi hata kizazi na ingawa kwa kuwepo kwa dawa na elimu kuhusu ugonjwa huu lakini bado maambukizi yapo , kwa hiyo yafuatayo ni mambo yanayosababisha kuwepo kwa magonjwa haya .

 

 

2. Kujamiiana na watu mbalimbali.

Kuna watu ambao wanajaamiana na watu tofauti tofauti bila kutumia kinga hali ambayo usababisha kuenea kwa magonjwa ya zinaa, kwa sababu Kuna vijana ambao Wana wachumba zaidi ya mmoja na pia hawatumii kinga na wakati mwingine Kuna tabia ya kufanya ngono na wanawake wanaouza miili yao bila kutumia kinga hali ambayo usababisha kuenea kwa magonjwa ya zinaa.

 

 

3. Mila na desturi.

Kuna baadhi ya Mila na desturi za baadhi ya jamii usababisha kuenea kwa magonjwa ya zinaa, kwa mfano tabia ya kukuketa wanawake ambapo unakuta wembe mmoja unatumika kwa akina dada zaidi ya mmoja ikitokea mmoja ana ugonjwa huo usababisha wengine kupata, na pia Kuna tabia ya kurithishwa wanawake endapo mme wake amefariki hali  ambayo usababisha kuenea kwa magonjwa ya zinaa Kama aliyefariki alikuwa na ugonjwa huo.

 

 

4. Kuwepo na vita au makazi ya wakimbizi.

Kwa wakati mwingine kuwepo kwa vita usababisha watu kuishi kama wakimbizi na wakati mwingine kuwepo kwenye kambi Moja unakuta wengine wanakuwa hawana wake zao au hawana waume zao kwa hiyo uanza kujamiiana endapo mmoja akiwa na ugonjwa huu akajamiiana na mwingine anaweza kupata magonjwa, kwa hiyo tunapaswa kutoa elimu na kuwepo kwa kinga kwenye kambi za wakimbizi.

 

 

5. Pia Kuna sababu ya umri.

Kwa wakati mwingine umri unaleta shida hasa kwa vijana ambao wameanza kubarehe kuanzia miaka kumi na mitano na kuendelea wanakuwa na wapenzi wengi hali inayosababisha kuwepo kwa ugonjwa wa zinaa.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2625

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 Kitabu cha Afya     👉4 web hosting     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

Dalili za ugonjwa wa herpes simplex au vipele kwenye midomo na sehemu za siri

Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa wa vipele kwenye midomo na sehemu za siri ambao kwa kitaalamu huitwa herpes zoster. Kwa hiyo ili kugundua kubwa mtu ana Ugonjwa huu Dalili kama hizi zifuatazo zinaweza kutokea kwa mgonjwa.

Soma Zaidi...
Dalili za minyoo ya tumbo

Posti hii inaelezea kuhusiana na dalili za minyoo ya tumbo ambapo minyoo hawa husababishwa na mtu kula vyakula vichafu ambavyo havijaiva vizuri au maji machafu pia au bacteria.

Soma Zaidi...
Mambo ya kuzingatia kabla ya upasuaji,

Upasuaji ni kundi la ki medical linalohusu kutoa kiungo kisichohitajika kwenye mwili.

Soma Zaidi...
Nini husababisha maumivu ya tumbo chini ya kitovu kwa wanawake na wanaume

Somo hili linakwenda kukueleza vitu vinavyosababisha maumivu ya tumbo chini ya kitovu

Soma Zaidi...
NAMNA YA KUISHI NA VIDONDA VYA TUMBO

NAMNA YA KUISHI NA VIDONDA VYA TUMBO Unaweza kupata nafuu kutoka kwa maumivu ya kidonda cha tumbo ikiwa utafata taratibu za kiafya kama:- 1.

Soma Zaidi...
Je unaweza sex na mwanamke mwenye HIV na ukaenda kupima wiki moja na ukagundurika kwa vipimo vya maabara

Utakapofanya ngono na aliyeathirika haimaanishi na wewe kuwa lazima utakuwa umeathirika. Kuathirika kuna mambo mengi lazima yafanyike.

Soma Zaidi...