Magonjwa ya zinaa
Posti hii inahusu magonjwa ya zinaa, ni magonjwa yanayosambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya kujamiiana pasipo kutumia kinga au kwa lugha nyingine tunaita ngono zembe.
Mambo yanayochangia kuwepo au kuenea kwa magonjwa ya zinaa.
1. Pamoja na kuwepo kwa magonjwa haya ya zinaa Kunaa mambo yanayochangia zaidi kuwepo na kuenea kwa magonjwa haya kutoka kizazi hata kizazi na ingawa kwa kuwepo kwa dawa na elimu kuhusu ugonjwa huu lakini bado maambukizi yapo , kwa hiyo yafuatayo ni mambo yanayosababisha kuwepo kwa magonjwa haya .
2. Kujamiiana na watu mbalimbali.
Kuna watu ambao wanajaamiana na watu tofauti tofauti bila kutumia kinga hali ambayo usababisha kuenea kwa magonjwa ya zinaa, kwa sababu Kuna vijana ambao Wana wachumba zaidi ya mmoja na pia hawatumii kinga na wakati mwingine Kuna tabia ya kufanya ngono na wanawake wanaouza miili yao bila kutumia kinga hali ambayo usababisha kuenea kwa magonjwa ya zinaa.
3. Mila na desturi.
Kuna baadhi ya Mila na desturi za baadhi ya jamii usababisha kuenea kwa magonjwa ya zinaa, kwa mfano tabia ya kukuketa wanawake ambapo unakuta wembe mmoja unatumika kwa akina dada zaidi ya mmoja ikitokea mmoja ana ugonjwa huo usababisha wengine kupata, na pia Kuna tabia ya kurithishwa wanawake endapo mme wake amefariki hali ambayo usababisha kuenea kwa magonjwa ya zinaa Kama aliyefariki alikuwa na ugonjwa huo.
4. Kuwepo na vita au makazi ya wakimbizi.
Kwa wakati mwingine kuwepo kwa vita usababisha watu kuishi kama wakimbizi na wakati mwingine kuwepo kwenye kambi Moja unakuta wengine wanakuwa hawana wake zao au hawana waume zao kwa hiyo uanza kujamiiana endapo mmoja akiwa na ugonjwa huu akajamiiana na mwingine anaweza kupata magonjwa, kwa hiyo tunapaswa kutoa elimu na kuwepo kwa kinga kwenye kambi za wakimbizi.
5. Pia Kuna sababu ya umri.
Kwa wakati mwingine umri unaleta shida hasa kwa vijana ambao wameanza kubarehe kuanzia miaka kumi na mitano na kuendelea wanakuwa na wapenzi wengi hali inayosababisha kuwepo kwa ugonjwa wa zinaa.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
๐1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina ๐2 Kitabu cha Afya ๐3 Simulizi za Hadithi Audio ๐4 Bongolite - Game zone - Play free game ๐5 Kitau cha Fiqh ๐6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
Maumivu wakati wa hedhi
โMaumivu wakati wa hedhi, kitaalamu yakijulikana kama Dysmenorrhea, ni changamoto inayowaathiri mamilioni ya wanawake duniani kote. Wakati maumivu mepesi yakichukuliwa kama hali ya kawaida ya mabadiliko ya mwili, maumivu makali yanayomzuia mwanamke kufanya shughuli zake za kila siku yanaweza kuwa ishara ya matatizo makubwa ya kiafya. Makala haya yanajadili aina za maumivu haya, vyanzo vyake vikuu, njia za nyumbani na za kitabibu za kupata suluhisho, pamoja na ukweli wa kisayansi dhidi ya dhana potofu.
Soma Zaidi...Dalili za mtu mwenye ugonjwa wa kuishiwa damu
Posti hii inahusu zaidi dalili za mtu mwenye ugonjwa wa kupungukiwadamu, ni dalili zinazoonekana kwa mtu Mwenye tatizo la upungufu wa damu.
Soma Zaidi...Choo kuwa kigumu (Constipation): Vyakula na vinywaji vya kusaidia.
Choo kigumu ni changamoto inayowatesa watu wengi, ikiwemo maumivu ya tumbo, kuhisi mzito, na kukosa raha. Mara nyingi, tatizo hili husababishwa na ukosefu wa nyuzi lishe (fiber), kutokunywa maji ya kutosha, au kutokuwa na utaratibu mzuri wa maisha. Habari njema ni kwamba, kwa kufanya mabadiliko machache kwenye lishe yako, unaweza kurudisha mfumo wako wa mmengโenyo wa chakula kwenye hali ya kawaida.
Soma Zaidi...Madhara ya ugonjwa wa ukimwi kwenye jamii.
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea ikiwa Ugonjwa huu wa ukimwi ukishasmbaa kutoka sehemu moja kwenda nyingine na kuleta madhara makubwa kama ifuatavyo.
Soma Zaidi...Watu walio hatarini kupata ugonjwa wa pumu
Kila mtu anaweza kupata ugonjwa wa pumu, hata hivyo kuna ambao wapo hatarini zaidi kupata pumu.
Soma Zaidi...Dalili za mimba ya wiki mbili unazopaswa kujua
โPost hii inaangazia kile kinachotokea mwilini mwako katika wiki ya pili ya ujauzito. Ingawa wiki ya pili mara nyingi huchukuliwa kama kipindi ambacho mwili unajiandaa kuachilia yai, tutaangazia ishara za mwanzo kabisa za utungaji wa mimba, jinsi ya kuzitambua, na hatua za kuchukua ili kuhakikisha afya njema.
Soma Zaidi...