Posti hii inahusu magonjwa ya zinaa, ni magonjwa yanayosambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya kujamiiana pasipo kutumia kinga au kwa lugha nyingine tunaita ngono zembe.
1. Pamoja na kuwepo kwa magonjwa haya ya zinaa Kunaa mambo yanayochangia zaidi kuwepo na kuenea kwa magonjwa haya kutoka kizazi hata kizazi na ingawa kwa kuwepo kwa dawa na elimu kuhusu ugonjwa huu lakini bado maambukizi yapo , kwa hiyo yafuatayo ni mambo yanayosababisha kuwepo kwa magonjwa haya .
2. Kujamiiana na watu mbalimbali.
Kuna watu ambao wanajaamiana na watu tofauti tofauti bila kutumia kinga hali ambayo usababisha kuenea kwa magonjwa ya zinaa, kwa sababu Kuna vijana ambao Wana wachumba zaidi ya mmoja na pia hawatumii kinga na wakati mwingine Kuna tabia ya kufanya ngono na wanawake wanaouza miili yao bila kutumia kinga hali ambayo usababisha kuenea kwa magonjwa ya zinaa.
3. Mila na desturi.
Kuna baadhi ya Mila na desturi za baadhi ya jamii usababisha kuenea kwa magonjwa ya zinaa, kwa mfano tabia ya kukuketa wanawake ambapo unakuta wembe mmoja unatumika kwa akina dada zaidi ya mmoja ikitokea mmoja ana ugonjwa huo usababisha wengine kupata, na pia Kuna tabia ya kurithishwa wanawake endapo mme wake amefariki hali ambayo usababisha kuenea kwa magonjwa ya zinaa Kama aliyefariki alikuwa na ugonjwa huo.
4. Kuwepo na vita au makazi ya wakimbizi.
Kwa wakati mwingine kuwepo kwa vita usababisha watu kuishi kama wakimbizi na wakati mwingine kuwepo kwenye kambi Moja unakuta wengine wanakuwa hawana wake zao au hawana waume zao kwa hiyo uanza kujamiiana endapo mmoja akiwa na ugonjwa huu akajamiiana na mwingine anaweza kupata magonjwa, kwa hiyo tunapaswa kutoa elimu na kuwepo kwa kinga kwenye kambi za wakimbizi.
5. Pia Kuna sababu ya umri.
Kwa wakati mwingine umri unaleta shida hasa kwa vijana ambao wameanza kubarehe kuanzia miaka kumi na mitano na kuendelea wanakuwa na wapenzi wengi hali inayosababisha kuwepo kwa ugonjwa wa zinaa.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Post hii inahusu zaidi mambo yanayochangia katika makuzi ya mtoto, mtoto katika makuzi yake anahitaji kutunzwa vizuri Ili akue kwa afya nzuri bila magonjwa
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuweza kupambana na fangasi za ukeni ili kuweza kujiepusha na madhara mbalimbali kwenye maisha ambayo ni pamoja na ugumba na Maambukizi kwenye via vya uzazi.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kupambana na kisukari
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi sababu za maumivu ambayo yanasikika kwenye magoti, huu ni ugonjwa ambao umewapata walio wengi na bado ni kilio kwa walio wengi kwa vijana na kwa wazee, Kuna wataalamu mbalimbali ambao wameweza kugundua sababu za maumivu kwenye mago
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maradhi ya macho,dalili na matibabu yake
Soma Zaidi...Kisukari cha Aina ya 2, ambacho wakati mmoja kilijulikana kama Kisukari cha watu wazima au kisichotegemea insulini, ni ugonjwa sugu unaoathiri jinsi mwili wako unavyobadilisha sukari (glucose), chanzo muhimu cha nishati ya mwili wako.
Soma Zaidi...