picha

Magonjwa ya zinaa

Posti hii inahusu magonjwa ya zinaa, ni magonjwa yanayosambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya kujamiiana pasipo kutumia kinga au kwa lugha nyingine tunaita ngono zembe.

Mambo yanayochangia kuwepo au kuenea kwa magonjwa ya zinaa.

1. Pamoja na kuwepo kwa magonjwa haya ya zinaa Kunaa mambo yanayochangia zaidi kuwepo na kuenea kwa magonjwa haya kutoka kizazi hata kizazi na ingawa kwa kuwepo kwa dawa na elimu kuhusu ugonjwa huu lakini bado maambukizi yapo , kwa hiyo yafuatayo ni mambo yanayosababisha kuwepo kwa magonjwa haya .

 

 

2. Kujamiiana na watu mbalimbali.

Kuna watu ambao wanajaamiana na watu tofauti tofauti bila kutumia kinga hali ambayo usababisha kuenea kwa magonjwa ya zinaa, kwa sababu Kuna vijana ambao Wana wachumba zaidi ya mmoja na pia hawatumii kinga na wakati mwingine Kuna tabia ya kufanya ngono na wanawake wanaouza miili yao bila kutumia kinga hali ambayo usababisha kuenea kwa magonjwa ya zinaa.

 

 

3. Mila na desturi.

Kuna baadhi ya Mila na desturi za baadhi ya jamii usababisha kuenea kwa magonjwa ya zinaa, kwa mfano tabia ya kukuketa wanawake ambapo unakuta wembe mmoja unatumika kwa akina dada zaidi ya mmoja ikitokea mmoja ana ugonjwa huo usababisha wengine kupata, na pia Kuna tabia ya kurithishwa wanawake endapo mme wake amefariki hali  ambayo usababisha kuenea kwa magonjwa ya zinaa Kama aliyefariki alikuwa na ugonjwa huo.

 

 

4. Kuwepo na vita au makazi ya wakimbizi.

Kwa wakati mwingine kuwepo kwa vita usababisha watu kuishi kama wakimbizi na wakati mwingine kuwepo kwenye kambi Moja unakuta wengine wanakuwa hawana wake zao au hawana waume zao kwa hiyo uanza kujamiiana endapo mmoja akiwa na ugonjwa huu akajamiiana na mwingine anaweza kupata magonjwa, kwa hiyo tunapaswa kutoa elimu na kuwepo kwa kinga kwenye kambi za wakimbizi.

 

 

5. Pia Kuna sababu ya umri.

Kwa wakati mwingine umri unaleta shida hasa kwa vijana ambao wameanza kubarehe kuanzia miaka kumi na mitano na kuendelea wanakuwa na wapenzi wengi hali inayosababisha kuwepo kwa ugonjwa wa zinaa.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2326

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

DALILI ZA MINYOO: maumivu ya tumbo, kichwa, kuwashwa, kutapika damu, moyo kuumwa, ukuaji hafifu, udhaifu na kuchoka

DALILI ZA MINYOO Wakati mwingine ni vigumu sana kujua kama una minyoo, kwani minyoo wanaweza kukaa ndani ya mwili kwa muda mrefu bila ya kuonesha dalili yeyote, ama madhara yeyote.

Soma Zaidi...
Namna Ugonjwa wa UKIMWI unavyoambukizwa.

UKIMWI (acquired immunodeficiency syndrome) ni hali ya kudumu, inayoweza kutishia maisha inayosababishwa na virusi vya ukimwi (VVU) Kwa kuharibu mfumo wako wa kinga, VVU huingilia uwezo wa mwili wako wa kupambana na viumbe vinavyosababisha magonjwa. Inawe

Soma Zaidi...
Mbinu za kupunguza Magonjwa ya kuambukiza.

Posti hii inahusu zaidi mbinu mbalimbali ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kupunguza kiwango cha kuwepo kwa magonjwa ya kuambukiza, kwa hiyo zifuatazo ni mbinu ambazo zinapaswa kutumika ili kupunguza kiwango cha magonjwa ya kuambukiza.

Soma Zaidi...
Dawa za kutuliza vvu zinaongeza damu

Hakuna dawa ya UKIMWI ya kutibu kuondoa virusi mwilini, lakini zipo dawa za kuweza kupunguza makali ya virusi hawa. Hivi unesha jiuliza kuwa je zile dawa zinaongeza damu?

Soma Zaidi...
Fangasi wa kwenye uke.

Fangasi hawa kitaalamu wanafahamika kama vagina yeast infection na majina mengine ya kitaalamu ni kama vagina candidiasis, u vulvovaginal candidiasis au candidal vaginitis.

Soma Zaidi...