Magonjwa ya zinaa

Posti hii inahusu magonjwa ya zinaa, ni magonjwa yanayosambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya kujamiiana pasipo kutumia kinga au kwa lugha nyingine tunaita ngono zembe.

Mambo yanayochangia kuwepo au kuenea kwa magonjwa ya zinaa.

1. Pamoja na kuwepo kwa magonjwa haya ya zinaa Kunaa mambo yanayochangia zaidi kuwepo na kuenea kwa magonjwa haya kutoka kizazi hata kizazi na ingawa kwa kuwepo kwa dawa na elimu kuhusu ugonjwa huu lakini bado maambukizi yapo , kwa hiyo yafuatayo ni mambo yanayosababisha kuwepo kwa magonjwa haya .

 

 

2. Kujamiiana na watu mbalimbali.

Kuna watu ambao wanajaamiana na watu tofauti tofauti bila kutumia kinga hali ambayo usababisha kuenea kwa magonjwa ya zinaa, kwa sababu Kuna vijana ambao Wana wachumba zaidi ya mmoja na pia hawatumii kinga na wakati mwingine Kuna tabia ya kufanya ngono na wanawake wanaouza miili yao bila kutumia kinga hali ambayo usababisha kuenea kwa magonjwa ya zinaa.

 

 

3. Mila na desturi.

Kuna baadhi ya Mila na desturi za baadhi ya jamii usababisha kuenea kwa magonjwa ya zinaa, kwa mfano tabia ya kukuketa wanawake ambapo unakuta wembe mmoja unatumika kwa akina dada zaidi ya mmoja ikitokea mmoja ana ugonjwa huo usababisha wengine kupata, na pia Kuna tabia ya kurithishwa wanawake endapo mme wake amefariki hali  ambayo usababisha kuenea kwa magonjwa ya zinaa Kama aliyefariki alikuwa na ugonjwa huo.

 

 

4. Kuwepo na vita au makazi ya wakimbizi.

Kwa wakati mwingine kuwepo kwa vita usababisha watu kuishi kama wakimbizi na wakati mwingine kuwepo kwenye kambi Moja unakuta wengine wanakuwa hawana wake zao au hawana waume zao kwa hiyo uanza kujamiiana endapo mmoja akiwa na ugonjwa huu akajamiiana na mwingine anaweza kupata magonjwa, kwa hiyo tunapaswa kutoa elimu na kuwepo kwa kinga kwenye kambi za wakimbizi.

 

 

5. Pia Kuna sababu ya umri.

Kwa wakati mwingine umri unaleta shida hasa kwa vijana ambao wameanza kubarehe kuanzia miaka kumi na mitano na kuendelea wanakuwa na wapenzi wengi hali inayosababisha kuwepo kwa ugonjwa wa zinaa.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 2007

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉5 web hosting    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Namna ya kuzuia virusi vya ukimwi

Posti hii inaelezea kuhusiana na kujikinga au kuzuia virusi vya ukimwi.

Soma Zaidi...
Aina za ajali kwenye kifua,

Post hii inahusu Zaidi aina za ajali kwenye kifua,pamoja na kifua kuwa na sehemu mbalimbali na pia na ajali ambazo utokea Huwa za aina mbalimbali kama tutakavyoona.

Soma Zaidi...
Ndugu mke Wang viungo vina mlegea miguu inamuaka moto nn tatozo

Je unasumbuliwa na tatizo la kukosa nguvu, kuchoka ama kuhisi viungi vinelegea. Endelea na post hii.

Soma Zaidi...
Sababu zinazoweza kumfanya figo kuharibika.

Posti hii inahusu zaidi sababu za kufanya figo kuharibika.hili ni janga ambalo linawakumba Watu wengi siku hizi na kusababisha kupoteza maisha kwa wagonjwa wa figo hasa hasa kwa wale ambao hawana uwezo wa kulipia hela ya kusafishia figo.

Soma Zaidi...
Samahan naomb kujua staili za tendo la ndoa

Post hii inakwenda kujibu swali la muulizaji. Kuhusu syyle za tendo la ndoa

Soma Zaidi...
Dalili za Ugonjwa wa kula kupindukia

Ugonjwa wa kula kupindukia ni ugonjwa mbaya wa ulaji ambapo mara kwa mara unatumia kiasi kikubwa cha chakula na kuhisi huwezi kuacha kula.

Soma Zaidi...
VYANZO VYA MINYOO: nyama isiyowiva, maji machafu, kinyesi, uchafu wa mazingira, udongo

VYNZO VYA MINYOO Kama tulivyoona hapo mwanzo kuusu aina za minyoo, pia tumeona vyanzo vya minyoo hao kulingana na aina zao.

Soma Zaidi...
Njia za kusambaa kwa ugonjwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine

Posti hii inahusu zaidi jinsi magonjwa yanavyosambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.

Soma Zaidi...
Homa ya Dengue, dalili za homa ya dengue na Njia ya kujikinga nayo

HOMA YA DENGUEHoma ya dengue ni miongoni mwa maradhi hatari ambayo husambazwa na mbu.

Soma Zaidi...
Dalili za ugonjwa wa Saratani.

Saratani inahusu ugonjwa wowote kati ya idadi kubwa ya magonjwa ambayo yanaonyeshwa na ukuaji wa seli zisizo za kawaida ambazo hugawanyika bila kudhibitiwa na kuwa na uwezo wa kupenya na kuharibu tishu za kawaida za mwili. Saratani mara nyingi ina uwezo

Soma Zaidi...