Dalili za gonorrhea - gonoria
Jifunze dalili za gonorrhea na namna inavyoambukiza, zipi athari za gonori kwa wanawae na wanaume
Dalilii za gonorrhea
Gonorrhea au gonoria ni moja kati ya magonjwa yanayoenezwa kupitia ngono. Huweza kusababishwa na bakteria na kuathiri wanaume na wanawake. Kuweza kuathiri mdomo, koo, mkundu na sehemu za siri kwa wanaume na wanawake. Huweza kuambukizwa kwa kupitia ngono ya mdomo, ngono ya ukeni ama kwenye mkundu. Kwa watoto huweza kuathiri macho. Gonorrhea (gonoria) huambukizwa kutoka kwa mama kuja kwa mtoto wakati wa kujifunguwa.
Dalili za gonoria (gonorrhea) zinaweza kuchelewa kuonekana kwa wanawake kuliko kwa wanaume. Wapo wengine hawaonyeshi dalili yeyote ile hadi hali itakapokuwa ni mbaya zaidi. Kwa mara nyingi dalili za gonoria (gonorrhea) huonekana kuanzia siku 2 mpaka 7 baada ya kuambukizwa. Na kwa wanawake inaweza kuchelewa zaidi hadi mwezi.
Ni zipi dalili za gonoria (gonorrhea)?
Dalili za gonoria (gonorrhea) unaweza kuwa na dalili tofautitofauti kulingana na jinsia. Dalili kwa wanawae na kwa wanaume zinaweza kutofautiana kulingana na maumbile ya jinsia hizi. Muda wa kutokea dalili hizi pia hutofautiana. Pia huweza kuahiri maeneo mengi mwilini.
Dalili za gonorrhea kwa wanaume:-
1.Maumivu wakati wa kukojoa
2.Kutokwa na majimaji kama usaha kwenye uume.
3.Kuvimba pamoja na maumivu ya korodani.
Dalili za gonorrhea kwa wanawake
1.Kutokwa na uchafu sehemu za siri
2.Maumivu makali ya maeneo ya nyonga
3.Maumivu makali wakati wa kukojoa
4.Kutokwa na damu kabla ya hedhi na baada ya hedhi
Dalili za gonoria (gonorrhea) katika maeneo mengine ya mwili:
1.Maumivu ya mkundu, na kutokwa na kama kinyesi pamoja na maumivu ya tumbo na mvurugiko.
2.Maumivu ya macho, kushindwa kuvumilia mwanga mkali, na macho kutoa kama usaha
3.Vidonga vya koo na kuvimba kwa tezi na lumph kwenye shingo
4.Maumivu ya viungio pamoja na kuwa na joto.
Ni nini chanzo na sababu ya gonoria (gonorrhea)
Kama nilivyotangulia kukuambia hapo juu kuwa gonoria huambukizwa na bakteria. Bakteria hawa hufahamika kwa jina la bacterium Neisseria gonorrhoeae. Na huenezwa kwa njia ya kufanya ngono ya mdomo, mkundu ama ukeni.
Waliohatarini kupata gonorrhea (gonoria)
Watu wa umri wowote wanaweza kupata ugonjwa huu. Hata hivyo kuna ambao wapo hatarini zaidi. Kwa wanawake walio zaidi ya miaka 25 wapo hatarini zaidi. Na wanaume ambao wanashiriki ngono ya mkundu wapo hatarini zaidi. Pia wafuatao wanaweza kuwa hatarini kupata gonorrhea:-
1.Kuanza mahusiano na mpenzi mpya
2.Kuwa na wapenzi zaidi ya mmoja (michepuko)
3.Kuwa na penzi ambayo ana wapenzi wengine (michepuko zaidi)
4.Kuwa na maambukizi ya goniria hapo nyuma ama kuwa na maambukizi mengine ya magonjwa ya ngono.
MADHARA YA GONORIA (GONORRHEA) ENDAPO HAITATIBIWA
Endapo gonoria itachelewa kutibiwa inaweza kuleta madhaya mengi ndani ya mwili kuanzia ugumba, kudhoofu mwili, maumivu na mengineye. Yafuatayo ni madhara ya kuchelewa kutibu gonoria:-
1.Ugumba kwa wanawake. Ugonjwa huu kwa mwanamke unakula via vya uzazi kwa fujo sana. Unaathiri mirija ya falopia ambayo nduo inayohusika kubeba yai na utungaji mzima wa mimba na kusababisha PID yaani Pelvic Inflamatory Deseases. Hivyo mwanamke anahitajika atibiwe mapema kabla madhara hayajakuwa makubwa.
2.Ugumba kwa wanaume. Kwa wanaume gonoria huathiri vimirija vijidogo vilivyopo kwenye korodani. Mirija hii hujulikana kama epididymis. Hali hii hupelekea kuharibika kwa mirija hii hivyo kushindwa kubeba mbegu za kiume kuzitoa nje. Ugonjwa unaosababishwa na uharibifu huu hujullukana kama epididymitis.
3.Mashambukizi ya viungo vingine vya mwili na kuleta homa, upele, vidonda, maimivu ya viungo, kukaza na kuvimba kwa viungio.
4.Huongeza hatari zaidi kwa mwenye VVU na UKIMWI. Watu wenye VVU na UKIMWI ni rahisi kueneza gonoria kwenda kwa mwingine.
5.Kwa watoto waliop[ata gonoria wakati wa lujifunguwa wanaweza kupata upofu na madhara mengine kati afya zao.
NJIA ZA KUPAMBANA NA KUKABILIANA NA GONORIA (GONORRHEA)
1.Kuwa mwaminifu katika mahusiano wacha kuchepuka
2.Hakikisha mwenza wako yupo salama
3.Usishiriki ngono na mtu aliyeathiriwa na magonjwa ya ngono bila kinga
4.Tumia kondomu
5.Pima mara kwa mara gonoria.
.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
๐1 Madrasa kiganjani ๐2 Dua za Mitume na Manabii ๐3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina ๐4 Bongolite - Game zone - Play free game ๐5 web hosting ๐6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Saratani ya matiti: Jinsi ya kujipima na kupata vipimo.
โSaratani ya matiti ni miongoni mwa aina za saratani zinazoongoza kwa kuathiri wanawake duniani kote. Hata hivyo, kutokana na maendeleo ya tiba, saratani hii inaweza kutibika vyema ikiwa itagundulika katika hatua za awali. Makala hii inatoa mwongozo wa kitaalamu kuhusu umuhimu wa uchunguzi wa awali, hatua kwa hatua za jinsi ya kujipima mwenyewe nyumbani, na taratibu za kliniki kama mammography. Tunasisitiza kuwa elimu na ufahamu ndio silaha kuu ya kupambana na ugonjwa huu.
Soma Zaidi...Mimba kuharibika (Miscarriage): Sababu na dalili zake.
Mimba kuharibika ni kupotea kwa ujauzito kabla ya wiki ya 20 ya ujauzito. Hali hii ni jambo linaloweza kuleta huzuni kubwa kwa familia. Ingawa inaweza kutokea ghafla, ni muhimu kuelewa kuwa mara nyingi husababishwa na sababu za kibiolojia zisizo chini ya uwezo wa mama. Makala hii inaelezea sababu za kawaida, dalili za tahadhari, na hatua za kuchukua baada ya kupitia hali hii.
Soma Zaidi...Homa za mara kwa mara: Chanzo chake na nini cha kufanya.
Homa sio ugonjwa; ni silaha ya mwili wako. Inapopanda, inamaanisha mfumo wako wa kinga unawaka moto kupambana na adui aliyepo ndani. Lakini, je, inakuwaje unapopata homa hizo mara kwa mara? Homa za mara kwa mara ni kengele ya onyo kwamba kuna kitu hakiko sawa ambacho hakijatibiwa kikamilifu. Makala haya yanakusaidia kutambua nini cha kufanya ili kuondokana na mzunguko huu wa maumivu
Soma Zaidi...Maumivu ya kichwa cha mara kwa mara (Migraine): Dalili na tiba.
Migraine si maumivu ya kawaida ya kichwa; ni hali ya mfumo wa neva inayoweza kuathiri vibaya maisha ya kila siku ya mtu. Inajidhihirisha kwa maumivu makali ya upande mmoja wa kichwa, yanayoambatana na kichefuchefu, kutapika, na unyeti mkubwa kwa mwanga na sauti. Makala haya yanafafanua kwa kina kile kinachotokea wakati wa shambulio la migraine, jinsi ya kutofautisha na maumivu mengine ya kichwa, na mikakati ya kitaalamu ya kudhibiti na kutibu hali hii.
Soma Zaidi...Namna ya Kumtunza Mtoto Njiti
โKumtunza mtoto aliyezaliwa kabla ya muda (mtoto njiti) kunahitaji umakini mkubwa, uvumilivu, na upendo. Post hii inatoa mwongozo muhimu kuhusu huduma za msingi nyumbani, ikiwa ni pamoja na joto, lishe, na usafi, ili kuhakikisha mtoto anakua na kuwa na afya njema.
Soma Zaidi...