Dalili za gonorrhea - gonoria

Jifunze dalili za gonorrhea na namna inavyoambukiza, zipi athari za gonori kwa wanawae na wanaume

Dalili za gonorrhea - gonoria

Dalilii za gonorrhea



Gonorrhea au gonoria ni moja kati ya magonjwa yanayoenezwa kupitia ngono. Huweza kusababishwa na bakteria na kuathiri wanaume na wanawake. Kuweza kuathiri mdomo, koo, mkundu na sehemu za siri kwa wanaume na wanawake. Huweza kuambukizwa kwa kupitia ngono ya mdomo, ngono ya ukeni ama kwenye mkundu. Kwa watoto huweza kuathiri macho. Gonorrhea (gonoria) huambukizwa kutoka kwa mama kuja kwa mtoto wakati wa kujifunguwa.



Dalili za gonoria (gonorrhea) zinaweza kuchelewa kuonekana kwa wanawake kuliko kwa wanaume. Wapo wengine hawaonyeshi dalili yeyote ile hadi hali itakapokuwa ni mbaya zaidi. Kwa mara nyingi dalili za gonoria (gonorrhea) huonekana kuanzia siku 2 mpaka 7 baada ya kuambukizwa. Na kwa wanawake inaweza kuchelewa zaidi hadi mwezi.



Ni zipi dalili za gonoria (gonorrhea)?
Dalili za gonoria (gonorrhea) unaweza kuwa na dalili tofautitofauti kulingana na jinsia. Dalili kwa wanawae na kwa wanaume zinaweza kutofautiana kulingana na maumbile ya jinsia hizi. Muda wa kutokea dalili hizi pia hutofautiana. Pia huweza kuahiri maeneo mengi mwilini.



Dalili za gonorrhea kwa wanaume:-
1.Maumivu wakati wa kukojoa
2.Kutokwa na majimaji kama usaha kwenye uume.
3.Kuvimba pamoja na maumivu ya korodani.



Dalili za gonorrhea kwa wanawake
1.Kutokwa na uchafu sehemu za siri
2.Maumivu makali ya maeneo ya nyonga
3.Maumivu makali wakati wa kukojoa
4.Kutokwa na damu kabla ya hedhi na baada ya hedhi



Dalili za gonoria (gonorrhea) katika maeneo mengine ya mwili:
1.Maumivu ya mkundu, na kutokwa na kama kinyesi pamoja na maumivu ya tumbo na mvurugiko.
2.Maumivu ya macho, kushindwa kuvumilia mwanga mkali, na macho kutoa kama usaha
3.Vidonga vya koo na kuvimba kwa tezi na lumph kwenye shingo
4.Maumivu ya viungio pamoja na kuwa na joto.



Ni nini chanzo na sababu ya gonoria (gonorrhea)
Kama nilivyotangulia kukuambia hapo juu kuwa gonoria huambukizwa na bakteria. Bakteria hawa hufahamika kwa jina la bacterium Neisseria gonorrhoeae. Na huenezwa kwa njia ya kufanya ngono ya mdomo, mkundu ama ukeni.



Waliohatarini kupata gonorrhea (gonoria)
Watu wa umri wowote wanaweza kupata ugonjwa huu. Hata hivyo kuna ambao wapo hatarini zaidi. Kwa wanawake walio zaidi ya miaka 25 wapo hatarini zaidi. Na wanaume ambao wanashiriki ngono ya mkundu wapo hatarini zaidi. Pia wafuatao wanaweza kuwa hatarini kupata gonorrhea:-




1.Kuanza mahusiano na mpenzi mpya
2.Kuwa na wapenzi zaidi ya mmoja (michepuko)
3.Kuwa na penzi ambayo ana wapenzi wengine (michepuko zaidi)
4.Kuwa na maambukizi ya goniria hapo nyuma ama kuwa na maambukizi mengine ya magonjwa ya ngono.



MADHARA YA GONORIA (GONORRHEA) ENDAPO HAITATIBIWA
Endapo gonoria itachelewa kutibiwa inaweza kuleta madhaya mengi ndani ya mwili kuanzia ugumba, kudhoofu mwili, maumivu na mengineye. Yafuatayo ni madhara ya kuchelewa kutibu gonoria:-



1.Ugumba kwa wanawake. Ugonjwa huu kwa mwanamke unakula via vya uzazi kwa fujo sana. Unaathiri mirija ya falopia ambayo nduo inayohusika kubeba yai na utungaji mzima wa mimba na kusababisha PID yaani Pelvic Inflamatory Deseases. Hivyo mwanamke anahitajika atibiwe mapema kabla madhara hayajakuwa makubwa.

2.Ugumba kwa wanaume. Kwa wanaume gonoria huathiri vimirija vijidogo vilivyopo kwenye korodani. Mirija hii hujulikana kama epididymis. Hali hii hupelekea kuharibika kwa mirija hii hivyo kushindwa kubeba mbegu za kiume kuzitoa nje. Ugonjwa unaosababishwa na uharibifu huu hujullukana kama epididymitis.

3.Mashambukizi ya viungo vingine vya mwili na kuleta homa, upele, vidonda, maimivu ya viungo, kukaza na kuvimba kwa viungio.

4.Huongeza hatari zaidi kwa mwenye VVU na UKIMWI. Watu wenye VVU na UKIMWI ni rahisi kueneza gonoria kwenda kwa mwingine.

5.Kwa watoto waliop[ata gonoria wakati wa lujifunguwa wanaweza kupata upofu na madhara mengine kati afya zao.



NJIA ZA KUPAMBANA NA KUKABILIANA NA GONORIA (GONORRHEA)
1.Kuwa mwaminifu katika mahusiano wacha kuchepuka
2.Hakikisha mwenza wako yupo salama
3.Usishiriki ngono na mtu aliyeathiriwa na magonjwa ya ngono bila kinga
4.Tumia kondomu
5.Pima mara kwa mara gonoria.



.





                   



Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 1844

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰2 Kitau cha Fiqh    ๐Ÿ‘‰3 Madrasa kiganjani    ๐Ÿ‘‰4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    ๐Ÿ‘‰5 Bongolite - Game zone - Play free game    ๐Ÿ‘‰6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Namna ya kuzuia uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo.

Posti hii inahusu zaidi namna ya kuzuia uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo,ni njia ambazo mtu anaweza kutumia Ili kuzuia uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo.zifuatazo ni njia zinazoweza kutumika kama mtu amepata uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo.

Soma Zaidi...
DALILI ZA UTUMBO KUZIBA

Kuziba kwa utumbo ni kuziba kwa chakula au kimiminika kisipite kwenye utumbo mwembamba au utumbo mpana (colon). Kuziba kwa matumbo kunaweza kusababishwa na mikanda ya nyuzi kwenye fumbatio ambayo huunda baada ya upasuaji, mifuko iliyovimba au iliyoambuk

Soma Zaidi...
Dalili na Ishara za mawe kwenye figo

Mawe kwenye figo yana sababu nyingi na yanaweza kuathiri sehemu yoyote ya njia yako ya mkojo kutoka kwa figo hadi kibofu chako.

Soma Zaidi...
Sababu zinazoweza kumfanya figo kuharibika.

Posti hii inahusu zaidi sababu za kufanya figo kuharibika.hili ni janga ambalo linawakumba Watu wengi siku hizi na kusababisha kupoteza maisha kwa wagonjwa wa figo hasa hasa kwa wale ambao hawana uwezo wa kulipia hela ya kusafishia figo.

Soma Zaidi...
Dalili za mkojo mchafu na rangi za mkojo na mkojo mchafu

Hapautajifunza rangi kuu za mkojo na dalili zako kiafya, mkojo mchafu na dalili zake

Soma Zaidi...
je maambukizi ya virus vya ukimwi yataonekana kwenye kupimo baada ya siku ngap??

Ni muda gani nitaanza kuona dalili za HIV na kilimo kitaonyesha kuwa nimeathirika?

Soma Zaidi...
Je mtu anaweza kushiriki mapenzi na mtu mwenye maambukizi ya ukimwi pasipo kuambukizwa?

Naomba kuuliza swaliJe mtu anaweza kushiriki mapenzi na mtu mwenye maambukizi ya ukimwi pasipo kuambukizwa?

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa homa ya uti wa mgongo

Posti hii inahusu zaidi Ugonjwa wa uti wa mgongo, ni ugonjwa unaoshambulia sehemu inayofunika ubongo na pia sehemu ya spinal cord

Soma Zaidi...
Fahamu Ugonjwa wa Saratani ya seli nyeupe.

Posti hii inazungumzia kuhusiana naร‚ย Sarataniร‚ย ambayo hutokea katika aina ya seli nyeupe ya damu inayoitwa seli ya plasma. Seli za plasma hukusaidia kupambana na maambukizo kwa kutengeneza kingamwili zinazotambua na kushambulia vijidudu. Pia husababish

Soma Zaidi...
Dalili za minyoo na sababu zake

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za minyoo na sababu zake

Soma Zaidi...