Njia za kuondokana na fangasi
Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuweza kupambana na fangasi za ukeni ili kuweza kujiepusha na madhara mbalimbali kwenye maisha ambayo ni pamoja na ugumba na Maambukizi kwenye via vya uzazi.
Njia za kuzuia fangasi.
1. Kunywa maji mengi angalau glass nane kwa siku,
Kwa kufanya hivyo unaweza kusaidia kiwango cha kupunguza fangasi kwenye maisha kwa sababu maji yanasaidia kutoa fangasi ambao wapo tayari kwenye sehemu mbalimbali za mwili au kwenye via vya uzazi.
2. Jaribu kuepuka matumizi ya vileo vikali na hasa matumizi ya pombe na kahawa kwa sababu ni vitu ambavyo usababisha kuwepo kwa fangasi, kwa kufanya hivyo utaweza kupunguza kiwango cha fangasi.
3. Kunywa maji mengi baada ya kujamiiana na kojoa baada ya kujamiiana, kwa sababu kama kuna fangasi wataweza kutoka na kuepuka kuendelea kuwepo katika sehemu mbalimbali.
4. Kwa kawaida tunapaswa kutawadha kuanzia mbele kwenda nyuma, kwa sababu ukianzia nyuma kwenda mbele kuna bakteria ambao wanaweza kutoka kwenye njia ya haja kubwa na kuingia kwenye uke hali ambayo Usababisha kuwepo kwa fangasi.
5 kwa kawaida tunapaswa kukata makucha makubwa kwa sababu mtu akitoka choo anaweza kuja na hao fangasi na kuweza kusababisha kuendelea kwa kuenea kwa fangasi bila kuwepo aina yoyote ya uponyaji.
6. Daima tumia pedi ukiwa kwenye siku zako za mwezi na pedi hiyo isizidi masaa mawili kwa hiyo baada ya masaa mawili unapaswa kubadilika hiyo aina ya pedi na kuanza kutumia nyingine.
7. Epuka matumizi ya vipodozi kwenye sehemu za siri, kwa kawaida kuna wanawake au wasichana kabla ya kujamiiana uweka vipodozi kwenye sehemu za siri kwa hiyo vipodozi hivyo ni hatari kwa afya.
8. Daima vaa nguo za ndani za pamba.
Kwa kufanya hivyo utaweza kupunguza njia ya kuenea kwa fangasi, kwa hiyo ni vizuri kabisa kuendelea kuendelea kupambana na fangasi ili kuweza kuepuka matatizo mbalimbali kama vile ugumba na Maambukizi kwenye via vya ya uzazi
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 Bongolite - Game zone - Play free game 👉3 Simulizi za Hadithi Audio 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
Dalili na namna ya kujizuia na malaria
Postii hii inshusiana na dalili na ishara za kujikinga au kuzuia malaria kwa Njia mbalimbali.
Soma Zaidi...Vyakula vinavyosaidia afya ya ubongo
Je, umewahi kuhisi ukungu wa akili (brain fog) au kusahau mambo madogo madogo? Ubongo ndio injini ya mwili wako, na unahitaji mafuta sahihi ili kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa. Makala hii inajadili vyakula vitano muhimu vilivyothibitishwa kisayansi kuboresha kumbukumbu, kuongeza umakini, na kulinda ubongo wako dhidi ya kuzeeka
Soma Zaidi...Dalili za ugonjwa wa uvimbe na mashambulizi ya bacteria kwenye korodani
Posti hii inaonyesha dalili,Sababu,na namna ya kujikinga na ugonjwa wa uvimbe na mashambulizi ya bacteria kwenye korodani ambao kitaalamu hujulikana Kama orchitis.
Soma Zaidi...Namna ya Kuzuia Mtoto mwenye kifua kikuu (TB).
posti hii inazungumzia kuhusiana na Ugonjwa wa kifua kikuu kwa watoto chini ya miaka mitano. Kifua kikuu ni ugonjwa sugu wa kuambukiza na anuwai ya magonjwa ya kliniki yanayosababishwa na Mycobacterium tuberculosis complex.
Soma Zaidi...Sababu za kuumwa na tumbo, chini ya kitomvu ama upande wa kulia
Post hii inakwenda kukutajia baadhi tu ya sababu zinazopelekea kuumwa na tumbo. Hali hizi zinawweza kuwapata watu wa jinsia zote katika umri wowote ule. Ijapokuwa nyingine si kwa wote ni kwa baadhi ya watu. hapa nitakuletea sababu 5 tu.
Soma Zaidi...Njia za kuzuia uwepo wa ugonjwa wa Bawasili.
Posti hii inahusu zaidi njia au mbinu ambazo zinaweza kutumika ili kuweza kuepuka kuwepo kwa ugonjwa wa Bawasili kwenye jamii, hizi ni njia za awali za kupambana na kuwepo kwa Ugonjwa wa Bawasili.
Soma Zaidi...