Njia za kuondokana na fangasi
Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuweza kupambana na fangasi za ukeni ili kuweza kujiepusha na madhara mbalimbali kwenye maisha ambayo ni pamoja na ugumba na Maambukizi kwenye via vya uzazi.
Njia za kuzuia fangasi.
1. Kunywa maji mengi angalau glass nane kwa siku,
Kwa kufanya hivyo unaweza kusaidia kiwango cha kupunguza fangasi kwenye maisha kwa sababu maji yanasaidia kutoa fangasi ambao wapo tayari kwenye sehemu mbalimbali za mwili au kwenye via vya uzazi.
2. Jaribu kuepuka matumizi ya vileo vikali na hasa matumizi ya pombe na kahawa kwa sababu ni vitu ambavyo usababisha kuwepo kwa fangasi, kwa kufanya hivyo utaweza kupunguza kiwango cha fangasi.
3. Kunywa maji mengi baada ya kujamiiana na kojoa baada ya kujamiiana, kwa sababu kama kuna fangasi wataweza kutoka na kuepuka kuendelea kuwepo katika sehemu mbalimbali.
4. Kwa kawaida tunapaswa kutawadha kuanzia mbele kwenda nyuma, kwa sababu ukianzia nyuma kwenda mbele kuna bakteria ambao wanaweza kutoka kwenye njia ya haja kubwa na kuingia kwenye uke hali ambayo Usababisha kuwepo kwa fangasi.
5 kwa kawaida tunapaswa kukata makucha makubwa kwa sababu mtu akitoka choo anaweza kuja na hao fangasi na kuweza kusababisha kuendelea kwa kuenea kwa fangasi bila kuwepo aina yoyote ya uponyaji.
6. Daima tumia pedi ukiwa kwenye siku zako za mwezi na pedi hiyo isizidi masaa mawili kwa hiyo baada ya masaa mawili unapaswa kubadilika hiyo aina ya pedi na kuanza kutumia nyingine.
7. Epuka matumizi ya vipodozi kwenye sehemu za siri, kwa kawaida kuna wanawake au wasichana kabla ya kujamiiana uweka vipodozi kwenye sehemu za siri kwa hiyo vipodozi hivyo ni hatari kwa afya.
8. Daima vaa nguo za ndani za pamba.
Kwa kufanya hivyo utaweza kupunguza njia ya kuenea kwa fangasi, kwa hiyo ni vizuri kabisa kuendelea kuendelea kupambana na fangasi ili kuweza kuepuka matatizo mbalimbali kama vile ugumba na Maambukizi kwenye via vya ya uzazi
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 Kitau cha Fiqh 👉3 web hosting 👉4 Kitabu cha Afya 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Dalili za miguu kufa ganzi
Posti hii inahusu zaidi dalili mbalimbali ambazo Uweza kujitokeza na kuona kwamba ni Dalili za miguu kufa ganzi, pengine utokea kwa watu wote na pengine huwa ni kwa ghafla
Soma Zaidi...Zifahmu Dalili za homa ya ini Kali ya pombe.
Posti hii inaonyesha dalili na Mambo Hatari yanayosababisha homa ya ini Kali ya pombe.
Soma Zaidi...Walio kwenye hatari ya kupata usaha kwenye mapafu
Post hii inahusu Zaidi watu walio kwenye hatari ya kupata usaha kwenye mapafu, pamoja na kuwepo Kwa sababu zinazopekekea kupata tatizo la kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu ila Kuna watu wenye hali Fulani wako kwenye hatari ya kupata usaha kwenye mapafu kama
Soma Zaidi...Dalili za HIV na UKIMWI kwenye Ulimi na Mdomo
Dalili za HIV na UKIMWI kwenye mdomo na ulimi utaziomna hapa. hizi zinaweza kuwa ndio za kwanza kwa ambaye hajapima HIV
Soma Zaidi...