picha

Njia za kuondokana na fangasi

Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuweza kupambana na fangasi za ukeni ili kuweza kujiepusha na madhara mbalimbali kwenye maisha ambayo ni pamoja na ugumba na Maambukizi kwenye via vya uzazi.

Njia za kuzuia fangasi.

1.  Kunywa maji mengi angalau glass nane kwa siku,

Kwa kufanya hivyo unaweza kusaidia kiwango cha kupunguza fangasi kwenye maisha kwa sababu maji yanasaidia kutoa fangasi ambao wapo tayari kwenye sehemu mbalimbali za mwili au kwenye via vya uzazi.

 

2. Jaribu kuepuka matumizi ya vileo vikali na hasa matumizi ya pombe na kahawa kwa sababu ni vitu ambavyo usababisha kuwepo kwa fangasi, kwa kufanya hivyo utaweza kupunguza kiwango cha fangasi.

 

3. Kunywa maji mengi baada ya kujamiiana na kojoa baada ya kujamiiana, kwa sababu kama kuna fangasi wataweza kutoka na kuepuka kuendelea kuwepo katika sehemu mbalimbali.

 

4. Kwa kawaida tunapaswa kutawadha kuanzia mbele kwenda nyuma, kwa sababu ukianzia nyuma kwenda mbele kuna bakteria ambao wanaweza kutoka kwenye njia ya haja kubwa na kuingia kwenye uke hali ambayo Usababisha kuwepo kwa fangasi.

 

5 kwa kawaida tunapaswa kukata makucha makubwa kwa sababu mtu akitoka choo anaweza kuja na hao fangasi na kuweza kusababisha kuendelea kwa kuenea kwa fangasi bila kuwepo aina yoyote ya uponyaji.

 

6. Daima tumia pedi ukiwa kwenye siku zako za mwezi na pedi hiyo isizidi masaa mawili kwa hiyo baada ya masaa mawili unapaswa kubadilika hiyo aina ya pedi na kuanza kutumia nyingine.

 

7. Epuka matumizi ya vipodozi kwenye sehemu za siri, kwa kawaida kuna wanawake au wasichana kabla ya kujamiiana uweka vipodozi kwenye sehemu za siri kwa hiyo vipodozi hivyo ni hatari kwa afya.

 

8. Daima vaa nguo za ndani za pamba.

Kwa kufanya hivyo utaweza kupunguza njia ya kuenea kwa fangasi, kwa hiyo ni vizuri kabisa kuendelea kuendelea kupambana na fangasi ili kuweza kuepuka matatizo mbalimbali kama vile ugumba na Maambukizi kwenye via vya ya uzazi

 

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2235

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 Bongolite - Game zone - Play free game     👉4 web hosting     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 ai web app    

Post zinazofanana:

Koo langu limekauka yaweza kuwa ni muadhirika?

kuwashwa na koo ni katika dalili za kuwa na maambukizi mwilini. Kuwa na maambukizi haimaanishi ni HIV ama UKIMWI laa hili ni neno pana. Hapa nitakujuza kwa ufupi kuhusu swali hilo la muulizaji kuwa anawashwa na koo.

Soma Zaidi...
Fahamu Ugonjwa unaosababisha madhara kwenye mapafu

Posti hii inaelezea kuhusiana na Magonjwa yanayosababisha madhara kwenye mapafu na kitaalamu hujulikana Ugonjwa wa Acute Respiratory Distress Syndrome (ARDS) hutokea wakati Majimaji yanapojaa kwenye vifuko vidogo vya hewa nyororo (alveoli) kwenye mapafu

Soma Zaidi...
Athari za kutokunywa maji ya kutosha kwa afya ya figo.

Figo ni kiungo muhimu kinachohusika na kusafisha damu na kudhibiti uwiano wa maji mwilini. Makala hii inachunguza kwa kina uhusiano wa moja kwa moja kati ya ulaji wa maji na afya ya figo. Tutajadili jinsi upungufu wa maji (dehydration) unavyoweza kusababisha magonjwa sugu ya figo, mawe kwenye figo, na shinikizo la damu, pamoja na kutoa mwongozo wa kisayansi wa kiasi sahihi cha maji unachohitaji ili kulinda afya yako.

Soma Zaidi...
Sababu za maumivu wakati wa kujamiiana

​Maumivu wakati wa kujamiiana (kitaalamu dyspareunia) ni tatizo linalowasumbua wanawake wengi, ingawa mara nyingi halizungumzwi wazi kutokana na unyanyapaa au aibu. Maumivu haya yanaweza kusababishwa na sababu za kisaikolojia, matatizo ya kimwili, au mabadiliko ya kihomoni. Makala haya yanachambua vyanzo vikuu vya maumivu hayo na kutoa ukweli wa kisayansi (Fact Check) ili kukusaidia kujua hatua za kuchukua.

Soma Zaidi...
Dalili za saratani ya koo

Saratani ya Koo inarejelea Vivimbe vya Saratani vinavyotokea kwenye koo lako (koromeo), sanduku la sauti (larynx) au tonsils.

Soma Zaidi...