Dalili za VVU


image


Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za VVU


DALILI ZA VVU

Dalilili za VVU huweza kutokea kuanzia wiki 2 mpaka 4 toka kuambukizwa. Lakini pia kwa baadhi ya ya watu inaweza kutokea mapema kabisa mnamo wiki ya kwanza. Na watu wengine dalili huizi zinaweza kutokea baadaye sana mpaka wiki ya sita. Dalili hizi si lazima mtu azipate zote. Dalili za mwanza zo VVU (HIV) ni pamoja na:-

 

Dalili za VVU katika hatuwa ya kwanza

1.Homa

2.Kuhisi baridi ama kutetemeka

3.Uota upele

4.Kutokwa na jasho wakatio wa usiku

5.Maumivu ya misuli

6.Kupata vidonda vya koo, ama kuwasha kwa koo.

7.Uchovu mkali usio elezeka

8.Kuvimba kwa tezi node za lymph yaani kuvimba tezi za mtoki mapajani, kwapa na shingoni.

9.Kupata vidonda kwenye mdomo

 

Dalili za VVU katika hatuwa ya pili

Baada ya dalili za awali katika hatuwa ya kwanza hadi kufikia wiki ya sita dalili za awali zitapotea. Kisha mtu ataingia katika hatuwa ya 2. hatuwa hii hujulikana kama clinical latency Stage ama pia huitwa chronic HIV infections. Hatuwa hii inaweza kuchukuwa mpaka miaka 10 toka kuambukizwa.

 

Watu waliokuwepo katika hatuwa hii hawana dalili yeyote ile. Kama mtu atatumia ART anaweza kudumu katika hatuwa hii kwa makumi ya miaka, ila kwa ambao hawajaanza kutumia ART wanaweza kupita kwa haraka kwenye hatuwa hii. Katika wakati huu mfumo wa kinga unaendelea kuharibiwa, ila uharibifu utakuwa mdogo ama hakuna endapo mtu ataanza kutumia ART au ARV.

 

HATUWA YA MWISHO NI UKIMWI

Ikitokea muathirika hakutimia ART basi virusi vitaendelea kuathiri mwili wake na kumaliza seli za CD4. hizi ndizo seli za kinga ya mwili yaani zinalinda mwili dhidi ya mashambulizi ya vijidudu kama virusi, bakteria, fangasi na vinginevyo. Mtu wa kawaida ana seli za cd4 kuanzia 500 mpaka 1500 katika kipimo kimoja. Sasa zikishuka mapaka kufikia 200 mgonjwa huyu ataambiwa ana Upungufu wa kinga Mwilini yaani UKIMWI. Mtu huyu atakuwa na dalili zifuatazo:-

 

Dalili za Ukiwmi:-

1.Kupunguwa uzito kwa haraka bila ya sababu maalumu ijulikanayo

2.Kupata homa kali za mara kwa mara na kutokwa na jasho jingi wakati wa usiku.

3.Kuchovu mkali sana usiojulikana sababu.

4.Kuendelea kuvimba kwa tezi za mtoki, kwapa na shingo

5.Kuharisha kunakoendelea zaidi ya wiki moja

6.Kutokwa na vidonda kwenye mdomo, ulimi, mkundu na sehemu za siri.

7.Kubana kwa pumzi

8.Kupoteza kumbukumbu, kukasirika mara kwa mara, ama kupoteza uwezo wa kuthibiti akili (kuchanganyikiwa)

9.Kuota mapele, majipu, mabumbuza kwenye ngozi, kope, pua na mdomoni



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    2 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    3 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    4 Download App zetu hapa ujifunze zaidi    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Mafidodo (mafindofindo) au tonsils kweye koo je inaweza ikawa Ni moja kati ya dalil za ukimwi
Tezi za lymph huanza kuonyesha dalili za kuwa mwili upo katika mapambano dhidi ya vijidudu vya maradhi. Ishara ni pale utakapoona tezi za lymph zina maumivu. Tezi hizi hupatikana kwenye mapaja, kwapa nashingo. Soma Zaidi...

image Dalili za VVU
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za VVU Soma Zaidi...

image Vipimo vya VVU
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu vipimo mbalimbali vinavyotumika kupima VVU Soma Zaidi...

image Undetectable viral load ni nini?
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maana ya undetectable viral load Soma Zaidi...

image Utaratibu wa maisha kwa aliye athirika
Somo hili linakwenda kukuletea utaratibu wa maisha kwa aliye athirika Soma Zaidi...

image Kushiriki ngono na mtu aliye na VVU na UKIMWI
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu namna ya kushiriki ngono na mtu aliye na VVU na UKIMWI Soma Zaidi...

image Dalili za ukimwi za kwenye ulimi na mdomo
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za ukimwi za kwenye ulimi na mdomo Soma Zaidi...

image Matibabu ya VVU na UKIMWI
Somo Hili linakwenda kukuletea matibabu ya VVU/UKIMWI Soma Zaidi...

image Je mtu akapima ukimwi na kile kipimo kidogo .je kina usahihi au la ..na pia kama inaonyesha mistari miwili.
Hivi umeshawahi kuwazakuwa jekipimo cha HIV ni sahihi kwa kiasi gani. Unadhani huwa kinakoseaga kutoa majibu? Soma Zaidi...

image Haya hayawezi kuambukiza UKIMWI
Somo hili linakwenda kukuletea mambo ambayo hayawezi kuambukiza UKIMWI Soma Zaidi...