Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za VVU
DALILI ZA VVU
Dalilili za VVU huweza kutokea kuanzia wiki 2 mpaka 4 toka kuambukizwa. Lakini pia kwa baadhi ya ya watu inaweza kutokea mapema kabisa mnamo wiki ya kwanza. Na watu wengine dalili huizi zinaweza kutokea baadaye sana mpaka wiki ya sita. Dalili hizi si lazima mtu azipate zote. Dalili za mwanza zo VVU (HIV) ni pamoja na:-
Dalili za VVU katika hatuwa ya kwanza
1.Homa
2.Kuhisi baridi ama kutetemeka
3.Uota upele
4.Kutokwa na jasho wakatio wa usiku
5.Maumivu ya misuli
6.Kupata vidonda vya koo, ama kuwasha kwa koo.
7.Uchovu mkali usio elezeka
8.Kuvimba kwa tezi node za lymph yaani kuvimba tezi za mtoki mapajani, kwapa na shingoni.
9.Kupata vidonda kwenye mdomo
Dalili za VVU katika hatuwa ya pili
Baada ya dalili za awali katika hatuwa ya kwanza hadi kufikia wiki ya sita dalili za awali zitapotea. Kisha mtu ataingia katika hatuwa ya 2. hatuwa hii hujulikana kama clinical latency Stage ama pia huitwa chronic HIV infections. Hatuwa hii inaweza kuchukuwa mpaka miaka 10 toka kuambukizwa.
Watu waliokuwepo katika hatuwa hii hawana dalili yeyote ile. Kama mtu atatumia ART anaweza kudumu katika hatuwa hii kwa makumi ya miaka, ila kwa ambao hawajaanza kutumia ART wanaweza kupita kwa haraka kwenye hatuwa hii. Katika wakati huu mfumo wa kinga unaendelea kuharibiwa, ila uharibifu utakuwa mdogo ama hakuna endapo mtu ataanza kutumia ART au ARV.
HATUWA YA MWISHO NI UKIMWI
Ikitokea muathirika hakutimia ART basi virusi vitaendelea kuathiri mwili wake na kumaliza seli za CD4. hizi ndizo seli za kinga ya mwili yaani zinalinda mwili dhidi ya mashambulizi ya vijidudu kama virusi, bakteria, fangasi na vinginevyo. Mtu wa kawaida ana seli za cd4 kuanzia 500 mpaka 1500 katika kipimo kimoja. Sasa zikishuka mapaka kufikia 200 mgonjwa huyu ataambiwa ana Upungufu wa kinga Mwilini yaani UKIMWI. Mtu huyu atakuwa na dalili zifuatazo:-
Dalili za Ukiwmi:-
1.Kupunguwa uzito kwa haraka bila ya sababu maalumu ijulikanayo
2.Kupata homa kali za mara kwa mara na kutokwa na jasho jingi wakati wa usiku.
3.Kuchovu mkali sana usiojulikana sababu.
4.Kuendelea kuvimba kwa tezi za mtoki, kwapa na shingo
5.Kuharisha kunakoendelea zaidi ya wiki moja
6.Kutokwa na vidonda kwenye mdomo, ulimi, mkundu na sehemu za siri.
7.Kubana kwa pumzi
8.Kupoteza kumbukumbu, kukasirika mara kwa mara, ama kupoteza uwezo wa kuthibiti akili (kuchanganyikiwa)
9.Kuota mapele, majipu, mabumbuza kwenye ngozi, kope, pua na mdomoni
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowPosti hii inahusu zaidi ugonjwa wa Dondakoo na namna unavyoweza kuenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine.
Soma Zaidi...Posti hii inaelezea kuhusiana na mambo hatari yanayosababisha ugonjwa wa moyo.
Soma Zaidi...Weupe kwenye ulimi unaweza kuwa ni hali ya kawaida. Weupe huu ukichanganyika na utandu huwenda ikaashiria uwepo wa hali fulani za kiafya.
Soma Zaidi...Mrija wa mkojo hutoa mkojo nje ya mwili lakini mrija huu unapoziba hufanya utoaji wa mkojo kutoka kwa shida au maumivu
Soma Zaidi...Hapa utajifunza sababu zinzopelekea mdomo kubadilika ladha na kuwa mchungu, ama mchachu.
Soma Zaidi...Post yetu Leo inaenda kuzungumzia Maumivu ya nyuma ni malalamiko ya kawaida. Kwa upande mkali, unaweza kuchukua hatua za kuzuia au kupunguza matukio mengi ya maumivu ya mgongo. Ikiwa kinga itashindikana, matibabu rahisi ya nyumbani na mbinu sahihi za m
Soma Zaidi...Dr huwa nasikia maumivu makali sana juu ya tumbo yn kama kuna moto hivi na mgongon kama unadungwa sindano hivi je hizo ni dalili za vidonda vya tumbo?
Soma Zaidi...Ujue ugonjwa wa Njia ya mkojo unaoitwa urethra stricture. Ambapo kwenye hii posti inaonyesha dalili na Sababu zinazopelekea Njia ya mkojo kuwa ngumu,nyembamba,na kovu.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dalili za kansa, ni dalili ambazo utokea kwa mtu Mwenye tatizo la ugonjwa wa Kansa ingawa sio lazima dalili hizi kutokea tukadhani kuwa ni Kansa Ila zilizonyingi huwa ni kweli dalili za kansa.
Soma Zaidi...