Dalili za VVU

Dalili za VVU

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za VVU

Download Post hii hapa

DALILI ZA VVU

Dalilili za VVU huweza kutokea kuanzia wiki 2 mpaka 4 toka kuambukizwa. Lakini pia kwa baadhi ya ya watu inaweza kutokea mapema kabisa mnamo wiki ya kwanza. Na watu wengine dalili huizi zinaweza kutokea baadaye sana mpaka wiki ya sita. Dalili hizi si lazima mtu azipate zote. Dalili za mwanza zo VVU (HIV) ni pamoja na:-

 

Dalili za VVU katika hatuwa ya kwanza

1.Homa

2.Kuhisi baridi ama kutetemeka

3.Uota upele

4.Kutokwa na jasho wakatio wa usiku

5.Maumivu ya misuli

6.Kupata vidonda vya koo, ama kuwasha kwa koo.

7.Uchovu mkali usio elezeka

8.Kuvimba kwa tezi node za lymph yaani kuvimba tezi za mtoki mapajani, kwapa na shingoni.

9.Kupata vidonda kwenye mdomo

 

Dalili za VVU katika hatuwa ya pili

Baada ya dalili za awali katika hatuwa ya kwanza hadi kufikia wiki ya sita dalili za awali zitapotea. Kisha mtu ataingia katika hatuwa ya 2. hatuwa hii hujulikana kama clinical latency Stage ama pia huitwa chronic HIV infections. Hatuwa hii inaweza kuchukuwa mpaka miaka 10 toka kuambukizwa.

 

Watu waliokuwepo katika hatuwa hii hawana dalili yeyote ile. Kama mtu atatumia ART anaweza kudumu katika hatuwa hii kwa makumi ya miaka, ila kwa ambao hawajaanza kutumia ART wanaweza kupita kwa haraka kwenye hatuwa hii. Katika wakati huu mfumo wa kinga unaendelea kuharibiwa, ila uharibifu utakuwa mdogo ama hakuna endapo mtu ataanza kutumia ART au ARV.

 

HATUWA YA MWISHO NI UKIMWI

Ikitokea muathirika hakutimia ART basi virusi vitaendelea kuathiri mwili wake na kumaliza seli za CD4. hizi ndizo seli za kinga ya mwili yaani zinalinda mwili dhidi ya mashambulizi ya vijidudu kama virusi, bakteria, fangasi na vinginevyo. Mtu wa kawaida ana seli za cd4 kuanzia 500 mpaka 1500 katika kipimo kimoja. Sasa zikishuka mapaka kufikia 200 mgonjwa huyu ataambiwa ana Upungufu wa kinga Mwilini yaani UKIMWI. Mtu huyu atakuwa na dalili zifuatazo:-

 

Dalili za Ukiwmi:-

1.Kupunguwa uzito kwa haraka bila ya sababu maalumu ijulikanayo

2.Kupata homa kali za mara kwa mara na kutokwa na jasho jingi wakati wa usiku.

3.Kuchovu mkali sana usiojulikana sababu.

4.Kuendelea kuvimba kwa tezi za mtoki, kwapa na shingo

5.Kuharisha kunakoendelea zaidi ya wiki moja

6.Kutokwa na vidonda kwenye mdomo, ulimi, mkundu na sehemu za siri.

7.Kubana kwa pumzi

8.Kupoteza kumbukumbu, kukasirika mara kwa mara, ama kupoteza uwezo wa kuthibiti akili (kuchanganyikiwa)

9.Kuota mapele, majipu, mabumbuza kwenye ngozi, kope, pua na mdomoni

Download Post hii hapa

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 2254

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Dalili za upungufu wa maji mwilini.
Dalili za upungufu wa maji mwilini.

Upungufu wa maji mwilini hutokea unapotumia au kupoteza Majimaji mengi zaidi ya unayonywa, na mwili wako hauna maji ya kutosha na Majimaji mengine ya kufanya kazi zake za kawaida. Usipochukua nafasi ya Vimiminika vilivyopotea, utapungukiwa na maji.

Soma Zaidi...
Dalili za ugonjwa wa uvimbe na mashambulizi ya bacteria kwenye korodani
Dalili za ugonjwa wa uvimbe na mashambulizi ya bacteria kwenye korodani

Posti hii inaonyesha dalili,Sababu,na namna ya kujikinga na ugonjwa wa uvimbe na mashambulizi ya bacteria kwenye korodani ambao kitaalamu hujulikana Kama orchitis.

Soma Zaidi...
Yajue magonjwa nyemelezi.
Yajue magonjwa nyemelezi.

Posti hii inahusu zaidi magonjwa nyemelezi ambayo kwa kawaida utokea pale ambapo kinga ya mwili inashuka.

Soma Zaidi...
Fahamu Ugonjwa unaohusiana na kuzidi kwa joto  mwilini (anhidrosis) ama heatshock
Fahamu Ugonjwa unaohusiana na kuzidi kwa joto mwilini (anhidrosis) ama heatshock

posti hii inazungumzia kuhusiana na Ugonjwa na Ugonjwa unaohusiana na joto ambao hujulikana Kama Anhidrosis ni kutoweza jasho kawaida. Usipotoa jasho mwili wako hauwezi kujipoza, jambo ambalo linaweza kusababisha joto kupita. wakati mwingine inaweza k

Soma Zaidi...
Uchunguzi wa kuharisha damu na tiba yake
Uchunguzi wa kuharisha damu na tiba yake

Posti hii inahusu zaidi uchunguzi wa kuharisha damu na Tiba yake, ni Ugonjwa ambao unaowashambulia sana watoto hasa wenye chini ya umri wa miaka mitano, kwa hiyo huoaugonjwa tunaweza kuutambua na kutibu kwa njia zifuatazo.

Soma Zaidi...
Dalili za kipindupindu na njia za kujilinda na kipindupindu.
Dalili za kipindupindu na njia za kujilinda na kipindupindu.

Post hii inazungumzia zaidi kuhusiana na ugonjwa wa kipindupindu.kipindupindu ni ugonjwa unaosababishwa na mdudu ambaye kwa kitaalamu anaitwa vibrio cholera.mdudu huyu hushambulia utumbo mdogo na kusababisha madhara mengi.

Soma Zaidi...
Dalili za mkojo mchafu na rangi za mkojo na mkojo mchafu
Dalili za mkojo mchafu na rangi za mkojo na mkojo mchafu

Hapautajifunza rangi kuu za mkojo na dalili zako kiafya, mkojo mchafu na dalili zake

Soma Zaidi...
Dalili za minyoo
Dalili za minyoo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za minyoo

Soma Zaidi...
Namna ya kufanya usafi wa sikio
Namna ya kufanya usafi wa sikio

Post hii inahusu zaidi namna ya kufanya usafi wa sikio, sikio ni mojawapo ya ogani ambayo usaidia kusikia,kwa hiyo sikio linapaswa kusafishwa kwa uangalifu kama tutakavyoona hapo chini.

Soma Zaidi...
Dalili za Pua iliyovunjika
Dalili za Pua iliyovunjika

posti hii inahusu dalili za Pua iliyovunjika, pia inaitwa fracture ya pua, ni kuvunjika au kupasuka kwa mfupa katika pua yako

Soma Zaidi...