NI WATU GANI WALIO HATARINI ZAIDI KUPATA UKIMWI?

Post hii itakwena kukufundisha kuhusu historia fupi ya Ukimwi na matibabu yake. Ni wapi wapo hatarini kupata maambukizi na ni kitu gani wafanye?

Ukimwi ni moja ya matatizo ya kiafya ambayo yanaathiri afya ya mwili, akili na kijamii. Toka dunia imeanza kutambuwa ugonjwa huu miaka ya 1980 mpaka sasa tayari mamilioni ya watu wamesha kufa kutokana na maradhi yanayohusiana na UKIMWI. kila mtu anaweza kupata ukimwi awe mtoto ama mtumzima. Lakini wapo watu ambao wapo hatarini Zaidi. Je na wewe ni miongoni mwao, je unataka kujuwa ni tahadhari zipi watumie, na dawa zipi watumie? Endelea na Makala hii upate majibu yako.

 

Kutokana na mendeleo ya sayansi na teknolojia hasa katika Nyanja za afya, leo hii watu walio hatarini Zaidi kupata maambukizi wanaweza kupewa dawa za kusaidia kuwakinga na kuwapunguzia hatari ya kuweza kupata maambukizi mapya. Hata jhivyo elimu Zaidi bado inatolewa kuwasaidi watu hawa kuweza kujilinda na kujikinga na maabukizi ya VVU na UKIMWI. Bilas haka ungependa kuwajuwa watu hawa pamoja na tahadhari wanazopatiwa na wanazopasa kuzitumia. Basi endelea na Makala hii hadi mwisho.

 

Je ni kina nani hao walio hatari Zaidi kupata maambukizi?

Kama nilivyokueleza hapo mwanzo kuwa kila mtu yupo hatarini kupata maambukizi bila ya kujali umri, eneo, jinsia wala muonekano. Lakini wapo watu ambao wao wapo hatarini Zaidi. Hatari hii hutokana na maeneo wanayoishi, jamii wanayoishi, tabia zao na shughuli wanazofanya. Hapa nitakuletea baadhi tu ya watu ambao wapo hatarini Zaidi kulingana na vigezo hivyo. Watu haw ani kama:-

  1. Walio hatarini kulingana na shughuli zao: kundi hili huchukuwa watu ambao shughuli zaoza utafutaji ndio zinawaweka katika mazingira hatarishi ya kupata maambukizi. Watu walio katika kundi hili ni pamoja na:-
  2. Wauguzi katika wodi za waathirika.
  3. Wanaofanya shuguli za kujiuza.
  4. Wanaosaidia waathirika walio wagonjwa wasioweza kujisaidia wenyewe baadhi yam abo kama kuoga, kufuwa, kujisafisha na mengineyo

 

  1. Walio hatarini kutokana na tabia zao ama namna ambavyo wanaishi. Kundi hili linakusanya watu ambao wanajiingiza katika hatari ya kupata maambukizi kutokana na namna ambavyo wamezoea kuisha ama kutokana na tabia zao. Watu hawa ni kama:-
  2. Watu wenye wapenzi zaidi ya mmoja, na hao wapenzi wao wakawa na wapenzi wengine
  3. Watu wanaoshiriki ngono kinyume na maumbile
  4. Wasagaji wanaoshirikiana vifaa vya kufanyia ngono
  5. Watu wanaojiuza kingono
  6. Wanaofanya ngono na watu wasiowajuwa
  7. Watumiaji madawa ya kulevya kwa njia ya kujidunga na wakawa wanashirikiana vifaa vya kujidungia madawa.

 

  1. Watu walio hatarini kutokana na jamii wanazoishi;watu hawa ni wale ambao wanaishi kwenye jamii ambayo idadi ya waathirika ni kubwa ukilinganisha na maeneo mengine. Pia kuna ambao wanaishi na waathirika katika ndoa zao. Hawa pia wapo hatarini lakini wakifata ushauri vyema wataweza kupunguza hatari ya maambukizi kwao na kwa watoto wao. Watoto wanaonyonya wakiwa na umri zaidi ya miezi sita hawa pia wapo hatarini kupata maambukizi.

 

  1. Watotonwanaonyonya ama walio matumboni pia wapo hatarini kupata maambukizo, kwani endapo mama muathirika atafanya uzembe anaweza kuhatarisha maisha ya mtoto wake anayenyonya ama aliye tumboni.

 

Nini nifanye endapo ninaishi katika mazingira hatarishi ya kupata maambukizi?

Kama upo hatarini kupata maambukizi, ni vyema ufike kituo cha afya na uonane na wataalamu wa ushauri nasaha. Hawa ni wataalamu ambao watakupatia maelekezo ya kufanya, na ushauri juu ya kujilinda na maambukizi kulingana na hali ya sehemu unayoishi.

 

Kama tatizo ni tabia ama namna ambavyo unavyoishi ndio hukutia katika hatari ya kupata maambukizi, jitahidi kubadili tabia na kuwa muaminifu. Kwa washiriki wa ngono kinyume na maumbie hii tabia ni hatari zaidi kupata maambukizi. Matumizi ya kondomu ni muhimu kama upo hatarini na unaishi na muathirika. Ni vyema kumuachisha ziwa mtoto mapema iwezekanavyo hata kabla ya kuota mengo yanayong’ata.

 

Mama mjamzito akiwa muathirika ahakikishe anafata masharti yote aliyopewa, ana awe anahudhuria kituo cha afya kama alivyopangiwa. Ameze dawa vyema na kwa utaratibu. Lishe bora kwa mama mnyonyeshaji na mwenye ujauzito ni muhimu sana. Wakifanya hivi wanaweza kupunguza hatari ya watoto wao kupata maambukizi.

 

Nini nifanye endapo ninahisi kuwa nimepata maambukizi ama nimeshiriki ngono na muathirika?

Hili ni katika maswali mengi yaliyopata kuulizwa na watu mitandaoni. Nini mtu afanye endapo atafanya ngono na muathirika ama nini mtu afanye endapo atahisi kuwa amepata maambukizi. Jibu la maswahi haya linaweza kuwa fupi tu nalo ni kumwambia aende kituo cha afya kisha akutane na watoa ushauri nasaha. Majibu zaidi juu ya maswli yake yatakayotokana na swali hili atayapata huko.

 

Mtu huyu anatakiwa afike kituo cha afya kwa sababu si kila anayeshiriki ngono na muathirika naye atakuwa na maambukizi. Kuna sababu nyingi zinazofanya mtu ashiriki ngono zembe na muatirika na asipate maambukizi. Hivyo huwenda naye akaondolewa hofu kutokana na maelezo yake ikawa hakuna haja ya kuishi kwa hofu kuwa ni muathirika.

 

Pia kituo cha afya anaweza kupatiwa dawa za kutumia iwe kama kinga ya kuzuia maambukizi mapya endapo atakuwa amewahi ndani ya muda muafaka. Siku hizi wauguzi wanaweza kujiweka salama kwa ailimia zaidi ya 90 baada ya kuingia katika hatari ya kupata maambikizi kama kujichoma sindano iliyomchoma muathirika na namna nyinginezo. Watu wanaobakwa hupatiwa dawa hizi iwe kama kinga endapo kutatokea maabukizi.

Ni matibabu gani hupatiwa mtu aliye hisi kupata maambukizi?

Endapo itahitajika na mtu akiwa amewahi kufika kituo cha afya kuna dawa anaweza kupewa ili kumlinda na maambukizi. Kuna matibabu aina 2 ambao ni PrEP na PEP. Dawa hizi hutumika kulingana na mazingira hatarishi yaliyompata mtu, na ni kwa kiasi gani huwenda atakuwa amepata maambukizi. Sasa hebu tuone nana ambavyo dawa hizi hutumika na je ni kwa kiasi gani mtu atakuwa salama.

 

  1. Je matibabu yaitwayo PrEP yapo vipi?

PrEP ni ufupisho wa maneno pre-exposure prophylaxis. Daw hii hupatiwa mtu ambaye anahisi huwenda atakuwa amepata maambukizi. Kwa mfano mtu aliyeshiriki ngono akiwa na kondomu na mwenye maambukizi ama awe anamuhisi lakini hana uhakika kuwa ana maambukizi. Kwa hiyo kabla ya kupewa dawa hizi mtu huyo kwanza atafanyiwa vipimo kujuwa kama hana virusi kisha ndipo apatiwe dawa.

 

  1. Je matibabu yaitwayo PEP ipo vipi?

PEP kifupisho cha maneno post-exposure prophylaxis. Dawa hizi hupatiwa mtu ambaye amepata maambukizi mapya. Kwa mfano amejishoma na sindano ambayo amechomwa muathirika. Ama ameshiriki ngono zembe na mtu muathirika ama mtu aliyebakwa naye atapewa dawa hii.

 

Kuna dawa nyingi ambazo zipo kwenye matibabu haya mawili. Lakini pia zipo dawa mabazo zinafanya kazi zote mbili kama PrEP na kama PEP. Kwa mfano dawa iitwayo Truvada hii inafanya kazi zote mbili. Baada ya kumeza dawa hizi unaweza kuona mabadiliko kama:-

  1. Kichefuchefu, kuharishama akutapika
  2. Maumivu ya kichwa na kizunguzungu
  3. Hasira na mvurugiko wa mawazo
  4. Infection kwenye koo
  5. Upele
  6. Kukosa usingizi

Tukitane makala inayofata tutakapoona mambo kadhaa kuhusu vidonda vya tumbo.

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 1506

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Ugonjwa wa surua kwa watoto.

Surua ni ugonjwa wa kuambukiza unaosababishwa na homa na upele mwekundu, unaotokea utotoni. Wakati mtu aliye na virusi akikohoa au kupiga chafya, matone yaliyoambukizwa huenea angani na kutua kwenye sehemu zilizo karibu. Mtoto anaweza kupata virusi kwa ku

Soma Zaidi...
Chanzo cha VVU na UKIMWI

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu vyanzo m ali mbali vinavyohisiwa kuwa chanzo cha UKIMWI

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa pepopunda kwa watoto

Pepopunda ni ugonjwa hatari wa kutishia maisha unaosababishwa na sumu inayojulikana Kama tetanospasmin inayotolewa kwenye majeraha yaliyoambukizwa. Bakteria ya pepopunda huingia kwenye mwili wa mtoto mchanga kupitia kisiki cha kitovu ambacho kimekatwa na

Soma Zaidi...
Dalili za Ugonjwa wa pombe wakati Mtoto akiwa tumboni

Ugonjwa wa ulevi wakati Mtoto akiwa tumboni (fetasi) ni hali ya mtoto inayotokana na unywaji pombe wakati wa ujauzito wa mama. Ugonjwa wa pombe wa fetasi husababisha uharibifu wa ubongo na matatizo ya ukuaji.

Soma Zaidi...
Ijuwe saratani ya kibofu cha nyongo

Makala hii inakwenda kukufahamishavkuhusu saratani yavkibifu cha mkojo.

Soma Zaidi...
Sababu za kutokea kwa maumivu ya jino

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za kutokea kwa maumivu ya jino

Soma Zaidi...
Dawa za kutibu kiungulia

Somo hili linakwenda kukueleza baadhi ya dawa za kutibu kiungulia

Soma Zaidi...
Yajue magonjwa ya kurithi.

Posti hii inahusu zaidi Magonjwa vya kurithi ambayo mara nyingi utokea kwenye jamii ni magonjwa ambayo yanaweza kutokea kwenye familia na wanafamilia walio wengi wakaweza kupata ugonjwa huo Magonjwa yenyewe ni kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
Aina za kisukari

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu aina za kisukari

Soma Zaidi...
Dalili za UKIMWI

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za UKIMWI

Soma Zaidi...