Post hii itakwena kukufundisha kuhusu historia fupi ya Ukimwi na matibabu yake. Ni wapi wapo hatarini kupata maambukizi na ni kitu gani wafanye?
Ukimwi ni moja ya matatizo ya kiafya ambayo yanaathiri afya ya mwili, akili na kijamii. Toka dunia imeanza kutambuwa ugonjwa huu miaka ya 1980 mpaka sasa tayari mamilioni ya watu wamesha kufa kutokana na maradhi yanayohusiana na UKIMWI. kila mtu anaweza kupata ukimwi awe mtoto ama mtumzima. Lakini wapo watu ambao wapo hatarini Zaidi. Je na wewe ni miongoni mwao, je unataka kujuwa ni tahadhari zipi watumie, na dawa zipi watumie? Endelea na Makala hii upate majibu yako.
Kutokana na mendeleo ya sayansi na teknolojia hasa katika Nyanja za afya, leo hii watu walio hatarini Zaidi kupata maambukizi wanaweza kupewa dawa za kusaidia kuwakinga na kuwapunguzia hatari ya kuweza kupata maambukizi mapya. Hata jhivyo elimu Zaidi bado inatolewa kuwasaidi watu hawa kuweza kujilinda na kujikinga na maabukizi ya VVU na UKIMWI. Bilas haka ungependa kuwajuwa watu hawa pamoja na tahadhari wanazopatiwa na wanazopasa kuzitumia. Basi endelea na Makala hii hadi mwisho.
Je ni kina nani hao walio hatari Zaidi kupata maambukizi?
Kama nilivyokueleza hapo mwanzo kuwa kila mtu yupo hatarini kupata maambukizi bila ya kujali umri, eneo, jinsia wala muonekano. Lakini wapo watu ambao wao wapo hatarini Zaidi. Hatari hii hutokana na maeneo wanayoishi, jamii wanayoishi, tabia zao na shughuli wanazofanya. Hapa nitakuletea baadhi tu ya watu ambao wapo hatarini Zaidi kulingana na vigezo hivyo. Watu haw ani kama:-
Nini nifanye endapo ninaishi katika mazingira hatarishi ya kupata maambukizi?
Kama upo hatarini kupata maambukizi, ni vyema ufike kituo cha afya na uonane na wataalamu wa ushauri nasaha. Hawa ni wataalamu ambao watakupatia maelekezo ya kufanya, na ushauri juu ya kujilinda na maambukizi kulingana na hali ya sehemu unayoishi.
Kama tatizo ni tabia ama namna ambavyo unavyoishi ndio hukutia katika hatari ya kupata maambukizi, jitahidi kubadili tabia na kuwa muaminifu. Kwa washiriki wa ngono kinyume na maumbie hii tabia ni hatari zaidi kupata maambukizi. Matumizi ya kondomu ni muhimu kama upo hatarini na unaishi na muathirika. Ni vyema kumuachisha ziwa mtoto mapema iwezekanavyo hata kabla ya kuota mengo yanayong’ata.
Mama mjamzito akiwa muathirika ahakikishe anafata masharti yote aliyopewa, ana awe anahudhuria kituo cha afya kama alivyopangiwa. Ameze dawa vyema na kwa utaratibu. Lishe bora kwa mama mnyonyeshaji na mwenye ujauzito ni muhimu sana. Wakifanya hivi wanaweza kupunguza hatari ya watoto wao kupata maambukizi.
Nini nifanye endapo ninahisi kuwa nimepata maambukizi ama nimeshiriki ngono na muathirika?
Hili ni katika maswali mengi yaliyopata kuulizwa na watu mitandaoni. Nini mtu afanye endapo atafanya ngono na muathirika ama nini mtu afanye endapo atahisi kuwa amepata maambukizi. Jibu la maswahi haya linaweza kuwa fupi tu nalo ni kumwambia aende kituo cha afya kisha akutane na watoa ushauri nasaha. Majibu zaidi juu ya maswli yake yatakayotokana na swali hili atayapata huko.
Mtu huyu anatakiwa afike kituo cha afya kwa sababu si kila anayeshiriki ngono na muathirika naye atakuwa na maambukizi. Kuna sababu nyingi zinazofanya mtu ashiriki ngono zembe na muatirika na asipate maambukizi. Hivyo huwenda naye akaondolewa hofu kutokana na maelezo yake ikawa hakuna haja ya kuishi kwa hofu kuwa ni muathirika.
Pia kituo cha afya anaweza kupatiwa dawa za kutumia iwe kama kinga ya kuzuia maambukizi mapya endapo atakuwa amewahi ndani ya muda muafaka. Siku hizi wauguzi wanaweza kujiweka salama kwa ailimia zaidi ya 90 baada ya kuingia katika hatari ya kupata maambikizi kama kujichoma sindano iliyomchoma muathirika na namna nyinginezo. Watu wanaobakwa hupatiwa dawa hizi iwe kama kinga endapo kutatokea maabukizi.
Ni matibabu gani hupatiwa mtu aliye hisi kupata maambukizi?
Endapo itahitajika na mtu akiwa amewahi kufika kituo cha afya kuna dawa anaweza kupewa ili kumlinda na maambukizi. Kuna matibabu aina 2 ambao ni PrEP na PEP. Dawa hizi hutumika kulingana na mazingira hatarishi yaliyompata mtu, na ni kwa kiasi gani huwenda atakuwa amepata maambukizi. Sasa hebu tuone nana ambavyo dawa hizi hutumika na je ni kwa kiasi gani mtu atakuwa salama.
PrEP ni ufupisho wa maneno pre-exposure prophylaxis. Daw hii hupatiwa mtu ambaye anahisi huwenda atakuwa amepata maambukizi. Kwa mfano mtu aliyeshiriki ngono akiwa na kondomu na mwenye maambukizi ama awe anamuhisi lakini hana uhakika kuwa ana maambukizi. Kwa hiyo kabla ya kupewa dawa hizi mtu huyo kwanza atafanyiwa vipimo kujuwa kama hana virusi kisha ndipo apatiwe dawa.
PEP kifupisho cha maneno post-exposure prophylaxis. Dawa hizi hupatiwa mtu ambaye amepata maambukizi mapya. Kwa mfano amejishoma na sindano ambayo amechomwa muathirika. Ama ameshiriki ngono zembe na mtu muathirika ama mtu aliyebakwa naye atapewa dawa hii.
Kuna dawa nyingi ambazo zipo kwenye matibabu haya mawili. Lakini pia zipo dawa mabazo zinafanya kazi zote mbili kama PrEP na kama PEP. Kwa mfano dawa iitwayo Truvada hii inafanya kazi zote mbili. Baada ya kumeza dawa hizi unaweza kuona mabadiliko kama:-
Tukitane makala inayofata tutakapoona mambo kadhaa kuhusu vidonda vya tumbo.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kujikinga na magonjwa, kwa kawaida tunajua wazi kuwa magonjwa yapo na yanasambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na mengine hayasambai yanaweza kumpata mtu mmoja akapona au magonjwa mengine si ya kupona
Soma Zaidi...Posti hii inahusu namna madonda koo yanavyotokea, ni jinsi na namna Magonjwa haya au Maambukizi yanavyotokea na kuweza kusababisha madhara kwa watu.
Soma Zaidi...Post hii inakwenda kukujulisha dalili za kuwa huwenda una fangasi sehemu zako za siri.
Soma Zaidi...Tezi dume ambayo haijashuka si ya kawaida kwa ujumla, lakini ni ya kawaida kwa wavulana waliozaliwa kabla ya wakati.na muda mwingine zikipanda tumboni huwa hazishuki kabisa kwenye korodani.
Soma Zaidi...Kila mtu anaweza kupata ugonjwa wa pumu, hata hivyo kuna ambao wapo hatarini zaidi kupata pumu.
Soma Zaidi...posti hii inaelezea kuhusiana na dalilili na Mambo ya hatari ya Macho makavu hutokea wakati machozi yako hayawezi kutoa unyevu wa kutosha kwa macho yako. Machozi yanaweza kuwa duni kwa sababu nyingi. Kwa mfano, Macho makavu yanaweza ku
Soma Zaidi...posti hii inahusu dalili za Homa ya Manjano ni maambukizi ya virusi yanayoenezwa na aina fulani ya mbu. Maambukizi hayo ni ya kawaida zaidi na kuathiri wasafiri na wakazi wa maeneo hayo.
Soma Zaidi...Afya ya tumbo ni ishara tosha ya umadhibuti wa afya ya mtu. Maradhi mengi wanayouguwa watu chanzo kile mti anachokula. Yapo maradhi sugu kama saratani ambayo husababishwa pia na vyakula. Post hii itakwenda kujibu swalo la muulizaji kuhusu maumivu ya tumbo
Soma Zaidi...DALILI ZA HIV ZA MWANZO NA DALILI ZA UKIMWI ZA MWANZO Kama ilivyo magonjwa mengi hupitia hatua kadha kadha na kuonyesha dalili kadha katika hatua hizo.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa Bawasili, ni Dalili ambazo ujitokeza kwa mgonjwa ambaye ana ugonjwa wa Bawasili.
Soma Zaidi...