picha

Njia za kufanya ukiwa na tatizo la uti wa mgongo.

Posti hii inahusu zaidi Njia za kufanya Ili kupunguza maumivu ya tatizo la uti wa mgongo, ni njia unazopaswa kufanya pale unapokuwa na tatizo la uti wa Mgongo.

Njia za kufanya ukiwa na tatizo la uti wa mgongo.

1.Tumia vitu vya moto.

Kama Kuna tatizo la uti wa mgongo,lazima kutumia vitu vya moto zaidi kuliko vya baridi Ili kupunguza hali ya kusinyaa kwa misuli na kufanya misuli kutanuka na maumivu huwa kidogo sana.mfano kuweka maji ya moto kwenye taulo na kujikanda na taulo la moto kwenye sehemu ya maumivu.

 

2. Tumia barafu kama mtu amepata ajali Ili kupunguza moto ambao upo kwenye pingili, pengine kama ni kuvunjika pingili zinakuwa za moto sana na kusababisha maumivu Ili kupunguza maumivu makali kwenye uti wa mgongo, barafu inabidi itolewe Ili kupunguza joto ambalo upelekea maumivu na kitendo hiki kisizidi dakika Kumi.

 

3. Mazoezi mepesi yatumike.

Mtu mwenye matatizo ya uti wa mgongo mazoezi mepesi yatumike Ili kufanya mwili kutanuka na kuruhusu kuruhusu damu ipite na pengine sehemu iliyokuwa umepata shida inaweza kurudi kwa kutumia mazoezi na mazoezi yasiwe makali sana kwa sababu yanaweza kusababisha kuvunjika zaidi, kwa hiyo mazoezi ni ya lazima.

 

4.Acha kubeba vitu vizito.

Kwa mtu mwenye matatizo ya uti wa mgongo anapaswa kuepuka kubeba vitu vizito kwa sababu katika kubeba vitu vizito Kuna hatari unaweza kusababisha maumivu zaidi na kumpelekea ulemavu wa kudumu, kwa hiyo watu wenye matatizo ya uti wa mgongo wanapaswa kuacha kubeba vitu vizito.

 

5.Tumia godoro gumu wakati wa kulala.

Wakati wa kulala wenye matatizo ya uti wa mgongo wanapaswa kulalia magodoro magumu Ili kufanya pingili zikae kwenye sehemu yake kwa sababu katika kutumia godoro matatizo ya mgongo yanaweza kupungua na kuwa kwenye hali ya kawaida.

 

6.Tumia mshipi wa mgongo

Watu wenye matatizo ya uti wa Mgongo wanapaswa kutumia mshipi wa kufungia mgongo Ili kuufanya mgongo uweze kushikana vizuri na pingili zinaweza kurudi kwenye hali yake kawaida, kwa kufanya hivyo mtu anaweza kukaa kwa mda mrefu kusimama kwa mda mrefu akiwa amefunga mgongo wake.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 3237

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉5 ai web app     👉6 web hosting    

Post zinazofanana:

Njia za kupambana na kuzuia gonorrhea

Somo hili linakwenda kukueleza baadhi ya njia za kupambana na kuzuia gonorrhea

Soma Zaidi...
Madhara ya kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu

Post hii inahusu Zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea Kwa mgonjwa mweye usaha kwenye mapafu.

Soma Zaidi...
Nini kinasababisha kizunguzungu?

Posti hii inaelezea kuhusiana na dalili za kizunguzungu zinazotekea katika mwili wa binadamu

Soma Zaidi...
Dalili za kuvimbiwa kwa watoto.

Kuvimbiwa kwa watoto ni shida ya kawaida. Kuvimbiwa kwa watoto mara nyingi huonyeshwa na kinyesi kisicho kawaida au kinyesi ngumu na kavu.

Soma Zaidi...
Dalili za tetekuwanga

Tetekuwanga (varisela) ni maambukizi ya virusi ambayo husababisha kuwasha, upele kama vile malengelenge. Tetekuwanga huambukiza sana watu ambao hawajapata ugonjwa huo wala kupewa chanjo dhidi yake. Kabla ya chanjo ya kawaida ya tetekuwanga, karibu watu

Soma Zaidi...
Dalili za Maambukizi kwenye mifupa

Posti hii inahusu zaidi dalili za Maambukizi kwenye mifupa, ni dalili ambazo ukionyesha kwa mtu mwenye Maambukizi kwenye mifupa.

Soma Zaidi...