Njia za kufanya ukiwa na tatizo la uti wa mgongo.
Posti hii inahusu zaidi Njia za kufanya Ili kupunguza maumivu ya tatizo la uti wa mgongo, ni njia unazopaswa kufanya pale unapokuwa na tatizo la uti wa Mgongo.
Njia za kufanya ukiwa na tatizo la uti wa mgongo.
1.Tumia vitu vya moto.
Kama Kuna tatizo la uti wa mgongo,lazima kutumia vitu vya moto zaidi kuliko vya baridi Ili kupunguza hali ya kusinyaa kwa misuli na kufanya misuli kutanuka na maumivu huwa kidogo sana.mfano kuweka maji ya moto kwenye taulo na kujikanda na taulo la moto kwenye sehemu ya maumivu.
2. Tumia barafu kama mtu amepata ajali Ili kupunguza moto ambao upo kwenye pingili, pengine kama ni kuvunjika pingili zinakuwa za moto sana na kusababisha maumivu Ili kupunguza maumivu makali kwenye uti wa mgongo, barafu inabidi itolewe Ili kupunguza joto ambalo upelekea maumivu na kitendo hiki kisizidi dakika Kumi.
3. Mazoezi mepesi yatumike.
Mtu mwenye matatizo ya uti wa mgongo mazoezi mepesi yatumike Ili kufanya mwili kutanuka na kuruhusu kuruhusu damu ipite na pengine sehemu iliyokuwa umepata shida inaweza kurudi kwa kutumia mazoezi na mazoezi yasiwe makali sana kwa sababu yanaweza kusababisha kuvunjika zaidi, kwa hiyo mazoezi ni ya lazima.
4.Acha kubeba vitu vizito.
Kwa mtu mwenye matatizo ya uti wa mgongo anapaswa kuepuka kubeba vitu vizito kwa sababu katika kubeba vitu vizito Kuna hatari unaweza kusababisha maumivu zaidi na kumpelekea ulemavu wa kudumu, kwa hiyo watu wenye matatizo ya uti wa mgongo wanapaswa kuacha kubeba vitu vizito.
5.Tumia godoro gumu wakati wa kulala.
Wakati wa kulala wenye matatizo ya uti wa mgongo wanapaswa kulalia magodoro magumu Ili kufanya pingili zikae kwenye sehemu yake kwa sababu katika kutumia godoro matatizo ya mgongo yanaweza kupungua na kuwa kwenye hali ya kawaida.
6.Tumia mshipi wa mgongo
Watu wenye matatizo ya uti wa Mgongo wanapaswa kutumia mshipi wa kufungia mgongo Ili kuufanya mgongo uweze kushikana vizuri na pingili zinaweza kurudi kwenye hali yake kawaida, kwa kufanya hivyo mtu anaweza kukaa kwa mda mrefu kusimama kwa mda mrefu akiwa amefunga mgongo wake.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
๐1 kitabu cha Simulizi ๐2 web hosting ๐3 Kitau cha Fiqh ๐4 Dua za Mitume na Manabii ๐5 Madrasa kiganjani ๐6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Dalili kuu za minyoo
Minyoo ni katika viume wanyonyaji, wanaoishi katika miili ya viumbe hai na kujipatia chakula humo. Minyoo wanaweza kuishi kwenye maeneo yenye majimaji kama kwenye maji, ndani ya viumembe hai kama mtu, ngombe, ngure na paka. Minyoo pia wanaweza kuishi kwen
Soma Zaidi...Dalili za vidonda vya tumbo, matibabu na dawa zake, sababu za kutokea kwake
Utajifunza chanzo cha vidonda vya tumbo, dalili zake, dawa na matibabu yake pamoja na njia za kujilinda na vidonda vya tumbo
Soma Zaidi...Dalili za ukimwi za kwenye ulimi na mdomo
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za ukimwi za kwenye ulimi na mdomo
Soma Zaidi...Maumivu makali ya tumbo la chango wakati wa hedhi na sababu zake
Kwa nini unapata maumivu makali wakati wa kuingia hedhi, je unajuwa sababu za maumivu makali ya tumbo la chago.
Soma Zaidi...Saratani ya tishu zinazounda Damu mwilini (leukemia)
Post hii inaelezea kuhusiana naรย Sarataniรย ya tishu zinazounda damu mwilini, ikijumuisha uboho na mfumo wa limfu.ugonjwa huu kitaalamu huitwa leukemia.
Soma Zaidi...