Njia za kufanya ukiwa na tatizo la uti wa mgongo.
Posti hii inahusu zaidi Njia za kufanya Ili kupunguza maumivu ya tatizo la uti wa mgongo, ni njia unazopaswa kufanya pale unapokuwa na tatizo la uti wa Mgongo.
Njia za kufanya ukiwa na tatizo la uti wa mgongo.
1.Tumia vitu vya moto.
Kama Kuna tatizo la uti wa mgongo,lazima kutumia vitu vya moto zaidi kuliko vya baridi Ili kupunguza hali ya kusinyaa kwa misuli na kufanya misuli kutanuka na maumivu huwa kidogo sana.mfano kuweka maji ya moto kwenye taulo na kujikanda na taulo la moto kwenye sehemu ya maumivu.
2. Tumia barafu kama mtu amepata ajali Ili kupunguza moto ambao upo kwenye pingili, pengine kama ni kuvunjika pingili zinakuwa za moto sana na kusababisha maumivu Ili kupunguza maumivu makali kwenye uti wa mgongo, barafu inabidi itolewe Ili kupunguza joto ambalo upelekea maumivu na kitendo hiki kisizidi dakika Kumi.
3. Mazoezi mepesi yatumike.
Mtu mwenye matatizo ya uti wa mgongo mazoezi mepesi yatumike Ili kufanya mwili kutanuka na kuruhusu kuruhusu damu ipite na pengine sehemu iliyokuwa umepata shida inaweza kurudi kwa kutumia mazoezi na mazoezi yasiwe makali sana kwa sababu yanaweza kusababisha kuvunjika zaidi, kwa hiyo mazoezi ni ya lazima.
4.Acha kubeba vitu vizito.
Kwa mtu mwenye matatizo ya uti wa mgongo anapaswa kuepuka kubeba vitu vizito kwa sababu katika kubeba vitu vizito Kuna hatari unaweza kusababisha maumivu zaidi na kumpelekea ulemavu wa kudumu, kwa hiyo watu wenye matatizo ya uti wa mgongo wanapaswa kuacha kubeba vitu vizito.
5.Tumia godoro gumu wakati wa kulala.
Wakati wa kulala wenye matatizo ya uti wa mgongo wanapaswa kulalia magodoro magumu Ili kufanya pingili zikae kwenye sehemu yake kwa sababu katika kutumia godoro matatizo ya mgongo yanaweza kupungua na kuwa kwenye hali ya kawaida.
6.Tumia mshipi wa mgongo
Watu wenye matatizo ya uti wa Mgongo wanapaswa kutumia mshipi wa kufungia mgongo Ili kuufanya mgongo uweze kushikana vizuri na pingili zinaweza kurudi kwenye hali yake kawaida, kwa kufanya hivyo mtu anaweza kukaa kwa mda mrefu kusimama kwa mda mrefu akiwa amefunga mgongo wake.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 kitabu cha Simulizi 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
Uvimbe wa mishipa midogo ya Damu kwenye ngozi
Posti hii inazungumzia kuhusiana na uvimbe wenye uchungu wa mishipa midogo ya damu kwenye ngozi yako ambayo hutokea kutokana na ongezeko la joto la ghafla kutokana na halijoto ya baridi. Pia inajulikana kama pernio, chilblain inaweza kusababisha kuwasha,
Soma Zaidi...Dalili ya pressure ya kupanda
Post ya leo inaenda kufundisha dalili na hatari za presha ya kupanda. Presha ni ugonjwa unaosababishwa na baadhi ya vitu mbalimbali.pressure hujulikana kwa jina lingine ambolo ni hypertension (pressure ya kupanda). presha hugundulika pale ambapo presha ya
Soma Zaidi...Dalili za fangasi uken
Posti hii inahusu zaidi dalili za fangasi uken, hizi ni baadhi ya dalili ambazo ujitokeza kwa mtu Mwenye tatizo la fangasi uken.
Soma Zaidi...Matumizi ya chumvi nyingi: Hatari kwa afya ya moyo.
Katika ulimwengu wa kisasa, mtindo wa maisha na vyakula vilivyosindikwa vimesababisha ongezeko kubwa la ulaji wa chumvi kupita kiasi. Makala hii inachunguza uhusiano wa moja kwa moja kati ya ulaji wa sodiamu na magonjwa ya moyo. Tutajadili jinsi chumvi inavyoathiri shinikizo la damu, utaratibu wa uharibifu wa mishipa ya damu, na hatua za kivitendo unazoweza kuchukua ili kupunguza matumizi yake kwa maisha bora na marefu.
Soma Zaidi...Ugonjwa wa Dondakoo na namna unavyoweza kuenea
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa Dondakoo na namna unavyoweza kuenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine.
Soma Zaidi...