picha

Njia za kufanya ukiwa na tatizo la uti wa mgongo.

Posti hii inahusu zaidi Njia za kufanya Ili kupunguza maumivu ya tatizo la uti wa mgongo, ni njia unazopaswa kufanya pale unapokuwa na tatizo la uti wa Mgongo.

Njia za kufanya ukiwa na tatizo la uti wa mgongo.

1.Tumia vitu vya moto.

Kama Kuna tatizo la uti wa mgongo,lazima kutumia vitu vya moto zaidi kuliko vya baridi Ili kupunguza hali ya kusinyaa kwa misuli na kufanya misuli kutanuka na maumivu huwa kidogo sana.mfano kuweka maji ya moto kwenye taulo na kujikanda na taulo la moto kwenye sehemu ya maumivu.

 

2. Tumia barafu kama mtu amepata ajali Ili kupunguza moto ambao upo kwenye pingili, pengine kama ni kuvunjika pingili zinakuwa za moto sana na kusababisha maumivu Ili kupunguza maumivu makali kwenye uti wa mgongo, barafu inabidi itolewe Ili kupunguza joto ambalo upelekea maumivu na kitendo hiki kisizidi dakika Kumi.

 

3. Mazoezi mepesi yatumike.

Mtu mwenye matatizo ya uti wa mgongo mazoezi mepesi yatumike Ili kufanya mwili kutanuka na kuruhusu kuruhusu damu ipite na pengine sehemu iliyokuwa umepata shida inaweza kurudi kwa kutumia mazoezi na mazoezi yasiwe makali sana kwa sababu yanaweza kusababisha kuvunjika zaidi, kwa hiyo mazoezi ni ya lazima.

 

4.Acha kubeba vitu vizito.

Kwa mtu mwenye matatizo ya uti wa mgongo anapaswa kuepuka kubeba vitu vizito kwa sababu katika kubeba vitu vizito Kuna hatari unaweza kusababisha maumivu zaidi na kumpelekea ulemavu wa kudumu, kwa hiyo watu wenye matatizo ya uti wa mgongo wanapaswa kuacha kubeba vitu vizito.

 

5.Tumia godoro gumu wakati wa kulala.

Wakati wa kulala wenye matatizo ya uti wa mgongo wanapaswa kulalia magodoro magumu Ili kufanya pingili zikae kwenye sehemu yake kwa sababu katika kutumia godoro matatizo ya mgongo yanaweza kupungua na kuwa kwenye hali ya kawaida.

 

6.Tumia mshipi wa mgongo

Watu wenye matatizo ya uti wa Mgongo wanapaswa kutumia mshipi wa kufungia mgongo Ili kuufanya mgongo uweze kushikana vizuri na pingili zinaweza kurudi kwenye hali yake kawaida, kwa kufanya hivyo mtu anaweza kukaa kwa mda mrefu kusimama kwa mda mrefu akiwa amefunga mgongo wake.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2021/12/06/Monday - 05:41:51 pm Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 3098

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii    👉2 web hosting    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Dalili kuu za minyoo

Minyoo ni katika viume wanyonyaji, wanaoishi katika miili ya viumbe hai na kujipatia chakula humo. Minyoo wanaweza kuishi kwenye maeneo yenye majimaji kama kwenye maji, ndani ya viumembe hai kama mtu, ngombe, ngure na paka. Minyoo pia wanaweza kuishi kwen

Soma Zaidi...
Athari za ugonjwa wa Dondakoo

Posti hii inahusu zaidi athari za ugonjwa wa Dondakoo,hali hii utokea iwapo ugonjwa haukutibiwa mapema au umetibiwa lakini bado Kuna matokea hasi ambayo yanaweza kujitokeza kama ifuayavyo.

Soma Zaidi...
Namna ya kutoa huduma kwa mgonjwa wa Dengue.

Posti hii inahusu zaidi huduma anayopaswa kupata mgonjwa wa ndengue, kwa sababu tunafahamu wazi Ugonjwa huu hauna dawa ila kuna huduma muhimu ambayo anaweza kupata na akaendelea vizuri.

Soma Zaidi...
Je maumivu juu ya kitovu ni miongoni mwa dalili za mimba?

Dalili za mimba zinaweza kuanzia kuonekana mapema ndani ya wiki ya kwanza, japo sio rahisi nabhakuna uthibitishobwa uhakika juu ya kauli hii. Makala hii itakwebda kujibubswali la msingi la muuulizaji kama maumivu ya tumbo ni dalili ya ujauzito.

Soma Zaidi...
Ujuwe ugonjwa wa ebola, dalili zake na jinsi unavyoweza kusambazwa.

Posti hii inahusu sana kuhusu ugonjwa wa ebora. Ugonjwa huu usababishwa na virusi.Virusi hivyo husababisha kutokwa na damu nyingi mwilini kutokana na kupasuka kwa mishipa ya damu

Soma Zaidi...
Upungufu wa damu unaosababishwa na minyoo.

Post hii inahusu zaidi upungufu wa damu unaosababishwa na minyoo dalili zake na namna ya kumsaidia mgonjwa mwenye tatizo hilo.

Soma Zaidi...
Ujuwe mlo sahihi kwa mgonjwa wa vidonda vya tumbo

Post hii itakwenda kuangalia mlo sahihi wa mwenye vidonda vya tumbo. Hata utajifunza ni vyakula vipi hapaswi kula na vipi ana paswa kula.

Soma Zaidi...
Tatizo la damu kutokufikia tishu baada ya kutokea jeraha kwenye tishu (gangrene)

Posti hii inazungumzia kuhusiana na tatizo la damu kutokufikia tishu baada ya kutokea jeraha kwenye tishu ambao hujulikana Kama gangrene inahusu kifo cha tishu za mwili kutokana na ukosefu wa mtiririko wa damu au maambukizi ya bakteria. Ugonjwa wa gangre

Soma Zaidi...