Matibabu ya vidonda vya tumbo

Makala hii inakwenda kukufundisha kuhusu matibabu ya vidonda vyatumbo. Pia utajifunza kwa nini kunakuwa na vidonda vya tumbo sugu.

MATIBABU NA DAWA Z VIDONDA VYA TUMBO:

 

Nini vidonda vya tumbo, na zipi aina zake

Vidonda vya tumbo kitaalamu hufahamika kama ulcers, ni vidonda vinavyotokea kwenye tumbo. Vidonda hivi vimepewa majina mbalimbalu kulingana na aina zake. Vipo ambavyo huitwa gastric ulcers ambavyo ni vile avinavyotokea kwenye tumbo la chakula. Aina nyingine huitwa esophangeal ulcers hivi ni vile vinavyotokea kwenye sehemu inayojulikana kama esophagus, ni sehemu inayounganisha koo la chakula na tumbo la chakula. Na aina ya mwisho hujulikana kama duodenal ulcers hivi hutokea kwenye sehemu ya juu ya utumbo mdogo inayofahamika kama duodenum.

 

 

Kwa siku za mwanzo ni ngumu kugunduwa kama una vidonda vya tumbo. Vipimo vinahitajika kugundua kama una vidonda vya tumbo. Kwa kuwa vidonda vya tumbo vina sababu nyingi na hutokea kidogo kidogo, basi hata matibabu yake yanaweza kuchelewa. Endelea na makala hii hadi mwisho, nitakujuza vipimo vipi hutumika kutibu vidonda vya tumbo na ni matibabu gani yanahitajika kulingana na aina ya vidonda na sababu za kutokea kwake.

 

Vipimo vya vidonda vya tumbo:

Vipimo vya vidonda vya tumbo vimegawanyika katika makundi mengi. Na hata gharama za vipimo vyake zinatofautiana kulingana na kipimo kilichotumika. Hivyo kaama una dalili za vidonda na umepima huna badili aina nyingine ya kipimo. Aina hizo ni kama:-

 

  1. Aina ya kwanza ya kipimo ni ila ambayo lwngo lake kubwa ni kuchunguza kama ndani ya tumbo kuna bakteria aina ya H.pylori. Hawa ndio bakteria ambao wanasababisha vidonda vya tumbo kwa kiasi kikubwa. Vipimo hivi mara nyingi ni kwa njia ya kinyesi. Hata hivyo vinaweza kufanyika kwa njia ya pumzi (hewa) ama damu lakini njia hizi sio sahihi kuliko kwa kutumia kinyesi

 

  1. Kwa kutumia kifaa cha kuingiza tumboni kinachojulikana kama endoscope. Hiki hungizwa ndani ya tumbo kisha humulika kama katochi. Kwa msaada wa kifaa hiki vidonda vya tumbbo vinaweza kuonekana kwa macho

 

  1. Kwa kutumia x-ray hii ni x-ray aalimu kwa lengo la kuchunguza safu za juu za tumbo. Kipimo hiki pia hufahamika kwa jina la barium swallow.

 

Matibabu na dawa za vidonda vya tumbo:

Kama ulivyojifunza huko juu kuwa matibabu ya vidonda vya tumbo hutolewa kwa kulingana na aina ya vidonda na kulingana na sababu zake. Kama sababu ni bakteria mgonjwa atapewa dawa za kuuwa bakteria. Kama  sababu ni ongezeko la tindikali tumboni mgonjwa atapewa dawa ya kupunguza uzalishaji wa tindikali tumboni. Dawa za vidonda vya tumbo ni kama:-

 

  1. dawa za kuuwa bakteria wanaosababisha vidonda vya tumbo. Dawa hizo ni kama
  2. Amoxicillin (amoxil)
  3. Cacithromycin (Biaxin)
  4. Metronidazole (flagyl)
  5. Tinidazole (tindamax)
  6. Tetracycline (tetracycline HCL
  7. Levofloxacin (levaquin)

 

  1. dawa za kuzuia uzalishwaji wa tindikali za tumboni. Dawa hizo ni kama:-
  2. Omeprazole,
  3. lansoprazole,
  4. Rabeprazole
  5. Esomeprazole
  6. Pantoprazole

 

  1. Dawa za kupunguza uzalishwaji wa tindikali tumboni. Hiki ni kama
  2. Ranitidine
  3. Famotidine
  4. Cimetidine
  5. Nizatidine

 

  1. Dawa za kulinda ukuta laini wa tumbo hizi hujulikana kama cytoprotective agent. Dawa hizi ni kama sucralfate na misoprostol

 

Dawa mbadala za vidonda vya tumbo.

Tofauti na dawa hizo lakini pia vidonda vya tumbo viaweza kutibiwa na tiba mbadala. Kuwa makini sana na tiba hizi kwa sababu hazina vipimo maalumu. Tiba hizi mara nyingi hufanya kazi vyema kama sababu ya vidonda ni bakteria. Lakini kama sababu ni nyingine tiba hizi sio sahihi sana. Tiba hizi hujumuisha

  1. Karoti, kabichi na bamia (hizi unaweza kutengeneza juisi yake).
  2. Asali
  3. Kitunguu thaumu
  4. Shubiri

 

Athari za kutotibu vidonda vya tumbo:

Ugonjwa wowote unaweza kuwa na madhara zaidi endapo utachelewa kutibiwa. Hali hii pia ni kwa vidonda vya tumbo. Endapo havitatibiwa badi athari mbaya zaidi inaweza kutokea. Ni kawaida kwa vidonda vya tumbo kusababisha kifo ila kama havitatibiwa mwisho wake unawez akuwa kifo. Hebu tuone athari za kutotibu vidonda vya tumbo:-

 

  1. Kuvuja kwa damu ndani ya tumbo. Damu hii unaweza kuiona kwenye kinyesi ama kinyesi kuwa cheui sana amakuwa na damu. Hali kama hii inaweza kusababisha upungufu wa damu mwilini.

 

  1. Chakula kinaweza kupita bila ya kumeng’enywa. Kutokana na kuwepo vidonda kkwenye utumbo mdogo, chakula kinaweza kupita hata bila ya kumeng;enywa na kuingia kwenye damu kwa ajili ya kutumika mwilini. Endapo hali kama hii itatokea mtu anaweza kushiba kwa haraka sana na anaweza kupoteza uzitoto kutokana na kukosa virutubisho.

 

  1. Pia vidonda vya tumbo visipotibiwa vinaweza kusababisha maambukizi ya magonjwa mengine tumboni.
  2. Vinaweza kupelekea utumbo kukatwa. Yesendapo eneo la jeraha limekuwa kubwa na gumu kutibika tiba mbadala ni kuondoa kipande cha utumbo kilichoharibika.

 

Mambo hatari kwa mwenye vidonda vya tumbo:

  1. Kunywa pombe
  2. Kuvuta sigara
  3. Kula vyakula vyenye uchachu sana
  4. Kuwa na misongo ya mawazo
  5. Kukaa na njaa kwa muda mrefu
  6. Kula vyakula vyenye pilipili kwa wingi
  7. Kula vyakula vyenye chumvi sansa

 

Tukutane makala ijayo tuakapoangalia kuhusu dalili za minyoo na sababu zake.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 1889

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Dalili za fangasi wa kucha.

Posti hii inazungumzia kuhusiana na dalili,sababu za Hatari,na namna ya kujizuia na fangasi wa kucha.

Soma Zaidi...
VIRUSI VYA KORONA AU CORONA (CORONAVIRUS)

Virusi vya korona ni katika aina za virusi ambavyo asili yake ni kutoka kwa wanyama na kuja kwa binadamu.

Soma Zaidi...
MALARIA INATOKEAJE? (Namna ambavyo malaria inatokea, inaanza na inavyoathiri afya)

Kama tulivyokwisha kuona kuwa malaria inaweza kuambukizwa kwa kung'atwa na mbu aina ya anophelesi.

Soma Zaidi...
Kushiriki ngono na mtu aliye na VVU na UKIMWI

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu namna ya kushiriki ngono na mtu aliye na VVU na UKIMWI

Soma Zaidi...
Madhara ya Tiba homoni kwa wagonjwa wa saratani

Posti hii inahusu zaidi madhara ya Tiba homoni, ni madhara- ambayo utokea kwa mgonjwa anayetumia homoni kama Tiba kwenye kutibu saratani.

Soma Zaidi...
KUJIANDAA KWA AJILI YA KUMUONA DAKTARI

KUJIANDAA KWA AJILI YA KUMUONA DAKTARI Fanya miadi na daktari wako wa kawaida ikiwa una ishara au dalili zinazokupa wasiwasi.

Soma Zaidi...
Tiba ya vidonda vya tumbo na dawa zake

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu Tina ya vidonda vya tumbo na dawa zake

Soma Zaidi...
Daliliza shinikizo la Chini la damu.

Shinikizo la chini la damu (hypotension) litaonekana kuwa jambo la kujitahidi. Hata hivyo, kwa watu wengi, shinikizo la chini la damu linaweza kusababisha dalili za Kizunguzungu na kuzirai. Katika hali mbaya, shinikizo la chini la damu linawez

Soma Zaidi...
AFYA NA MAGONJWA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
Dawa za kutibu kiungulia

Somo hili linakwenda kukueleza baadhi ya dawa za kutibu kiungulia

Soma Zaidi...