Matibabu ya vidonda vya tumbo


image


Makala hii inakwenda kukufundisha kuhusu matibabu ya vidonda vyatumbo. Pia utajifunza kwa nini kunakuwa na vidonda vya tumbo sugu.


MATIBABU NA DAWA Z VIDONDA VYA TUMBO:

 

Nini vidonda vya tumbo, na zipi aina zake

Vidonda vya tumbo kitaalamu hufahamika kama ulcers, ni vidonda vinavyotokea kwenye tumbo. Vidonda hivi vimepewa majina mbalimbalu kulingana na aina zake. Vipo ambavyo huitwa gastric ulcers ambavyo ni vile avinavyotokea kwenye tumbo la chakula. Aina nyingine huitwa esophangeal ulcers hivi ni vile vinavyotokea kwenye sehemu inayojulikana kama esophagus, ni sehemu inayounganisha koo la chakula na tumbo la chakula. Na aina ya mwisho hujulikana kama duodenal ulcers hivi hutokea kwenye sehemu ya juu ya utumbo mdogo inayofahamika kama duodenum.

 

 

Kwa siku za mwanzo ni ngumu kugunduwa kama una vidonda vya tumbo. Vipimo vinahitajika kugundua kama una vidonda vya tumbo. Kwa kuwa vidonda vya tumbo vina sababu nyingi na hutokea kidogo kidogo, basi hata matibabu yake yanaweza kuchelewa. Endelea na makala hii hadi mwisho, nitakujuza vipimo vipi hutumika kutibu vidonda vya tumbo na ni matibabu gani yanahitajika kulingana na aina ya vidonda na sababu za kutokea kwake.

 

Vipimo vya vidonda vya tumbo:

Vipimo vya vidonda vya tumbo vimegawanyika katika makundi mengi. Na hata gharama za vipimo vyake zinatofautiana kulingana na kipimo kilichotumika. Hivyo kaama una dalili za vidonda na umepima huna badili aina nyingine ya kipimo. Aina hizo ni kama:-

 

  1. Aina ya kwanza ya kipimo ni ila ambayo lwngo lake kubwa ni kuchunguza kama ndani ya tumbo kuna bakteria aina ya H.pylori. Hawa ndio bakteria ambao wanasababisha vidonda vya tumbo kwa kiasi kikubwa. Vipimo hivi mara nyingi ni kwa njia ya kinyesi. Hata hivyo vinaweza kufanyika kwa njia ya pumzi (hewa) ama damu lakini njia hizi sio sahihi kuliko kwa kutumia kinyesi

 

  1. Kwa kutumia kifaa cha kuingiza tumboni kinachojulikana kama endoscope. Hiki hungizwa ndani ya tumbo kisha humulika kama katochi. Kwa msaada wa kifaa hiki vidonda vya tumbbo vinaweza kuonekana kwa macho

 

  1. Kwa kutumia x-ray hii ni x-ray aalimu kwa lengo la kuchunguza safu za juu za tumbo. Kipimo hiki pia hufahamika kwa jina la barium swallow.

 

Matibabu na dawa za vidonda vya tumbo:

Kama ulivyojifunza huko juu kuwa matibabu ya vidonda vya tumbo hutolewa kwa kulingana na aina ya vidonda na kulingana na sababu zake. Kama sababu ni bakteria mgonjwa atapewa dawa za kuuwa bakteria. Kama  sababu ni ongezeko la tindikali tumboni mgonjwa atapewa dawa ya kupunguza uzalishaji wa tindikali tumboni. Dawa za vidonda vya tumbo ni kama:-

 

  1. dawa za kuuwa bakteria wanaosababisha vidonda vya tumbo. Dawa hizo ni kama
  2. Amoxicillin (amoxil)
  3. Cacithromycin (Biaxin)
  4. Metronidazole (flagyl)
  5. Tinidazole (tindamax)
  6. Tetracycline (tetracycline HCL
  7. Levofloxacin (levaquin)

 

  1. dawa za kuzuia uzalishwaji wa tindikali za tumboni. Dawa hizo ni kama:-
  2. Omeprazole,
  3. lansoprazole,
  4. Rabeprazole
  5. Esomeprazole
  6. Pantoprazole

 

  1. Dawa za kupunguza uzalishwaji wa tindikali tumboni. Hiki ni kama
  2. Ranitidine
  3. Famotidine
  4. Cimetidine
  5. Nizatidine

 

  1. Dawa za kulinda ukuta laini wa tumbo hizi hujulikana kama cytoprotective agent. Dawa hizi ni kama sucralfate na misoprostol

 

Dawa mbadala za vidonda vya tumbo.

Tofauti na dawa hizo lakini pia vidonda vya tumbo viaweza kutibiwa na tiba mbadala. Kuwa makini sana na tiba hizi kwa sababu hazina vipimo maalumu. Tiba hizi mara nyingi hufanya kazi vyema kama sababu ya vidonda ni bakteria. Lakini kama sababu ni nyingine tiba hizi sio sahihi sana. Tiba hizi hujumuisha

  1. Karoti, kabichi na bamia (hizi unaweza kutengeneza juisi yake).
  2. Asali
  3. Kitunguu thaumu
  4. Shubiri

 

Athari za kutotibu vidonda vya tumbo:

Ugonjwa wowote unaweza kuwa na madhara zaidi endapo utachelewa kutibiwa. Hali hii pia ni kwa vidonda vya tumbo. Endapo havitatibiwa badi athari mbaya zaidi inaweza kutokea. Ni kawaida kwa vidonda vya tumbo kusababisha kifo ila kama havitatibiwa mwisho wake unawez akuwa kifo. Hebu tuone athari za kutotibu vidonda vya tumbo:-

 

  1. Kuvuja kwa damu ndani ya tumbo. Damu hii unaweza kuiona kwenye kinyesi ama kinyesi kuwa cheui sana amakuwa na damu. Hali kama hii inaweza kusababisha upungufu wa damu mwilini.

 

  1. Chakula kinaweza kupita bila ya kumeng’enywa. Kutokana na kuwepo vidonda kkwenye utumbo mdogo, chakula kinaweza kupita hata bila ya kumeng;enywa na kuingia kwenye damu kwa ajili ya kutumika mwilini. Endapo hali kama hii itatokea mtu anaweza kushiba kwa haraka sana na anaweza kupoteza uzitoto kutokana na kukosa virutubisho.

 

  1. Pia vidonda vya tumbo visipotibiwa vinaweza kusababisha maambukizi ya magonjwa mengine tumboni.
  2. Vinaweza kupelekea utumbo kukatwa. Yesendapo eneo la jeraha limekuwa kubwa na gumu kutibika tiba mbadala ni kuondoa kipande cha utumbo kilichoharibika.

 

Mambo hatari kwa mwenye vidonda vya tumbo:

  1. Kunywa pombe
  2. Kuvuta sigara
  3. Kula vyakula vyenye uchachu sana
  4. Kuwa na misongo ya mawazo
  5. Kukaa na njaa kwa muda mrefu
  6. Kula vyakula vyenye pilipili kwa wingi
  7. Kula vyakula vyenye chumvi sansa

 

Tukutane makala ijayo tuakapoangalia kuhusu dalili za minyoo na sababu zake.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    2 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    3 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    4 Download App zetu hapa ujifunze zaidi    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Njia za kuondokana na fangasi
Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuweza kupambana na fangasi za ukeni ili kuweza kujiepusha na madhara mbalimbali kwenye maisha ambayo ni pamoja na ugumba na Maambukizi kwenye via vya uzazi. Soma Zaidi...

image Fahamu kuhusu Ugonjwa wa Bawasili
Posti hii inahusu zaidi juu ya ugonjwa wa Bawasili, ni ugonjwa unaotokea kwenye njia ya haja kubwa hali ambayo upelekea kuwepo kwa uvimbe au nyama ambazo uonekana hadi nje, kwa lugha ya kitaalamu ujulikana kama haemorrhoid au pokea. Soma Zaidi...

image Huduma kwa watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi
Posti hii inahusu zaidi huduma ambazo wagonjwa wanaoishi na maambukizi ya virus vya ukimwi wanaweza kupata, huduma hii utolewa hasa kwa wale ambao wamejitokeza kupima afya zao na kujua wazi hali zao na kwa wale wanaofatilia huduma hii wanaweza kuishi vizuri na kuwa na afya nzuri. Soma Zaidi...

image Maumivu ya tumbo chini ya kifua, upande wa kulia na chini ya kitomvu.
Afya ya tumbo ni ishara tosha ya umadhibuti wa afya ya mtu. Maradhi mengi wanayouguwa watu chanzo kile mti anachokula. Yapo maradhi sugu kama saratani ambayo husababishwa pia na vyakula. Post hii itakwenda kujibu swalo la muulizaji kuhusu maumivu ya tumbo. Soma Zaidi...

image Kichaa cha mbwa.
Post hii inahusu zaidi kichaa cha mbwa,au kwa kitaalamu huitwa rabies, utokea pale mtu anapongatwa na mnyama ambaye ni jamii ya mtu au mbwa mwenyewe Soma Zaidi...

image Matibabu kwa mtu mwenye kiungulia
Posti hii inahusu zaidi matibabu kwa mtu mwenye kiungulia,ni tiba ambayo mtu anapaswa kutumia kama ana tatizo la kiungulia Soma Zaidi...

image Dalili za kasoro ya moyo ya kuzaliwa kwa watu wazima
Ugonjwa wa moyo wa kuzaliwa nao (kasoro ya moyo ya kuzaliwa) ni hali isiyo ya kawaida katika muundo wa moyo wako unaozaliwa nao. utu uzima. Ingawa maendeleo ya kimatibabu yameboreshwa, watu wazima wengi walio na ugonjwa wa moyo wa kuzaliwa wanaweza wasipate uangalizi ufaao wa ufuatiliaji.Iwapo ulikuwa na kasoro ya kuzaliwa iliyorekebishwa ukiwa mtoto mchanga, kuna uwezekano bado unahitaji utunzaji ukiwa mtu mzima.Inapaswa kushauriana na dactari ikiwa kuna uwezekano wa kuwa na matatizo, au ikiwa uko katika hatari kubwa ya matatizo mengine ya moyo kama mtu mzima. Soma Zaidi...

image Sababu za kuwepo kwa saratani ya inni.
Posti hii inahusu zaidi sababu mbalimbali za kuwepo kwa saratani ya ini, saratani hii imekuwa tishio kwa wengi ila ni vizuri kujua baadhi ya sababu ambazo uchangia sana kuwepo kwa tatizo hili la saratani ya inni. Soma Zaidi...

image Walio katika hatari ya kupata homa ya inni
Posti hii inahusu zaidi watu walio katika hatari ya kupata homa ya ini,kwa sababu ya hali zao mbalimbali wanaweza kupata ugonjwa huu. Soma Zaidi...

image Fahamu kuhusu Ugonjwa wa ukoma
Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa ukoma, ni Ugonjwa unaosababishwa na mdudu anayeitwa mycobacterium leprae, mdudu huyu kwa kawaida uathiri sana sehemu za ngozi na sehemu za Neva mbalimbali za mwili Soma Zaidi...