Matibabu ya vidonda vya tumbo

Makala hii inakwenda kukufundisha kuhusu matibabu ya vidonda vyatumbo. Pia utajifunza kwa nini kunakuwa na vidonda vya tumbo sugu.

MATIBABU NA DAWA Z VIDONDA VYA TUMBO:

 

Nini vidonda vya tumbo, na zipi aina zake

Vidonda vya tumbo kitaalamu hufahamika kama ulcers, ni vidonda vinavyotokea kwenye tumbo. Vidonda hivi vimepewa majina mbalimbalu kulingana na aina zake. Vipo ambavyo huitwa gastric ulcers ambavyo ni vile avinavyotokea kwenye tumbo la chakula. Aina nyingine huitwa esophangeal ulcers hivi ni vile vinavyotokea kwenye sehemu inayojulikana kama esophagus, ni sehemu inayounganisha koo la chakula na tumbo la chakula. Na aina ya mwisho hujulikana kama duodenal ulcers hivi hutokea kwenye sehemu ya juu ya utumbo mdogo inayofahamika kama duodenum.

 

 

Kwa siku za mwanzo ni ngumu kugunduwa kama una vidonda vya tumbo. Vipimo vinahitajika kugundua kama una vidonda vya tumbo. Kwa kuwa vidonda vya tumbo vina sababu nyingi na hutokea kidogo kidogo, basi hata matibabu yake yanaweza kuchelewa. Endelea na makala hii hadi mwisho, nitakujuza vipimo vipi hutumika kutibu vidonda vya tumbo na ni matibabu gani yanahitajika kulingana na aina ya vidonda na sababu za kutokea kwake.

 

Vipimo vya vidonda vya tumbo:

Vipimo vya vidonda vya tumbo vimegawanyika katika makundi mengi. Na hata gharama za vipimo vyake zinatofautiana kulingana na kipimo kilichotumika. Hivyo kaama una dalili za vidonda na umepima huna badili aina nyingine ya kipimo. Aina hizo ni kama:-

 

  1. Aina ya kwanza ya kipimo ni ila ambayo lwngo lake kubwa ni kuchunguza kama ndani ya tumbo kuna bakteria aina ya H.pylori. Hawa ndio bakteria ambao wanasababisha vidonda vya tumbo kwa kiasi kikubwa. Vipimo hivi mara nyingi ni kwa njia ya kinyesi. Hata hivyo vinaweza kufanyika kwa njia ya pumzi (hewa) ama damu lakini njia hizi sio sahihi kuliko kwa kutumia kinyesi

 

  1. Kwa kutumia kifaa cha kuingiza tumboni kinachojulikana kama endoscope. Hiki hungizwa ndani ya tumbo kisha humulika kama katochi. Kwa msaada wa kifaa hiki vidonda vya tumbbo vinaweza kuonekana kwa macho

 

  1. Kwa kutumia x-ray hii ni x-ray aalimu kwa lengo la kuchunguza safu za juu za tumbo. Kipimo hiki pia hufahamika kwa jina la barium swallow.

 

Matibabu na dawa za vidonda vya tumbo:

Kama ulivyojifunza huko juu kuwa matibabu ya vidonda vya tumbo hutolewa kwa kulingana na aina ya vidonda na kulingana na sababu zake. Kama sababu ni bakteria mgonjwa atapewa dawa za kuuwa bakteria. Kama  sababu ni ongezeko la tindikali tumboni mgonjwa atapewa dawa ya kupunguza uzalishaji wa tindikali tumboni. Dawa za vidonda vya tumbo ni kama:-

 

  1. dawa za kuuwa bakteria wanaosababisha vidonda vya tumbo. Dawa hizo ni kama
  2. Amoxicillin (amoxil)
  3. Cacithromycin (Biaxin)
  4. Metronidazole (flagyl)
  5. Tinidazole (tindamax)
  6. Tetracycline (tetracycline HCL
  7. Levofloxacin (levaquin)

 

  1. dawa za kuzuia uzalishwaji wa tindikali za tumboni. Dawa hizo ni kama:-
  2. Omeprazole,
  3. lansoprazole,
  4. Rabeprazole
  5. Esomeprazole
  6. Pantoprazole

 

  1. Dawa za kupunguza uzalishwaji wa tindikali tumboni. Hiki ni kama
  2. Ranitidine
  3. Famotidine
  4. Cimetidine
  5. Nizatidine

 

  1. Dawa za kulinda ukuta laini wa tumbo hizi hujulikana kama cytoprotective agent. Dawa hizi ni kama sucralfate na misoprostol

 

Dawa mbadala za vidonda vya tumbo.

Tofauti na dawa hizo lakini pia vidonda vya tumbo viaweza kutibiwa na tiba mbadala. Kuwa makini sana na tiba hizi kwa sababu hazina vipimo maalumu. Tiba hizi mara nyingi hufanya kazi vyema kama sababu ya vidonda ni bakteria. Lakini kama sababu ni nyingine tiba hizi sio sahihi sana. Tiba hizi hujumuisha

  1. Karoti, kabichi na bamia (hizi unaweza kutengeneza juisi yake).
  2. Asali
  3. Kitunguu thaumu
  4. Shubiri

 

Athari za kutotibu vidonda vya tumbo:

Ugonjwa wowote unaweza kuwa na madhara zaidi endapo utachelewa kutibiwa. Hali hii pia ni kwa vidonda vya tumbo. Endapo havitatibiwa badi athari mbaya zaidi inaweza kutokea. Ni kawaida kwa vidonda vya tumbo kusababisha kifo ila kama havitatibiwa mwisho wake unawez akuwa kifo. Hebu tuone athari za kutotibu vidonda vya tumbo:-

 

  1. Kuvuja kwa damu ndani ya tumbo. Damu hii unaweza kuiona kwenye kinyesi ama kinyesi kuwa cheui sana amakuwa na damu. Hali kama hii inaweza kusababisha upungufu wa damu mwilini.

 

  1. Chakula kinaweza kupita bila ya kumeng’enywa. Kutokana na kuwepo vidonda kkwenye utumbo mdogo, chakula kinaweza kupita hata bila ya kumeng;enywa na kuingia kwenye damu kwa ajili ya kutumika mwilini. Endapo hali kama hii itatokea mtu anaweza kushiba kwa haraka sana na anaweza kupoteza uzitoto kutokana na kukosa virutubisho.

 

  1. Pia vidonda vya tumbo visipotibiwa vinaweza kusababisha maambukizi ya magonjwa mengine tumboni.
  2. Vinaweza kupelekea utumbo kukatwa. Yesendapo eneo la jeraha limekuwa kubwa na gumu kutibika tiba mbadala ni kuondoa kipande cha utumbo kilichoharibika.

 

Mambo hatari kwa mwenye vidonda vya tumbo:

  1. Kunywa pombe
  2. Kuvuta sigara
  3. Kula vyakula vyenye uchachu sana
  4. Kuwa na misongo ya mawazo
  5. Kukaa na njaa kwa muda mrefu
  6. Kula vyakula vyenye pilipili kwa wingi
  7. Kula vyakula vyenye chumvi sansa

 

Tukutane makala ijayo tuakapoangalia kuhusu dalili za minyoo na sababu zake.

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 1744

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Kivimba kwa mishipa ya Damu

Posti hii inaelezea kuhusiana na Ugonjwa wa kuvimba kwa mishipa yako ya damu. Inasababisha mabadiliko katika kuta za mishipa ya damu, ikiwa ni pamoja na kuimarisha, kudhoofisha, kupungua na kupungua. Mabadiliko haya huzuia mtiririko wa damu, na kusababi

Soma Zaidi...
Matatizo yanayosababisha mshtuko wa moyo.

Mshtuko wa moyo hutokea wakati mtiririko wa damu kwa moyo umezuiwa, mara nyingi kwa mkusanyiko wa mafuta, cholesterol na vitu vingine, ambayo huunda plaque katika mishipa inayolisha moyo (mishipa ya moyo). Mtiririko wa damu ulioingiliwa unaweza kuharibu

Soma Zaidi...
Aina za fangasi

Somo hili linakwenda kukuletea baadhi ya aina za fangasi

Soma Zaidi...
Fahamu Ugonjwa wa Maambukizi kwenye mfupa

posti hii inazungumzia kuhusiana na Ugonjwa wa Maambukizi kwenye mfupa ambao kitaalamu hujulikana Kama

Soma Zaidi...
Dalili za anemia ya upungufu wa vitamin.

Anemia ya upungufu wa vitamini ni ukosefu wa seli nyekundu za damu zenye afya unaosababishwa na kiasi kidogo cha vitamini fulani kuliko kawaida.

Soma Zaidi...
Msaada kwa aliye na uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo.

Posti hii inahusu zaidi msaada kwa aliye na uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo, ni huduma maalumu ambayo utolewa kwa mtu ambaye ana uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo. Zifuatazo ni huduma maalumu kwa mwenye uvimbe kwenye kibofu Cha mkojo.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa homa ya uti wa mgongo

Posti hii inahusu zaidi Ugonjwa wa uti wa mgongo, ni ugonjwa unaoshambulia sehemu inayofunika ubongo na pia sehemu ya spinal cord

Soma Zaidi...
Ni zipi dalili za awali za pumu

Kabla ya kubanwa zaidi na pumu, kuna dalili za awali zinzznza kujitokeza, na hapo ndipo utakapoanza kuchukuwa tahadhari. Makala hii itakwenda kukujulisha zaidi kuhusu dalili hizo.

Soma Zaidi...
Ulemavu wa ubongo na mfumo wa fahamu -multiple sclerosis

Posti hii inazungumzia kuhusiana na dadili na sababu zinazopelekea Ugonjwa wa ulemavu wa ubongo na mfumo wa fahamu ambao kitaalamu hujulikana Kama multiple sclerosis.

Soma Zaidi...
Dalili za UTI

Somo hili linakwenda kukuletea dalili za UTI

Soma Zaidi...