picha

Matibabu ya vidonda vya tumbo

Makala hii inakwenda kukufundisha kuhusu matibabu ya vidonda vyatumbo. Pia utajifunza kwa nini kunakuwa na vidonda vya tumbo sugu.

MATIBABU NA DAWA Z VIDONDA VYA TUMBO:

 

Nini vidonda vya tumbo, na zipi aina zake

Vidonda vya tumbo kitaalamu hufahamika kama ulcers, ni vidonda vinavyotokea kwenye tumbo. Vidonda hivi vimepewa majina mbalimbalu kulingana na aina zake. Vipo ambavyo huitwa gastric ulcers ambavyo ni vile avinavyotokea kwenye tumbo la chakula. Aina nyingine huitwa esophangeal ulcers hivi ni vile vinavyotokea kwenye sehemu inayojulikana kama esophagus, ni sehemu inayounganisha koo la chakula na tumbo la chakula. Na aina ya mwisho hujulikana kama duodenal ulcers hivi hutokea kwenye sehemu ya juu ya utumbo mdogo inayofahamika kama duodenum.

 

 

Kwa siku za mwanzo ni ngumu kugunduwa kama una vidonda vya tumbo. Vipimo vinahitajika kugundua kama una vidonda vya tumbo. Kwa kuwa vidonda vya tumbo vina sababu nyingi na hutokea kidogo kidogo, basi hata matibabu yake yanaweza kuchelewa. Endelea na makala hii hadi mwisho, nitakujuza vipimo vipi hutumika kutibu vidonda vya tumbo na ni matibabu gani yanahitajika kulingana na aina ya vidonda na sababu za kutokea kwake.

 

Vipimo vya vidonda vya tumbo:

Vipimo vya vidonda vya tumbo vimegawanyika katika makundi mengi. Na hata gharama za vipimo vyake zinatofautiana kulingana na kipimo kilichotumika. Hivyo kaama una dalili za vidonda na umepima huna badili aina nyingine ya kipimo. Aina hizo ni kama:-

 

  1. Aina ya kwanza ya kipimo ni ila ambayo lwngo lake kubwa ni kuchunguza kama ndani ya tumbo kuna bakteria aina ya H.pylori. Hawa ndio bakteria ambao wanasababisha vidonda vya tumbo kwa kiasi kikubwa. Vipimo hivi mara nyingi ni kwa njia ya kinyesi. Hata hivyo vinaweza kufanyika kwa njia ya pumzi (hewa) ama damu lakini njia hizi sio sahihi kuliko kwa kutumia kinyesi

 

  1. Kwa kutumia kifaa cha kuingiza tumboni kinachojulikana kama endoscope. Hiki hungizwa ndani ya tumbo kisha humulika kama katochi. Kwa msaada wa kifaa hiki vidonda vya tumbbo vinaweza kuonekana kwa macho

 

  1. Kwa kutumia x-ray hii ni x-ray aalimu kwa lengo la kuchunguza safu za juu za tumbo. Kipimo hiki pia hufahamika kwa jina la barium swallow.

 

Matibabu na dawa za vidonda vya tumbo:

Kama ulivyojifunza huko juu kuwa matibabu ya vidonda vya tumbo hutolewa kwa kulingana na aina ya vidonda na kulingana na sababu zake. Kama sababu ni bakteria mgonjwa atapewa dawa za kuuwa bakteria. Kama  sababu ni ongezeko la tindikali tumboni mgonjwa atapewa dawa ya kupunguza uzalishaji wa tindikali tumboni. Dawa za vidonda vya tumbo ni kama:-

 

  1. dawa za kuuwa bakteria wanaosababisha vidonda vya tumbo. Dawa hizo ni kama
  2. Amoxicillin (amoxil)
  3. Cacithromycin (Biaxin)
  4. Metronidazole (flagyl)
  5. Tinidazole (tindamax)
  6. Tetracycline (tetracycline HCL
  7. Levofloxacin (levaquin)

 

  1. dawa za kuzuia uzalishwaji wa tindikali za tumboni. Dawa hizo ni kama:-
  2. Omeprazole,
  3. lansoprazole,
  4. Rabeprazole
  5. Esomeprazole
  6. Pantoprazole

 

  1. Dawa za kupunguza uzalishwaji wa tindikali tumboni. Hiki ni kama
  2. Ranitidine
  3. Famotidine
  4. Cimetidine
  5. Nizatidine

 

  1. Dawa za kulinda ukuta laini wa tumbo hizi hujulikana kama cytoprotective agent. Dawa hizi ni kama sucralfate na misoprostol

 

Dawa mbadala za vidonda vya tumbo.

Tofauti na dawa hizo lakini pia vidonda vya tumbo viaweza kutibiwa na tiba mbadala. Kuwa makini sana na tiba hizi kwa sababu hazina vipimo maalumu. Tiba hizi mara nyingi hufanya kazi vyema kama sababu ya vidonda ni bakteria. Lakini kama sababu ni nyingine tiba hizi sio sahihi sana. Tiba hizi hujumuisha

  1. Karoti, kabichi na bamia (hizi unaweza kutengeneza juisi yake).
  2. Asali
  3. Kitunguu thaumu
  4. Shubiri

 

Athari za kutotibu vidonda vya tumbo:

Ugonjwa wowote unaweza kuwa na madhara zaidi endapo utachelewa kutibiwa. Hali hii pia ni kwa vidonda vya tumbo. Endapo havitatibiwa badi athari mbaya zaidi inaweza kutokea. Ni kawaida kwa vidonda vya tumbo kusababisha kifo ila kama havitatibiwa mwisho wake unawez akuwa kifo. Hebu tuone athari za kutotibu vidonda vya tumbo:-

 

  1. Kuvuja kwa damu ndani ya tumbo. Damu hii unaweza kuiona kwenye kinyesi ama kinyesi kuwa cheui sana amakuwa na damu. Hali kama hii inaweza kusababisha upungufu wa damu mwilini.

 

  1. Chakula kinaweza kupita bila ya kumeng’enywa. Kutokana na kuwepo vidonda kkwenye utumbo mdogo, chakula kinaweza kupita hata bila ya kumeng;enywa na kuingia kwenye damu kwa ajili ya kutumika mwilini. Endapo hali kama hii itatokea mtu anaweza kushiba kwa haraka sana na anaweza kupoteza uzitoto kutokana na kukosa virutubisho.

 

  1. Pia vidonda vya tumbo visipotibiwa vinaweza kusababisha maambukizi ya magonjwa mengine tumboni.
  2. Vinaweza kupelekea utumbo kukatwa. Yesendapo eneo la jeraha limekuwa kubwa na gumu kutibika tiba mbadala ni kuondoa kipande cha utumbo kilichoharibika.

 

Mambo hatari kwa mwenye vidonda vya tumbo:

  1. Kunywa pombe
  2. Kuvuta sigara
  3. Kula vyakula vyenye uchachu sana
  4. Kuwa na misongo ya mawazo
  5. Kukaa na njaa kwa muda mrefu
  6. Kula vyakula vyenye pilipili kwa wingi
  7. Kula vyakula vyenye chumvi sansa

 

Tukutane makala ijayo tuakapoangalia kuhusu dalili za minyoo na sababu zake.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2776

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 web hosting     πŸ‘‰2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     πŸ‘‰3 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰4 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰5 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     πŸ‘‰6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

Samahan naomb kujua staili za tendo la ndoa

Post hii inakwenda kujibu swali la muulizaji. Kuhusu syyle za tendo la ndoa

Soma Zaidi...
Fahamu ugonjwa wa kaswende wakati wa ujauzito.

Post hii inahusu zaidi ugonjwa wa kaswende wakati wa ujauzito, kaswende inaweza kukaa kwa mtu zaidi ya miaka mingi bila kuleta madhara ya moja kwa moja lakini kadiri ya siku zinavyokwenda madhara utokea hasa wakati wa ujauzito, madhara hayo umwadhiri mtot

Soma Zaidi...
Mimba Changa Hukaa Wiki Ngapi? Fahamu Kipindi Hiki Muhimu

​Neno "mimba changa" hutumiwa sana katika mazungumzo ya kila siku, lakini kitaalamu linawakilisha miezi mitatu ya kwanza ya ujauzito, inayojulikana kama Trimester ya Kwanza. Makala haya yanajadili umri kamili wa mimba changa kwa wiki, mabadiliko makuu yanayotokea kwa mama na kiumbe, ishara za hatari za kuchunguza, na ukweli wa kisayansi dhidi ya dhana potofu kuhusu kipindi hiki.

Soma Zaidi...
Samaani nilikuwa nauriza ninasumburiwa na fanga ya mdomoni naomba ushauri

Fangasi mdomoni wanaweza kuwa tatizo endapo hawatatibiwa mapema. Wanaweza kuongeza majeraha kwenye kinywa.

Soma Zaidi...
Aina za kisukari

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu aina za kisukari

Soma Zaidi...
ugonjwa wa Malaria dalili zake na chanzo chake.

Malaria ni moja ya magonjwa hatari yanayoongoza katika vifo vya watoto wengi duniani walio chni ya umri wa miaka 5. Katika post hii utakwend akujifunza kuhusuugonjwa huu jinsi unavyotokea, hatuwa zake na dalili zake.

Soma Zaidi...