Dalili za Ukimwi

Makala hii itaeleza dalili za ukimwi, dalili za VVU, magonjwa nyemelezi na matumizi ya ARV

Dalili za Ukimwi

ELIMU YA KUHUSU HIV NA UKIMWI


Ni nini maana ya Ukimwi?
UKIMWI ni ufupisho wa maneno “upungufu wa kinga mwilini” ni hali sugu, inayoweza kutishia maisha inayosababishwa na virusi vya Ukimwi (VVU). Kwa kuharibu mfumo wako wa kinga, VVU huingilia uwezo wa mwili wako kupambana na viumbe vinavyosababisha magonjwa. Viumbe hivyo ni kama bakteria, virusi, protozoa, fangasi na vinginevyo.




Nini maana ya Virusi Vya Ukimwi (VVU)?
VVU ni ufupisho wa maneno Virusi Vya Ukimwi, ni virusi vinavyosababisha upungufu wa kinga mwilini. Hudhoofisha mwili uwezo wake kujilinda dhidi ya vijidudu vya maradhi. Neon hili kwa lugha ya kiingereza hufupishwa kama HIV.




VVU ni maambukizo ya zinaa. Yanayoweza pia kuenezwa kwa kuongezewa damu iliyoambukizwa au kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto wakati wa ujauzito, wakati wa kujifungua au kunyonyesha. Inaweza kuchukua miaka mimngi huwenda 5 mpaka 10 kabla ya VVU kudhoofisha kinga yako ya mwili hadi kufikia ukimwi.



Je ipo tiba ya VVU na UKIMWI?
Hakuna tiba ya VVU / UKIMWI, lakini kuna dawa ambazo zinaweza kupunguza kasi ya ukuaji wa magonjwa na uharibifu wa kinga ya mwili. Dawa hizi zimepunguza vifo vya UKIMWI katika mataifa mengi yaliyoendelea. Lakini VVU inaendelea kupunguza idadi ya watu barani Afrika, Haiti na sehemu za Asia. Dawa hizi mimkusanyiko wa dawa nyingi kwa pamoja hufahamika kama ARV yaani Ant-Retrovirus na matibabu yake hufahamika kama ART yaani Ant-Retroval Therapy. Dawa hizi piazimegawanyika katika makundi mengi kama NRTIs, NNRTs, Protease inhibitors na nyinginezo kibao.




DALILI ZA VVU NA UKIMWI NI ZIPI?
Dalili za VVU na UKIMWI hutofautiana, kulingana na awamu ya maambukizo, muda kutoka maambukizo yalipotokea pia afya ya mtu kabla ya maambukizo.
Hatua ya kwanza ya maambukizi (Primary infection)

Watu wengi walioambukizwa na VVU hupata ugonjwa unaofanana na Homa ndani ya mwezi mmoja au miwili baada ya virusi kuingia mwilini. Hivyo kutengeneza dalili za awali za VVU na UKIMWI. Dalili hizi si lazima zimpate kila mtu, wapp wengine hawazipati kabisa. Sana dalili hizi hutokea wiki mbili toka kupata maambukizi mpaka wiki nne kisha hupotea. Kwa baadhi ya watu zinaweza kuanzia wiki ya kwanza, na wengine kuishia wiki ya sita. Dalili hizo ni:-




1.Kupatwa na homa.
2.Maumivu ya kichwa yasiyo na sababu
3.Maumivu ya misuli
4.Kuota upele
5.Kupatwa na baridi ama kuhisi baridi.
6.Kukauka na koo ama kupatwa na vidonda kooni.
7.Kupatwa na Vidonda vya kinywa au sehemu za siri
8.Kuvimba kwa Tezi za limfu kwenye mapaja, makwapa na haswa kwenye shingo
9.Mwili kuwa na Maumivu bila ya sababu maalumu.
10.Kutokwa na Jasho la usiku
11.Kuharisha



Ingawa katika kipindi hiki kiwango cha virusi sio rahisi kuviona kwa vipimo vya kawaida vinavyotumika kupima, lakini ni kuwa katika kipindi hiki kiwango cha virusi ni kingi sana kwenye damu, na muathirika anaweza kumuambukiza mwengine kwa urahisi sana. Baada ya wiki sita dalili hizi hupotea na hazitajirudia tena. Hapa virusi vitatulia ndani ya mwili kwa miaka mingi bila ya kuonyesha dalili yeyote ile, huku vukiendelea kuharibu kinga ya mwili kidogokidogo.




Hatuwa ya pili Toka kuambukizwa.
Kama tulivyoona dalili za VVU katika hatuwa ya kwanza. Sasa hutokea kwa baadhi ya watu kuwa tezi za limfu zisivimbe wakati wa hatuwa ya kwanza, ila zikavimba katika hatuwa hii ya pili. Tofauti na hili hakuna dalili nyingine maalumu ya VVU katika hatuwa hii ya pili. Hatuwa hii inaweza kuchukuwa mpaka miaka 10. Kwa watu wengi ni kati ya miaka 4 mpaka 10 ila wengine mara chache hutokea ikawa chini ya hapo.




Baada ya maambukizi ya Awali
Hiki ni kipindi cha miaka kadhaa baada ya kuambukizwa. Katika wakati huu hakuna dalili ya VVU inayoonekana. Hata hivyo kadri iaka inavyosonga mbele ndivyo seli zinavyozidi kudhoofu. Wakati virusi vinaendelea kuongezeka na kuharibu seli za kinga, unaweza kupata maambukizo kidogo au ishara sugu na dalili kama vile:




1.Homa
2.Uchovu
3.Node za mtoki, kwapa, na shingo kuvimba – na hii ndio mara nyingi moja ya ishara za kwanza za maambukizo ya VVU
4.Kuhara
5.Kupungua uzito
6.Kikohozi
7.Kupumua kwa pumzi




Kuendelea kwa UKIMWI
Ikiwa hautapata matibabu maalumu ya ART na kutumia ARV mapema iwezekanavyo kwa ajili ya kuthibiti maambukizo yako ya VVU, ugonjwa huendelea hadi kufikia kuwa UKIMWI kwa takriban miaka 10. Wakati huu ukiwa na UKIMWI unakua, mfumo wako wa kinga umeharibiwa sana, na hivyo kukufanya uweze kuambukizwa na magonjwa nyemelezi – Mgonjwa nyemelezi ni magonjwa ambayo hayangemsumbua mtu aliye na kinga nzuri.



DALILI ZA UKIMWI.
Mpaka kufikia hapa ndipo mgonjwa huambiwa ana UKIMWI. Kumbuka mpaka kufikia hapa tayari miaka Zaidi ya mine hadi 10 itakuwa imepita. Baadhi ya tafiti zinaonyesha kuwa endapo mgonjwa hatatumia matibabu maalubu ya ARV hatoweza kuzidi miaka 3. Sasa hebu tuzione dalili na Ishara za UKIMWI katika hatua hii:-




1.Kutokwa na jasho jingi wakati wa usiku
2.Kutetemeka kwa homa au Homa juu inayofikia nyuzi 100 F (38 C) na kudumu kwa wiki kadhaa
3.Kikohozi
4.Kupumua kwa pumzi za taabu
5.Kuhara kusiko kata
6.Utando mweupe wa kudumu au vidonda visivyo vya kawaida kwenye ulimi wako au kinywani mwako
7.Maumivu ya kichwa mara kwa mara
8.Uchovu wa kudumu, usioelezewa
9.kuona maluweluwe
10.Kupungua uzito bila ya sababu maalumu
11.Vipele kwenye ngozi au majipu




NJIA AMBAZO VVU HUAMBUKIZWA;
Kuna nadharia nyingi zinaelezea ni namna gani ambazo VVU huambukizwa. Katika hizo kuna mbazo ni Imani potofu kabisa na hazifai kukubaliwa. Hapa nitakuletea njia ambazo zinaambukiza VVU. Njia hizo ni:-
1.Kwa kufanya mapenzi (ngono). Unaweza kuambukizwa ikiwa unafanya ngono ya uke, ya mkundu au ya mdomo na mwenzi aliyeambukizwa VVU ambaye damu yake au shahawa zake au majimaji ya ukeni huingia mwilini mwako kwa kupitia michubuko midogo, ama vidonda ama mikato ama sehemu iliyowazi inayoruhusi kufikiwa damu kwa urahisi. Na hii ndiyo njiainayoongoza katika kuambukiza VVU



2. Kwa kuongezewa damu kutoka kwa aliye athirka. Katika namn nyingine, virusi vinaweza kuambukizwa kupitia kuongezewa damu. Kwa sasa si sana njia hii maana damu anayopatiwa mgonjwa itapitia uchunguzi wa kina kabla ya kuongezewa ijapokuwa madhaifu ya kibinadamu yanaweza kufanyika.



3. Kwa kushirikiana matumizi ya sindano na vitu vyenye ncha kali kama visu na viwembe. VVU vinaweza kuambukizwa kupitia sindano, inaweza kutokea wakatiwa matibabu yatakayofayika chini ya utaratibu. Inaweza pia kuwa watumiaji a madawa ya kulevya hushirikiana sana matumizi ya sindano. Endapo mtumiaji wa kwana ana VVU na akajidunga ama kujikata, kisha akachukuwa mtumiaji mwinine na kujidunga ama kujikata muda mfupi toka mtumiaji wenye VVU kutumia.



4. Wakati wa ujauzito au kujifungua au kupitia kunyonyesha. Mama walioambukizwa VVU wanaweza kuambukiza watoto wao endapo hwatakuwa makini. Mama mjamzito mwenye VVU anatakiwa atumie dozi haraka iwezekanavyo ili kuepushamaambukizi kwa mtoto. Hata hivypo inampasa azalie hospitali ili uangalifu zaidi ufanyike wakati a kujifunguwa.



HAYA HAYAWEZI KUAMBUKIZA VVU
1.Mate
2.Mkojo
3.Kugusana mikono ama kukumbatia
4.Kula pamoja
5.Kucheza pamoja.
6.Kung’atwa na mbu



SASA UKIMWI UNATOKEAJE?
Seli ndio matofali yaliyojengea miili yetu. Ndani ya miili yetu kuna aina nyingi za seli, na seli za damu. Ndani ya damu pekee kuna aina zisizopunguwa tatu za seli. Kuna seli hai nyekundu, nyeupe na seli sahani. Kila seli kati ya hizi ina kazi zake. Sasa hii seli hai nyeupe yenyewe ndio inakazi ya kupigana na vijidudu vya maradhi vinapoingia katika miili yetu. Vijidudu hivyo vinaweza kuwa bakteria, virusi ama fangasi. Seli hizi ndizo ambazo ambazo huitwa CD4.



Sasa virusi vya VVU vinapoingia mwilini vinaanza kuharibi hizi seli ambazo zinalinda mwili. Kawaida mtu anaweza kuwa na seli hizi 500 mapa 1500 katika kipimo kimoja. Sasa VVU vinaanza kuziharibu hizi na kupunguza idadi yake. Na kila seli hizi zikipunguwa ndipo mfumo wa kinga unavyoendelea kuharibika na ndivyo maradhi yanapozidi kupata nafasi ya kuingia mwilini.



Sasa endapo zimeharibiwa na kufika idadi ya 200 katika kipimo kimoja hapa mtu huyu ataambiwa ana Upungufu wa Kinga Mwilini yaani UKIMWI. Katika hatuwa hii mtu atakuwa akinyemelewa na maradhi nyemelezi kama fangasi, kifuwa kikuu, na mengineyo.



Endapo mgonjwa atatumia ARV mapema anaweza kukaa miaka mimngi sana bila ya kufikia hatuwa hii. Kuna umuhimu wa kutumia ARV mapema, sababu hizo ni kama:-
1.Kupungua maambukizi ya VVU
2.Kulinda afya ya mtu
3.Kupunguza uharibifu wa seli
4.Kulinda mwili dhidi ya maradhi nyemelezi.







                   



Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 1315

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Homa ya Dengue, dalili za homa ya dengue na Njia ya kujikinga nayo

HOMA YA DENGUEHoma ya dengue ni miongoni mwa maradhi hatari ambayo husambazwa na mbu.

Soma Zaidi...
Dalili za ugonjwa sugu wa Figo.

Ugonjwa sugu wa figo, pia huitwa kushindwa kwa figo sugu, huelezea upotevu wa taratibu wa utendakazi wa figo. Figo zako huchuja taka na Majimaji kupita kiasi kutoka kwa damu yako, ambayo hutolewa kwenye mkojo wako. Ugonjwa sugu wa figo unapofikia hatua

Soma Zaidi...
Fahamu Ugonjwa wa Saratani ya uke

Saratani ya uke ni Saratani adimu inayotokea kwenye uke wako mrija wa misuli unaounganisha uterasi na sehemu zako za siri. Saratani ya uke mara nyingi hutokea katika seli zilizo kwenye uso wa uke wako, ambao wakati mwingine huitwa njia ya uzazi. Wan

Soma Zaidi...
Virusi vinavyopelekea Kuharisha Sana na Kutapika Sana(norovirus)

Maambukizi ya Norovirus yanaweza kusababisha kutapika sana na Kuhara. Virusi huambukiza sana na kwa kawaida huenea kupitia chakula au maji ambayo yamechafuliwa na kinyesi wakati wa kutayarisha. Unaweza pia kuambukizwa kwa kuwasiliana kwa karibu na mtu

Soma Zaidi...
Njia za kuondokana na fangasi

Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kuweza kupambana na fangasi za ukeni ili kuweza kujiepusha na madhara mbalimbali kwenye maisha ambayo ni pamoja na ugumba na Maambukizi kwenye via vya uzazi.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa Dondakoo na namna unavyoweza kuenea

Posti hii inahusu zaidi ugonjwa wa Dondakoo na namna unavyoweza kuenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine.

Soma Zaidi...
Mzio (aleji) na Dalili zake

Posti hii inahusu zaidi mzio na Dalili zake ni Dalili ambazo ujitokeza kwa mtu mwenye mzio, kuna wakati watu wengine ushindwa kutambua kuwa ni mzio au la, lakini leo tunaenda kujua Dalili za mzio kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa kisukari

Ugonjwa wa kisukari hurejelea kundi la magonjwa yanayoathiri jinsi mwili wako unavyotumia sukari kwenye damu (glucose). Glucose ni muhimu kwa afya yako kwa sababu ni chanzo muhimu cha nishati kwa seli zinazounda misuli na tishu zako. Pia ndio chanzo ki

Soma Zaidi...
Jinsi ya kujikinga na mafua (common cold)

Posti hii inazungumzia dalili na namna ya kujikinga tusipate mafua .mafua kwa jina lingine hujulikana Kama baridi ya kawaida (common cold).baridi ya kawaida husababishwa na virusi kwenye pua na hutoa makamasi.

Soma Zaidi...
Dalili na ishara za shambulio la moyo

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Dalili na ishara za shambulio la moyo. Shambulio la moyo huzuia damu yenye oksijeni kufika kwenye moyo hivyo hupelekea tishu kufa. Na Ugonjwa huu mtu akicheleweshewa matibabu huweza kupata mshtuko wa moyo mpaka kifo.

Soma Zaidi...