Dalili za upungufu wa homoni ya progesterone
Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo zinaweza kutokea iwapo Kuna upungufu wa homoni ya progesterone.
Dalili za upungufu wa homoni ya progesterone.
1. Pre menstrual syndrome ( ni hali ambayo uwakumba wanawake) kwa kawaida uanza wiki Moja Hadi mbili kabla ya kuona siku zake za mwezi , mwanamke anaweza kuona uchovu miwasho ya ukeni uwepo wa vipele vyekundu na vyeusi na pengine vipele hivyo vinaweza kutokea kwenye sehemu zake za Siri pamoja na usoni na pia mwanamke anaweza kuwa na mabadiliko ya mood kama ifuatavyo.
2. Kutokwa na mimba .
Kama Mama ana mimba inaweza kutoka kwa sababu ya kutokuwepo kwa homoni ya projestron kwa sababu usaidia katika makuzi makubwa ya mtoto.
3. Kuongezeka uzito kwa ghafla.
Kuna wakati mwingine unaweza kuona mwanamke anaongezeka Uzito ghafla ukadhani labda maisha yamemkubali kumbe ni upungufu wa homoni aina ya progesterone.
4 . Kuwepo kwa wasi wasi ambao haukuwepo hapo mwanzoni hali hii utokea ghafla kwa wanawake kila kitu anachokifanya anakifanya kwa wasi wasi mkubwa sana.
5. Kukosa usingizi.
Hali hii utokea sana kwa wamama ambao Wana upungufu wa homoni hii hasa wale akina Mama walioingia kwenye menopause wanaopatwa na hali ya kukoka usingizi.
6. Maumivu au uvimbe kwenye maziwa
Kwa kawaida maumivu kwenye maziwa utokea na kwa mara nyingine uvimbe, kwa upande wa uvimbe matibabu yanaoaswa kutolewa Ili kuepuka matatizo mengine yaliyo makubwa zaidi.
7. Kuwepo kwa kizungu zungu mara kwa mara.
Kama homoni hii ya progesterone imepungua utasikia akina Mama walio wengi Wanalalamika kuhusu kizungu zungu.
8. Kuwepo kwa ugumba.
Kwa kawaida homoni ya progesterone inasaidia sana kwenye makuzi ya mtoto kwa hiyo ikikosa usababisha Mama kukosa mtoto inawezekana mimba ikawa imeshatungwa ikatoka au mimba haitungwi kabisa.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 Simulizi za Hadithi Audio 👉4 ai web app 👉5 Dua za Mitume na Manabii 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
Ay ni iv kipimo cha mimb uanz kutoa majb ndan ya mda gan wik mwez au iko vipi?
Kipimo cha Mlimba huweza kuonyesha mimba changa mapema sana. Pia ni rahisi kutumia na kinapatikana kwa bei nafuu. Je ungeoendavkujuwa ni muda gani kinatoa majibu sahihi?
Soma Zaidi...Malengo ya huduma za uzazi kwa akina Mama.
Posti huu inahusu zaidi malengo ya huduma za uzazi kwa akina Mama, ni huduma muhimu ambazo zimetolewa kwa akina Mama ili kuweza kuepuka hatari mbalimbali zinazowakumba akina Mama wakati wa ujauzito, kujifu na malezi ya watoto chini ya miaka mitano.
Soma Zaidi...Sababu za kutoona hedhi kwa wakati
Posti hii inahusu zaidi sababu za kukosa hedhi wakati mda wa kuona hedhi umefika ni tatizo linalowasumbua baadhi ya wasichana wachache katika jamii na hii ni kwa sababu zifuatazo.
Soma Zaidi...Je inaweza ukaingia period wakati unaujauzito?
Ukiwa mjamzito unaweza kushuhudia kutokwa na damu. Je damu hii ni ya hedhi?
Soma Zaidi...Hatua za ukuwaji was mimba na dalili zake
Somo hili linakwenda kukuletea hatua za ukuaji mimba na dalili zake
Soma Zaidi...Sababu za Mayai kushindwa kuzalishwa kwa mwanamke
Posti hii inahusu zaidi sababu za kushindwa kuzalishwa mayai kwa mwanamke, ni tatizo ambalo utokea kwa mwanamke ambapo mwanamke anashindwa kuzalisha mayai.
Soma Zaidi...