Dalili za upungufu wa homoni ya progesterone
Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo zinaweza kutokea iwapo Kuna upungufu wa homoni ya progesterone.
Dalili za upungufu wa homoni ya progesterone.
1. Pre menstrual syndrome ( ni hali ambayo uwakumba wanawake) kwa kawaida uanza wiki Moja Hadi mbili kabla ya kuona siku zake za mwezi , mwanamke anaweza kuona uchovu miwasho ya ukeni uwepo wa vipele vyekundu na vyeusi na pengine vipele hivyo vinaweza kutokea kwenye sehemu zake za Siri pamoja na usoni na pia mwanamke anaweza kuwa na mabadiliko ya mood kama ifuatavyo.
2. Kutokwa na mimba .
Kama Mama ana mimba inaweza kutoka kwa sababu ya kutokuwepo kwa homoni ya projestron kwa sababu usaidia katika makuzi makubwa ya mtoto.
3. Kuongezeka uzito kwa ghafla.
Kuna wakati mwingine unaweza kuona mwanamke anaongezeka Uzito ghafla ukadhani labda maisha yamemkubali kumbe ni upungufu wa homoni aina ya progesterone.
4 . Kuwepo kwa wasi wasi ambao haukuwepo hapo mwanzoni hali hii utokea ghafla kwa wanawake kila kitu anachokifanya anakifanya kwa wasi wasi mkubwa sana.
5. Kukosa usingizi.
Hali hii utokea sana kwa wamama ambao Wana upungufu wa homoni hii hasa wale akina Mama walioingia kwenye menopause wanaopatwa na hali ya kukoka usingizi.
6. Maumivu au uvimbe kwenye maziwa
Kwa kawaida maumivu kwenye maziwa utokea na kwa mara nyingine uvimbe, kwa upande wa uvimbe matibabu yanaoaswa kutolewa Ili kuepuka matatizo mengine yaliyo makubwa zaidi.
7. Kuwepo kwa kizungu zungu mara kwa mara.
Kama homoni hii ya progesterone imepungua utasikia akina Mama walio wengi Wanalalamika kuhusu kizungu zungu.
8. Kuwepo kwa ugumba.
Kwa kawaida homoni ya progesterone inasaidia sana kwenye makuzi ya mtoto kwa hiyo ikikosa usababisha Mama kukosa mtoto inawezekana mimba ikawa imeshatungwa ikatoka au mimba haitungwi kabisa.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 Dua za Mitume na Manabii 👉4 ai web app 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 web hosting
Post zinazofanana:
Tabia za Ute wa siku za hatari kupata mimba au ovulation
Posti hii inahusu zaidi tabia mbalimbali za Ute wa ovulation kwa sababu Ute huu huwa tofauti na Ute mwingine kwa sababu ya kuwepo kwa tabia zake za kipekee kama tutakavyoona.
Soma Zaidi...Sababu za maumivu wakati wa tendo la ndoa
Kama unapata maumivu wakati wa tendo la ndoa, suluhisho lako lipo kwenye makala hii
Soma Zaidi...Fahamu sifa za Ute wa siku za kupata mimba yaani ovulation day
Posti hii inahusu zaidi sifa za Ute wa ovulation, ni Ute ambao utokea siku za ovulation yaani siku ambazo ni tayari kwa kubeba mimba, yaani siku za upevishaji wa yai.
Soma Zaidi...Dalili za mwanzo za ujauzito katika wiki ya kwanza
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za mwanzo za ujauzito katika wiki ya kwanza
Soma Zaidi...Changamoto za kwenye ndoa kwa waliotoa mimba mara Kwa mara
Posti hii inahusu zaidi changamoto za kwenye ndoa kwa wale waliotoa mimba mara Kwa mara,hizi ni changamoto za wakati wa kufanya tendo na mme wake au mtu mwingine kwa ajili ya kupata mtoto.
Soma Zaidi...Utaratibu wa kushiriki tendo la ndoa kwa wajawazito
Jifunze muda ambao mjamzito hatatkiwa kishiriki tendo la ndoa. je kuna madhara kwa mjamzito kushiriki tendo la ndoa.
Soma Zaidi...