image

Kuandama kwa Mwezi na Kufunga ama kufungua ramadhani, sheria na hukumu za kuangalia mwezi

Kuandama kwa Mwezi na Kufunga ama kufungua ramadhani, sheria na hukumu za kuangalia mwezi

Kuonekana kwa mwezi wa Ramadhani



Swaumu ya Ramadhani inaanza kwa kuona mwezi baada ya siku ya 29 Shaaban au 30 Shaaban kama tunavyofahamshwa katika hadithi zifu atazo:
“Ibn Umar (r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: Msifunge mpaka muuone mwezi umeandama na msiache kufunga mpaka muone mwezi (wa Shawwal) umeandama. Kama kuna mawingu (hukuuona) hesabu kamili (siku 30). Katika simulizi nyingine amesema: Mwezi una masiku 29, kwa hiyo usifunge mpaka uone mwezi umeandama kama kuna mawingu subiri na kamilisha idadi ya siku 30.”
(Bukhari na Muslim)



Kutokana na Hadithi hii ni wazi kuwa watu hawaruhusiwi kufunga kwa kufuata kalenda. Inabidi juhudi za kuuangalia mwezi ziwepo kwa umma wa Waislamu tangu mwanandamo wa Shaaban.



“Abu Hurairah (r.a) ameeleza kuw a Mtume w a Allah ameagiza: Hesabu mwandamo wa Shaaban kwa ajili ya Ramadhani”. (Tirmidh).



Kwanini kufuata mwandamo wa mwezi?



Tunafunga kwa kuona mwezi kwa sababu ndivyo alivyotuamrisha Mtume wa Allah (s.w) kama tulivyojifunza kutokana na hadithi zilizonukuliwa hapo juu. Kumtii Mtume (s.a.w) ndio Uislamu. Rejea Qur-an katika aya zifuatazo:


“Sema: “Mtiini Mwenyezi Mungu na Mtume wake. Na mkikengeuka (Allah atakuadhibuni) kwani Allah hawapendi makafiri.” (3:32)


“… Na anachokuleteeni Mtume, kipokeeni, na anachowakataza
kiacheni…” (59:7).


“Anayemtii Mtume, kwa yakini amemtii Mw enyezi Mungu…” (4:80)


Pia amri hii ina hekima yake. Mwaka unaohesabiwa kwa mwandamo wa mwezi una siku 354 kwani kwa wastani mwezi mmoja una siku 29?. Mwaka unaohesabiwa kwa kufuata jua, muda ambao dunia huchukua kulizunguka jua una siku 365, saa 5, dakika 48 na nukta 46. Kwa hiyo ukilinganisha mwaka wa hesabu ya mwezi na mwaka wa hesabu ya jua, utaona kuwa mwaka wa mwezi ni mfupi kwa siku10 hivi. Hivyo mwezi wa Ramadhani hurudi nyuma siku kumi katika kila mwaka ukilinganisha na mwaka wa jua. Hivyo basi, mtu yeyote atakayejaaliwa kufunga muda wa miaka 36 hatakuwa na siku au msimu katika mwaka ambao hakuufunga. Yaani atawahi kufunga siku zote za jua, za mvua, za upepo, za shwari, za kusi, za kaskazi na kadhalika. Kama ingelikuwa inafuatwa kalenda ya mwaka wa jua, wengine daima wangalifunga nyakati za joto tu, wengine nyakati za baridi tu, wengine nyakati za njaa tu, wengine nyakati za mavuno na kadhalika ilimuradi pasingalikuwa na mabadiliko.


Ni lazima kila mfungaji aone mwezi?



Mwezi wa Ramadhani akiona mtu mmoja muadilifu inatosha na wengine waliobaki itawabidi wafunge. Hivi ndivyo alivyoamrisha Mtume (s.a.w) kama tunavyojifunza katika hadithi zifuatazo:



“Ibn Abbas (r.a) ameeleza kuwa Mwarabu wa Jangwani alikuja kwa Mtume (s.a.w) akasema: Hakika nimeuona mwezi wa Ramadhani umeandama. Mtume (s.a.w) akamuuliza: Unashuhudia kuw a hapana Mola ila Allah? “Ndio” alijibu. Akamuuliza tena: Unashuhudia kuwa Muhammad ni Mtume w a Allah? Akajibu “Ndio ”. Akasema (Mtume): Ee Bilal! Watangazie w atu kuw a haw ana budi kufunga kesho”. (Abu Daud, Tirm idh, Nisa i, Ibn Majah).



“Ibn Omar (r.a) ameeleza: Watu waliuona mwezi. Kisha nikamfahamisha Mtume (s.a.w): Hakika nimeuona. Kwa hiyo alifunga na aliwaamrisha watu wafunge”. (Abu Daud, Darimi).






                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 780


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 kitabu cha Simulizi    

Post zifazofanana:-

Kufunga Mwezi wa ramadhani kisheria
Soma Zaidi...

Hija ya Kuaga na Kutawafu kwa Mtume (s.a.w)
Hija ya Kuaga na Kutawafu kwa Mtume (s. Soma Zaidi...

Yanayofaa kwa maamuma katika kumfata imamu kwenye swala ya jamaa
Soma Zaidi...

sadaka
Soma Zaidi...

Jinsi ya kutwaharisha aina mbalimbali za najisi
Kila najisi ina namna yake ya kutwaharisha, hata hivyo namna hizo hufanana. Katika post hii utakwenda kujifunza jinsi ya kutwaharisha najisi mbalimbali. Soma Zaidi...

ZIJUE HUKUMU NA FADHILA ZA KUTOA ZAKA KATIKA UISLAMU
Zaka ni nini? Soma Zaidi...

Kwa nini waislamu wanaoa mke zaidi ya mmoja
Post hiibitakugundisha hekima ya kuruhusiwa kuoa mke zaidi ya mmoja katika sheria za kiislamu. Soma Zaidi...

Namna ya kutayamamu hatuwa kwa hatuwa
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi yavkutayamamu. Soma Zaidi...

MAANA YA ZAKA NA SADAKA KULUNGA NA KISHERIA PAMOJA NA TOFAUTI ZAO
MAANA YA ZAKA NA SADAKA KULUNGA NA KISHERIA PAMOJA NA TOFAUTI ZAO. Soma Zaidi...

Haki za viumbe na mazingira
Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Je manii ni twahara au najisi?
Post hii itakwenda kukufundisha hukumu ya manii kuwa ni twahara ama ni najis Soma Zaidi...

Jinsi ya kukaa itiqaf na taratibu zake
Hapa utajifunza kuhusu taratibu za ibada ya itiqaf yaani kukaa msikitini kwa ajili ya ibada. Soma Zaidi...