Kwa nini imefaradhishwa kufunga katika Mwezi wa ramadhani?

Kwa nini imefaradhishwa kufunga katika Mwezi wa ramadhani?

Kwa nini Funga imefaradhishwa Mwezi wa Ramadhani



Japo tumefahamishwa katika Qur-an kuwa, faradhi ya funga ni kwa umma zote hatufahamu umma zilizotangulia zilifaradhishiwa kufunga miezi gani au wakati gani wa mwaka. Umma huu umefaradhishiwa kufunga katika mwezi wa Ramadhani kwa sababu ndio mwezi ilipoanza kushuka Qur-an kama tunavyofahamishwa katika aya ifu atayo:


β€œ(Mw ezi huo mliofaradhishw a kufunga) ni mw ezi w a Ramadhani ambao ndani yake imeshuka hii Qur-an ili iwe uongozi kwa watu na hoja zilizowazi


za uongozi na upambanuzi. Atakayeshuhudia mwezi huu miongoni mwenu na afunge ....” (2:185).
Hivyo, Waislamu wameamrishwa kufunga katika mwezi wa Ramadhani ili pamoja na kutekeleza amri hii wafikie lengo lililoku su diwa, vile vle iwe ni kumbukumbu ya kushuka Qur-an, Mwongozo wa Allah (s.w) wa mwisho kwa wanaadamu. Ni kwa msingi huu kusoma Qur-an kwa wingi katika mwezi huu kumesisitizwa zaidi. Qur-an ilianza kumshukia Mtume (.s.a.w) alipokuwa Jabal-Hira, usiku wa manane katika usiku mmoja wa Mwezi wa Ramadhani. Usiku huo mtakatifu ni β€œLailatul’qadri” (Usiku Wenye Cheo) kama tunavyojifunza katika Suratul-Qadr.


Hakika Tumeiteremsha (Qur’an) katika usiku w a Laylatul Qadri. Na jambo gani litakalokujulisha ni nini huo usiku wa Laylatul Qadri? Huo usiku wa heshima ni bora kuliko miezi elfu. Huteremka Malaika na roho katika (usiku) huo kwa idhini ya Mola wao kwa kila jambo. Ni amani (usiku) huo mpaka mapambazuko ya alfajiri(97:1-5)




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 3006

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Kitabu cha Afya    πŸ‘‰2 Bongolite - Game zone - Play free game    πŸ‘‰3 Dua za Mitume na Manabii    πŸ‘‰4 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰5 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina   

Post zinazofanana:

Ufumbuzi wa tatizo la riba.

Uislamu ndio dini pekee ambayo inatoa ufumbuzi juu ya suala la riba.

Soma Zaidi...
Sera ya uchumi katika uislamu

Hapa utajifunza sera za kiuchumi katika uchumi wa kiislamu. Hapa utajifunza sera kuu tatu za uchumi wa kiislamu.

Soma Zaidi...
Je ni nani mwenye haki ya kutaliki

Hapabutajifunza endapp mwanamke anahitaji kuachwa ni nini anatakiwa afanye.

Soma Zaidi...
Taasisi za Kifedha Katika Mfumo wa Uchumi wa Kiislamu

- Ni taasisi za kifedha zinazohusika na kuhifadhi akiba na mali za watu zenye thamani kubwa kama dhahabu, n.

Soma Zaidi...
Dua ya kuzuru makaburi, na utaratibu wa kuzuru makaburi

Kuzuru makaburi ni katika matendo ya sunah yaani unapata thawabu kwa kwenda klizuru kaburi.

Soma Zaidi...
Swala ya ijumaa, nguzo zake, sharti zake na jinsi ya kuiswali

Post hii inakwenda kukugundisha kuhusu swala ya ijumaa taratibu zake na jinsi ya kuiiswali.

Soma Zaidi...