kuwa mwenye hikma au hekima na faida zake
Elimu, pamoja na ubora wake, hainufaishi bila ya kutumiwa kwa hekima.
2. Kuwa na Hekima
Elimu, pamoja na ubora wake, hainufaishi bila ya kutumiwa kwa hekima. Kufanya jambo kwa hekima ni kufanya jambo kwa kutumia ujuzi unaostahiki na kwa kufuata utaratibu unaostahiki kulingana na mahali na wakati kwa kuzingatia mwongozo na mipaka ya Allah (s.w) na Sunnah ya Mtume wake.
Kila Muumini anawajibika kufanya mambo yake yote kwa ujuzi wa kutosha. Kabla Muislamu hajafanya jambo lolote anatakiwa afahamu len
go la hilo analolifanya na je, hilo lengo linampelekea kumuabudu Mola wake na kuwa Khalifa wake au la. Baada ya kulifahamu lengo hanabudi kuwa na ujuzi na mbinu zinazostahiki kumfikisha kwenye lengo kwa wepesi na kwa ufanisi. Asichague njia ndefu na ngumu akaacha njia fupi na nyepesi inayowafikiana na mwongozo wa Allah (s.w) na Sunnah za Mitume wake.
Hekima ni katika vipengele vya tabia njema vilivyo azizi anavyotakiwa avipiganie Muumini ili awe na hadhi inayostahiki, hadhi ya Ukhalifa wa Allah (s.w) hapa ulimwenguni. Waumini hatuna budi kufanya mambo yetu kwa hekima na daima tumuombe Allah atuzidishie Hekima.
“(Allah) Humpa hikma amtakaye, na aliyepewa hikma bila shaka amepewa heri nyingi. Na hawakumbuki ila wenye akili.” (2:269).
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 Dua za Mitume na Manabii 👉3 Kitabu cha Afya 👉4 ai web app 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
Post zinazofanana:
Maana ya sunnah (suna) na maana ya hadithi
Post hii itakufundisha maana ya neno sunnah katika Uislamu. Pia utajifunza maana ya neno hadithi katika uislamu
Soma Zaidi...Ni zipi hadithi sahihi na hadithi Quds
Hapa tutajifunza maana ya hadithi sahihi na hadithi Quds na tofaiti zao.
Soma Zaidi...Uandishi wa hadithi wakati wa maswahaba
Nini kilichangia ongezeko la uandishi wa hadithi wakati wa maswahaba.
Soma Zaidi...hadithi ya 8
عَنْ ابْنِ عُمَرَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا، أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم قَالَ: "أُمِرْتُ أَنْ أُقَاتِلَ النَّاسَ حَتَّى ?...
Soma Zaidi...