kuwa mwenye hikma au hekima na faida zake

Elimu, pamoja na ubora wake, hainufaishi bila ya kutumiwa kwa hekima.

kuwa mwenye hikma au hekima na faida zake

2. Kuwa na Hekima

Elimu, pamoja na ubora wake, hainufaishi bila ya kutumiwa kwa hekima. Kufanya jambo kwa hekima ni kufanya jambo kwa kutumia ujuzi unaostahiki na kwa kufuata utaratibu unaostahiki kulingana na mahali na wakati kwa kuzingatia mwongozo na mipaka ya Allah (s.w) na Sunnah ya Mtume wake.



Kila Muumini anawajibika kufanya mambo yake yote kwa ujuzi wa kutosha. Kabla Muislamu hajafanya jambo lolote anatakiwa afahamu len

go la hilo analolifanya na je, hilo lengo linampelekea kumuabudu Mola wake na kuwa Khalifa wake au la. Baada ya kulifahamu lengo hanabudi kuwa na ujuzi na mbinu zinazostahiki kumfikisha kwenye lengo kwa wepesi na kwa ufanisi. Asichague njia ndefu na ngumu akaacha njia fupi na nyepesi inayowafikiana na mwongozo wa Allah (s.w) na Sunnah za Mitume wake.



Hekima ni katika vipengele vya tabia njema vilivyo azizi anavyotakiwa avipiganie Muumini ili awe na hadhi inayostahiki, hadhi ya Ukhalifa wa Allah (s.w) hapa ulimwenguni. Waumini hatuna budi kufanya mambo yetu kwa hekima na daima tumuombe Allah atuzidishie Hekima.



“(Allah) Humpa hikma amtakaye, na aliyepewa hikma bila shaka amepewa heri nyingi. Na hawakumbuki ila wenye akili.” (2:269).



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sunnah Main: Dini File: Download PDF Views 1085

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 web hosting    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Simulizi za Hadithi Audio    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Uandishi wa hadithi wakati wa Matabii tabiina (tabiitabiina)

Hii ni historia ya uandishi wa hadithi wakati wa tabii tabiina. Yaani wafuasi wa wale wafuasi wa Masahaba

Soma Zaidi...
Dua za kumuomba Allah wakati wa shida na tabu ama matatizo

Post hii inakwenda kukufundisha dua ambazo ni muhimu kuzisoma wakayi wa shida na taabu.

Soma Zaidi...
Uandishi wa hadithi wakati wa maswahaba

Nini kilichangia ongezeko la uandishi wa hadithi wakati wa maswahaba.

Soma Zaidi...
Dua ambazo hutumiwa katika swala

Post hii inakwenda kukugundisha dua ambazo itazitumia katika swala yako.

Soma Zaidi...
Dua za kuomba wakati unapokuwa na hasira ama ukiwa umekasirika

Post hii itakueleza ni dua gani unatakiwa uzisome wakati unapokiwa na hasira ama pale unapokasirika.

Soma Zaidi...
NAMNA AMBAZO DUA HUJIBIWA

NAMNA AMBAYO ALLAH HUJIBU DUA.

Soma Zaidi...
Al-Arba uwn An-Nawawiyyah hadithi ya 7: Nasaha katika dini

Post hii itakufundisha umuhimu wa nasaha katika dini

Soma Zaidi...