Maswali mbalimbali yanayohusu elimu ya dini ya kiislamu na mwongozo wa elimu na elimu mazingira.
Zoezi la 1.
1.(a) Elimu ni nini?
(b) Mtu aliyeelimika ni mtu wa aina gani?
(c) Unatoa maoni gani iwapo wanaojua watakuwa sawa na wasiojua kiutendaji?
2.(a) “….Sema, Je! Wanaweza kuwa sawa wale wanaojua na wale wasiojua?.....(39:9). Kwa nini wanaojua hawawi sawa na wasiojua?
(b) Kwa kutumia ushahidi wa aya, onesha kuwa elimu ndio takrima ya kwanza aliyokirimiwa mwanaadamu na Mola wake.
3.Kwa ushahidi wa aya za Qur’an, eleza kwa nini Uislamu umeipa elimu nafasi ya kwanza kabla ya jambo lolote?
4.(a) Nini chanzo cha elimu na fani zote?
(b) “Soma kwa jina la Mola wako aliyeumba…….” (96:1).
(i) Kutokana na aya hii, fafanua nini maana ya kusoma ‘kwa jina la Allah’
(ii) Orodhesha njia tano anazotumia Allah (s.w) katika kuwaelimisha wanaadamu.
5 (a) Bainisha ni upi mgawanyo sahihi na usio sahihi juu ya elimu katika Uislamu.
(b) Tofautisha kati ya elimu ya mwongozo(faradh ‘Ain) na elimu ya mazingira (faradh kifaya).
6.‘Mgawanyo wa Elimu Dunia na Akhera (dini) haukubaliki (haupo) katika Uislamu’. Eleza ni kwa nini kwa kutoa sababu zisizopungua tano.
7.(a) Ni ipi elimu yenye manufaa?
(b) Eleza kwa ufupi, kwa nini ili Uislamu usimame katika jamii, hatuna budi kutotenganisha ‘Elimu ya Mwongozo na Elimu ya Mazingira’?
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet.
Soma Zaidi...Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet.
Soma Zaidi...Ibada yavfubga ni katika ibadavanbazo hufanya nakaribia dini zote kubwa. Ibada hii imekuwaikikabiliw na naswlo mengi.
Soma Zaidi...ุนููู ุฃูุจูู ุญูู ูุฒูุฉู ุฃูููุณู ุจููู ู ูุงูููู ุฑูุถููู ุงูููู ุนููููู ุฎูุงุฏูู ู ุฑูุณูููู ุงูููููู ุตูู ุงููู ุนููู ู ุณูู ุนููู ุงููููุจูููู ุตูู ุงููู ุนููู ?...
Soma Zaidi...Mnafiki ni yule anayeukubaliย Uislamu mdomoni (kwa kauli tu) lakini moyoni mwake na katika matendo yake anaukanusha.
Soma Zaidi...Na kuwapambanua wale waliokuwa wanafiki.
Soma Zaidi...