picha

Zoezi

Maswali mbalimbali yanayohusu elimu ya dini ya kiislamu na mwongozo wa elimu na elimu mazingira.

Zoezi la 1.

1.(a)  Elimu ni nini?

(b)  Mtu aliyeelimika ni mtu wa aina gani?

(c)  Unatoa maoni gani iwapo wanaojua watakuwa sawa na wasiojua kiutendaji?

 

2.(a)  “….Sema, Je! Wanaweza kuwa sawa wale wanaojua na wale wasiojua?.....(39:9).   Kwa nini wanaojua hawawi sawa na wasiojua?

(b) Kwa kutumia ushahidi wa aya, onesha kuwa elimu ndio takrima ya kwanza aliyokirimiwa mwanaadamu na Mola wake.

 

3.Kwa ushahidi wa aya za Qur’an, eleza kwa nini Uislamu umeipa elimu nafasi ya kwanza kabla ya jambo lolote?

 

4.(a)  Nini chanzo cha elimu na fani zote?

(b)  “Soma kwa jina la Mola wako aliyeumba…….” (96:1).

      (i)  Kutokana na aya hii, fafanua nini maana ya kusoma ‘kwa jina la Allah’

      (ii) Orodhesha njia tano anazotumia Allah (s.w) katika kuwaelimisha wanaadamu.

 

5 (a)  Bainisha ni upi mgawanyo sahihi na usio sahihi juu ya elimu katika Uislamu.

(b) Tofautisha kati ya elimu ya mwongozo(faradh ‘Ain) na elimu ya mazingira (faradh kifaya).

 

6.‘Mgawanyo wa Elimu Dunia na Akhera (dini) haukubaliki (haupo) katika Uislamu’. Eleza ni kwa nini kwa kutoa sababu zisizopungua tano.

 

7.(a)   Ni ipi elimu yenye manufaa?

(b)  Eleza kwa ufupi, kwa nini ili Uislamu usimame katika jamii, hatuna budi kutotenganisha ‘Elimu ya Mwongozo na Elimu ya Mazingira’?

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Jifunze Main: Post File: Download PDF Views 2946

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii     👉2 Kitau cha Fiqh     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 web hosting     👉5 Bongolite - Game zone - Play free game     👉6 Madrasa kiganjani    

Post zinazofanana:

Kitabu Cha Quran na sayansi

Kupata kitabu hiki download faili la PDF hapo chini na usome bila ya internet.

Soma Zaidi...
Uhakiki wa hadithi za mtume

Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Je wajuwa kuwa jua hujizungurusha kwenye mhimili wake?

Tulipokuwa shule tulisoma kuwa jua halizunguruki, ila dunia ndio huzunguka jua.

Soma Zaidi...
NENO LA AWALI

Darasa la elimu inayohusu ujauzito na namna ya kulea mimba

Soma Zaidi...
HADITHI YA MZEE WA KWANZA NA MBUZI

Download kitabu Hiki Bofya hapa HADITHI YA MZEE WA KWANZA NA MBUZI WAKE.

Soma Zaidi...
(ix)Wenye kuhifadhi swala

Waumini wa kweli waliofuzu huhifadhi swala kwa kutekeleza kwa ukamilifu shuruti zote za swala nguzo zote za swala na huswali kama alivyoswali Mtume (s.

Soma Zaidi...