picha

Zoezi

Maswali mbalimbali yanayohusu elimu ya dini ya kiislamu na mwongozo wa elimu na elimu mazingira.

Zoezi la 1.

1.(a)  Elimu ni nini?

(b)  Mtu aliyeelimika ni mtu wa aina gani?

(c)  Unatoa maoni gani iwapo wanaojua watakuwa sawa na wasiojua kiutendaji?

 

2.(a)  “….Sema, Je! Wanaweza kuwa sawa wale wanaojua na wale wasiojua?.....(39:9).   Kwa nini wanaojua hawawi sawa na wasiojua?

(b) Kwa kutumia ushahidi wa aya, onesha kuwa elimu ndio takrima ya kwanza aliyokirimiwa mwanaadamu na Mola wake.

 

3.Kwa ushahidi wa aya za Qur’an, eleza kwa nini Uislamu umeipa elimu nafasi ya kwanza kabla ya jambo lolote?

 

4.(a)  Nini chanzo cha elimu na fani zote?

(b)  “Soma kwa jina la Mola wako aliyeumba…….” (96:1).

      (i)  Kutokana na aya hii, fafanua nini maana ya kusoma ‘kwa jina la Allah’

      (ii) Orodhesha njia tano anazotumia Allah (s.w) katika kuwaelimisha wanaadamu.

 

5 (a)  Bainisha ni upi mgawanyo sahihi na usio sahihi juu ya elimu katika Uislamu.

(b) Tofautisha kati ya elimu ya mwongozo(faradh ‘Ain) na elimu ya mazingira (faradh kifaya).

 

6.‘Mgawanyo wa Elimu Dunia na Akhera (dini) haukubaliki (haupo) katika Uislamu’. Eleza ni kwa nini kwa kutoa sababu zisizopungua tano.

 

7.(a)   Ni ipi elimu yenye manufaa?

(b)  Eleza kwa ufupi, kwa nini ili Uislamu usimame katika jamii, hatuna budi kutotenganisha ‘Elimu ya Mwongozo na Elimu ya Mazingira’?

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2021/12/21/Tuesday - 03:19:21 pm Topic: Jifunze Main: Dini File: Download PDF Views 2821

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Kwanini Ni muhimu kusimamisha uislamu katika jamii

Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Je wajuwa kuwa jua hujizungurusha kwenye mhimili wake?

Tulipokuwa shule tulisoma kuwa jua halizunguruki, ila dunia ndio huzunguka jua.

Soma Zaidi...
Neno la awali

Asalaamu alykum warahmatullah wabarakaatuh Sifanjema zinamstahikia Allah Mola wa viumbe, muumba wa mbingu na ardhi na vilivyomo.

Soma Zaidi...