Zoezi

Maswali mbalimbali yanayohusu elimu ya dini ya kiislamu na mwongozo wa elimu na elimu mazingira.

Zoezi la 1.

1.(a)  Elimu ni nini?

(b)  Mtu aliyeelimika ni mtu wa aina gani?

(c)  Unatoa maoni gani iwapo wanaojua watakuwa sawa na wasiojua kiutendaji?

 

2.(a)  “….Sema, Je! Wanaweza kuwa sawa wale wanaojua na wale wasiojua?.....(39:9).   Kwa nini wanaojua hawawi sawa na wasiojua?

(b) Kwa kutumia ushahidi wa aya, onesha kuwa elimu ndio takrima ya kwanza aliyokirimiwa mwanaadamu na Mola wake.

 

3.Kwa ushahidi wa aya za Qur’an, eleza kwa nini Uislamu umeipa elimu nafasi ya kwanza kabla ya jambo lolote?

 

4.(a)  Nini chanzo cha elimu na fani zote?

(b)  “Soma kwa jina la Mola wako aliyeumba…….” (96:1).

      (i)  Kutokana na aya hii, fafanua nini maana ya kusoma ‘kwa jina la Allah’

      (ii) Orodhesha njia tano anazotumia Allah (s.w) katika kuwaelimisha wanaadamu.

 

5 (a)  Bainisha ni upi mgawanyo sahihi na usio sahihi juu ya elimu katika Uislamu.

(b) Tofautisha kati ya elimu ya mwongozo(faradh ‘Ain) na elimu ya mazingira (faradh kifaya).

 

6.‘Mgawanyo wa Elimu Dunia na Akhera (dini) haukubaliki (haupo) katika Uislamu’. Eleza ni kwa nini kwa kutoa sababu zisizopungua tano.

 

7.(a)   Ni ipi elimu yenye manufaa?

(b)  Eleza kwa ufupi, kwa nini ili Uislamu usimame katika jamii, hatuna budi kutotenganisha ‘Elimu ya Mwongozo na Elimu ya Mazingira’?

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Jifunze Main: Dini File: Download PDF Views 2237

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

(ix)Wenye kuhifadhi swala

Waumini wa kweli waliofuzu huhifadhi swala kwa kutekeleza kwa ukamilifu shuruti zote za swala nguzo zote za swala na huswali kama alivyoswali Mtume (s.

Soma Zaidi...
Uandishi wa hadithi wakati wa tabii tabiina

Sunnah na hadithi (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Husimamisha swala

Husimamisha swala katika maisha yao yote.

Soma Zaidi...
quran na sayansi

2:UUMBWAJI KWA MAJI YA UZAZIUumbwaji wa mwanadamu umepitia hatua mbalimbali na haya yote yamefanywa kwa sababumaalumu ili tipate mazingatio.

Soma Zaidi...