Ndoa ya mke zaidi ya mmoja katika uislamu na taratibu zake, faida zake na namna ya kuitekeleza

- Je, Ukeweza, (ndoa ya mke zaidi ya mmoja) humdhalilisha mwanamke?

Ndoa ya mke zaidi ya mmoja katika uislamu na taratibu zake, faida zake na namna ya kuitekeleza

Ruhusa ya Ndoa ya Mke Zaidi ya Mmoja.

- Je, Ukeweza, (ndoa ya mke zaidi ya mmoja) humdhalilisha mwanamke?



Jibu ndio:

- Kama ndoa hiyo imekusudiwa kumfanya mwanamke nguvu kazi ya uchumi, kuwa mwangalizi wa himaya ya mumewe tu, n.k.


- Kumzalia watoto wengi kama nguvu kazi ya uchumi, ulinzi wa mali yake tu, na kukosekana malengo ya ndoa, n.k.


- Kukosekana uadilifu na haki zake za msingi za kuolewa na kutekeleza majukumu yake ya msingi ili kufikia lengo kuumbwa kwake.


- Kunyanyaswa kama kupigwa, kutohurumiwa, kutukanwa, kutothaminiwa au kutengwa katika mahitaji ya kimaisha na kukidhi haja za kimwili pia.


Jibu hapana

- Kama ndoa inakusudiwa kumhifadhi na kumsitiri mwanamke na kila aina ya uovu na uchafu wa matamanio ya kimwili.


- Ikiwa ni kwa ajili ya kuwahifadhi na kuwasitiri wajane walioachwa na waume wao bado wakihitaji malezi ya ndoa.


- Ikiwa ni kuwanusuru, kuwahifadhi na kuwasitiri wanawake wema waliokosa waume wa kuwaoa wasijejiingiza katika machafu.




Sababu ya kuruhusiwa kuoa mke zaidi ya mmoja

Mafunzo ya Qur’an (57:25) na (4:3) yanatoa sababu zifuatazo;

i. Ukewenza ni ruhusa kutoka kwa Allah (s.w), hivyo wanaume hawana budi kuipokea kwa lengo la kumcha Allah (s.w).


ii. Ukewenza ni fursa pekee kwa wanaume waislamu wema, waadilifu kuwaoa wanawake hawa ili wasijekuolewa na wanaume waovu.


iii. Ukewenza hupelekea hifadhi kwa wajane, mayatima na wanawake wema wanaohitaji hifadhi, malezi, n.k.


iv. Ukewenza unaruhusika tu kwa kufanya uadilifu kwa wanawake wote katika kukidhi matamanio ya kimwili.




Hekima ya Ukewenza (kuoa mke zaidi ya mmoja)

Kuna sababu za kibinafsi, kimaadili, kiuchumi na kijamii kama ifuatavyo;

i. Kama mke ni tasa, hawezi kuzaa:

- Ikiwa mume anahitaji mtoto wa kumrithi kisheria na mkewe hawezi kuzaa hanabudi kuoa mke mwingine lakini akae kwa wema na wanawake wote.


ii. Kama mke ana maradhi ya kudumu:

- Kama mke ana ugonjwa wa kudumu na hawezi kumkidhia mahitaji ya kimwili, mume hanabudi kuoa mke mwingine na kuishi nao kwa wema.


iii. Kuwahifadhi Wanawake wajane na walioachika:

- Wanaume wanalazimika kuoa wake zaidi ya mmoja kama kuna wanawake wajane waliofiwa na waume zao au walioacha.


iv. Kuwapa hifadhi wanawake waliozidi idadi ya wanaume katika jamii:

- Kama wanawake watakuwa wengi katika jamii, italazimika wanaume kuoa wake zaidi ya mmoja ili kuepusha kuenea machafu na maovu.


v. Kuwapa hifadhi na malezi watoto yatima:

- Mwanamke akifiwa na mume na ana watoto, malezi kamili hukosekana kama wazazi, hivyo kuolewa kunaboresha malezi kwa watoto walioachwa.



                   

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 1231

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰2 Bongolite - Game zone - Play free game    πŸ‘‰3 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰4 Simulizi za Hadithi Audio    πŸ‘‰5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    πŸ‘‰6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Mda wa mwisho wa kula daku mwezi wa ramadhani

Post hii fupi itakwenda kukujulisha utaratibu wa kula daku.

Soma Zaidi...
Ni nini maana ya twahara na kujitwaharisha?

Posti hii inakwendabkukujiulisha maana ya twahara na jinsi ya kujitwaharisha.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kumuosha maiti wa kiislami mwanaume au mwanamke

Post hii inakwenda kukufundisha hatuwa kwa hatuwa jinsi ya kumuosha maiti wa kiislamu

Soma Zaidi...
Jinsi ya kutwaharisha Aina mbalimbali za Najisi katika uislamu

Katika somo hili utakwedna kujifunza jinsi ya kutwaharisha aina mbalimbali za najisi kwa mujibu wa mafundiso ya Mtume Muhammad (s.a.w)

Soma Zaidi...
Haki za muislamu kwa muislamu mwenziwe

Hizi ndio haki kuu tano unazopasa kumpatia Muislamu mwenzio.

Soma Zaidi...
Riba na Madhara Yake Katika Jamii

- Riba ni kipato chochote kile cha ziada kutokana na mkopo au mtaji bila kushiriki katika faida au hasara.

Soma Zaidi...
Wenye ruhusa za kutofunga ramadhan

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Ni ipi hukumu ya muislamu anayekula mwezi wa Ramadhani bila ya sababu ya kisheria

Endapo muislamu hatafunga mwezi wa Ramadhani bila ya ruhusa je atatakiwa afanye nini. Je ataweza kuilipa funga hiyo?

Soma Zaidi...
Sifa za imamu wa swala ya jamaa

Post hii inakwenda kukupa sifa za imamu wa msikitini anayepasa kuswalisha swala ya jamii.

Soma Zaidi...