Nasaha za Lut(a.s) kwa Watu Wake

Nabii Lut(a.

Nasaha za Lut(a.s) kwa Watu Wake

Nasaha za Lut(a.s) kwa Watu Wake


Nabii Lut(a.s), kama Mitume wengine walivyofanya aliwanasihi watu wake wamuamini Allah(s.w) na wamche ipasavyo na waogope adhabu yake ambayo ikimfika mtu hapana awezaye kuizuia au kuiondosha.



(Wakumbushe) alipowaambia ndugu yao, (Nabii) Lut: โ€œJe, hamuogopi?โ€ โ€œBila shaka mimi kwenu ni Mtume muaminifu.โ€ โ€œBasi Mcheni Mwenyezi Mungu na nitiini.(26:161-163)




โ€œWala sikutakini ujira juu yake; ujira wangu hauko ila kwa (Mwenyezi Mungu) Mola wa walimwengu wote.โ€ โ€œJe, mnawaingilia wanaume katika viumbe (vyake Mwenyezi Mungu)!โ€ โ€œNa mnawacha alichokuumbieni Mola wenu katika wake zenu? Kweli nyinyi ni watu mnaoruka mipaka (mliyowekewa).โ€(26:164-166)



Na (wakumbushe) Lut alipowambia watu wake: โ€œJe, mnaufanya uchafu, na hali mnaona?โ€ Mnawaingilia wanaume kwa matamanio mabaya badala ya wanawake? Hakika nyinyi ni watu mfanyao ya ujinga kabisa. (27:54-55)



Pamoja na nasaha hizi nzuri zilizoambatana na hoja madhubuti, hawakumuamini Lut(a.s) ila watu wachache tu. Lakini hatukupata humo ila nyumba moja tu yenye Waislamu. (51:36)




Jawabu la Makafiri Dhidi ya Nasaha za Nabii Lut(a.s)


Pamoja na Nabii Lut(a.s) kuwanasihi kwa maneno ya hekima na hoja zilizo wazi, watu wake hawakuwa tayari kabisa kuacha maovu yale.



Naapa kwa umri wako! Hakika wao walikuwa katika ulevi wao (wa maovu); wanahangaika ovyo. (15:72)
Walishakuwa walevi wa machafu hayo na walipania kumfukuza Nabii Lut na wale walioamini pamoja naye ambao huchukia ubaladhuli huo.



โ€œBasi haikuwa jawabu ya watu wake ila kusema: Wafukuzeni wafuasi wa Lut katika mji wenu, hao ni watu wanaojitakasa, (basi wasikae na sisi wachafu)โ€ (27:56)



โ€œWakasema: Kama usipoacha, ee Lut (kutukataza haya), bila shaka utakuwa miongoni mwa wanaofukuzwa (katika nchi hii).โ€ (26:167)



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1194

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Dua za Mitume na Manabii    ๐Ÿ‘‰2 Simulizi za Hadithi Audio    ๐Ÿ‘‰3 Madrasa kiganjani    ๐Ÿ‘‰4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    ๐Ÿ‘‰5 Bongolite - Game zone - Play free game    ๐Ÿ‘‰6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana: