Nadharia ya uchumi wa kiislamu


image


Dhana ya uchumi wa kiislamu imejegwa jui ya ukati na kati. Dhana hii imetofautiana sana na dhana nyinginezo kama ubepari na ujamaa.


1.Nadharia ya uchumi wa Kiislamu
Mfumo wa uchumi katika Uislamu ni utaratibu utokanao na Qur-an na Sunnah juu ya uzalishaji, umilikaji, usambazaji, na utumiaji wa mali na huduma pamoja na miiko yake. Kwa msingi huo, uchumi huo umejengwa juu ya fikra ya ukati na kati (Iqtisaad), hivyo umetofautiana na mifumo mingine iliyobuniwa na watu.

 

Dhana (concept) ya ukati (Iqtisaad) katika shughuli za kiuchumi ni kule kutoa uhuru kwa mtu binafsi (sekta binafsi) kuchuma na kumiliki mali ili iwe motisha kwake ya kuchapa kazi wakati huo huo serikali ikisimamia na kutoa miongozo katika uzalishaji na ugawaji, na vile vile kuwa na sekta zake (sekta za umma) ili kila mwana jamii apate haki za kimsingi. Mifumo iliyobuniwa na watu imeathiriwa na udhaifu wa kibinaadamu wa kuelemea upande huu au ule.

 


Ipo mifumo ya kiuchumi kama vile ubepari ambao umeelemea mno katika ubinafsi kiasi ambacho umepuuza kabisa haki za kijamii. Katika mfumo huu (ubepari) umma hauna chake; mali, huduma na shughuli mbali mbali hubinafsishwa. Wachache chini ya mfumo huu ndio hunufaika na rasilimali za Taifa. Hujilimbikizia mali, na motisha yao ya uzalishaji ni ile faida waipatayo. Serikali kuu ya mfumo huu wa kibepari hushirikiana na wachache hao waliohodhi mali, kuwanyonya walio wengi.

 


Pia, kuna mfumo wa uchumi wa Kikomunist au Kijamaa ambao nadharia yake imeelemea mno katika “usawa” wa sare kiasi cha kudhoofisha mno motisha ya watu binafsi na hivyo kupelekea kukosekana kwa ufanisi katika uzalishaji. Katika mfumo huu mali na shughuli mbali mbali hutaifishwa (toka milki ya watu binafsi kuwa milki ya taifa).

 

Ukweli ni kwamba huwa si mali ya taifa kama inavyotangazwa bali mbiu ya “usawa”, na “mali ya umma”, chini ya mfumo huu, ni mwavuli tu uliokinga kikundi cha watu kilichojipa mamlaka ya uendeshaji wa nchi kwa sura ya chama au serikali kwa maslahi ya kikundi hicho. Kikundi hicho ndicho humiliki na kutafuna mali huku wananchi wengi wakiendelea kudhulumiwa kwa sababu mbali mbali. Hivyo hakuna usawa ulio chini ya mfumo huu bali ni ubinafsi ule ule ambao huhamishwa toka kwa mtu binafsi kwenda kwenye kikundi fulani.



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Download App zetu hapa ujifunze zaidi       ðŸ‘‰    2 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    3 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    4 Jifunze Fiqh    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Jinsi ya kutawadha hatuwa kwa hatuwa
Kutawadha ni katika ibada muhimu za mwanzo kutakiwa kuzijuwa na ni lazima. Swala yako haitaweza kutimia bila ya kujuwa udhu. Inakupasa kujuwa nguzo za udhu, yanayoharibu udhu na namna ya kutawadha kifasaha. Hapa utajifunza hatuwa za kutawadha Soma Zaidi...

image Kwa nini waislamu wanaoa mke zaidi ya mmoja
Post hiibitakugundisha hekima ya kuruhusiwa kuoa mke zaidi ya mmoja katika sheria za kiislamu. Soma Zaidi...

image Jinsi ya kuswali kuswali swala ya maiti
Post hii itakufundisha kuhusu swala ya maiti, nguzo za swala ya maiti, sharti za swwla ya maiti na jinsi ya kuiswali. Soma Zaidi...

image Mambo anayofanyiwa mtu anayekaribia kufa
Haya ni maandalizi anayofanyiwa mtu aliye katika kilevi cha kifo yaani sakaratul maut Soma Zaidi...

image Jinsi ya kiswali swala ya tahajud na swala za usiku yaani qiyamu layl
Post hii itakujuza jinsi ya kiswali swala ya tahajudi. Pia utajifunza jinsi ya kuswali swala za usikubyaanibqiyamublayl Soma Zaidi...

image Jinsi ambavyo mgonjwa anatakiwa aswali
Post hii inakwenda kukufundisha jinsi ambavyo mgonjwa anatakiwa aswali kulingana na ugonjwa wake. Soma Zaidi...

image Zijuwe funga za sunnah na jinsi ya kuzifunga
Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu funga za sunnah na jinsi ya kuzigunga. Soma Zaidi...

image Jinsi ya kuswali swala vitani
Post hii itakufundisha taratibu zinazofanyika ilibkuswalibukiwa vitani. Soma Zaidi...

image Utaratibu wa kuzuru makaburi na dua zinazosomwa wakati wa kuzuru kaburi
Post hii itakufundisha taratibu zinazofanyika katika kuzuru kaburi la muislamu. Soma Zaidi...

image Nadharia ya uchumi wa kiislamu
Dhana ya uchumi wa kiislamu imejegwa jui ya ukati na kati. Dhana hii imetofautiana sana na dhana nyinginezo kama ubepari na ujamaa. Soma Zaidi...