image

NGUZO ZA UISLAMU: SWALA NA SHAHADA NA FAIDA ZAKE

NGUZO ZA UISLAMU.

NGUZO ZA UISLAMU: SWALA NA SHAHADA NA FAIDA ZAKE

NGUZO ZA UISLAMU: SWALA NA SHAHADA NA FAIDA ZAKE

NGUZO ZA UISLAMU.
1. Maana ya Shahada.
Shahada mbili ndio nguzo ya kwanza ya Uislamu na ndio kiingilio cha mtu katika Uislamu kwa kuyakinishwa moyoni, kutamkwa kinywani na kuthibitishwa kwa vitendo.
Rejea Qur’an (41:30-31), (2:8) na (33:40).

2. Maana ya Kusimamisha Swala.
Ni kuswali kwa kutekeleza kikamilifu nguzo, sharti zote za swala na kuwa na unyenyekevu (khushui) ndani ya swala.

Nafasi na Umuhimu wa Kusimamisha Swala katika Uislamu.
Swala imesisitizwa na ina umuhimu katika Uislamu kwa sababu zifuatazo;

i.Kusimamisha Swala ni Amri ya Mwenyezi Mungu (s.w).
Mwenyezi Mungu (s.w) ameamrisha waumini (waislamu) wote wasimamishe swala zote za faradh na sunnah ipasavyo.
Rejea Qur’an (29:45), (4:103) na (14:31).

ii.Kusimamisha swala ni nguzo ya Pili ya Uislamu.
Baada ya shahada mbili, nguzo ya pili na ya msingi mno katika Uislamu ni kusimamisha swala.

iii.Swala humtakasa muislamu na mambo machafu na maovu.
Bila shaka swala ikiswaliwa vilivyo humuepusha mja na mambo machafu na maovu.
Rejea Qur’an (29:45).

iv.Swala ni amali ya mwanzo kabisa kuhesabiwa siku ya Qiyama.
Swala ya muumini ikitengemaa vizuri ndio sababu ya kufaulu kwake Duniani na Akhera pia.
Rejea Qur’an (23:1-2,9), (87:14-15) na (22:34-35).

v.Kutosimamisha swala ni sababu ya mtu kuingizwa motoni.
Hii ni baada ya muislamu Kupuuza swala kwa kutozingatia sharti na nguzo zake kikamilifu na kukosa unyenyekevu (khushui) ndani ya swala.
Rejea Qur’an (74:42-47), (68:42-43) na (107:4-5).

Lengo la Kusimamisha Swala.
Lengo kuu la kusimamisha swala ni kumkinga mja na mambo machafu na maovu kwa kutekeleza kikamilifu sharti, nguzo na sunnah za swala pamoja na kuwa na khushui ndani ya swala kama ifuatavyo;
i.Swala inamtakasa mja kwa kuzingatia na kutekeleza sharti zake zote kikamilifu ambazo ni kuwa twahara, sitara (kujisitiri), kuchunga wakati wa swala na kuelekea Qibla.
ii. Swala inamtakasa mja kwa kutekeleza kikamilifu nguzo na sunnah za swala kama kumsifu na kumtukuza Mwenyezi Mungu (s.w), kusoma Qur’an, kutoa ahadi ya kujisalimisha kwa Mwenyezi Mungu (s.w), kuomba dua na kutekeleza vitendo vyote vya swala.

Faida (matunda) ya kusimamisha swala katika jamii.
Swala za faradhi zikisimamishwa vilivyo faida zifuatazo hupatikana katika jamii;

i.Usafi na unadhifu wa mwili.
Kwani muislamu hawezi kuswali mpaka ahakikishe kuwa msafi (twahara) kikamilifu katika nguo na mwili pia na sehemu ya kuswalia.
Rejea Qur’an (7:31).

ii.Utakaso wa Nafsi.
Kwa kutekeleza sharti na nguzo za swala pamoja na mnyenyekevu katika swala, hupelekea mja kuwa mtiifu ipasavyo kwa Mola wake muda wote.

iii.Swala za jamaa huimarisha udugu, umoja na usawa.
Kuswali katika jamaa huleta udugu, umoja na usawa wa kweli na kuepusha mfarakano, chuki na ubaguzi miongoni mwa waislamu.
Rejea Qur’an (49:10,13).

iv.Swala za jamaa huwafunza waislamu uongozi bora.
Swala huongozwa na imamu (kiongozi) wa waumini husika anayetokana na wao kutokana na sifa maalumu za kuwa kiongozi.



Kwa nini Wengi wanaoswali hawafikii Lengo la Swala zao?
Miongoni mwa sababu ya wengi kutofikia malengo ya swala zao ingawa wanaziswali misikitini tena kwa jamaa ni;

1.Hawajui lengo halisi la swala.
Waislamu wengi huswali kwa lengo la kufutiwa madhambi na kupata thawabu na sio kuepukana na machafu na maovu, ambalo ndio lengo kuu la swala. Kupata thawabu na kufutiwa madhambi ni matunda ya swala.
Rejea Qur’an (29:45) na (72:23).

2.Waislamu wengi hawana ujuzi sahihi juu ya swala.
Pamoja na waislamu wengi kutekeleza swala zao kwa jamaa lakini wengi wao hawajui kabisa miiko, sharti na nguzo za swala ila wanafuata mkumbo tu.
Rejea Qur’an (7:205), (7:55) na (4:142).

3.Waislamu wengi hawahifadhi swala zao.
Pamoja na kuswali kwao bado wengi hawazingatii na kutekeleza kikamilifu sharti na nguzo za swala zao inavyotakiwa.
Rejea Qur’an (107:4-5) na (23:1,8).

4.Wengi hawaswali kwa Unyenyekevu swala zao.
Kukosa unyenyekevu (utulivu wa mwili, fikra na uzingativu) hupelekea mwenye kuswali kutofikia lengo na matunda ya swala.
Rejea Qur’an (29:45), (23:1-2) na (23:10-11).

5.Kutosimamisha Swala za jamaa ipasavyo.
Waislamu wengi hawaswali jamaa misikitini au hawazingatia sharti za swala ya jamaa kama kunyoosha safu ipasavyo, kugusanisha mabega, vidole, n.k.
Rejea Qur’an (23:1-2).





                   





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 490


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

Je mahari inashusha hadhi ya mwanamke katika jamii
Unadhani mwanamke kupewa mahari kitendo hiki kinaweza kushusha hadhi yake? Soma Zaidi...

Ni upibutaratibu wa kuingia eda na kutoka eda
Katika uislamu hakuna sheria ya mwanamke kuingizwa eda na kutolewa eda kama ilivyozoeleka. Endelea na post hii ujifunze zaidi Soma Zaidi...

Nini maana ya najisi, na ni zipi Najisi katika uislamu na aina za najisi
Soma Zaidi...

Zoezi la 6 kusimamisha swala
Zoezi hili linamaswali mbalimbali kuhusiana na swala na masharti ya swala. Soma Zaidi...

Mgawanyiko katika kuitumia mali unayomiliki
Unajuwa namna ambavyo matumizi ya mali yako, yanavyogawanywa? Jifunze hapa mgawanyiko wa mali yako. Soma Zaidi...

Sanda ya mwanaume na namna ya kumkafini
Mambo ya faradh kwa maiti ya muislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mazao ambayo inapasa kutolewa zaka
Soma Zaidi...

Je manii ni twahara au najisi?
Post hii itakwenda kukufundisha hukumu ya manii kuwa ni twahara ama ni najis Soma Zaidi...

Haki za maadui katika vita (mateka wa kivita)
Haki na uadilifu katika uislamu (EDK form 3: Dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mda wa mwisho wa kula daku mwezi wa ramadhani
Post hii fupi itakwenda kukujulisha utaratibu wa kula daku. Soma Zaidi...

Zijuwe funga za kafara na jinsi ya kuzigunga
Post hii itakufundisha kuhusu funga za kafara, zinavyotokea na na jinsi ya kuzifunga. Soma Zaidi...

Misingi ya fiqh
Kwenye kipengele hichi tutajifinza vyanzo mbalimbali vya sheria ua kiislamu. Soma Zaidi...