Yunus(a.s) Kulingania Uislamu kwa Watu Wake

Nabii Yunus(a.

Yunus(a.s) Kulingania Uislamu kwa Watu Wake

Yunus(a.s) Kulingania Uislamu kwa Watu Wake


Nabii Yunus(a.s) alitumwa kufikisha ujumbe wa Allah(s.w) kwa watu laki moja na zaidi wa mji wa Ninawah (Nineveth) katika nchi ya Assyria. Ninawah ni mji wa zamani sana ambao hauko katika ramani hivi sasa. Mji huo ulikuwa kandokando ya mto Tigris sehemu iliyo mkabala na mji wa kisasa, Mosul, kilometa 368 kaskazini ya kaskazini magharibi mwa mji wa Baghdad.



Nabii Yunus(a.s) aliwalingania Uislamu watu wa mji ule, lakini walimkanusha. Allah(s.w) alimuagiza Nabii Yunus awaonye watu wake juu ya adhabu itakayowafika baada ya muda maalumu uliowekwa endapo wataendelea kumuasi. Yunus(a.s) alipoona kuwa muda wa adhabu unakaribia na bado watu wake wameshikilia msimamo wao wa kukanusha ujumbe wake, alikata tamaa na kuamua kuondoka kwenye mji ule kuihami nafsi yake na adhabu ya Allah, bila ya kupewa ruhsa ya kuhama na Mola wake kama walivyopewa ruhusa Mitume wengine.



Watu wa mji ule walipoona adhabu inakaribia, walimuamini Nabii Yunus kuwa ni Mtume wa haki, wakamuamini Allah(s.w) na kumnyenyekea ipasavyo na kumuomba msamaha kwa maovu yao. Allah(s.w) kwa rehema yake aliwasamehe na kuwaondolea adhabu ile kama tunavyojifunza katika Qur-an:




Kwanini usiweko mji ulioamini (upesi kabla ya kuadhibiwa), ili imani yake iwafae? Isipokuwa watu wa Yunus (tu ndio walioamini mara walipohisi kuwa adhabu inakuja. Basi wakaokoka). Walipoamini tuliwaondolea adhabu ya hizya katika maisha ya dunia na tukawastarehesha kwa muda (tulioutaka). (10:98)



Nabii Yunus(a.s) hakujua yaliyopita nyuma yake. Alipoona adhabu haikushuka alichelea kuwa watu wa mji ule watazidi kumkanusha. Akakimbilia Pwani ambako alipata jahazi akaingia. Jahazi ilisheheni kiasi kwamba halikuweza kwenda. Ikapigwa kura ili itakaye muangukia atoswe baharini. Ikamuangukia Nabii Yunus(a.s) akatoswa baharini na kumezwa na chewa (samaki mkubwa)



Na hakika Yunusi alikuwa miongoni mwa Mitume. (Kumbukeni) alipokimbilia katika jahazi iliyosheheni.(37:139-140)




Na wakapiga kura. Basi akawa miongoni mwa walioshindwa (ikapasa atupwe baharini). Mara samaki alimmeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa. Basi isingelikuwa ya kwamba yeye alikuwa ni miongoni mwa waliokuwa wanamuabudu (Mwenyezi Mungu vilivyo). (37:141-143)

Bila shaka angalikaa tumboni mwake mpaka siku watakakayofufuliwa (viumbe). (37:144)



                   

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1002

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana: