Yunus(a.s) Kulingania Uislamu kwa Watu Wake

Yunus(a.s) Kulingania Uislamu kwa Watu Wake

Nabii Yunus(a.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Yunus(a.s) Kulingania Uislamu kwa Watu Wake

Yunus(a.s) Kulingania Uislamu kwa Watu Wake


Nabii Yunus(a.s) alitumwa kufikisha ujumbe wa Allah(s.w) kwa watu laki moja na zaidi wa mji wa Ninawah (Nineveth) katika nchi ya Assyria. Ninawah ni mji wa zamani sana ambao hauko katika ramani hivi sasa. Mji huo ulikuwa kandokando ya mto Tigris sehemu iliyo mkabala na mji wa kisasa, Mosul, kilometa 368 kaskazini ya kaskazini magharibi mwa mji wa Baghdad.



Nabii Yunus(a.s) aliwalingania Uislamu watu wa mji ule, lakini walimkanusha. Allah(s.w) alimuagiza Nabii Yunus awaonye watu wake juu ya adhabu itakayowafika baada ya muda maalumu uliowekwa endapo wataendelea kumuasi. Yunus(a.s) alipoona kuwa muda wa adhabu unakaribia na bado watu wake wameshikilia msimamo wao wa kukanusha ujumbe wake, alikata tamaa na kuamua kuondoka kwenye mji ule kuihami nafsi yake na adhabu ya Allah, bila ya kupewa ruhsa ya kuhama na Mola wake kama walivyopewa ruhusa Mitume wengine.



Watu wa mji ule walipoona adhabu inakaribia, walimuamini Nabii Yunus kuwa ni Mtume wa haki, wakamuamini Allah(s.w) na kumnyenyekea ipasavyo na kumuomba msamaha kwa maovu yao. Allah(s.w) kwa rehema yake aliwasamehe na kuwaondolea adhabu ile kama tunavyojifunza katika Qur-an:




Kwanini usiweko mji ulioamini (upesi kabla ya kuadhibiwa), ili imani yake iwafae? Isipokuwa watu wa Yunus (tu ndio walioamini mara walipohisi kuwa adhabu inakuja. Basi wakaokoka). Walipoamini tuliwaondolea adhabu ya hizya katika maisha ya dunia na tukawastarehesha kwa muda (tulioutaka). (10:98)



Nabii Yunus(a.s) hakujua yaliyopita nyuma yake. Alipoona adhabu haikushuka alichelea kuwa watu wa mji ule watazidi kumkanusha. Akakimbilia Pwani ambako alipata jahazi akaingia. Jahazi ilisheheni kiasi kwamba halikuweza kwenda. Ikapigwa kura ili itakaye muangukia atoswe baharini. Ikamuangukia Nabii Yunus(a.s) akatoswa baharini na kumezwa na chewa (samaki mkubwa)



Na hakika Yunusi alikuwa miongoni mwa Mitume. (Kumbukeni) alipokimbilia katika jahazi iliyosheheni.(37:139-140)




Na wakapiga kura. Basi akawa miongoni mwa walioshindwa (ikapasa atupwe baharini). Mara samaki alimmeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa. Basi isingelikuwa ya kwamba yeye alikuwa ni miongoni mwa waliokuwa wanamuabudu (Mwenyezi Mungu vilivyo). (37:141-143)

Bila shaka angalikaa tumboni mwake mpaka siku watakakayofufuliwa (viumbe). (37:144)



                   

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1139

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Mafunzo Yatokanayo na mambo Aliyofanya Mtume (s.a.w) Katika Kuanzisha Dola ya Kiislamu
Mafunzo Yatokanayo na mambo Aliyofanya Mtume (s.a.w) Katika Kuanzisha Dola ya Kiislamu

Kwanza, ili tuweze kusimamisha Uislamu katika jamii hatunabudi kuanzisha na kuendeleza vituo vya harakati, misikiti ikiwa ndio vitovu.

Soma Zaidi...
Muhutasari wa sifa za wanafiki
Muhutasari wa sifa za wanafiki

Kwa kuzingatia aya zote tulizozipitia juu ya wanafikitunaweza kutoa majumuisho ya sifa za wanafiki kama ifuatavyo:- (1)Hutenda kinyume cha imani wanaodai kuwa nayo.

Soma Zaidi...
Vita vya Al Fijar na sababu zake
Vita vya Al Fijar na sababu zake

Historia na shida ya Mtume Muhammad S.A.W, sehemu ya 12. Hapa utajifunza kuhusu kutokea kwa vita vya al fijar.

Soma Zaidi...