picha

Yunus(a.s) Kulingania Uislamu kwa Watu Wake

Nabii Yunus(a.

Yunus(a.s) Kulingania Uislamu kwa Watu Wake

Yunus(a.s) Kulingania Uislamu kwa Watu Wake


Nabii Yunus(a.s) alitumwa kufikisha ujumbe wa Allah(s.w) kwa watu laki moja na zaidi wa mji wa Ninawah (Nineveth) katika nchi ya Assyria. Ninawah ni mji wa zamani sana ambao hauko katika ramani hivi sasa. Mji huo ulikuwa kandokando ya mto Tigris sehemu iliyo mkabala na mji wa kisasa, Mosul, kilometa 368 kaskazini ya kaskazini magharibi mwa mji wa Baghdad.



Nabii Yunus(a.s) aliwalingania Uislamu watu wa mji ule, lakini walimkanusha. Allah(s.w) alimuagiza Nabii Yunus awaonye watu wake juu ya adhabu itakayowafika baada ya muda maalumu uliowekwa endapo wataendelea kumuasi. Yunus(a.s) alipoona kuwa muda wa adhabu unakaribia na bado watu wake wameshikilia msimamo wao wa kukanusha ujumbe wake, alikata tamaa na kuamua kuondoka kwenye mji ule kuihami nafsi yake na adhabu ya Allah, bila ya kupewa ruhsa ya kuhama na Mola wake kama walivyopewa ruhusa Mitume wengine.



Watu wa mji ule walipoona adhabu inakaribia, walimuamini Nabii Yunus kuwa ni Mtume wa haki, wakamuamini Allah(s.w) na kumnyenyekea ipasavyo na kumuomba msamaha kwa maovu yao. Allah(s.w) kwa rehema yake aliwasamehe na kuwaondolea adhabu ile kama tunavyojifunza katika Qur-an:




Kwanini usiweko mji ulioamini (upesi kabla ya kuadhibiwa), ili imani yake iwafae? Isipokuwa watu wa Yunus (tu ndio walioamini mara walipohisi kuwa adhabu inakuja. Basi wakaokoka). Walipoamini tuliwaondolea adhabu ya hizya katika maisha ya dunia na tukawastarehesha kwa muda (tulioutaka). (10:98)



Nabii Yunus(a.s) hakujua yaliyopita nyuma yake. Alipoona adhabu haikushuka alichelea kuwa watu wa mji ule watazidi kumkanusha. Akakimbilia Pwani ambako alipata jahazi akaingia. Jahazi ilisheheni kiasi kwamba halikuweza kwenda. Ikapigwa kura ili itakaye muangukia atoswe baharini. Ikamuangukia Nabii Yunus(a.s) akatoswa baharini na kumezwa na chewa (samaki mkubwa)



Na hakika Yunusi alikuwa miongoni mwa Mitume. (Kumbukeni) alipokimbilia katika jahazi iliyosheheni.(37:139-140)




Na wakapiga kura. Basi akawa miongoni mwa walioshindwa (ikapasa atupwe baharini). Mara samaki alimmeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa. Basi isingelikuwa ya kwamba yeye alikuwa ni miongoni mwa waliokuwa wanamuabudu (Mwenyezi Mungu vilivyo). (37:141-143)

Bila shaka angalikaa tumboni mwake mpaka siku watakakayofufuliwa (viumbe). (37:144)



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1939

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani    👉2 Dua za Mitume na Manabii    👉3 kitabu cha Simulizi    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 web hosting   

Post zinazofanana:

tarekh 10

KULELEWA NA BABA YAKE MDOGOBaada ya kufariki kwa mzee huyu, kiongozi mkubwa wa maquraysh na makkah, kiongozi ambaye jeshi la Abrah liliangamizwa ndani ya utawala wake.

Soma Zaidi...
Mapambano ya waislamu dhidi ya maadui wa kiyahudi madina

Mayahud Mwanzoni Mayahud walipoona kuwa Waislamu wanafunga siku ya Ashura pamoja nao na wanaelekea Qibla cha Baitul- Muqaddas pamoja nao hawakuonyesha chuki ya dhahiri dhidi ya Mtume(s.

Soma Zaidi...
tarekh

MAPIGANO YA AL-FIJAR (MAPIGANO YA UOVU).

Soma Zaidi...
Kuanzishwa kwa dola ya kiislamu madinah

Dola ya kiislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mafunzo yatokanayo na hijrah ya mtume na maswahaba wake

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...