Mipaka katika kuwatii Wazazi
Pamoja na msisitizo huu mkubwa wa kuwatii wazazi, utii wetu kwao ni lazima ulandane na utii wetu kwa Mwenyezi Mungu (s.w) na Mtume wake. Endapo watatuamrisha tufanye jambo lolote lile Iinalokwenda kinyume na maamrisho ya Mwenyezi Mungu (s.w) na Mtume wake tutalazimika kutowatii na kubakisha utii wetu kwa Mwenyezi Mungu (s.w) na Mtume wake kama inavyobainishwa katika aya zifuatazo:
Na tumemuusia mwanaadamu afanye wema kwa wazazi wake; na kama wakikushurutiza kunishirikisha na yale usiyo na ilimu nayo, basi usiwatii, kwangu ndiyo marejeo yenu, basi nitakwambieni mliyokuwa mkiyatenda. (29:8).
Na (wazazi wako) wakikushurutisha kunishirikisha na (yale) ambayo huna ilimu nayo, usiwatii, lakini kaa nao kwa wema hapa duniani; shika njia ya wale wanaoelekea kwangu, kisha marejeo yenu ni kwangu, hapo nitakuambieni mliyokuwa mkiyatenda. (3 1:15).
Hata hivyo, pamoja na aya hizi kutukataza kuwa tusiwatii wazazi wetu endapo watatuamrisha kumshikirikisha Mwenyezi Mungu (utii kwa yeyote yule kinyume na Mwenyezi Mungu ni shiriki), bado tunasisitizwa tuwaheshimu, tuwahurumie na kuwatendea wema kwa kadiri ya uwezo wetu wote katika mambo yote ya kheri. Hana radhi ya Mwenyezi Mungu (s.w) yeyote yule atakayewavunjia heshima na kuwatendea visivyo wazazi wake na hata wazazi wa wengine. Hebu tuzingatie Hadith ifuatyo:
Abdallah bin Umar amesimulia kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu amesema:Katika madhambi makubwa, ni mtu kuwatukana wazazi wake. Wakauliza (Maswahaba); Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Mtu anawezaje kuwatukana wazazi wake? "Ndio" al/ibu Mtume, anamtukana baba wa mwingine ambaye humrudishia kwa kumtukania baba yake na anamtukana mama wa mwingine ambaye humrudishia tusi hilo kwa mama yake. (Bukhari na Muslim).
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download
Download NowJe! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sunnah Main: Post File: Download PDF Share On Facebook or Whatsapp Views 470
Sponsored links
👉1
Madrasa kiganjani
👉2
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
👉3
Simulizi za Hadithi Audio
👉4
kitabu cha Simulizi
👉5
Kitau cha Fiqh
👉6
Kitabu cha Afya
HADITHI YA 34 YEYOTE ATAKAYEONA KITENDO KIOVU AKIONDOE KWA MKONO WAKE
Soma Zaidi...
DUA ZENYE MANENO HAYA HUJIBIWA
SIFA ZA (MANENO NA MATAMSHI YA) DUA YENYE KUJIBIWA. Soma Zaidi...
JINSI YA KUOMBA DUA ILI IKUBALIWE NA ALLAH
Kukubaliwa kwa dua kunategemea mahusiano yako na Allah. hata hivyo kuna baadhi ya mabo ukiyafanya dua yako inaweza kukubaliwa kwa haraka zaidi. Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi ya kuomba dua ikubaliwe. Soma Zaidi...
ni nyakati zipi ambazo dua hukubaliwa kwa haraka?
Dua ni moja ya ibada ambazo zinamfanya mja awe karibu na Mweznyezi Mungu. Allah amesisitiza tumuombe dua kwa shida zetu zote, pia akaahidi kuwa atatujibu maombi yetu muda wowote tutakao muomba. Sasa ni zipi nyakati nzuri zaidi kuomb adua? Soma Zaidi...
Hadithi Ya 21: Sema Namuamini Allah Kisha Kuwa Mwenye Msimamo
Soma Zaidi...
Historia ya Imamu Bukhary Muandishi wa Hadithi za Mtume s.sa. w
Hii ni historia ya Imamu Bukhary pamoja na kitabu chake cha sahihul Bukhari. Soma Zaidi...
DUA ZA WAKATI WA SHIDA
DUA ZA WAKATI WA SHIDA 1. Soma Zaidi...
Hadithi Ya 40: Kuwa Duniani Kama Vile Mgeni Au Mpita Njia
Soma Zaidi...