Mipaka katika kumtii mzazi, na mambo yasiyopasa kumtii mzazi

Mipaka katika kumtii mzazi, na mambo yasiyopasa kumtii mzazi

Mipaka katika kuwatii Wazazi



Pamoja na msisitizo huu mkubwa wa kuwatii wazazi, utii wetu kwao ni lazima ulandane na utii wetu kwa Mwenyezi Mungu (s.w) na Mtume wake. Endapo watatuamrisha tufanye jambo lolote lile Iinalokwenda kinyume na maamrisho ya Mwenyezi Mungu (s.w) na Mtume wake tutalazimika kutowatii na kubakisha utii wetu kwa Mwenyezi Mungu (s.w) na Mtume wake kama inavyobainishwa katika aya zifuatazo:



Na tumemuusia mwanaadamu afanye wema kwa wazazi wake; na kama wakikushurutiza kunishirikisha na yale usiyo na ilimu nayo, basi usiwatii, kwangu ndiyo marejeo yenu, basi nitakwambieni mliyokuwa mkiyatenda. (29:8).


Na (wazazi wako) wakikushurutisha kunishirikisha na (yale) ambayo huna ilimu nayo, usiwatii, lakini kaa nao kwa wema hapa duniani; shika njia ya wale wanaoelekea kwangu, kisha marejeo yenu ni kwangu, hapo nitakuambieni mliyokuwa mkiyatenda. (3 1:15).



Hata hivyo, pamoja na aya hizi kutukataza kuwa tusiwatii wazazi wetu endapo watatuamrisha kumshikirikisha Mwenyezi Mungu (utii kwa yeyote yule kinyume na Mwenyezi Mungu ni shiriki), bado tunasisitizwa tuwaheshimu, tuwahurumie na kuwatendea wema kwa kadiri ya uwezo wetu wote katika mambo yote ya kheri. Hana radhi ya Mwenyezi Mungu (s.w) yeyote yule atakayewavunjia heshima na kuwatendea visivyo wazazi wake na hata wazazi wa wengine. Hebu tuzingatie Hadith ifuatyo:



Abdallah bin Umar amesimulia kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu amesema:Katika madhambi makubwa, ni mtu kuwatukana wazazi wake. Wakauliza (Maswahaba); Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Mtu anawezaje kuwatukana wazazi wake? "Ndio" al/ibu Mtume, anamtukana baba wa mwingine ambaye humrudishia kwa kumtukania baba yake na anamtukana mama wa mwingine ambaye humrudishia tusi hilo kwa mama yake. (Bukhari na Muslim).




                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sunnah Main: Dini File: Download PDF Views 633

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

Ijuwe swala ya Mtume na fadhila zake na jinsi ya kumswalia Mtume.

Post hii itakufundisha jinsi ya kumswalia mtume, pamoja na kuzijuwa fadhila unazopata kwa kumswalia Mtume

Soma Zaidi...
DUA DHIDI YA WASIWASI, UCHAWI NA MASHETANI

DUA ZA KUONDOA WASIWASI, SIHIRI NA UCHAWI 1.

Soma Zaidi...
NAFASI YA SUNNAH KATIKA UISLAMU

Nafasi ya Sunnah katika UislamuMtume Muhammad (s.

Soma Zaidi...
DUA 94 - 114

DUA ZA KUONDOA WASIWASI, SIHIRI NA UCHAWI 94.

Soma Zaidi...
Maana ya Hadith al Quds na Hadith an-Nabawiy

Katika somo hili utakwenda kujifunza maana ya hadithi al Quds na Hadith an-Nabawiy

Soma Zaidi...
ADHKAR NA DUA

ADHKARI MBALIMBALI NA DUA Hapa tutajifunza dua mbalimbali ambazo ni adhkari.

Soma Zaidi...
NAFASI YA SUNNAH KATIKA UISLAMU

Nafasi ya Sunnah katika UislamuMtume Muhammad (s.

Soma Zaidi...
Historia ya uandishi wa Hadithi, na ni kwa nini wakati wa Mtunme hakukuwa na uandishibmkubwa wa hadithi

Hapa utakwendabkuijuwabhistoria ya uandishi wa hadithi. Pia utaijuwa sababu iliyopelekea uandishi wa hadithi kuwa mdogo .

Soma Zaidi...
Namna ambazo Allah hujibu dua ya mwenye kuomba.

Post hii inakwenda kukufundisha namna ama staili ambazo Allah hujibu dua za watu.

Soma Zaidi...