DUA ZA KUONDOA WASIWASI, WOGA NA KUJIKINGA NA UCHAWI, NA MASHETANI


image


Post hii itakufundisha dua za kuomba wakati wa woga, wasiwasi na kujikinga na wachawi na mashetani



DUA ZA KUONDOA WASIWASI, SIHIRI NA UCHAWI
1.Kutaka hifadha dhidi ya vitimbi vya shetani na wasiwasi ni jambo ambalo Allah ametuamrisha kulifanya. Hivi pia ndivyo ambavyo mtume wetu alikuwa akifanya. Amesema Allah (s.w): “Na sema: Mola wangu Mlezi! Najikinga kwako na wasiwasi wa mashet'ani. Na najikinga kwako, Mola wangu Mlezi, wasinikaribie.” Quran surat al-an-muumin aya ya 97-98).

Hivyo hapa tunajifunza kuwa ukitaka kujikinga na wasiwasi na vitimbi vya shetani unatakiwa useme maneno haya aliyotufundisha Allah (s.w) ambayo ni kusema “RABBI A’UUDHUBIKA MIN-HAMAZAATISH-SHAYAATWIN, WA A-’UUDHUBIKA AN-YAHDUDUUN” katika dua hii herufi D hap utaona imepigiwa msitari. Hiyo ni herufi ض ambayo hainna mwenzie kwenye kiswahili. Fatilia kwa wasomi wakufundishe inavyosomwa. Kwa kiarabu dua hii ni hii chukua msahafu wako fungua surat al-muumin aya ya 97-98 وَقُل رَّبِّ أَعُوذُ بِكَ مِنْ هَمَزَاتِ الشَّيَاطِينِ ﴿٩٧﴾ وَأَعُوذُ بِكَ رَبِّ أَن يَحْضُرُونِ ﴿٩٨﴾

2.mwenye kutaka kuikinga nyumba yake na mwili wake pamoja na ahali zake dhidi ya uchawi na majini masi asome surat al-baqara japo mara moja kila baada ya siku tatu, au asome ayat al-qursiy na aya mbili za mwisho za surat al-baqara japo mara moja kwa siku au asubhi na jioni. Au asome sura al-mu’awidhatayn yaani surat al-falaq na surat an-na sura hizi asome pamoja na surat al-ikhlas kwa utaratibu aloufanya Mtume (s.a.w), tutauzungumza hapa. Hebu tuone kwanza faida za sura hizi kwa mapokezi ya hadithi zilizo sahihi

1.Surat al-fatiha.
Amesimulia Ibn ‘Abas kuwa “wakati ambao jibril alikuwa amekaa na Mtume akasikia sauti ya mlango uliofunguliwa juu yake akanyanyu kichwa chake kisha akasema “hiyo ni nsauti ya mlango uliopo mbinguni umefunguliwa siku ya leo, na katu haujawahi kufunguliwa ila ni leo tu (ndio mara ya kwanza kufunguliwa).

Basi akashuka Malaika kutoka kwenye mlango huu akasema (Jibril) huyu ni malaika ameshuka duniani na hajawahi kushuka kamwe ila ni leo tu akatoa salamu (malaika huyo) kisha akasema (kumwambia mtume) tuo habari za furaha kwa nuru mbili ulizopewa na hakuwahi kupewa mtume yeyote kabla yako kamwe (ambazo ni) surat al-fatiha na aya za mwisho za surat al-baqarah hatusoma herufi yeyote isipokuwa utapewa” (amepokea Muslim). Amesema Mtume “surat al-fatiha ni dawa ya kila gonjwa” amepokea Bayhaqiy)

2.surat al-baqarah Amesema Mtume “…Mwenye kuisoma katika nyumba yake usiku hatoingia shetani nyumba hiyo kwa muda wa siku tatu, na mwenye kuisoma mchana hatoingia shetani nyumba hiyo kwa michana mitatu” (amepokea Ibn hiban, tabrany na Bayhaqiy). 3.ayat al-qursiy.
Amesema Mtume “katika surat al-baqarah kuna aya iliyobora kuliko aya zote haitasomwa aya hiyo kwenye nyumba yenye shetani ila atatoka kwenye nyumba hiyo, (aya hiyo ni) ayat al-kursy) (amepokea Al-Haakim na Bayhaqiy)

3.aya za mwisho za surat al-baqarah
Amesema Mtume hakika Allah ameimalizia surat al-baqarah kwa aya zilizo tukufu (zilizotoka) kwenye hazina chini ya ‘arshi basi jifundisheni aya hizo na muwafundishe wake zenu na watoto wenu. Kwani mna ndani ya aya hizo dua, qiraa na dua” (amepokea Al-Haakim kutoka kwa Abuu Dhari).
Pia Amesema mtume “aya mbili za mwisho za surat al-baqarah mwenye kuzisoma usiku zitamtosheleza” (amepokea bukhari,Muslim,Ahmad na Ibn Maajah kutoka kwa ibnmas’ud)

4.Suratul ikhlas, nasi na falaq
Amesimulia ‘Abdallah Ibnhabib kuwa Mtume amesema “QUL HUWA LLAHU AHADU na mu’awadhatayn (qul a’udhu birabin-nasi na qul a’udhu birabil-falaq) (mwenye kuzisoma ) asubuhi na jioni zinatosheleza kwa kila kitu.(amepokea ahmad, Tirmidh na Nisai).

Hizi ni baadhi tu ya sura mahususi ambazo Mtume alikuwa akiwasisitiza masahaba zake wazisome. Sura nyingine ni kama al-imran, al-an’am, al-israa, al-kahaf, surat musabahat(sura zilizoanzwa na tasbih nnazo zipo saba), surat al-mulkk, surat ar-rahman, surat al-waqi’a, surat al-zalzala, surat at-takathur, surat al-fiyl, surat al-kafiruun, surat yasin n.k. Kupata faida zaidi ya sura hizi download App yetu iiitwayo darsa za quran, utafaidiza zaidi.

Sasa hebu tuone namna ambavyo Mtume (s.a.w) katika maisha yake tunapata mafunzo alivyokuwa akitumia sura hizi kama ni kinga na dawa kwa mambo mbalimbali:-

1.Mtume (s.a.w) amesema:”mwenye kusoma aya kumi nne za mwanzo katika surat al-baqarah, na ayat al-qursiy na aya mbili baada ya aya hii, na aya mbili zilizo mwishoni mwa surat al-baqarah hataingia katika nyumba hiyo shetani mpaka asubuhi” (amepokea hadithi tabrany na Alhakim akaisahihisha).

2.Mtume alikuwa anapokwenda kulala anasoma sura na aya hizi, kwa utaratibu huu:- Alikuwa Mtume (s.a.w) akienda kulala usiku, akiweka pamoja viganja vyake kisha akivipulizia na akivisomea suratul-Ikhlas, suratul Falaq na Suratun-Naas, kisha akipangusa kwa hivyo viganja vyake kiasi anachoweza katika mwili wake, akianza kichwani, usoni na mbele (akifanya hivyo mara tatu.) (Bukhari na Muslimu)

Mtume (s.a.w) amesema: "Ukienda kulala soma Ayatulkursiyyu kwani Allah ataendelea kukuhifadhi, wala hakukaribii shetani mpaka asubuhi." (Al-Bukhari)

Mwenyezi Mungu, hakuna Mola ila yeye, ndiye mwenye uhai wa milele, msimamia kila jambo. Kusinzia hakumshiki wala kulala. Ni vyake (peke yake vyote) vilivyomo mbinguni na vilivyomo ardhini. Na nani huyo awezaye kuombea mbele yake bila ya idhini yake? Anayajua yaliyo mbele yao (viumbe) na (yaliyo) nyuma yao; wala (hao viumbe) hawalijui lolote katika ilimu yake ila kwa alipendalo. Enzi yake imeenea mbinguni na ardhini, wala kuvilinda hivyo hakumshindi; Na yeye (pekee) ndiye aliye juu na ndiye aliye mkuu." (2:255)

Alikuwa Mtume (s.a.w) akitaka kulala, anaweka mkono wake wa kulia chini ya shavu lake, kisha anasema: "Allahumma qiniy a'dhaabaka yaumatab-a'thu i'baadaka." "Ee! Allah nikinge mimi kwa adhabu yako siku utakapowafufua waja wako."

Pia Mtume (s.a.w) wakati wa kulala alikuwa akisema: “Allahumma Bismika amuutu wa-ahyaa. “Kwa jina lako, Ee Allah ninakufa na nina kuwa hai." uzi na ndiye Mwenye hikima (2:32)

3.Dua pindi uonaposhetani au unapotishwa na shetani
Ikitokea Mtu ameona shetani au ametishwa na shetani anatakiwa kuleta isti’adha na asema “A’UDHU BILLAHI MINKA” mara tatu kisha aseme “AL-’ANUKA BILA’ANATIL-LLAHI TAAMMAH” mara tatu. Hakika shetani anakimbia ukisema maneno hayo. Hatika mapokezi ukimuona shetani akikutisha au hakukutisha soma adhana hakika shetani hukimbia adhana. Katika hadithi alopokea muslim mtume (s.a.w) amesema “hakika shetani hukimbia pindi adhana ya swala inaposomwa”

Kwa ufupi zipo dua nyingi lakini qurani inatosha kabisa kufanya kila tunalolitaka. Qurani inatosha kuwa kinga ya wachawi, majini na vijicho. Dua zaidi tumeziwekakwenye App yetu iitwayo swala na dua. Tumeweka kule kwa kuhofia kuirefusha app ii kuwa ndefu zaidi. Tunasikiliza mawazo yenu wasomaji zaidi. Kuiboresha App hii. Darsa hii imewekwa kutegemea na michango na maoni ya masomaji wetu. Tutaendelea kufanya hivu zaidi.


 



Sponsored Posts


  👉    1 Mafunzo ya php       👉    2 Mafunzo ya html kwa kiswahili       👉    3 Madrasa kiganjani       👉    4 Jifunze fiqh       👉    5 Hadiythi za alif lela u lela       👉    6 Maktaba ya vitabu    





Je una umaswali, maoni ama mapendekezo?
Download App yetu kuwasiliana nasi




Post Nyingine


image Adhkari unazoweza kuomba kila siku
Hapa nitakuletea baadhi tu ya adhkari ambazo ni muhimu kwa muislamu Soma Zaidi...

image Namna ambazo Allah hujibu dua ya mwenye kuomba.
Post hii inakwenda kukufundisha namna ama staili ambazo Allah hujibu dua za watu. Soma Zaidi...

image Ijuwe swala ya Mtume na fadhila zake na jinsi ya kumswalia Mtume.
Post hii itakufundisha jinsi ya kumswalia mtume, pamoja na kuzijuwa fadhila unazopata kwa kumswalia Mtume Soma Zaidi...

image Adabu za kuomba dua kuifanya dua yako ikubaliwe kwa haraka
Post hii inakwenda kukugundisha adabu zinazotakikana kwa mwenye kuomba dua. Soma Zaidi...

image Dua ambazo hutumiwa katika swala
Post hii inakwenda kukugundisha dua ambazo itazitumia katika swala yako. Soma Zaidi...

image Maana ya dua na fadhila zake
Dua ni moja ya Ibada ambazo tunatakiwa kuziganya kila siku. Kuna fadhila nyingi sana za kuomba dua. Post hiibitakwenda kukujuza fadhila za kuomba dua. Soma Zaidi...

image Masharti ya kukubaliwa kwa dua
Post hii itakwenda kukugundisha masharti yanayofungamana na kukubaliwa kwa dua. Soma Zaidi...

image JINSI YA KUOMBA DUA ILI IKUBALIWE NA ALLAH
Kukubaliwa kwa dua kunategemea mahusiano yako na Allah. hata hivyo kuna baadhi ya mabo ukiyafanya dua yako inaweza kukubaliwa kwa haraka zaidi. Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu jinsi ya kuomba dua ikubaliwe. Soma Zaidi...

image Jinsi ya kuzuru makaburi na dua unazotakiwa kuzisoma ukiwa makaburini.
Posti hii inakwenda kukufundisha maneno unayotakiwa kuyasema unapozuru makaburi. Soma Zaidi...

image Matamshi ambayo ukimwambia Allah kwenye dua yako basi hujibiwa kwa haraka dua hiyo
Post hii inakwenda kukufundisha matamshi ambayo mtu akiyatamka Allah hujibu dua hiyo kwa urahisi. Soma Zaidi...