Maana ya dua na fadhila zake

Dua ni moja ya Ibada ambazo tunatakiwa kuziganya kila siku. Kuna fadhila nyingi sana za kuomba dua. Post hiibitakwenda kukujuza fadhila za kuomba dua.

DUA
Kwa ufupi dua ni kumuomba Allah akuondoshee lililobaya, ama linalo kuudhi ama akupe jambo fulani. Na dua ni ibada kama ibada nyingine.

Dua ni jambo lenye kupendeza kama walivyosema maulamaa na masalafi wema walotangulia. Umuhimu wa dua na msisitizo wake unapatikana katika quran na sunnah.

Dua zimesisitizwa sana katika quran na sunnah hata mtume akasema لِيَسْأَلْ أَحَدُكُمْ رَبَّهُ حَاجَتَهُ حَتَّى يَسْأَلَهُ الْمِلْحَ “na aombe mmoja wenu haya yake (dua) kwa Allah mpaka chumvi.…”. Hivyo si kuomba mambo kakubwa tu na matatizo tulonayo ila mpaka chumvi.

FADHILA ZA DUA
1.Dua ni ibada. Basi utambue ewe ndugu muislamu kuwa dua ni ibada. Imepokewa hadithi kutoka kwa Nuuman Ibn Bashir رضىالله عنه kuw Mtume wa Allah صليالله عليه وسلم amesema "‏ الدُّعَاءُ هُوَ الْعِبَادَةُ“hakika dua ni ibada” (imepokewa na Tirmidh na ameisahihisha).

2.Dua ndio jambo tukufu zaidi kwa Allah kama Mtume صليالله عليه وسلم aliposema katika hadithi iliyosimuliwa na Abu Huraurah رضىالله عنه kuwa Mtume amesema “hakuna kitu kitukufu mbele ya Allah kuliko dua” (imapokewa na tirmidh, imam Ahmad na Alhaakim kwa isnad sahihi) لَيْسَ شَيْءٌ أَكْرَمَ عَلَى اللَّهِ تَعَالَى مِنَ الدُّعَاءِ “

3.Allah anamchukia mtu ambaye hamuombi. Abuu Hurairah رضىالله عنه amesema kuwa Mtume صليالله عليه وسلم amesema "‏ مَنْ لَمْ يَسْأَلِ اللَّهَ يَغْضَبْ عَلَيْهِ ‏" “mtu yeyote ambaye hamuombi Allah, Allah humchukia mtu huyo” (amepokea hadithi tirmidh)

4.Allah anapenda kuombwa. Katika masimulizi ya Ibn Mas’ud رضىالله عنه Mtume صلّي الله عليه وسلّم amesema “muombeni Allah katika fadhila zake, hakika Mwenyezimungu Mtukufu (غزّ وجلّ) anapenda kuombwa” (amepokea Tirmidh).

5.Dua ni malango wa rehema. Katika masimulizi ya ibn ‘Umar رضىالله عنه kuwa Mtume صلّي الله عليه وسلّم amesema "‏ مَنْ فُتِحَ لَهُ مِنْكُمْ بَابُ الدُّعَاءِ فُتِحَتْ لَهُ أَبْوَابُ الرَّحْمَةِ وَمَا سُئِلَ اللَّهُ شَيْئًا يَعْنِي أَحَبَّ إِلَيْهِ مِنْ أَنْ يُسْأَلَ الْعَافِيَةَ ‏"‏ “mwenye kufunguliwa mlango wa dua, hufunguliwa mlango wa rehema.…” (amepokea Tirmidh).

6.Dua huondosha mabalaa na majanga. Katika masimulizi ya Ibn ‘Umar, رضىالله عنه Mtume صلّي الله عليه وسلّم amesema “hakika dua hunufaisha kwa (hukinga) yale yanayoshuka (yanayotokea), na yale ambayo hayajashuaka ( hayajatokea). Basi jilazimisheni na (kuomba) dua enyi waja wa Allah.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sunnah Main: Dini File: Download PDF Views 5899

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Vyanzo vitano vya elimu zote duniani: Chanzo cha Elimu ni Allah (s.w)

Kama tunavyojifunza katika surat ‘Alaq (96:4-5), chanzo cha elimu au mkufunzi wa binadamu ni Allah (s.

Soma Zaidi...
DUA YA MUUMINI NA DUA YA KAFIRI

DUA YA KAFIRI NA DUA YA MUUMINI.

Soma Zaidi...
Uislamu ni Nasaha (kunasihiana) kwa Mwenyezi Mungu, Kitabu chake Mtume wake , Viongozi na waislamu wote

عَنْ أَبِي رُقَيَّةَ تَمِيمِ بْنِ أَوْسٍ الدَّارِيِّ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ النَّبِيَّ صلى الله عليه وسلم قَالَ: "الدِّينُ النَّصِ?...

Soma Zaidi...
Matamshi ambayo ukimwambia Allah kwenye dua yako basi hujibiwa kwa haraka dua hiyo

Post hii inakwenda kukufundisha matamshi ambayo mtu akiyatamka Allah hujibu dua hiyo kwa urahisi.

Soma Zaidi...
UKITAKA KUOMBA BASI MUOMBE ALLAH, UKIMKUMBUKA WAKATI WA RAHA ATAKUKUMBUKA WAKATI WA DHIKI, SHIDA NA TAABU

عَنْ عَبْدِ اللَّهِ بْنِ عَبَّاسٍ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: "كُنْت خَلْفَ رَسُولِ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم يَوْمًا، فَقَالَ: ي...

Soma Zaidi...
Darsa za Dua

Download kitabu hiki na upate kusoma zaidi ya dua 120, pamoja na darsa mbalimbali za dini ya kiislamu.

Soma Zaidi...
MUISLAMU ALIYE BORA NI YULE ANAYEWACHA MAMBO YASIYO MUHUSU

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم "مِنْ حُسْنِ إسْلَامِ الْمَرْءِ تَرْكُهُ مَ?...

Soma Zaidi...