picha

Mfumo wa ulinzi na usalama katika fola ya uislamu madinah

Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Dola (serikali) ya Kiislamu Madinah iliposimama na kuanza kazi za kuongoza jamii iliandamwa na maadui wa kila aina. Mtume (s.a.w) aliweka mikakati na mbinu madhubuti za kuilinda na kuihami serikali yake ikiwa ni pamoja na;

 

  1. Misafara ya Kujihami (Patrol) na Upelelezi.

Mtume (s.a.w) aliweka watu maalum kwa ajili ya kulinda mipaka ya Dola na kupeleleza harakati za maadui dhidi ya Uislamu na waislamu.

Rejea Qur’an (4:71).

 

  1. Kuweka Mikataba ya amani.

Mtume (s.a.w) aliweka mikataba ya amani na makabila ambayo hayakusilimu yaliyopembezoni mwa Dola ya Kiislamu kama, Banu Dumra, Mudlaj, n.k.

Rejea Qur’an (9:13-15).

 

  1. Kupigana vita.

Njia hii ililazimika kutumika baada ya kuzidi uonevu, dhuluma na choko choko za wazi dhidi ya Waislamu na Uislamu.

Rejea Qur’an (2:193), (9:111) na (9:29)

 

  1. Sera ya wazi juu ya wanafiki.

Mtume (s.a.w) alichukua tahadhari na hatua dhidi ya wanafiki waliojidhihirisha wazi kutengana na ummah wa waislamu kwa kuwatenga.

Rejea Qur’an (9:73), (9:84) na (9:80).

 

  1. Sera ya Uislamu juu ya amani.

Mtume (s.a.w) alitekeleza na kuelekeza mafundisho ya Uislamu juu ya kutunza na kulinda amani kama fursa na dhamana katika kueneza Uislamu. 

Rejea Qur’an (8:61), (16:90), (2:84), (8:5-8).



 

  1. Uhusiano wa Kiplomasia na nchi za nje.

Mtume (s.a.w) aliweka sera ya wazi juu ya uandikashaji na utekelezaji wa mikataba mbali mbali na maadui wa Uislamu kama Aqaba, Hudaybiyah, n.k.

Rejea Qur’an (5:8), (42:40-42), (60:8).

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF Views 2262

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii     👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉3 Simulizi za Hadithi Audio     👉4 Kitabu cha Afya     👉5 Bongolite - Game zone - Play free game     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Mtume Muhammad s.a. w akutana na Bahira

Sura na historia ya Mtume Muhammad s.a. w sehemu ya 11

Soma Zaidi...
tarekh 06

MAISHA YA UTOTONI YA MTUME S.

Soma Zaidi...
HISTORIA YA MTUME DHUL-KIFL(A.S)

Mtume Dhul-kifl ananasibishwa na Ezekiel anayetajwa ndani ya Biblia.

Soma Zaidi...
Kazi na wajibu wa khalifa katika dola ya kiislamu

Kazi na Wajibu wa KhalifaKhalifa katika Serikali ya Kiislamu ndiye mtendaji mkuu wa Serikali kama alivyokuwa Mtume(s.

Soma Zaidi...