Mfumo wa ulinzi na usalama katika fola ya uislamu madinah

Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Dola (serikali) ya Kiislamu Madinah iliposimama na kuanza kazi za kuongoza jamii iliandamwa na maadui wa kila aina. Mtume (s.a.w) aliweka mikakati na mbinu madhubuti za kuilinda na kuihami serikali yake ikiwa ni pamoja na;

 

  1. Misafara ya Kujihami (Patrol) na Upelelezi.

Mtume (s.a.w) aliweka watu maalum kwa ajili ya kulinda mipaka ya Dola na kupeleleza harakati za maadui dhidi ya Uislamu na waislamu.

Rejea Qur’an (4:71).

 

  1. Kuweka Mikataba ya amani.

Mtume (s.a.w) aliweka mikataba ya amani na makabila ambayo hayakusilimu yaliyopembezoni mwa Dola ya Kiislamu kama, Banu Dumra, Mudlaj, n.k.

Rejea Qur’an (9:13-15).

 

  1. Kupigana vita.

Njia hii ililazimika kutumika baada ya kuzidi uonevu, dhuluma na choko choko za wazi dhidi ya Waislamu na Uislamu.

Rejea Qur’an (2:193), (9:111) na (9:29)

 

  1. Sera ya wazi juu ya wanafiki.

Mtume (s.a.w) alichukua tahadhari na hatua dhidi ya wanafiki waliojidhihirisha wazi kutengana na ummah wa waislamu kwa kuwatenga.

Rejea Qur’an (9:73), (9:84) na (9:80).

 

  1. Sera ya Uislamu juu ya amani.

Mtume (s.a.w) alitekeleza na kuelekeza mafundisho ya Uislamu juu ya kutunza na kulinda amani kama fursa na dhamana katika kueneza Uislamu. 

Rejea Qur’an (8:61), (16:90), (2:84), (8:5-8).



 

  1. Uhusiano wa Kiplomasia na nchi za nje.

Mtume (s.a.w) aliweka sera ya wazi juu ya uandikashaji na utekelezaji wa mikataba mbali mbali na maadui wa Uislamu kama Aqaba, Hudaybiyah, n.k.

Rejea Qur’an (5:8), (42:40-42), (60:8).

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1509

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Kitabu cha Afya    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana: