Navigation Menu



image

Kuzaliwa kwa Musa(a.s) na kukua kwake na maisha ya ujana wake na kupata Elimu

Musa(a.

Kuzaliwa kwa Musa(a.s) na kukua kwake na maisha ya ujana wake na kupata Elimu

Kuzaliwa kwa Musa(a.s) na kukua kwake na maisha ya ujana wake na kupata Elimu


Musa(a.s) alizaliwa wakati bado msako unafanywa na askari wa Firauni kumwua kila mtoto wa kiume wa Kiisrail anayezaliwa. Kwa rehema zake Allah(s.w) mama yake Musa alijifungua bila kutambulika kwa askari wa Firauni. Na ili kumlinda zaidi Allah(s.w) alimteremshia Wahy mama yake Musa.




Ya kwamba mtie sandukuni, kisha litie mtoni, na mto utamtupa ufukoni ili amchukue adui yangu na adui yake (amlee kwa vizuri Naye ni Firaun). Na nimekutilia mapenzi yatokanayo kwangu (ili upendwe na watu wote), na ili ulelewe machoni mwangu.(20:39)



Baada ya kumtupa mtoni, mama yake akamtuma dada yake Musa kufuatilia:

Akamwambia dada yake: “Mfuate”. Basi yeye akamwangalia kwa mbali bila wao kumjua (28:11)



Kitoto Musa kiliokotwa na kufikishwa kwa Firaun. Mkewe Firaun akamrai mumewe kuwa wasimuue bali wamfanye mtoto wao wa kulea.



Na mkewe Firauni akasema (Kumwambia mumewe) “Usimuuwe, atakuwa kiburudisho cha macho kwangu na kwako; na msimuuwe;huwenda atatunufaisha, au tumpange kuwa mtoto wetu,walisema haya hali ya kuwa hawatambui(kuwa atakuwa adui yao)”(28:9)



Watu wa Firauni walipomwokota Musa bila shaka walitambua kuwa ni mtoto wa Kiisrail na walimpeleka kwa Firauni ili auawe kama watoto wengine Wakiisrail. Lakini mke wa Firauni alivutiwa na uzuri wa mtoto Musa. Ambaye kwa kweli Allah(s.w) alimfanya awe ni mwenye kupendeza machoni kwa watu. Allah(s.w) Ajaalia Musa(a.s) Kunyonyeshwa na Mama Yake Mzazi



Kwa uwezo wake, Mwenyezi Mungu aliharamisha Musa asinyonyeshwe na yeyote yule isipokuwa mama yake. Hivyo, dada yake Musa alijitokeza nyumbani kwa Firauni na kupendekeza:

“.........Basi akasema: Je nikuonesheni watu wa nyumba watakaomlea kwa ajili yenu, na pia watakuwa wema kwake? (28:12)



Dada yake Musa(a.s) alimpendekeza mama yake ambaye Firauni hawakumjua kuwa ndiye mama mzazi wa Nabii Musa(a.s). Ombi hilo lilikubaliwa na Musa(a.s)alirejeshwa kwa mama yake:



Basi tukamrejesha kwa mama yake ili macho yake yaburudike, wala asihuzunike; na ajue ya kwamba ahadi ya Mwenyezi Mungu ni kweli, lakini watu wengi hawajui (28:13)


Allah(s.w) Amruzuku Musa(a.s) Elimu


Ili kuweza kutekeleza jukumu la kutetea haki za binadamu na kuwaongoza watu katika njia iliyonyooka, Mwenyezi Mungu akamjaalia Musa elimu ya kutosha na akili yenye upeo mkubwa wa kupembua mambo. Tunafahamishwa kuwa:



Na Musa alipofikia baleghe yake na kustawi, tulimpa akili na elimu, na hivi ndivyo tunavyowalipa watu wema (28:14)



                   






           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu image Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira Main: Post File: Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 1986


Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Kitau cha Fiqh     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    

Post zifazofanana:-

Chanzo cha vita vya Ngamia Vita Kati ya Bibi Aisha na Khalifa Ali
Soma Zaidi...

Watu wa Mji Waliomuua Muislamu kwa Kuwa Amewasadikisha Wajumbe wa Allah(s.w)
Katika Suratul Yassin Allah(s. Soma Zaidi...

Kuingia Kwa Uislamu Tanzania na Afrika Mashariki
Soma Zaidi...

Maandalizi ya Hijra ya Mtume na Mafunzo tunayoyapata kutoka katika hijra hii
Maandalizi ya Hijra ya Mtume (s. Soma Zaidi...

tarekh 5
KUZALIWA KWA MTUME (S. Soma Zaidi...

Musa(a.s)Kupewa Utume Rasmi
Musa alipotimiza muda, alifunga safari na ahali zake kurejea Misri. Soma Zaidi...

NDOA YA MTUME S.A.W NA BI KHADIJA (HADIJA) BINTI KHUWALD
MTUME Muhammad (s. Soma Zaidi...

Uendeshaji wa dola ya uislamu madinah
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Mkataba wa 'Aqabah na vipiengele vyake na mafunzo tunayoyapata katika mkataba wa aqaba
Mtume (s. Soma Zaidi...

HISTORIA YA NABII AYYUUB(A.S)
Ayyuub(a. Soma Zaidi...

Sifa au vigezo vya dini sahihi
Dini sahihi anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...

Kazi na wajibu wa khalifa katika dola ya kiislamu
Kazi na Wajibu wa KhalifaKhalifa katika Serikali ya Kiislamu ndiye mtendaji mkuu wa Serikali kama alivyokuwa Mtume(s. Soma Zaidi...