NINI MAANA YA MINYOO: vimelea wa minyoo (parasites)

MINYOO NI NINI?

NINI MAANA YA MINYOO: vimelea wa minyoo (parasites)

NINI MAANA YA MINYOO?

MINYOO NI NINI?
Minyoo ni katika vimelea ama wadudu wanaoishi ndani ya kiumbe aliye hai. Wanaweza kuishi kwenye wanyama kama ngo’ombe, ngurue na mbuzi, pia wanaweza kuishi ndani ya binadamu. Wanajipatia mahitaji humo kama chakula, hewa na kila wanachohitaji. Wakiwa wanaishi ndani ya mwili wa kiumbe hai wanaweza kusababisha madhara makubwa sana katika afya ya mtu. Wadudu hawa kitaalamu wanatambulika kama parasitic worm.

Katika makala hii tutakwenda kujifunza, dalili, sababu, matibabu na njia za kupambana na minyoo katika mazingira yetu. Pia tutaona madhara ya kiafya yanayoletwa na kuishi na minyoo mwilini. Endelea kuwa nasi upate faida hii

Hatari ya kupata minyoo ni kubwa sana maeneo ya vijijini ama katika maeneo ambayo hali ya usafi sionzuri. Nchi zinazoendelea kama nchi za afrika ni katika maeneo ambayo yanakabil;iwa sana na minyoo kuliko nchi zilizo endelea.

Wataalamu wanatueleza kuwa kuna aina zaidi ya 300,000 (laki tatu) za minyoo. Na katika aina hizi kuna aina 300 (mia tatu) za minyoo ambao wanaweza kuishi ndani ya mwili wa mwanadamu na kumuathiri kwa namna moja ama nyingine.

Minyoo wanazaliana kwa kutaga mayai, na mayai yao yanatofautiana ukubwa, kuna ambayo yanaonekana kwa macho na mengine ni madogo zaidi kwa kuonekana kwa macho. Kuna aina za minyoo hutaga mayai bila ya kuhitaji kuwepo kwa dume, kwani kuna minyoo ambayo ina jinsia zote kwa pamoja (hermaphroditc).

Minyoo huweza kutaga mayai zaidi ya mara sita kwa siku. Na idadi ya mayai yao ni kati ya mayai 3000, mpaka 700000. na mayai yao yanaweza kudumu kwa miezi mingi biala ya kufa, na yanaweza kuvumialia hali mbalimbali za joto.


                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 1782

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 web hosting    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina   

Post zinazofanana:

Dalili za minyoo na sababu zake

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za minyoo na sababu zake

Soma Zaidi...
Sababu za Uvimbe wa tishu za Matiti kwa wavulana au wanaume

posti hii inazungumzia kuhusiana na uvimbe wa tishu za matiti kwa wavulana au wanaume, unaosababishwa na kutofautiana kwa homoni za estrojeni na testosterone. Pia unaweza kuathiri matiti moja au zote mbili, wakati mwingine bila usawa. Watoto wachanga,

Soma Zaidi...
DALILI ZA MINYOO: maumivu ya tumbo, kichwa, kuwashwa, kutapika damu, moyo kuumwa, ukuaji hafifu, udhaifu na kuchoka

DALILI ZA MINYOO Wakati mwingine ni vigumu sana kujua kama una minyoo, kwani minyoo wanaweza kukaa ndani ya mwili kwa muda mrefu bila ya kuonesha dalili yeyote, ama madhara yeyote.

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa Malengelenge sehemu za siri

Malengelenge sehemu za siri ni maambukizi ya kawaida ya zinaa ambayo huathiri wanaume na wanawake. Makala ya malengelenge sehemu za siri ni pamoja na maumivu, kuwasha na vidonda katika sehemu yako ya uzazi. Lakini huenda usiwe na dalili au ishara za mal

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa kuharisha na sababu zake.

Kuharisha ni Hali ya kupitisha kinyesi Cha maji chenye damu au kisicho na damu

Soma Zaidi...
Dalili na ishara za anemia ya minyoo

Posti hii inshusiana na dalili za anemia ya minyoo

Soma Zaidi...
Dalili za Kuvimbiwa kwa watoto

Posti hii inazungumzia kuhusiana Kuvimbiwa kwa watoto ni tatizo la kawaida.Kuvimbiwa kwa watoto mara nyingi kuna sifa ya kupata haja kubwa mara kwa mara au kinyesi kigumu, kikavu. Sababu mbalimbali zinaweza kusababisha kuvimbiwa kwa watoto.Sababu za kawa

Soma Zaidi...
Dalili za awali za ugonjwa wa kizukari

ugonjwa wa kisukari ni moja katika magonjwa hatari sana, na mpaka sasa bado hauna matibabu ya kuponya moja kwa moja

Soma Zaidi...
Namna ya kuzuia virusi vya ukimwi

Posti hii inaelezea kuhusiana na kujikinga au kuzuia virusi vya ukimwi.

Soma Zaidi...
Matibabu kwa mtu mwenye kiungulia

Posti hii inahusu zaidi matibabu kwa mtu mwenye kiungulia,ni tiba ambayo mtu anapaswa kutumia kama ana tatizo la kiungulia

Soma Zaidi...