Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo baada ya tendo la ndoa
MAUMIVU YA TUMBO BAADA YA TENDO LA NDOA
Mara nyingi maumivu ya tumbo baada ya tendo la ndoa sio tatizo sana kiasi cha kuogopa. Kwani hali hii husababishwa na gesi iliyoppntumboni mama kama uume ulikuwa ukiingia ndani sana, na hii hutokea endapo uume ni mrefu sana ama mtindo uliotumika katika tendo la ndoa. Tatizo la kupatwa na maumivu wakati wa tendo la ndoa ama baada hutambulika kama dyspareunia.
Inakadiriwa kuwa asilimia 10 mapka 20 ya wanawake huweza kusumbuliwa na tatizo hili. Ila pia tatizo hili si kwa wanawake tu hutokea pia kwa wanaume, ila kwa kiasi kidogo yapata lamda asilimia 5. lakini tatizo hili linatibika bila ya wasi hivyo si vyema kuendelea kuteseka.
Sababu za maumivu ya tumbo baada ya tendo la ndoa.Tofauti na sababu ya ya gesi ama uume kuingia ndani sana, tatizo hili linaweza kusababishwa na mambo yafuatayo:-
1.Fikra, hisia na mawazo ya mtu. Hii hutokea kama mtu ana misongo ya mawazo kibao, ama ana woga juu ya tendo la ndoa ama mahusianao yake na ya mwenzie sio mazuri lamada amembaka ama kumlazimisha, haya yote yanaweza kutengeneza mazingira ya kuumwa na tumbo baada ya tendo.
2.Endapo tendo la ndoa litafanyika kwa kiasi kuwa uume uliingia ndani sana. Hii inaweza kusababisha maumivu ya tumbo, ila ni ya muda mfupi na yataweza kuondoka baada ya kupumzika. Ni vyema kubadili mikao ama kupunguza kukandamiza sana uume.
3.Wakati mwingine hali huweza kutokea endapo mwanamke ameingia kileleni. Wakati wa kufika kileleni misuli inayozungukia mfumo wa uzazi, maeneo ya kiunoni na nyonga misuli hii kusinjaa na kujikaza na kusababisha maumivu ya chini ya tumbo. Hali jii kitaalamu hufahamika kama dysorgasmia.
Watu wanaosumbuliwa sana tatizo hili ni:-A.WajawazitoB.Wenye matatizo kwenye ovariC.wenye mashambulizi ya kwenye mfumo wa uzazi (PID)D.Wenye matatizo kwenye korodani.
4.Gesi; wakati wa kupushi uume ndani unaweza kupushi hewa kuingia ndani ya tumbo. Sasa kama hewa hii itanaswa sehmemu humo ndani inaweza kusababisha maumivu ya tumbo kwa juu ama kifuani. Mtu anaweza kuhisia kama gesi inatembea tumboni na maumivu haya yanaweza kuelekea maeneo mengine ya mwili.
5.Kama mtu anasumbuliwa na UTIUTI inaweza kuwa ni katika sababu za maumivu haya. Mtu pia anaweza kuhisi dalili kamaA.Maumivu wakati wa kukojoa kama anaunguaB.Kukojoa mara kwa maraC.Mkojo kuwa mchafuD.Kuwa na damu kwenye mkojoE.Maumivu ya mkundu.
6.Kuwa na maradhi ya ngono kama gonoria na chlamydia. Pia mtu anaweza kuona dalili kama:A.Kutoa harufu mbaya sehemu za siriB.Kutokwa na uchafu sehemu za siriC.Maumivu wakati wa kukojoa
7.Kama mfuko wa uzazi umeinama, hii inaweza kupelekea kuguswa kwa mfukowa uzazi wakati wa tendo la ndoa hivyo kupelekea maumivu
8.Kama kunashida kwenye ovari
9.Kama kuna uvimbe kwenye kizazi. Dalili zake ni kamaA.Kutokwa na damu nyingi wakati wa hedhiB.Hedhi kutokata ndani ya siki 7C.Kukosa chooD.Maumivu ya miguu ama mgongo
10.Kama mirija ya falopia imeziba.
11.Kama mwanaume ana maradhi kwenye mfumo wa uzazi.
?
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Sty ni uvimbe mwekundu, chungu karibu na ukingo wa kope ambalo linaweza kuonekana kama jipu au chunusi. Sties mara nyingi hujazwa na usaha. Mtindo kawaida huunda nje ya kope lako. Lakini wakati mwingine inaweza kuunda kwenye sehemu ya ndani ya kope lak
Soma Zaidi...Poliomyelitis ni kuvimba kwa suala la kijivu la uti wa mgongo na wakati mwingine sehemu ya chini ya ubongo
Soma Zaidi...Je na wewe unasumbukiwa na kunggoka jwa kucha. Tatizo limekunaza una muda gani nalo?
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa upele, ni dalili au mwonekano wa mgonjwa wa upele.
Soma Zaidi...posti hii inazungumzia kuhusiana na Ugonjwa wa kifua kikuu kwa watoto chini ya miaka mitano. Kifua kikuu ni ugonjwa sugu wa kuambukiza na anuwai ya magonjwa ya kliniki yanayosababishwa na Mycobacterium tuberculosis complex.
Soma Zaidi...post hii inazungumzia kuhusiana na Ugonjwa wa kifaduro ambao hujulikana Kama Pertussis pia inajulikana kama kifaduro ni maambukizi ya bakteria ambayo huingia kwenye pua yako na koo.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukuletea orodha ya makunfi ya watu walio hatarini kupata UTI
Soma Zaidi...Ugonjwa wa degedege ni ugonjwa unaowapata sana watoto chini ya miaka mitano ingawa na watu wazima wanapatwa na ugonjwa huo
Soma Zaidi...