picha

Maumivu ya tumbo baada ya tendo la ndoa

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo baada ya tendo la ndoa

MAUMIVU YA TUMBO BAADA YA TENDO LA NDOA

 

Mara nyingi maumivu ya tumbo baada ya tendo la ndoa sio tatizo sana kiasi cha kuogopa. Kwani hali hii husababishwa na gesi iliyoppntumboni mama kama uume ulikuwa ukiingia ndani sana, na hii hutokea endapo uume ni mrefu sana ama mtindo uliotumika katika tendo la ndoa. Tatizo la kupatwa na maumivu wakati wa tendo la ndoa ama baada hutambulika kama dyspareunia.

 

Inakadiriwa kuwa asilimia 10 mapka 20 ya wanawake huweza kusumbuliwa na tatizo hili. Ila pia tatizo hili si kwa wanawake tu hutokea pia kwa wanaume, ila kwa kiasi kidogo yapata lamda asilimia 5. lakini tatizo hili linatibika bila ya wasi hivyo si vyema kuendelea kuteseka.

 

Sababu za maumivu ya tumbo baada ya tendo la ndoa.Tofauti na sababu ya ya gesi ama uume kuingia ndani sana, tatizo hili linaweza kusababishwa na mambo yafuatayo:-

 

1.Fikra, hisia na mawazo ya mtu. Hii hutokea kama mtu ana misongo ya mawazo kibao, ama ana woga juu ya tendo la ndoa ama mahusianao yake na ya mwenzie sio mazuri lamada amembaka ama kumlazimisha, haya yote yanaweza kutengeneza mazingira ya kuumwa na tumbo baada ya tendo.

 

2.Endapo tendo la ndoa litafanyika kwa kiasi kuwa uume uliingia ndani sana. Hii inaweza kusababisha maumivu ya tumbo, ila ni ya muda mfupi na yataweza kuondoka baada ya kupumzika. Ni vyema kubadili mikao ama kupunguza kukandamiza sana uume.

 

3.Wakati mwingine hali huweza kutokea endapo mwanamke ameingia kileleni. Wakati wa kufika kileleni misuli inayozungukia mfumo wa uzazi, maeneo ya kiunoni na nyonga misuli hii kusinjaa na kujikaza na kusababisha maumivu ya chini ya tumbo. Hali jii kitaalamu hufahamika kama dysorgasmia.

 

Watu wanaosumbuliwa sana tatizo hili ni:-A.WajawazitoB.Wenye matatizo kwenye ovariC.wenye mashambulizi ya kwenye mfumo wa uzazi (PID)D.Wenye matatizo kwenye korodani.

 

4.Gesi; wakati wa kupushi uume ndani unaweza kupushi hewa kuingia ndani ya tumbo. Sasa kama hewa hii itanaswa sehmemu humo ndani inaweza kusababisha maumivu ya tumbo kwa juu ama kifuani. Mtu anaweza kuhisia kama gesi inatembea tumboni na maumivu haya yanaweza kuelekea maeneo mengine ya mwili.

 

5.Kama mtu anasumbuliwa na UTIUTI inaweza kuwa ni katika sababu za maumivu haya. Mtu pia anaweza kuhisi dalili kamaA.Maumivu wakati wa kukojoa kama anaunguaB.Kukojoa mara kwa maraC.Mkojo kuwa mchafuD.Kuwa na damu kwenye mkojoE.Maumivu ya mkundu.

 

6.Kuwa na maradhi ya ngono kama gonoria na chlamydia. Pia mtu anaweza kuona dalili kama:A.Kutoa harufu mbaya sehemu za siriB.Kutokwa na uchafu sehemu za siriC.Maumivu wakati wa kukojoa

 

7.Kama mfuko wa uzazi umeinama, hii inaweza kupelekea kuguswa kwa mfukowa uzazi wakati wa tendo la ndoa hivyo kupelekea maumivu

 

8.Kama kunashida kwenye ovari

 

9.Kama kuna uvimbe kwenye kizazi. Dalili zake ni kamaA.Kutokwa na damu nyingi wakati wa hedhiB.Hedhi kutokata ndani ya siki 7C.Kukosa chooD.Maumivu ya miguu ama mgongo

 

10.Kama mirija ya falopia imeziba.

 

11.Kama mwanaume ana maradhi kwenye mfumo wa uzazi.

 

?

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 4223

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi     👉2 Simulizi za Hadithi Audio     👉3 Dua za Mitume na Manabii     👉4 ai web app     👉5 Madrasa kiganjani     👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    

Post zinazofanana:

Yajue magonjwa ya kurithi.

Posti hii inahusu zaidi Magonjwa vya kurithi ambayo mara nyingi utokea kwenye jamii ni magonjwa ambayo yanaweza kutokea kwenye familia na wanafamilia walio wengi wakaweza kupata ugonjwa huo Magonjwa yenyewe ni kama ifuatavyo.

Soma Zaidi...
Tetekuwanga kwa watu wazima: Ni hatari zaidi?

Tetekuwanga (Varicella) kwa kawaida huchukuliwa kama ugonjwa wa utotoni, na watoto wengi huupata na kupona bila matatizo makubwa. Hata hivyo, unapoupata ukiwa mtu mzima, hali inabadilika. Tetekuwanga kwa watu wazima huchukuliwa kuwa na hatari zaidi, ikiwa na uwezekano mkubwa wa kusababisha dalili kali na maambukizi ya viungo muhimu kama mapafu. Makala haya yanafafanua kwa nini hali hii ni hatari na nini unapaswa kufanya.

Soma Zaidi...
Maambukizi kwenye mifupa

Posti hii inahusu zaidi Maambukizi kwenye mifupa ambayo kwa kitaalamu huitwa Osteomyelitis, ugonjwa huu uaribu zaidi kwenye mifupa na sehemu nyingine ambazo zinakaribia kwenye mifupa

Soma Zaidi...
Sababu za Kupungua kwa Hamu ya Mapenzi

Makala hii inachunguza kwa kina sababu zinazosababisha kupungua kwa hamu ya tendo la ndoa (Low Libido). Tutaangalia vipengele vya kimwili, kisaikolojia, na mtindo wa maisha vinavyoweza kuathiri hali hii, pamoja na ukweli wa kisayansi kuhusu tatizo hili na hatua za kuchukua ili kuboresha afya ya mahusiano.

Soma Zaidi...
Maambukizi kwenye mrija wa mkojo(urethritis )

Posti hii inahusu zaidi maambukizi kwenye mrija wa mkojo, maambukizi haya usababishwa na virusi na bakteria.

Soma Zaidi...
Dalili za saratani ya tishu (leukemia)

Posti hii inazungumzia kuhusiana na saratani za tishu ambazo kitaalamu hujulikana Kama Leukemia kawaida huhusisha seli nyeupe za damu. Seli zako nyeupe za damu ni wapiganaji hodari wa maambukizo - kwa kawaida hukua na kugawanyika kwa utaratibu, kadri mwi

Soma Zaidi...