picha

Presha ya kushuka na matibabu yake

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu presha ya kushuka na matibabu yake

PRESHA YA KUSHUKA NA MATIBABU YAKE

 

Presha ya kushuka mara nyingi haina dalili za kutisha, pia haina shida sana ukilingnisha na presha ya kupanda. Kama unahisi dalili za presha ya kushuka kama kizunguzungu, kichwa kuwa chepesi wakati unaposimama na kuamka, huku mgandamizo wa damu kupunguwa hii hali inatambulika kama postural hypotension.

 

Kugundua presha ya kushuka daktari atakupima kwa kipimo maalumu. Pia vipo vipimo vngine kama vitahitajika zaidi, kama vile electrocardiogram (ECG), ultrasound pia kipimo cha damu kuangalia kiwango cha sukari kwenye damu na kuangalia kama kuna upungufu wa damu.

 

Utaratibu wa kuishi ukiwa na presha ya kushuka.Ningependa tu kukujulisha kuwa unaweza kuishi vyema ukiwa na presha ya kushuka, hata bila ya kutumia dawa za mahospitali. Kabla hatujaona dawa za mahospitali sasa nanakwenda kukueleza utaratibu wa lishe kwa mwenye prsha ya kushuka.

 

1.Kula chakula chenye chumvi zaidi2.Kula vyakula vyenye majimaji mengi kama matunda na mfano wake3.Punguza kunywa vilevi4.Kunywa maji mengi hasa wakati wa joto5.Fanya mazoezi ya mara kwa mara6.Unapolala tumia mto, yaani sehemu ya kichwa chako iwe juu7.Jizuie kubeba vitu vizito8.Washa kukaa maeneo yenye joto sana ma kuoga maji ya moto kwa muda mrefu.9.Acha kusimama wima sehemu moja kwa muda mrefu.

 

Dawa zinazotumika kutibu presha ya kushuka (hypotension)A.Fludrocortisone, zungumza na daktari kabla ya kutumiadawa hii.B.Midodrine.

 

Hakikisha dawa hizi humezi kiholela. Kabla ya kutumia dawa yeyote kwanza zungumza na daktari kwanza. Hii ni kwa ajili ya afya yako.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 1814

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 Bongolite - Game zone - Play free game     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 ai web app     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

Tatizo la kutokwa na damu baada ya tendo la ndoa.

Kutokwa na damu baada ya tendo la ndoa (post-coital bleeding) ni hali inayoweza kuleta hofu kwa wanawake wengi. Ingawa mara nyingi sababu zake si za kutisha, ni muhimu kuelewa visababishi mbalimbali vinavyoweza kuashiria matatizo ya kiafya yanayohitaji matibabu. Makala hii inachunguza kwa kina sababu za kibiolojia, maambukizi, na magonjwa yanayoweza kusababisha hali hii, ikitoa mwongozo wa wakati wa kumwona daktari.

Soma Zaidi...
Nini kinasababisha kizunguzungu?

Posti hii inaelezea kuhusiana na dalili za kizunguzungu zinazotekea katika mwili wa binadamu

Soma Zaidi...
Madhara ya utapia mlo (marasmus)

Utapiamlo Mkali sana (Marasmus) hufafanuliwa kama aina kali ya utapiamlo ambayo ina sifa ya kupoteza. Utapiamlo uliokithiri umeainishwa katika Utapiamlo Mkali sana (SAM) na Utapiamlo Uliokithiri wa Wastani (MAM), kulingana na kiwango cha kupoteza na kuw

Soma Zaidi...
Fahamu kuhusu magonjwa yasiyoambukizwa

Post hii inahusu magonjwa yasiyo ya kuambukizwa,haya ni magonjwa ambayo hayawezi kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda mwingine

Soma Zaidi...
Kupunguzwa kwa kiwosi cha lehemu (Cholesterol) mwilini.

Lehemu (cholesterol) ni kiambato muhimu katika mwili wa binadamu, lakini kiwango chake kinapozidi kiasi kinachohitajika, huwa hatari kubwa kwa mfumo wa moyo na mishipa ya damu. Makala hii inatoa uchambuzi wa kitaalamu kuhusu taratibu za kupunguza lehemu mbaya (LDL), umuhimu wa uwiano wa lehemu nzuri (HDL), na mikakati ya kisayansi ya kudhibiti lehemu kupitia lishe, mazoezi, na dawa.

Soma Zaidi...
Dalili na Ishara za upungufu wa muunganisho wa macho.

posti hii inaonyesha dalili za upungufu wa muunganisho wa macho. Upungufu wa muunganisho hutokea wakati macho yako hayafanyi kazi pamoja unapojaribu kuangazia kitu kilicho karibu nawe. Unaposoma au kutazama kitu kilicho karibu, macho yako yanahitaji k

Soma Zaidi...