Faida za Mchaichai (lemongrass)

Majani haya hutumika kama mbadala wa majani ya chai. Yana harufu nzuri na rangia ya kuvutia pindi yakitumiwa kama mbadala wa majani ya chai.

  1. husaiadia katika kuboresha mfumo wa meng’enyo wa chakula
  2. Mchaichai una virutubisho kama vitamini C na A, pia una madini
  3. Hutumika kama dawa ya kukosa choo, kujaa kwa gesi na kuvimbiwa
  4. Husaidia kutoa sumu mwilini
  5. Husaidia katika kudhibiti presha ya damu na kuishusha
  6. Husaidia katika kusafisha ini
  7. Huboresha afya ya moyo.
  8. Husaidia katika uunguzwaji wa fati na mafuta mwilini
  9. Huimarisha na kuboresha afya ya ngozi na nywele
  10. Husaidia katika kutibu mafua na homa ya mafua
  11. Hupunguza maumivu ya chango la kinamama.