Mbinu za Mtume Salih(a.s) Katika Kulingania Uislamu

Kama Mitume waliotangulia, Nabii Salih(a.

Mbinu za Mtume Salih(a.s) Katika Kulingania Uislamu

Mbinu za Mtume Salih(a.s) Katika Kulingania Uislamu


Kama Mitume waliotangulia, Nabii Salih(a.s) naye kwa kuzingatia mazingira ya watu wake, alitumia mbinu zifuatazo katika kuulingania Uislamu:



Kwanza, alijieleza kwa uwazi kuwa yeye ni Mtume wa Allah(s.w)



โ€œBila shaka mimi kwenu ni Mtume mwaminifu.โ€ (26:143)

Pili, aliwakumbusha watu wake neema za Allah(s.w) zilizo juu yao ili waone umuhimu wa kumshukuru na kumuabudu ipasavyo:




โ€œNa kumbukeni (Mwenyezi Mungu) alivyokufanyeni makhalifa baada ya โ€˜Ad na kukuwekeni vizuri katika ardhi mnajenga majumba makubwa ya kifalme katika nyanda zake, na mnachonga majumba katika majabali (yake). Basi zikumbukeni neema za Mwenyezi Mungu, wala msifisidi katika ardhi kwa kufanya uharibifu.โ€ (7:74)



โ€œJe (mnafikiri kuwa) mtaachwa salama katika haya yaliyopo hapa (kwenu):โ€ โ€œKatika mabustani na chemchem, (mito).โ€ โ€œNa mimea na mitende yenye makole mazuri.โ€ โ€œNa mnachonga milimani majumba mkistarehe tu basi.โ€ (26:146-149)



Tatu, aliwanasihi na kuwasisitiza watu wake wamche Allah(s.w)
na kumtii yeye badala ya kuwatii watu:



โ€œMcheni Allah na mtiini. Wala msitii amri za wale maasi (wenye kupindukia mipaka ya Allah). Ambao wanafanya uharibifu tu katika ardhi wala hawaitengenezi.โ€ (26:150-152)

Nne,alisisitiza kutohitajia ujira kwa watu wake, kama walivyozoea kutoa ujira kwa viongozi wao kwa ajili ya manufaa na starehe zao binafsi.



โ€œWala sikutakini ujira juu yake, ujira wangu hauko ila kwa Mola wa walimwengu wote.โ€ (26:145)

Tano, alionyesha muujiza wa jabali kuzaa ngamia jike kama dalili za Utume wake baada ya watu wake kumtaka afanye hivyo kwa uwezo wa Allah(s.w).



Akasema: โ€œEnyi watu wangu! Mnaonaje, kama ninazo dalili zilizo wazi zitokazo kwa Mola wangu (za kunionyesha ukweli wa haya), naye amenipa rehema kutoka kwake, basi ni nani atakayeninusuru kwa Mwenyezi Mungu kama nikimuasi? Basi hamtanizidishia kwa hayo mnayonitakia ila khasara.(11:63)



Enyi watu wangu! Huyu ngamia wa Mwenyezi Mungu ni Ishara kwenu (mliyoitaka kwangu ili kuonyesha ukweli wa Utume wangu). Basi muacheni ale katika ardhi ya Mwenyezi Mungu; wala msimguse kwa ubaya isije ikakuangamizeni adhabu iliyo karibu (na kukufikieni).โ€ (11:64)



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 1214

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Bongolite - Game zone - Play free game    ๐Ÿ‘‰2 Kitabu cha Afya    ๐Ÿ‘‰3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    ๐Ÿ‘‰4 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰5 Simulizi za Hadithi Audio    ๐Ÿ‘‰6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana: