Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Ismail(a.s)
Kutokana na Historia ya Nabii Ismail(a.
Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Ismail(a.s)
Kutokana na Historia ya Nabii Ismail(a.r) tunajifunza yafuatayo:
(i) Kila Muislamu anatakiwa kumuomba Allah(s.w) amruzuku mtoto mwema atakayesaidia kupeleka mbele harakati za kuhuisha na kusimamisha Uislamu katika jamii.
(ii) Mtoto mwema anayependwa na Allah(s.w) ni yule anayewatii wazazi wake katika mambo ya kheri.
(iii) Mtoto mwema hujitahidi kushiriki katika harakati za kuusimamisha Uislamu katika jamii.
(iv) Amri ya pili ya Allah(s.w) inayotukabili baada ya ile ya kusoma(kutafuta elimu) ni kusimamisha swala na kutoa katika vile Allah(s.w) alivyoturuzuku, kisha kuamrisha familia zetu na jamaa zetu wa karibu kufanya hivyo kisha tuilinganie jamii nzima kufanya hivyo.
(v) Kusema kweli na kutekeleza ahadi ni katika tabia njema anayoiridhia Allah(s.w).
(vi) Inatupasa kumuomba Allah(s.w) atupe yaliyo mema katika kila jambo tunalolikusudia kufanya.
(vii) Kuwa tayari kutoa nafsi zetu kwa ajili ya Allah(s.w)kama alivyokuwa tayari Ismail(a.s) kuchinjwa na baba yake katika kutekeleza amri ya Allah(s.w)
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Simulizi za Hadithi Audio 👉2 web hosting 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 kitabu cha Simulizi 👉6 Dua za Mitume na Manabii
Post zinazofanana:
Msimamo wa Nabii Hud(a.s) Dhidi ya Makafiri wa Kaumu Yake
Pamoja na kwamba alipingwa na nguvu za Dola ya makafiri wa kaumu yake, Mtume Hud(a.
Soma Zaidi...Mateso waliyoyapata waislamu wa mwanzo Maka, na orodha ya waislamu walioteswa vikali
Pili, Maquraish walimuendea Mtume(s.
Soma Zaidi...