picha

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Ismail(a.s)

Kutokana na Historia ya Nabii Ismail(a.

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Ismail(a.s)

Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Ismail(a.s)


Kutokana na Historia ya Nabii Ismail(a.r) tunajifunza yafuatayo:

(i) Kila Muislamu anatakiwa kumuomba Allah(s.w) amruzuku mtoto mwema atakayesaidia kupeleka mbele harakati za kuhuisha na kusimamisha Uislamu katika jamii.



(ii) Mtoto mwema anayependwa na Allah(s.w) ni yule anayewatii wazazi wake katika mambo ya kheri.



(iii) Mtoto mwema hujitahidi kushiriki katika harakati za kuusimamisha Uislamu katika jamii.



(iv) Amri ya pili ya Allah(s.w) inayotukabili baada ya ile ya kusoma(kutafuta elimu) ni kusimamisha swala na kutoa katika vile Allah(s.w) alivyoturuzuku, kisha kuamrisha familia zetu na jamaa zetu wa karibu kufanya hivyo kisha tuilinganie jamii nzima kufanya hivyo.



(v) Kusema kweli na kutekeleza ahadi ni katika tabia njema anayoiridhia Allah(s.w).



(vi) Inatupasa kumuomba Allah(s.w) atupe yaliyo mema katika kila jambo tunalolikusudia kufanya.



(vii) Kuwa tayari kutoa nafsi zetu kwa ajili ya Allah(s.w)kama alivyokuwa tayari Ismail(a.s) kuchinjwa na baba yake katika kutekeleza amri ya Allah(s.w)



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 2018-08-01 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 2145

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 ai web app    πŸ‘‰2 Simulizi za Hadithi Audio    πŸ‘‰3 kitabu cha Simulizi    πŸ‘‰4 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰5 web hosting    πŸ‘‰6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina   

Post zinazofanana:

Si Yesu Aliyesulubiwa (yesu hakufa msalabani wala hakusulubiwa

Katika Qur,an tukufu, Mwenyezi Mungu aliye muweza na mjuzi wa mambo anathibitisha kuwa aliyesulubiwa si Nabii Isa(a.

Soma Zaidi...
Historia ya Watoto Wawili wa Nabii Adam

β€œNa wasomee khabari za watoto wawili wa Adam kwa kweli, walipotoa sadaka, ikakubaliwa ya mmoja wao na ya mwingine haikukubaliwa Akasema (yule asiyekubaliwa sadaka yake): β€œNitakuua”.

Soma Zaidi...
Vita vya Al Fijar na sababu zake

Historia na shida ya Mtume Muhammad S.A.W, sehemu ya 12. Hapa utajifunza kuhusu kutokea kwa vita vya al fijar.

Soma Zaidi...