Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maradhi ya macho,dalili na matibabu yake
MARADHI YA MACHO
Matatizo ya macho yapo mengi katika jamii, lakini mara nyingi matatizo ya macho yanatibika iwapo mgonjwa ataonana na daktari mara atakapoona dalili. Miongoni mwa matatizo ya macho ni kupoteza uwezo wa kuona.
1.Kutoona karibu (long sightedness)Tatizo hili mara nyingi huwatokea watu wenye umri wa miaka 40 na kuendelea.
DaliliA.Katika mazingira ya kawaida anaona sawa sawaB.Kushindwa kusoma herufi ndogo ndogoC.Kushindwa kufanya kazi za sehemu ndogo ndogo mfano kutunga sindano.
Matibabu: Kutumia miwani ya kusomea.
2.Kutoona Mbali (short sightedness)A.Hayana umri maalumB.Myopia – haoni mbali vizuriC.Hyperopia – haoni mbali na kichwa kinauma akikosa kuvaa miwani yenye namba ndogo kusaidia lense.
NB: Mgonjwa anasoma karibu bila miwaniMatibabu: Kutumia miwani ya kuonea mbali
3.Mtoto wa Jicho (cataract)DaliliA.Kidoto cheupe katikati ya kioo cheusi cha jicho (kinafunika mboni ya jicho)B.Kidoto cheupe kisichobadilika kwa mwangazaC.Kupunguza nuru ya macho
NB - Mtu anaweza kuzaliwa nacho au kupata ukubwani, inaweza kuwa kwenye jicho moja au yote. Mgonjwa huona mchanganyiko wa rangi anapoangalia mwangaza kama taa za umeme au gari.
MatibabuMtoto wa Jicho huwa anatibika kwa upasuaji mdogo na kumuwezesha mgonjwa kuona tena.
4.Presha ya macho (glaucoma)Tatizo hili husababishwa na kuongezeka presha ya jicho (intraocular pressure) kutokana na kukosekana uwiano wa mzunguko wa majimaji ndani ya jicho (aqueous fluid) kinachotoka kidogo kuliko kinachoingia.
MatokeoGlaucoma hukandamiza na kuuharibu mshipa wa fahamu ya jicho na kusababisha kupungua kwa nuru na baadae kupoteza nuru ya macho.
Matibabu: Kuonana na daktari kwa ushauri na dawa
5.Macho tongoHutokea ama kwa mtu mmoja mmoja, makundi au kwa msimu.
Sababu:Vimelea ambavyo huzaliwa kwenye sehemu za uchafu Wakati wa msimu huambukiza kwa kukosa elimu ya afya, kwa mfano kutokuosha mikono baada ya kuamkiana na mgonjwa mwenye maradhi haya au kutumia vifaa vya macho kwa zaidi ya mtu mmoja kama vile miwani.
DaliliA.Kuhisi kama kuna mchanga ndani ya jichoB.Kuvimba mifuniko ya macho bila kupoteza nuru.C.Macho kuwa mekundu sana (conjuctivitis)D.Kutoka tongo kila mara
MatibabuMgonjwa atumie dawa alizoandikiwa na daktari tu, kwani dawa za matone za macho ni nyingi na zina kazi tofauti.
6.Matatizo ya sehemu nyeusi ya jicho (cornea)Kuna matatizo manne makubwa1. Kovu - kidoto/kibaka cheupe2. Kidonda - kidoto kijivujivu3. Kuingiwa na kitu - kemikali,mdudu, vumbi n.k4. Kutoboka na kutoa maji.Indhari: hali ya pili mpaka ya nne zikitokea mgonjwa akimbizwehospital wakati jicho limefunikwa baada ya huduma ya kwanza
DaliliKOVU1.Haina maumivu2.Jicho haliwi jekundu3.Jicho halivimbi4.kupungua nuru jicho
KIDONDAA.Kinayo maumivuB.Jicho lililoathirika huwaC.jekunduD.Jicho kupunguka nuruE.Kuuma jicho kwenyeF.mwangazaG.Kutoka machoziH.Jicho kuvimba
Kidonda kinaweza kusababishwa na bakteria, fangas, ukosefu wa vitamin A au kwa kuumia mfano; kujichoma na kitu chenye ncha au kitu kigumu, kuingiwa na kitu jichoni, kuungua au kuingia kemikali jichon.
Indhari: Iwapo jicho litaumia lifunike jicho lisipate mwangaza kisha mpeleke mgonjwa hospitali.
7. Kemikali na kuunguaKama mgonjwa ameingia kemikali kama vile acid, alkali, saruji, chokaa mtie maji ya mchuruziko kwa takriban dakika 15 mfululizo na baadae mpeleke hospitali
8.Macho kuwasha na kutokwa na machozi (conjuctivitis)Huwakumba zaidi watoto wa umri kati ya miaka 5 -15 ambao hupendelea kucheza sehemu za vumbi au kwenye muangaza mkali (pwani yenye mchanga mweupe sana)
Watu wazima wenye kufanya kazi kwenye viwanda vinavozalisha vumbi, na wenye pumu ya muda mrefu.
DaliliA.Macho kuwasha (Nuru ya macho haipungui)B.Macho kubadilika rangi (kahawia)C.Kutokwa na machozi mengi (sana)D.Kushindwa kuangalia kwenye muangaza mkali
MatibabuKusafisha macho mara kwa mara kwa maji safi.Kutumia dawa kwa maelekezo ya daktari
9.Kinundu katika mfuniko wa juu au chini wa jicho
DALILIA.Kinundu kisichoumaB.Mara nyingi hupona wenyewe au unaweza kukikanda kwa maji ya uvuguvugu.C.Kisipopona au kitakapokuwa kikubwa huhitaji upasuaji mdogo.
10.Uvimbe katika mfuniko wa jicho (cellulitis)
A.uvimbe kwenye mifuniko ya jichoB.inaweza kuzuwia jicho kucheza (kutembea tembea)C.mara nyingi hutokea baada ya kusambaa kwa maambukizoD.ya socket ya jicho kutoka pembezoni kwa saines (sinusitis) za puaE.husababisha kupoteza nuru za macho
Matibabu: Mpeleke mgonjwa kwa daktari wa masikio, pua na koo (ENT)
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowUmeionaje Makala hii.. ?
Tetekuwanga (varisela) ni maambukizi ya virusi ambayo husababisha kuwasha, upele kama vile malengelenge. Tetekuwanga huambukiza sana watu ambao hawajapata ugonjwa huo wala kupewa chanjo dhidi yake. Kabla ya chanjo ya kawaida ya tetekuwanga, karibu watu
Soma Zaidi...Posti hii inaelezea kuhusiana na dalili za kizunguzungu zinazotekea katika mwili wa binadamu
Soma Zaidi...Post hii inahusu Zaidi tatizo la kuwepo Kwa usaha kwenye mapafu,ni tatizo ambalo usababishwa na bakteria ambao uingia kwenye mapafu na kusababisha madhara na hatimaye mapafu kuwa na usaha .
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi sababu za kufanya figo kuharibika.hili ni janga ambalo linawakumba Watu wengi siku hizi na kusababisha kupoteza maisha kwa wagonjwa wa figo hasa hasa kwa wale ambao hawana uwezo wa kulipia hela ya kusafishia figo.
Soma Zaidi...Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu sababu za maumivu ya tumbo chini upande wa kushoto
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia kuhusiana na Saratani ambayo hutokea katika aina ya seli nyeupe ya damu inayoitwa seli ya plasma. Seli za plasma hukusaidia kupambana na maambukizo kwa kutengeneza kingamwili zinazotambua na kushambulia vijidudu. Pia husababish
Soma Zaidi...Shinikizo la chini la damu (hypotension) litaonekana kuwa jambo la kujitahidi. Hata hivyo, kwa watu wengi, shinikizo la chini la damu linaweza kusababisha dalili za Kizunguzungu na kuzirai. Katika hali mbaya, shinikizo la chini la damu linawez
Soma Zaidi...DAWA MBADALA ZA VIDONDA VYA TUMBO Dawa za kukabiliana na zaidi ambazo zina calcium carbonate (Tums, Rolaids), zinaweza kusaidia kutibu vidonda vya tumbo lakini hazipaswi kutumiwa kama matibabu ya msingi.
Soma Zaidi...