Maradhi ya macho

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maradhi ya macho,dalili na matibabu yake

MARADHI YA MACHO

Matatizo ya macho yapo mengi katika jamii, lakini mara nyingi matatizo ya macho yanatibika iwapo mgonjwa ataonana na daktari mara atakapoona dalili. Miongoni mwa matatizo ya macho ni kupoteza uwezo wa kuona.

 

1.Kutoona karibu (long sightedness)Tatizo hili mara nyingi huwatokea watu wenye umri wa miaka 40 na kuendelea.

 

DaliliA.Katika mazingira ya kawaida anaona sawa sawaB.Kushindwa kusoma herufi ndogo ndogoC.Kushindwa kufanya kazi za sehemu ndogo ndogo mfano kutunga sindano.

 

Matibabu: Kutumia miwani ya kusomea.

2.Kutoona Mbali (short sightedness)A.Hayana umri maalumB.Myopia – haoni mbali vizuriC.Hyperopia – haoni mbali na kichwa kinauma akikosa kuvaa miwani yenye namba ndogo kusaidia lense.

 

NB: Mgonjwa anasoma karibu bila miwaniMatibabu: Kutumia miwani ya kuonea mbali

 

3.Mtoto wa Jicho (cataract)DaliliA.Kidoto cheupe katikati ya kioo cheusi cha jicho (kinafunika mboni ya jicho)B.Kidoto cheupe kisichobadilika kwa mwangazaC.Kupunguza nuru ya macho

 

NB - Mtu anaweza kuzaliwa nacho au kupata ukubwani, inaweza kuwa kwenye jicho moja au yote. Mgonjwa huona mchanganyiko wa rangi anapoangalia mwangaza kama taa za umeme au gari.

 

MatibabuMtoto wa Jicho huwa anatibika kwa upasuaji mdogo na kumuwezesha mgonjwa kuona tena.

 

4.Presha ya macho (glaucoma)Tatizo hili husababishwa na kuongezeka presha ya jicho (intraocular pressure) kutokana na kukosekana uwiano wa mzunguko wa majimaji ndani ya jicho (aqueous fluid) kinachotoka kidogo kuliko kinachoingia.

 

MatokeoGlaucoma hukandamiza na kuuharibu mshipa wa fahamu ya jicho na kusababisha kupungua kwa nuru na baadae kupoteza nuru ya macho.

 

Matibabu: Kuonana na daktari kwa ushauri na dawa

 

5.Macho tongoHutokea ama kwa mtu mmoja mmoja, makundi au kwa msimu.

 

Sababu:Vimelea ambavyo huzaliwa kwenye sehemu za uchafu Wakati wa msimu huambukiza kwa kukosa elimu ya afya, kwa mfano kutokuosha mikono baada ya kuamkiana na mgonjwa mwenye maradhi haya au kutumia vifaa vya macho kwa zaidi ya mtu mmoja kama vile miwani.

 

DaliliA.Kuhisi kama kuna mchanga ndani ya jichoB.Kuvimba mifuniko ya macho bila kupoteza nuru.C.Macho kuwa mekundu sana (conjuctivitis)D.Kutoka tongo kila mara

 

MatibabuMgonjwa atumie dawa alizoandikiwa na daktari tu, kwani dawa za matone za macho ni nyingi na zina kazi tofauti.

 

6.Matatizo ya sehemu nyeusi ya jicho (cornea)Kuna matatizo manne makubwa1. Kovu - kidoto/kibaka cheupe2. Kidonda - kidoto kijivujivu3. Kuingiwa na kitu - kemikali,mdudu, vumbi n.k4. Kutoboka na kutoa maji.Indhari: hali ya pili mpaka ya nne zikitokea mgonjwa akimbizwehospital wakati jicho limefunikwa baada ya huduma ya kwanza

 

DaliliKOVU1.Haina maumivu2.Jicho haliwi jekundu3.Jicho halivimbi4.kupungua nuru jicho

 

KIDONDAA.Kinayo maumivuB.Jicho lililoathirika huwaC.jekunduD.Jicho kupunguka nuruE.Kuuma jicho kwenyeF.mwangazaG.Kutoka machoziH.Jicho kuvimba

 

Kidonda kinaweza kusababishwa na bakteria, fangas, ukosefu wa vitamin A au kwa kuumia mfano; kujichoma na kitu chenye ncha au kitu kigumu, kuingiwa na kitu jichoni, kuungua au kuingia kemikali jichon.

 

Indhari: Iwapo jicho litaumia lifunike jicho lisipate mwangaza kisha mpeleke mgonjwa hospitali.

 

7. Kemikali na kuunguaKama mgonjwa ameingia kemikali kama vile acid, alkali, saruji, chokaa mtie maji ya mchuruziko kwa takriban dakika 15 mfululizo na baadae mpeleke hospitali

 

8.Macho kuwasha na kutokwa na machozi (conjuctivitis)Huwakumba zaidi watoto wa umri kati ya miaka 5 -15 ambao hupendelea kucheza sehemu za vumbi au kwenye muangaza mkali (pwani yenye mchanga mweupe sana)

 

Watu wazima wenye kufanya kazi kwenye viwanda vinavozalisha vumbi, na wenye pumu ya muda mrefu.

 

DaliliA.Macho kuwasha (Nuru ya macho haipungui)B.Macho kubadilika rangi (kahawia)C.Kutokwa na machozi mengi (sana)D.Kushindwa kuangalia kwenye muangaza mkali

 

MatibabuKusafisha macho mara kwa mara kwa maji safi.Kutumia dawa kwa maelekezo ya daktari

 

9.Kinundu katika mfuniko wa juu au chini wa jicho

 

DALILIA.Kinundu kisichoumaB.Mara nyingi hupona wenyewe au unaweza kukikanda kwa maji ya uvuguvugu.C.Kisipopona au kitakapokuwa kikubwa huhitaji upasuaji mdogo.

 

10.Uvimbe katika mfuniko wa jicho (cellulitis)

 

A.uvimbe kwenye mifuniko ya jichoB.inaweza kuzuwia jicho kucheza (kutembea tembea)C.mara nyingi hutokea baada ya kusambaa kwa maambukizoD.ya socket ya jicho kutoka pembezoni kwa saines (sinusitis) za puaE.husababisha kupoteza nuru za macho

 

Matibabu: Mpeleke mgonjwa kwa daktari wa masikio, pua na koo (ENT)

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 3038

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 web hosting    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Dua za Mitume na Manabii    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Vidonda vya tumbo chanzo chake na dalili zake

Katika post hii utajifunz akuhusu vidonda vya tumbo na jinsi vinavyotokea. Utajifunza pia tahadhari anazopasa mtu achukuwe na vyakula salama anavyopaswa kula.

Soma Zaidi...
Fangasi wanaojulikana kama Blastomyces

Fangasi wanaojulikana kama Blastomyces, hawa ni fangasi wanaosababisha maradhi yajulikanayo kama blastomycosis.

Soma Zaidi...
Athari za Ugonjwa wa herpes simplex kwa watoto wadogo.

Posti hii inahusu zaidi athari za Ugonjwa wa herpes simplex kwa watoto wadogo, tunajua kubwa mama kama ana ugonjwa huu anaweza kumwambikiza mtoto na mtoto akazaliwa na Ugonjwa huu.

Soma Zaidi...
Sababu za mngurumo wa moyo

Mngurumo wa moyo ni sauti wakati wa mzunguko wa mapigo ya moyo wako kama vile kutetemeka inayotolewa na damu yenye msukosuko ndani au karibu na moyo wako. Sauti hizi zinaweza kusikika na kifaa kinachojulikana kama stethoscope. Mapigo ya moyo ya kawaida

Soma Zaidi...
DALILI ZA UTUMBO KUZIBA

Kuziba kwa utumbo ni kuziba kwa chakula au kimiminika kisipite kwenye utumbo mwembamba au utumbo mpana (colon). Kuziba kwa matumbo kunaweza kusababishwa na mikanda ya nyuzi kwenye fumbatio ambayo huunda baada ya upasuaji, mifuko iliyovimba au iliyoambuk

Soma Zaidi...
UGNJWA WA UTI

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
Ugonjwa wa UTI

Somo Hili linakwenda kukueleza kuhusu ugonjwa wa UTI

Soma Zaidi...
Dalili za maambukizi ya sikio kwa watu wazima

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Maambukizi ya sikio mara nyingi ni maambukizi ya bakteria au virusi ambayo huathiri sikio la kati, nafasi iliyojaa hewa nyuma ya ngoma ya sikio ambayo ina mifupa midogo ya sikio inayotetemeka. Maambukizi ya si

Soma Zaidi...
Kivimba kwa mishipa ya Damu

Posti hii inaelezea kuhusiana na Ugonjwa wa kuvimba kwa mishipa yako ya damu. Inasababisha mabadiliko katika kuta za mishipa ya damu, ikiwa ni pamoja na kuimarisha, kudhoofisha, kupungua na kupungua. Mabadiliko haya huzuia mtiririko wa damu, na kusababi

Soma Zaidi...
Sababu za Kutokwa Damu moja kwa moja bila kuganda (hemophilia).

Posti hii inaelezea kuhusiana na Damu kutokuganda ambalo hujulikana Kama Hemophilia, ni ugonjwa nadra ambapo damu yako haigandi kawaida kwa sababu haina protini za kutosha za kuganda. Ikiwa una tatizo la Damu kutokuganda, unaweza kuvuja damu kwa muda mre

Soma Zaidi...