picha

Maradhi ya macho

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maradhi ya macho,dalili na matibabu yake

MARADHI YA MACHO

Matatizo ya macho yapo mengi katika jamii, lakini mara nyingi matatizo ya macho yanatibika iwapo mgonjwa ataonana na daktari mara atakapoona dalili. Miongoni mwa matatizo ya macho ni kupoteza uwezo wa kuona.

 

1.Kutoona karibu (long sightedness)Tatizo hili mara nyingi huwatokea watu wenye umri wa miaka 40 na kuendelea.

 

DaliliA.Katika mazingira ya kawaida anaona sawa sawaB.Kushindwa kusoma herufi ndogo ndogoC.Kushindwa kufanya kazi za sehemu ndogo ndogo mfano kutunga sindano.

 

Matibabu: Kutumia miwani ya kusomea.

2.Kutoona Mbali (short sightedness)A.Hayana umri maalumB.Myopia – haoni mbali vizuriC.Hyperopia – haoni mbali na kichwa kinauma akikosa kuvaa miwani yenye namba ndogo kusaidia lense.

 

NB: Mgonjwa anasoma karibu bila miwaniMatibabu: Kutumia miwani ya kuonea mbali

 

3.Mtoto wa Jicho (cataract)DaliliA.Kidoto cheupe katikati ya kioo cheusi cha jicho (kinafunika mboni ya jicho)B.Kidoto cheupe kisichobadilika kwa mwangazaC.Kupunguza nuru ya macho

 

NB - Mtu anaweza kuzaliwa nacho au kupata ukubwani, inaweza kuwa kwenye jicho moja au yote. Mgonjwa huona mchanganyiko wa rangi anapoangalia mwangaza kama taa za umeme au gari.

 

MatibabuMtoto wa Jicho huwa anatibika kwa upasuaji mdogo na kumuwezesha mgonjwa kuona tena.

 

4.Presha ya macho (glaucoma)Tatizo hili husababishwa na kuongezeka presha ya jicho (intraocular pressure) kutokana na kukosekana uwiano wa mzunguko wa majimaji ndani ya jicho (aqueous fluid) kinachotoka kidogo kuliko kinachoingia.

 

MatokeoGlaucoma hukandamiza na kuuharibu mshipa wa fahamu ya jicho na kusababisha kupungua kwa nuru na baadae kupoteza nuru ya macho.

 

Matibabu: Kuonana na daktari kwa ushauri na dawa

 

5.Macho tongoHutokea ama kwa mtu mmoja mmoja, makundi au kwa msimu.

 

Sababu:Vimelea ambavyo huzaliwa kwenye sehemu za uchafu Wakati wa msimu huambukiza kwa kukosa elimu ya afya, kwa mfano kutokuosha mikono baada ya kuamkiana na mgonjwa mwenye maradhi haya au kutumia vifaa vya macho kwa zaidi ya mtu mmoja kama vile miwani.

 

DaliliA.Kuhisi kama kuna mchanga ndani ya jichoB.Kuvimba mifuniko ya macho bila kupoteza nuru.C.Macho kuwa mekundu sana (conjuctivitis)D.Kutoka tongo kila mara

 

MatibabuMgonjwa atumie dawa alizoandikiwa na daktari tu, kwani dawa za matone za macho ni nyingi na zina kazi tofauti.

 

6.Matatizo ya sehemu nyeusi ya jicho (cornea)Kuna matatizo manne makubwa1. Kovu - kidoto/kibaka cheupe2. Kidonda - kidoto kijivujivu3. Kuingiwa na kitu - kemikali,mdudu, vumbi n.k4. Kutoboka na kutoa maji.Indhari: hali ya pili mpaka ya nne zikitokea mgonjwa akimbizwehospital wakati jicho limefunikwa baada ya huduma ya kwanza

 

DaliliKOVU1.Haina maumivu2.Jicho haliwi jekundu3.Jicho halivimbi4.kupungua nuru jicho

 

KIDONDAA.Kinayo maumivuB.Jicho lililoathirika huwaC.jekunduD.Jicho kupunguka nuruE.Kuuma jicho kwenyeF.mwangazaG.Kutoka machoziH.Jicho kuvimba

 

Kidonda kinaweza kusababishwa na bakteria, fangas, ukosefu wa vitamin A au kwa kuumia mfano; kujichoma na kitu chenye ncha au kitu kigumu, kuingiwa na kitu jichoni, kuungua au kuingia kemikali jichon.

 

Indhari: Iwapo jicho litaumia lifunike jicho lisipate mwangaza kisha mpeleke mgonjwa hospitali.

 

7. Kemikali na kuunguaKama mgonjwa ameingia kemikali kama vile acid, alkali, saruji, chokaa mtie maji ya mchuruziko kwa takriban dakika 15 mfululizo na baadae mpeleke hospitali

 

8.Macho kuwasha na kutokwa na machozi (conjuctivitis)Huwakumba zaidi watoto wa umri kati ya miaka 5 -15 ambao hupendelea kucheza sehemu za vumbi au kwenye muangaza mkali (pwani yenye mchanga mweupe sana)

 

Watu wazima wenye kufanya kazi kwenye viwanda vinavozalisha vumbi, na wenye pumu ya muda mrefu.

 

DaliliA.Macho kuwasha (Nuru ya macho haipungui)B.Macho kubadilika rangi (kahawia)C.Kutokwa na machozi mengi (sana)D.Kushindwa kuangalia kwenye muangaza mkali

 

MatibabuKusafisha macho mara kwa mara kwa maji safi.Kutumia dawa kwa maelekezo ya daktari

 

9.Kinundu katika mfuniko wa juu au chini wa jicho

 

DALILIA.Kinundu kisichoumaB.Mara nyingi hupona wenyewe au unaweza kukikanda kwa maji ya uvuguvugu.C.Kisipopona au kitakapokuwa kikubwa huhitaji upasuaji mdogo.

 

10.Uvimbe katika mfuniko wa jicho (cellulitis)

 

A.uvimbe kwenye mifuniko ya jichoB.inaweza kuzuwia jicho kucheza (kutembea tembea)C.mara nyingi hutokea baada ya kusambaa kwa maambukizoD.ya socket ya jicho kutoka pembezoni kwa saines (sinusitis) za puaE.husababisha kupoteza nuru za macho

 

Matibabu: Mpeleke mgonjwa kwa daktari wa masikio, pua na koo (ENT)

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 3805

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     πŸ‘‰2 Bongolite - Game zone - Play free game     πŸ‘‰3 Dua za Mitume na Manabii     πŸ‘‰4 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰5 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

Dalili za mimba changa kutoka

Post hii inaenda kuzungumzia zaidi kuhusiana na mimba zinazoharibika . mimba huweza kuaribika au kutoka anzia miezi 3 na kuendelea .

Soma Zaidi...
Magonjwa yanayowashambulia watoto wachanga

Watoto wachanga ni watoto wenye umri chini ya miaka mitano, watoto hawa hushambulia na maginjwa mara kwa mara na kusababisha ukuaji wao kuwa dunk,

Soma Zaidi...
Upungufu wa Vitamini D: Dalili na jinsi ya kuipata.

Vitamini D, inayojulikana kama "vitamini ya jua," ni kirutubisho muhimu ambacho mwili huhitaji ili kudumisha mifupa imara, kuimarisha mfumo wa kinga, na kusaidia kazi za kimsingi za seli. Pamoja na umuhimu wake, upungufu wa vitamini D ni janga la kimya kimya linaloikumba dunia nzima. Makala haya yanaangazia kwa kina dalili za upungufu huu, sababu zake, na njia bora za kuhakikisha unapata viwango sahihi vya kirutubisho hiki ili kudumisha afya bora.

Soma Zaidi...
Dawa za kutibu fangasi sugu za ukeni (Vaginal Candidiasis).

Fangasi wa ukeni (Vaginal Candidiasis) husababishwa na kuzaliana kupita kiasi kwa fangasi aina ya Candida. Ingawa mara nyingi hutibika kwa dozi moja, baadhi ya wanawake hukumbwa na fangasi sugu (recurrent candidiasis)β€”hali inayojitokeza mara nne au zaidi kwa mwaka. Hii si hali ya kawaida na inahitaji mbinu madhubuti za kitabibu badala ya kutegemea dawa za dukani pekee. Makala haya yanakupa mwongozo wa tiba na hatua za kudumu za kuondoa kero hii.

Soma Zaidi...
Dalili za ugonjwa wa Saratani.

Saratani inahusu ugonjwa wowote kati ya idadi kubwa ya magonjwa ambayo yanaonyeshwa na ukuaji wa seli zisizo za kawaida ambazo hugawanyika bila kudhibitiwa na kuwa na uwezo wa kupenya na kuharibu tishu za kawaida za mwili. Saratani mara nyingi ina uwezo

Soma Zaidi...
Njia za Kuongeza Hamu ya Mapenzi kwa Mwanaume

​Kupungua kwa hamu ya mapenzi kwa mwanaume ni jambo linaloweza kusababishwa na mambo ya kisaikolojia, kimwili, au mtindo wa maisha. Makala haya yatajadili njia madhubuti za kuboresha hamu ya mapenzi kupitia mabadiliko ya afya, lishe, na mawasiliano.

Soma Zaidi...