image

Sababu za kutoshika mimba kwa mwanamke

Post hii inahusu zaidi sababu za kutoshika mimba kwa mwanamke, kuna kipindi ambacho mwanamke hushindwa kushika mimba kuna sababu mbalimbali mojawapo ni kama zifuatazo

Sababu za kutoshika mimba kwa mwanamke

1. Kutokuwa na uwiano mzuri wa homoni ambapo kwa kitaalamu huitwa hormonal imbalance, kwa hiyo ili mimba iweze kutungwa ni lazima kuwepo na usawa wa homoni yaani zote zilingane.

 

2. Ovari kushindwa kutoa mayai.

Kuna wakati mwingine ovary hazitoi mayai  hii ni kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi au tatizo lolote kwenye mfumo wa uzalishaji.

 

3. Kuziba kwa mirija ya uzazi ambayo kwa kitaalamu huitwa follapiani tube kwa hiyo mishipa hii ikiziba usababisha mayai kushindwa kukutana na mbegu za mwanaume wakati wa urutubishaji.

 

4. Kuna wakati mwingine mirija ya uzazi kujaa maji, hali hii utokea kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi kwenye mirija ya uzazi na ikishajaa maji usababisha mayai au yai kushindwa kukutana na mbegu za mwanaume.

 

5. Kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi.

Kuna wakati mwingine uvimbe kwenye uzazi usababisha mama kutozaa kwa sababu mtoto hawezi kupata sehemu ya kukaa na kukua.

 

6. Magonjwa mbalimbali na yenyewe usababisha mwanamke kushindwa kupata mimba, magonjwa kama kisonono, kaswende, kisukari na pia maambukizi kwenye via vya kiza, haya Magonjwa yakiwa sugu usababisha ugumba.

 

7. Kuwepo kwa msongo wa mawazo.

Kwa kawaida ili mimba iweze kushika mwanaume na mwanamke wanapaswa kuwa katika hali nzuri bila mawazo wakifanya hivyo ni rahisi kushika kwa mimba.

 

8. Utoaji wa mimba.

Kuna wakati mwingine kutoa mimba mara kwa mara nakwo usababisha kutoshika kwa mimba kwa sababu kuna wakati mwingine via vya uzazi vinakuwa vimechokonolewa vya kutosha na baadae mimba haiwezi kushika.

 

9. Matumizi ya pombe, bangi, sigara na ulevi wa kupindukia usababisha kutoshika kwa mimba kwa sababu baadhi ya vileo usababisha kupungua kwa homoni za uzazi.

 

10. Kuwa na uzito kupita kiasi.

Kwa kawaida uzito mkubwa nao ni sababu ya kutoshika mimba kwa sababu ili mimba ishike mwili wa mama unapaswa kuwa kwenye hali ya usawa .

 

11. Kwa hiyo baada ya kufahamu haya ni vizuri kurekebisha mtindo wa maisha kwa wale ambao wana changamoto za kutopata mimba ili waweze kupata watoto na ni vema kabisa kupata ushauri wa kitaalamu kama kuna tatizo la kukosa mimba.





           

Je! umeipenda hii post?
Ndio            Hapana            Save post

Rajabu Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF     Share On Facebook or Whatsapp Imesomwa mara 5984


Sponsored links
👉1 Kitau cha Fiqh     👉2 kitabu cha Simulizi     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Kitabu cha Afya    

Post zifazofanana:-

SABABU ZA KUKOSA HAMU YA TENDO LANDOA
Hii ni hali inayompata mtu kukosa hamu kabisa ya kushiriki kitendo chochote kinachohusiana na kufanya tendo landoa au bunyeto. Soma Zaidi...

je maumivu ya nyonga na tumbo la chini ni dalili ya mimba?
Nina swali langu:-je maumivu ya nyonga na tumbo la chini ni dalili ya mimba? Soma Zaidi...

Umuhimu wa uzazi wa mpango kwa Mama
Posti hii inahusu zaidi faida za uzazi wa mpango kwa akina Mama, tunajua wazi kubwa kuna faida kubwa za uzazi wa mpango kwa akina Mama pindi watumiapo njia hizi kwa uhakika zaidi. Soma Zaidi...

Kazi ya metronidazole
Posti hii zaidi kazi ya Dawa ya metronidazole katika kutibu Minyoo, ni aina ya Dawa ambayo imetumiwa na watu wengi wakaweza kupona na kuepukana na minyoo. Zifuatazo ni baadhi ya kazi za metronidazole. Soma Zaidi...

Maumivu wakati wa hedhi.
Posti hii inahusu zaidi maumivu wakati wa hedhi, haya ni maumivu ambayo utokea wakati wa hedhi kwa wanawake walio wengi, wengine huwa hawayapati kabisa na wengine hutapata na kwa kiwango kikubwa kutegemea na matatizo mbalimbali kama tutakavyoona. Soma Zaidi...

Hatari ya kutokwa na damu wakati wa ujauzito
Posti hii inahusu zaidi hatari za kutokwa na damu wakati wa ujauzito, hali hii utokea wakati wa ujauzito ambapo Kuna baadhi ya wajawazito utokwa na damu jambo ambalo hatupaswi kutarajia kwa sababu tunafahamu kabisa mama akishapata ujauzito na damu zinakom Soma Zaidi...

Dalili za kujifungua hatua kwa hatua
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za ujauzito baada ya tendo la ndoa Soma Zaidi...

Wajibu wa mjamzito katika utaratibu wa uleaji wa mimba
Posti hii inahusu zaidi wajibu wa Mama mjamzito katika kileo mimba sio yeye tu Bali na wote waliomzunguka wanapaswa kuhakikisha kuwa mama mjamzito anapaswa kufanyiwa huduma zote Ili kuweza kujifungua salama na bila shida yoyote. Soma Zaidi...

Mwanamke mwenye HIV akiwa mjamzito ama ananyonyesha
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu mwanamke mwenye HIV akiwa mjamzito ama anaenyonyesha Soma Zaidi...

Fahamu kuhusu mapacha wanaofanana
Post hii inahusu zaidi watoto mapacha wanaofanana,ni watoto wanaozaliwa wakiwa wanaofanana kwa sura na hata group la damu huwa ni Moja. Soma Zaidi...

Nataka nijue Kuwa njia yakuzuia mimba wakati Wakufany tendo La ndoa
Je ungependa kuijuwa Njia ya kuzuia mimba wakati wa tendo la ndoa?. Posti hii itakwenda kukufundisha ujanja huu. Soma Zaidi...

Dalili za PID
Posti hii inahusu zaidi dalili za PID maana yake ni maambukizi kwenye pelvic kwa kitaalamu huitwa pelvic infection disease, ni ugonjwa unaoshambulia sana wanawake na wasichana Soma Zaidi...