Menu



Sababu za kutoshika mimba kwa mwanamke

Post hii inahusu zaidi sababu za kutoshika mimba kwa mwanamke, kuna kipindi ambacho mwanamke hushindwa kushika mimba kuna sababu mbalimbali mojawapo ni kama zifuatazo

Sababu za kutoshika mimba kwa mwanamke

1. Kutokuwa na uwiano mzuri wa homoni ambapo kwa kitaalamu huitwa hormonal imbalance, kwa hiyo ili mimba iweze kutungwa ni lazima kuwepo na usawa wa homoni yaani zote zilingane.

 

2. Ovari kushindwa kutoa mayai.

Kuna wakati mwingine ovary hazitoi mayai  hii ni kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi au tatizo lolote kwenye mfumo wa uzalishaji.

 

3. Kuziba kwa mirija ya uzazi ambayo kwa kitaalamu huitwa follapiani tube kwa hiyo mishipa hii ikiziba usababisha mayai kushindwa kukutana na mbegu za mwanaume wakati wa urutubishaji.

 

4. Kuna wakati mwingine mirija ya uzazi kujaa maji, hali hii utokea kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi kwenye mirija ya uzazi na ikishajaa maji usababisha mayai au yai kushindwa kukutana na mbegu za mwanaume.

 

5. Kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi.

Kuna wakati mwingine uvimbe kwenye uzazi usababisha mama kutozaa kwa sababu mtoto hawezi kupata sehemu ya kukaa na kukua.

 

6. Magonjwa mbalimbali na yenyewe usababisha mwanamke kushindwa kupata mimba, magonjwa kama kisonono, kaswende, kisukari na pia maambukizi kwenye via vya kiza, haya Magonjwa yakiwa sugu usababisha ugumba.

 

7. Kuwepo kwa msongo wa mawazo.

Kwa kawaida ili mimba iweze kushika mwanaume na mwanamke wanapaswa kuwa katika hali nzuri bila mawazo wakifanya hivyo ni rahisi kushika kwa mimba.

 

8. Utoaji wa mimba.

Kuna wakati mwingine kutoa mimba mara kwa mara nakwo usababisha kutoshika kwa mimba kwa sababu kuna wakati mwingine via vya uzazi vinakuwa vimechokonolewa vya kutosha na baadae mimba haiwezi kushika.

 

9. Matumizi ya pombe, bangi, sigara na ulevi wa kupindukia usababisha kutoshika kwa mimba kwa sababu baadhi ya vileo usababisha kupungua kwa homoni za uzazi.

 

10. Kuwa na uzito kupita kiasi.

Kwa kawaida uzito mkubwa nao ni sababu ya kutoshika mimba kwa sababu ili mimba ishike mwili wa mama unapaswa kuwa kwenye hali ya usawa .

 

11. Kwa hiyo baada ya kufahamu haya ni vizuri kurekebisha mtindo wa maisha kwa wale ambao wana changamoto za kutopata mimba ili waweze kupata watoto na ni vema kabisa kupata ushauri wa kitaalamu kama kuna tatizo la kukosa mimba.

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea

Ndio     Hapana     Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 7100

Share On:

Facebook WhatsApp

Post zinazofanana:

Je kukosa hedhi kwa mwanmke anayenyonyesha ni dalili ya mimba

Kipimo cha mimba cha mkojo hakiwezi kyonyesha mimva changa sana. Hivyo kama ni mimba baada ya wikibpima tena itaweza kuonekana. Dalili hizobulizotaja pekee haziashirii mimba tu huwenda ni homoni zimebadilika kidogo, ama una uti.

Soma Zaidi...
Dalili za upungufu wa homoni ya progesterone

Posti hii inahusu zaidi dalili ambazo zinaweza kutokea iwapo Kuna upungufu wa homoni ya progesterone.

Soma Zaidi...
Ni ipi siku ya kupata ujauzito, na nitajuwaje kama nimepata ujauzito?

Hapa utajifunza siku nzuri kushoriki tendo la ndoa kupata ujauzito, dalili za siku hiyo na kuitafuta kwa mahesabu

Soma Zaidi...
Tatizo la kutokwa na majimaji kwenye uume.

Posti hii inahusu zaidi tatizo la kutokwa na majimaji kwenye uume, ni tatizo ambalo uwakumba baadhi ya wanaume kwa sababu mbalimbali na pia Ugonjwa huu unatibika hasa kwa wale wanaowahi kupata matibabu.

Soma Zaidi...
Je, mwanamke anapataje Ugonjwa wa Maambukizi ya mfumo wa Uzazi PID?

Posti hii inaelezea namna mwanamke anavyoweza kupata Ugonjwa wa Maambukizi ya mfumo wa Uzazi.

Soma Zaidi...
Ndug mi naitaj ushauri mimi nishaingia kwenye tendo dakika 7 tu nakua nishafika kilelen naomba ushauri ndugu

Kama unadhani una tatizo la kuwahi kufika kileleni basi post hii ni kwa ajili yako.

Soma Zaidi...
Mbinu za kupunguza Kichefuchefu

Point hii inahusu zaidi mbinu za kupunguza Kichefuchefu hasa kwa wagonjwa na watumiaji wa madawa mbalimbali yanayoweza kusababisha kichefuchefu.

Soma Zaidi...
Mambo muhimu ambayo mama mjamzito anatakiwa kuzingatia.

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Mambo ambayo mama mjamzito anatakiwa kuzingatia katika kipindi Cha ujauzito au mimba

Soma Zaidi...
Namna ya kuangalia kama mtoto aliyezaliwa anapumua

Posti hii inahusu zaidi mbinu za kuangalia kama mtoto anapumua pindi anapozaliwa,tunajua kabisa ili kujua na kuelewa kama mtoto yuko hai ni lazima kuangalia upumuaji wa mtoto,ambapo tunaitambua pale anapolia tu.

Soma Zaidi...