Sababu za kutoshika mimba kwa mwanamke
Post hii inahusu zaidi sababu za kutoshika mimba kwa mwanamke, kuna kipindi ambacho mwanamke hushindwa kushika mimba kuna sababu mbalimbali mojawapo ni kama zifuatazo
Sababu za kutoshika mimba kwa mwanamke
1. Kutokuwa na uwiano mzuri wa homoni ambapo kwa kitaalamu huitwa hormonal imbalance, kwa hiyo ili mimba iweze kutungwa ni lazima kuwepo na usawa wa homoni yaani zote zilingane.
2. Ovari kushindwa kutoa mayai.
Kuna wakati mwingine ovary hazitoi mayai hii ni kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi au tatizo lolote kwenye mfumo wa uzalishaji.
3. Kuziba kwa mirija ya uzazi ambayo kwa kitaalamu huitwa follapiani tube kwa hiyo mishipa hii ikiziba usababisha mayai kushindwa kukutana na mbegu za mwanaume wakati wa urutubishaji.
4. Kuna wakati mwingine mirija ya uzazi kujaa maji, hali hii utokea kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi kwenye mirija ya uzazi na ikishajaa maji usababisha mayai au yai kushindwa kukutana na mbegu za mwanaume.
5. Kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi.
Kuna wakati mwingine uvimbe kwenye uzazi usababisha mama kutozaa kwa sababu mtoto hawezi kupata sehemu ya kukaa na kukua.
6. Magonjwa mbalimbali na yenyewe usababisha mwanamke kushindwa kupata mimba, magonjwa kama kisonono, kaswende, kisukari na pia maambukizi kwenye via vya kiza, haya Magonjwa yakiwa sugu usababisha ugumba.
7. Kuwepo kwa msongo wa mawazo.
Kwa kawaida ili mimba iweze kushika mwanaume na mwanamke wanapaswa kuwa katika hali nzuri bila mawazo wakifanya hivyo ni rahisi kushika kwa mimba.
8. Utoaji wa mimba.
Kuna wakati mwingine kutoa mimba mara kwa mara nakwo usababisha kutoshika kwa mimba kwa sababu kuna wakati mwingine via vya uzazi vinakuwa vimechokonolewa vya kutosha na baadae mimba haiwezi kushika.
9. Matumizi ya pombe, bangi, sigara na ulevi wa kupindukia usababisha kutoshika kwa mimba kwa sababu baadhi ya vileo usababisha kupungua kwa homoni za uzazi.
10. Kuwa na uzito kupita kiasi.
Kwa kawaida uzito mkubwa nao ni sababu ya kutoshika mimba kwa sababu ili mimba ishike mwili wa mama unapaswa kuwa kwenye hali ya usawa .
11. Kwa hiyo baada ya kufahamu haya ni vizuri kurekebisha mtindo wa maisha kwa wale ambao wana changamoto za kutopata mimba ili waweze kupata watoto na ni vema kabisa kupata ushauri wa kitaalamu kama kuna tatizo la kukosa mimba.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉3 kitabu cha Simulizi 👉4 web hosting 👉5 Dua za Mitume na Manabii 👉6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
Maumivu ya uume baada ya tendo la ndoa
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maumivu ya uume baada ya tendo la ndoa
Soma Zaidi...Sababu za maumivu ya tumbo wakatu wa tendo la ndoa
Jifunze sababu kuu zinazosababisha kuhisi maumivu makali ya tumbo wakati wa kushiriki tendo la ndoa
Soma Zaidi...Namna za kujilinda na fangasi ukeni
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuepuka fangasi za ukeni, ni njia ambazo usaidia kuepuka madhara ya fangasi za ukeni.
Soma Zaidi...dalili za uchungu kwa mama mjamzito
Makala hii itakwenda kukufundisha baadhi ya dalili za uchungu kwa mama mjamzito.
Soma Zaidi...Uzazi wa mpango
Uzazi wa Mpango hutoa chaguo kwa familia kuwa na idadi ya watoto wanaotaka katika muda maalum, wanahisi na mbinu iliyoamuliwa. Uzazi wa mpango una faida kadhaa kwa mama wa mtoto, wanandoa na jamii Ujuzi wa mzunguko wa hedhi humwezesha mtoa huduma kumshaur
Soma Zaidi...