picha

Wajibu wa mjamzito katika utaratibu wa uleaji wa mimba

Posti hii inahusu zaidi wajibu wa Mama mjamzito katika kileo mimba sio yeye tu Bali na wote waliomzunguka wanapaswa kuhakikisha kuwa mama mjamzito anapaswa kufanyiwa huduma zote Ili kuweza kujifungua salama na bila shida yoyote.

Wajibu wa Mama mjamzito.

1. Mama mjamzito anapaswa kuwa na mda wa kutosha wa kupumzika.

Kwa sababu mama anakuwa na matalajio ya kujifungua salama anapaswa kupumzika kwa mda mrefu na hasa hasa anapaswa kuinua miguu juu anapokuwa amelala na anapaswa kulala chini wakati wa alfajiri hayo yote yana mpatia mazoezi ya kufaa na kutosha anapokaribia kujifungua na hivyo kumwezesha mtoto kukua vizuri na Baadae kujifungua bila shida, kwa hiyo jamii na ndugu wa familia wanapaswa kuhakikisha kuwa Mama anapata mda wa kutosha wa kupumzika.

 

2. Mama anapaswa kipata chakula Bora chenye virutubisho.

Kwa kumpatia Mama chakula chenye virutubisho umfanye Mama kuwa na madini yabayohitajika mwilini kama vile madini ya chuma ambayo usaidia wakati wa ujauzito, vyakula vyenye vitamini A ambavyo umsaidie mtoto aweze kuona, kwa hiyo Mama anapaswa kupatiwa Aina zote za vyakula kama vile wanga, protein, mafuta na mboga mboga za majani ambazo uongeza damu mwilni na wakati wa kujifungua anakuwa na damu ya kutosha. Kwa hiyo jamii ziachane na Mila potofu kuhusu vyakula kwa wanawake.

 

3. Kuepuka Aina yoyote ya kemikali .

Mama mjamzito anapaswa kuepuka Aina yoyote ya kemikali kama vile  pombe ambayo ikiingia ndani uweza kuaribu ubongo wa mtoto katika makuzi anapokuwa tumboni mwa mama,Moshi wa sigara nao ni hatari kwa Mama mjamzito kwa sababu unaweza kuharibu mapafu ya mtoto akiwa tumboni kwa mama, Madawa ya kulevya pia nayo ni hatari kwa afya ya Mama na Mtoto, kwa hiyo mtoto akiwa tumboni kwa mama anaweza kuzaliwa akiwa zezeta kwa Sababu ya madawa ya kulevya.

 

4. Kuwepo kwa mhudumu karibu na Mama mjamzito.

Mama mjamzito anapaswa kuwa na mhudumu wa karibu kwa mfano wataalamu wafya au mkunga Ili kuhakikisha kujua siku na mda wa kujifungua kwa Mama kwa kufanya hivyo tunaweza kuepusha madhara mbalimbali ambayo uweza kuwakuta wanawake wakati wa kujifungua kwa hiyo Mama mjamzito anapaswa kwenda klinic mara kwa mara Ili kuangalia afya yaka na maendeleo ya mtoto kwa ujumla .

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 2670

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio     👉2 Bongolite - Game zone - Play free game     👉3 Dua za Mitume na Manabii     👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

Mda wa kufanya tendo la ndoa baada ya kujifungua

Posti hii inahusu zaidi mda ambao mama anapaswa kukaa bila kufanya tendo la ndoa mara tu baada ya kujifungua.

Soma Zaidi...
Kutoka kwa mimba, sababu za kutoka kwa mimba, dalili za kutoka mimba na kuzuia mimba kuoka

Mimba inapotoka ina dalili, na zipo sababu kadhaa za kutoka kwa mimba. Je utazuiaje mimba kutoka. Soma makala hii

Soma Zaidi...
Mimi kwenye korodani yai moja limezungukwa na majimaji ,na haya maji yamekuwepo toka utotoni mwangu lakin bado sijayaona matatizo yake , je kitaaramu hii inaweza kua na athari gani? ,Naombeni ushauri

Korodani ni kiungo muhimu kwa mwanaume, katika afya ya uzazi. Unaweza kusema ni kiwanda cha kutengeneza mbegu za kiume. Kiungo hiki ni sawa na ovari kwa mwanamke.

Soma Zaidi...
Zijue Dalili za hatari kwa Mama mjamzito

Posti hii inahusu zaidi dalili za hatari kwa Mama mjamzito, ni Dalili ambazo ujitokeza kwa Mama mjamzito, hizi Dalili zisipofanyiwa kazi mapema zinaweza kuleta shida kwa Mama kwa hiyo jamii nzima inapaswa kujua Dalili hizi na kuchukua hatua endapo zitajio

Soma Zaidi...
Sababu za kutoshika mimba kwa mwanamke

Post hii inahusu zaidi sababu za kutoshika mimba kwa mwanamke, kuna kipindi ambacho mwanamke hushindwa kushika mimba kuna sababu mbalimbali mojawapo ni kama zifuatazo

Soma Zaidi...