picha

Wajibu wa mjamzito katika utaratibu wa uleaji wa mimba

Posti hii inahusu zaidi wajibu wa Mama mjamzito katika kileo mimba sio yeye tu Bali na wote waliomzunguka wanapaswa kuhakikisha kuwa mama mjamzito anapaswa kufanyiwa huduma zote Ili kuweza kujifungua salama na bila shida yoyote.

Wajibu wa Mama mjamzito.

1. Mama mjamzito anapaswa kuwa na mda wa kutosha wa kupumzika.

Kwa sababu mama anakuwa na matalajio ya kujifungua salama anapaswa kupumzika kwa mda mrefu na hasa hasa anapaswa kuinua miguu juu anapokuwa amelala na anapaswa kulala chini wakati wa alfajiri hayo yote yana mpatia mazoezi ya kufaa na kutosha anapokaribia kujifungua na hivyo kumwezesha mtoto kukua vizuri na Baadae kujifungua bila shida, kwa hiyo jamii na ndugu wa familia wanapaswa kuhakikisha kuwa Mama anapata mda wa kutosha wa kupumzika.

 

2. Mama anapaswa kipata chakula Bora chenye virutubisho.

Kwa kumpatia Mama chakula chenye virutubisho umfanye Mama kuwa na madini yabayohitajika mwilini kama vile madini ya chuma ambayo usaidia wakati wa ujauzito, vyakula vyenye vitamini A ambavyo umsaidie mtoto aweze kuona, kwa hiyo Mama anapaswa kupatiwa Aina zote za vyakula kama vile wanga, protein, mafuta na mboga mboga za majani ambazo uongeza damu mwilni na wakati wa kujifungua anakuwa na damu ya kutosha. Kwa hiyo jamii ziachane na Mila potofu kuhusu vyakula kwa wanawake.

 

3. Kuepuka Aina yoyote ya kemikali .

Mama mjamzito anapaswa kuepuka Aina yoyote ya kemikali kama vile  pombe ambayo ikiingia ndani uweza kuaribu ubongo wa mtoto katika makuzi anapokuwa tumboni mwa mama,Moshi wa sigara nao ni hatari kwa Mama mjamzito kwa sababu unaweza kuharibu mapafu ya mtoto akiwa tumboni kwa mama, Madawa ya kulevya pia nayo ni hatari kwa afya ya Mama na Mtoto, kwa hiyo mtoto akiwa tumboni kwa mama anaweza kuzaliwa akiwa zezeta kwa Sababu ya madawa ya kulevya.

 

4. Kuwepo kwa mhudumu karibu na Mama mjamzito.

Mama mjamzito anapaswa kuwa na mhudumu wa karibu kwa mfano wataalamu wafya au mkunga Ili kuhakikisha kujua siku na mda wa kujifungua kwa Mama kwa kufanya hivyo tunaweza kuepusha madhara mbalimbali ambayo uweza kuwakuta wanawake wakati wa kujifungua kwa hiyo Mama mjamzito anapaswa kwenda klinic mara kwa mara Ili kuangalia afya yaka na maendeleo ya mtoto kwa ujumla .

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 2438

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Kitabu cha Afya     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Mazoezi salama kwa mama mjamzito

Katika kipindi cha ujauzito, kufanya mazoezi kwa usahihi ni muhimu kwa afya ya mama na mtoto. Mazoezi haya yanasaidia kupunguza uchovu, kudhibiti uzito, kupunguza matatizo ya mgongo, na kuongeza hisia za furaha. Somo hili litatoa mwongozo wa aina za mazoezi zinazofaa kwa kila mwezi wa ujauzito, pamoja na mwongozo wa usalama wa kufanya mazoezi haya nyumbani.

Soma Zaidi...
Je tumbo huanza kukua baada ya mda gan?

Ni Swali kila mjamzito anataka kujiuliza hasa akiwa katika mimba ya kwanza. Wengine wanataka kujuwa ni muda gani anujuwe mavazi makubwa. Kama na wewe unataka kujuwa muda ambao tumbo huwa kubwa, endelea kusoma.

Soma Zaidi...
Dawa hatari kwa mwenye ujauzito

Hii ni orodha ya dawa ambazo hutumiwa sana na watu kutoka maduka ya dawa lakini sio salama kwa wajawazito.

Soma Zaidi...
Chanzo cha tatizo la mvurugiko wa hedhi.

Posti hii inahusu zaidi chanzo cha mvurugiko wa hedhi, Kuna kipindi hedhi uvurugika kabisa, pengine unaweza kupata hedhi mara mbili kwa mwezi au kukosa au pengine siku kuwa zaidi ya tano mpaka Saba au kuwa chache, hali hii utokea kwa sababu mbalimbali tut

Soma Zaidi...
Sababu za kupasuka kwa mfuko wa kizazi

Posti hii inahusu zaidi sababu za kupasuka kwa mfuko wa uzazi hasa mama anapokalibia kujifungua.

Soma Zaidi...
Kuvunjika kwa mtoto wakati wa kuzaliwa.

Post hii inahusu zaidi kuvunjika kwa mtoto wakati wa kuzaliwa, hali hii utokea kwa watoto wadogo wakati wa kuzaliwa kwa sababu maalum kama tutakavyoona.

Soma Zaidi...