Wajibu wa mjamzito katika utaratibu wa uleaji wa mimba


image


Posti hii inahusu zaidi wajibu wa Mama mjamzito katika kileo mimba sio yeye tu Bali na wote waliomzunguka wanapaswa kuhakikisha kuwa mama mjamzito anapaswa kufanyiwa huduma zote Ili kuweza kujifungua salama na bila shida yoyote.


Wajibu wa Mama mjamzito.

1. Mama mjamzito anapaswa kuwa na mda wa kutosha wa kupumzika.

Kwa sababu mama anakuwa na matalajio ya kujifungua salama anapaswa kupumzika kwa mda mrefu na hasa hasa anapaswa kuinua miguu juu anapokuwa amelala na anapaswa kulala chini wakati wa alfajiri hayo yote yana mpatia mazoezi ya kufaa na kutosha anapokaribia kujifungua na hivyo kumwezesha mtoto kukua vizuri na Baadae kujifungua bila shida, kwa hiyo jamii na ndugu wa familia wanapaswa kuhakikisha kuwa Mama anapata mda wa kutosha wa kupumzika.

 

2. Mama anapaswa kipata chakula Bora chenye virutubisho.

Kwa kumpatia Mama chakula chenye virutubisho umfanye Mama kuwa na madini yabayohitajika mwilini kama vile madini ya chuma ambayo usaidia wakati wa ujauzito, vyakula vyenye vitamini A ambavyo umsaidie mtoto aweze kuona, kwa hiyo Mama anapaswa kupatiwa Aina zote za vyakula kama vile wanga, protein, mafuta na mboga mboga za majani ambazo uongeza damu mwilni na wakati wa kujifungua anakuwa na damu ya kutosha. Kwa hiyo jamii ziachane na Mila potofu kuhusu vyakula kwa wanawake.

 

3. Kuepuka Aina yoyote ya kemikali .

Mama mjamzito anapaswa kuepuka Aina yoyote ya kemikali kama vile  pombe ambayo ikiingia ndani uweza kuaribu ubongo wa mtoto katika makuzi anapokuwa tumboni mwa mama,Moshi wa sigara nao ni hatari kwa Mama mjamzito kwa sababu unaweza kuharibu mapafu ya mtoto akiwa tumboni kwa mama, Madawa ya kulevya pia nayo ni hatari kwa afya ya Mama na Mtoto, kwa hiyo mtoto akiwa tumboni kwa mama anaweza kuzaliwa akiwa zezeta kwa Sababu ya madawa ya kulevya.

 

4. Kuwepo kwa mhudumu karibu na Mama mjamzito.

Mama mjamzito anapaswa kuwa na mhudumu wa karibu kwa mfano wataalamu wafya au mkunga Ili kuhakikisha kujua siku na mda wa kujifungua kwa Mama kwa kufanya hivyo tunaweza kuepusha madhara mbalimbali ambayo uweza kuwakuta wanawake wakati wa kujifungua kwa hiyo Mama mjamzito anapaswa kwenda klinic mara kwa mara Ili kuangalia afya yaka na maendeleo ya mtoto kwa ujumla .



Sponsored Posts


  ðŸ‘‰    1 Tunakukaribisha kwenye Maktaba yetu       ðŸ‘‰    2 Jifunze Fiqh       ðŸ‘‰    3 Madrasa kiganjani offline       ðŸ‘‰    4 Download App zetu hapa ujifunze zaidi    


Je una maswali, maoni ama ushauri, tutumie sms ✉ bofya hapa hapa, ama wasiliana nasi kwa WhatsApp bofya hapa



Post Nyingine


image Vyakula hatari kwa mwenye vidonda vya tumbo
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu vyakula hatari kwa mwenye vidonda vya tumbo Soma Zaidi...

image Huduma ya Kwanza kwa mtu aliyeng'atwa na nyoka
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu huduma ya Kwanza kwa mtu aliyeng'atwa na nyoka Soma Zaidi...

image Vidonda vya tumbo husababishwa na nini
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu visababishi vya vidonda vya tumbo Soma Zaidi...

image Tiba ya vidonda vya tumbo na dawa zake
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu Tina ya vidonda vya tumbo na dawa zake Soma Zaidi...

image Maumivu wakati wa tendo la ndoa na baada
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu maumivu wakati wa tendo la ndoa na baada Soma Zaidi...

image Jinsi mimba inavyotungwa mpaka mtoto kuingia kwenye mfuko wa uzazi
Post hii inahusu zaidi namna mimba inavyotungwa mpaka mtoto kuingia kwenye mfuko wa uzazi, mimba kutungwa ni kitendo ambapo mbegu za kiume kuungana na yai la kike na kutengeneza zygote. Soma Zaidi...

image Walio hatarini kupata gonorrhea (gonoria)
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu watu walio hatarini kupata gonorrhea gonoria Soma Zaidi...

image Huduma ya kwanza kwa aliyeungua moto
Post hii inahusu namna ya kutoa huduma ya kwanza kwa mtu aliyeungua moto, kuingia moto ni kitendo Cha kubabuka ngozi ya juu inaweza kuwa kwa kemikali,umeme na just, Soma Zaidi...

image Namna ya kutunza chumba cha upasuaji
Posti hii inahusu zaidi namna ya kutunza chumba cha upasuaji, chumba cha upasuaji ni tofauti na vyumba vingine kwenye hospitali kwa hiyo vinahitaji uangalizi wa hali ya juu sana ili kuepuka aina yoyote ya uchafu kuwepo kwenye chumba hicho, zifuatazo ni namna ya kutunza chumba cha upasuaji. Soma Zaidi...

image Faida za uzazi wa mpango kwa watoto.
Posti hii inahusu zaidi umuhimu wa uzazi wa mpango kwa watoto, sio akina Mama peke yao wanaofaidika na uzazi wa mpango vile vile na watoto wanafaidika na uzazi wa mpango kama ifuatavyo. Soma Zaidi...