picha

Mambo muhimu kwa wanawake kabla ya kubeba mimba

Posti hii inahusu zaidi mambo muhimu kwa wanawake kabla ya kubeba mimba,Ni mambo ya kuzingatia ili mama akija kubeba mimba awe mzima kimwili, ki afya na kisaikolojia na hivyo hivyo Mtoto atakayezaliwa atakuwa salama.

Mambo muhimu ya kuzingatia kwa wanawake kabla ya kubeba mimba.

1. Kwanza kabisa tunapaswa kujua kuwa kila mama anapaswa kujifungua mtoto salama kiafya, kiakili na kisaikolojia hili hayo yatimie ni lazima maandalizi ya mbali kuwepo yaani maandalizi kabla ya kubeba mimba kama tutakavyoona hapo chini.

 

2.kwanza kabisa historia ya Mama na baba wote inapaswa kujulikana kama wanatumia vileo vikali, wanavuta sigara na ni njia gani ya uzazi wa mpango wanayotumia au kama kuna Magonjwa ya kuridhi kwenye familia kama hayo yote yatajulikana ni vizuri kuwapa ushauri ni lini na wakati gani wanapaswa kukutana na kupata mtoto watajayemtaka wakiwa katika hali nzuri na kwa akili timamu 

 

3.Pia Mama anapaswa kupima urefu, uzito, mapigo ya moyo, msukumo wa damu, joto la mwili,upumuaji kuangalia matiti yake kama yana aina yoyote ya uvimbe na kuangalia kama mama ana ugonjwa wowote ambao akibeba mimba unaweza kuleta madhara kwake na kwa mtoto 

 

4. Kuangalia kama Mlay wa kizazi unaweza kufunga iwapo kama mimba ilitungwa na pia kuangalia kama kuna Maambukizi yoyote kwenye mlango wa kizazi hasa kansa ya mlango wa kizazi.

 

5. Kuangalia kama kuna aina yoyote ya Maambukizi hasa maambukizi ya Magonjwa ya a ngono kwa sababu mama akibeba mimba na magonjwa hayo mimba inaweza kutoka kwa hiyo Magonjwa haya kama yapo yatibiwe mara moja.

 

6. Pia mama anapaswa kupima wingi wa damu, group la damu, RH factor, maambukizi ya virus vya ukimwi, sukari, mkojo, antibodies na mambo mengine yote mawili na mama akikutwa na shida yoyote anaambiwa cha kufanya na akiona kubwa yuko salama anaweza kubeba mimba na mtoto natumaini atakuwa salama. Kwa hiyo akina Mama kabla ya kubeba mimba mnapaswa kufanya hivyo ili kupata watoto wenye afya njema.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 2300

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Madrasa kiganjani     👉2 Dua za Mitume na Manabii     👉3 kitabu cha Simulizi     👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉5 ai web app     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

Chanzo cha tezidume, dalili zake na tiba zake.

Post hii inakwenda kukufunza mambo mengi kuhusu tezi dume kama chanzo, dalili, matibabu, njia za kujikinga na mambo hatari yanayoweza kukusababishia kupata tezi dume.

Soma Zaidi...
Nia za kupima ujauzito ukiwa nyumbani, Njia kuu 10 za kiasili za kupima mimba changa

Kuna njia nyingi zinatajwa zinapima mimba kama chumvi, sukari, mafuta na sabuni. Hata hivyo zipo njia zaidi ya 10 za kiasili za kupima ujauzito. Utajifunza hapa zote

Soma Zaidi...
Faida za uzazi wa mpango kwa watu wenye ugonjwa wa Ukimwi

Posti hii inahusu zaidi faida za uzazi wa mpango kwa watu waliopata maambukizi ya ugonjwa wa Ukimwi, ni faida wanazozipata waathirika wa ugonjwa wa Ukimwi.

Soma Zaidi...
Njia za uzazi wa mpango kwa akina Mama kuanzia miezi sita baada ya kujifungua mpaka mwaka mmoja

Posti hii inahusu zaidi njia za uzazi wa mpango kwa mama aliyejifungua kuanzia miezi sita mpaka mwaka mmoja.

Soma Zaidi...
TATIZO LA KUVIMBA KWA USO NA MIGUU KWA WAJAWAZITO

KUVIMBA VYA MIGUU KWA WAJAWAZITO Kuvimba kwa miguu ni hali inayowapara wengi katika wajawazito.

Soma Zaidi...
Mm tumbo linaniuma mara kwa mara na linakua kama linages alaf kichwa kinauma mara kwa mara na nakosa choo wakati mwingine na kiuno kinauma je?inawezakua n ujauzito? Maana nilshirki tendo la ndoa siku ya tano baada ya kutoka hedhi

Dalili za mwanzo za ujauzito zinaweza kuwa ni changamoto kwamwanamke hasa ikiwa ndio mimba yake ya kwanza. Maumivu ya tumbo, kujaa kwa tumbo gesi, kukosa choo ama hamu ya kula na kadhalika huweza pia kuambatana na ujauzito.

Soma Zaidi...