picha

Mambo muhimu kwa wanawake kabla ya kubeba mimba

Posti hii inahusu zaidi mambo muhimu kwa wanawake kabla ya kubeba mimba,Ni mambo ya kuzingatia ili mama akija kubeba mimba awe mzima kimwili, ki afya na kisaikolojia na hivyo hivyo Mtoto atakayezaliwa atakuwa salama.

Mambo muhimu ya kuzingatia kwa wanawake kabla ya kubeba mimba.

1. Kwanza kabisa tunapaswa kujua kuwa kila mama anapaswa kujifungua mtoto salama kiafya, kiakili na kisaikolojia hili hayo yatimie ni lazima maandalizi ya mbali kuwepo yaani maandalizi kabla ya kubeba mimba kama tutakavyoona hapo chini.

 

2.kwanza kabisa historia ya Mama na baba wote inapaswa kujulikana kama wanatumia vileo vikali, wanavuta sigara na ni njia gani ya uzazi wa mpango wanayotumia au kama kuna Magonjwa ya kuridhi kwenye familia kama hayo yote yatajulikana ni vizuri kuwapa ushauri ni lini na wakati gani wanapaswa kukutana na kupata mtoto watajayemtaka wakiwa katika hali nzuri na kwa akili timamu 

 

3.Pia Mama anapaswa kupima urefu, uzito, mapigo ya moyo, msukumo wa damu, joto la mwili,upumuaji kuangalia matiti yake kama yana aina yoyote ya uvimbe na kuangalia kama mama ana ugonjwa wowote ambao akibeba mimba unaweza kuleta madhara kwake na kwa mtoto 

 

4. Kuangalia kama Mlay wa kizazi unaweza kufunga iwapo kama mimba ilitungwa na pia kuangalia kama kuna Maambukizi yoyote kwenye mlango wa kizazi hasa kansa ya mlango wa kizazi.

 

5. Kuangalia kama kuna aina yoyote ya Maambukizi hasa maambukizi ya Magonjwa ya a ngono kwa sababu mama akibeba mimba na magonjwa hayo mimba inaweza kutoka kwa hiyo Magonjwa haya kama yapo yatibiwe mara moja.

 

6. Pia mama anapaswa kupima wingi wa damu, group la damu, RH factor, maambukizi ya virus vya ukimwi, sukari, mkojo, antibodies na mambo mengine yote mawili na mama akikutwa na shida yoyote anaambiwa cha kufanya na akiona kubwa yuko salama anaweza kubeba mimba na mtoto natumaini atakuwa salama. Kwa hiyo akina Mama kabla ya kubeba mimba mnapaswa kufanya hivyo ili kupata watoto wenye afya njema.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Uzazi Main: Post File: Download PDF Views 2489

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game     👉2 Madrasa kiganjani     👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     👉4 Dua za Mitume na Manabii     👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     👉6 kitabu cha Simulizi    

Post zinazofanana:

Dalili za kupata uvimbe kwenye kizazi (fibroid)

Post hii inaenda kufundisha kuhusiana na uvimbe wa kizazi kwa wanawake. Uvimbe wa kizazi no uvimbe ambao hutokea kwenye tumbo la kizazi ambao unaweza kuwa ndan ya kizazi uvimbe huu ndan ya mwanamke hujulikana kama (uterine myoma au fibroid). Uvi

Soma Zaidi...
Mimi kwenye korodani yai moja limezungukwa na majimaji ,na haya maji yamekuwepo toka utotoni mwangu lakin bado sijayaona matatizo yake , je kitaaramu hii inaweza kua na athari gani? ,Naombeni ushauri

Korodani ni kiungo muhimu kwa mwanaume, katika afya ya uzazi. Unaweza kusema ni kiwanda cha kutengeneza mbegu za kiume. Kiungo hiki ni sawa na ovari kwa mwanamke.

Soma Zaidi...
Maumivu ya tumbo kabla ya kupata hedhi

Je unasumbuliwa na maumivu ya tumbo. Unadhani ni dalili za mimba na ukapima hakuna mimba.

Soma Zaidi...
Kiungulia kwa wajawazito, dawa yake na njia za kukabilianannacho

Wajawazito wamekuwa wakisumbuliwa sana na kiungulia, makala hii itakujulisha njia za kukabiliana na kiungulia, dalili zake na dawa zake

Soma Zaidi...
Faida za uzazi wa mpango kwa jamii

Posti hii inahusu zaidi faida za uzazi wa mpango kwa jamii, tunapaswa kujua kuwa uzazi wa mpango ukitumiwa vizuri na jamii nayo inapata faida kwa hiyo zifuatazo ni faida za uzazi wa mpango kwa jamii.

Soma Zaidi...
Mambo ya kuangalia kwa mtoto mdogo

Posti hii inahusu zaidi mambo ya kuangalia kwa mtoto mdogo chini ya umri wa miaka mitano ili kuweza kuweka afya yake kwenye njia safi.

Soma Zaidi...