Mambo muhimu kwa wanawake kabla ya kubeba mimba
Posti hii inahusu zaidi mambo muhimu kwa wanawake kabla ya kubeba mimba,Ni mambo ya kuzingatia ili mama akija kubeba mimba awe mzima kimwili, ki afya na kisaikolojia na hivyo hivyo Mtoto atakayezaliwa atakuwa salama.
Mambo muhimu ya kuzingatia kwa wanawake kabla ya kubeba mimba.
1. Kwanza kabisa tunapaswa kujua kuwa kila mama anapaswa kujifungua mtoto salama kiafya, kiakili na kisaikolojia hili hayo yatimie ni lazima maandalizi ya mbali kuwepo yaani maandalizi kabla ya kubeba mimba kama tutakavyoona hapo chini.
2.kwanza kabisa historia ya Mama na baba wote inapaswa kujulikana kama wanatumia vileo vikali, wanavuta sigara na ni njia gani ya uzazi wa mpango wanayotumia au kama kuna Magonjwa ya kuridhi kwenye familia kama hayo yote yatajulikana ni vizuri kuwapa ushauri ni lini na wakati gani wanapaswa kukutana na kupata mtoto watajayemtaka wakiwa katika hali nzuri na kwa akili timamu
3.Pia Mama anapaswa kupima urefu, uzito, mapigo ya moyo, msukumo wa damu, joto la mwili,upumuaji kuangalia matiti yake kama yana aina yoyote ya uvimbe na kuangalia kama mama ana ugonjwa wowote ambao akibeba mimba unaweza kuleta madhara kwake na kwa mtoto
4. Kuangalia kama Mlay wa kizazi unaweza kufunga iwapo kama mimba ilitungwa na pia kuangalia kama kuna Maambukizi yoyote kwenye mlango wa kizazi hasa kansa ya mlango wa kizazi.
5. Kuangalia kama kuna aina yoyote ya Maambukizi hasa maambukizi ya Magonjwa ya a ngono kwa sababu mama akibeba mimba na magonjwa hayo mimba inaweza kutoka kwa hiyo Magonjwa haya kama yapo yatibiwe mara moja.
6. Pia mama anapaswa kupima wingi wa damu, group la damu, RH factor, maambukizi ya virus vya ukimwi, sukari, mkojo, antibodies na mambo mengine yote mawili na mama akikutwa na shida yoyote anaambiwa cha kufanya na akiona kubwa yuko salama anaweza kubeba mimba na mtoto natumaini atakuwa salama. Kwa hiyo akina Mama kabla ya kubeba mimba mnapaswa kufanya hivyo ili kupata watoto wenye afya njema.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 kitabu cha Simulizi 👉2 ai web app 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Kuwepo kwa mabonge ya damu wakati wa hedhi
Posti hii inahusu zaidi kuwepo kwa mabonge ya damu wakati wa hedhi, tunajua kabisa wakati wa hedhi damu inapaswa kuwa nyepesi na ya kawaida ila kuna wakati mwingine inakuwa na mabonge zifuatazo ni sababu za kuwepo kwa mabonge ya damu wakati wa hedhi.
Soma Zaidi...Fahamu madhara ya Maambukizi ya mfumo wa Uzazi wa mwanamke PID
Posti hii inazungumzia kuhusiana na mathara yanayosababisha Ugonjwa wa Maambukizi ya mfumo wa Uzazi wa mwanamke
Soma Zaidi...Nia za kupima ujauzito ukiwa nyumbani, Njia kuu 10 za kiasili za kupima mimba changa
Kuna njia nyingi zinatajwa zinapima mimba kama chumvi, sukari, mafuta na sabuni. Hata hivyo zipo njia zaidi ya 10 za kiasili za kupima ujauzito. Utajifunza hapa zote
Soma Zaidi...Tatizo la kutokwa na majimaji kwenye uume.
Posti hii inahusu zaidi tatizo la kutokwa na majimaji kwenye uume, ni tatizo ambalo uwakumba baadhi ya wanaume kwa sababu mbalimbali na pia Ugonjwa huu unatibika hasa kwa wale wanaowahi kupata matibabu.
Soma Zaidi...siku za hatari
Hizi ni siku za hatari kupata ujauzito.Siku hizi ndio siku za kupata mimba kwa urahisi
Soma Zaidi...Maambukizi katika mfumo wa Uzazi wa mwanamke
Maambukizi kwenye Njia ya Uzazi kwa kifupi hujulikana Kama PID.ni Maambukizi ya mfumo wa Uzazi yanayoathiri wanawake, Maambukizi haya kwa Kawaida huhusisha sehemu Kama shingo ya uzazi,nyuma ya mfuko wa Uzazi na mirija ya uzazi.
Soma Zaidi...