Mambo muhimu kwa wanawake kabla ya kubeba mimba
Posti hii inahusu zaidi mambo muhimu kwa wanawake kabla ya kubeba mimba,Ni mambo ya kuzingatia ili mama akija kubeba mimba awe mzima kimwili, ki afya na kisaikolojia na hivyo hivyo Mtoto atakayezaliwa atakuwa salama.
Mambo muhimu ya kuzingatia kwa wanawake kabla ya kubeba mimba.
1. Kwanza kabisa tunapaswa kujua kuwa kila mama anapaswa kujifungua mtoto salama kiafya, kiakili na kisaikolojia hili hayo yatimie ni lazima maandalizi ya mbali kuwepo yaani maandalizi kabla ya kubeba mimba kama tutakavyoona hapo chini.
2.kwanza kabisa historia ya Mama na baba wote inapaswa kujulikana kama wanatumia vileo vikali, wanavuta sigara na ni njia gani ya uzazi wa mpango wanayotumia au kama kuna Magonjwa ya kuridhi kwenye familia kama hayo yote yatajulikana ni vizuri kuwapa ushauri ni lini na wakati gani wanapaswa kukutana na kupata mtoto watajayemtaka wakiwa katika hali nzuri na kwa akili timamu
3.Pia Mama anapaswa kupima urefu, uzito, mapigo ya moyo, msukumo wa damu, joto la mwili,upumuaji kuangalia matiti yake kama yana aina yoyote ya uvimbe na kuangalia kama mama ana ugonjwa wowote ambao akibeba mimba unaweza kuleta madhara kwake na kwa mtoto
4. Kuangalia kama Mlay wa kizazi unaweza kufunga iwapo kama mimba ilitungwa na pia kuangalia kama kuna Maambukizi yoyote kwenye mlango wa kizazi hasa kansa ya mlango wa kizazi.
5. Kuangalia kama kuna aina yoyote ya Maambukizi hasa maambukizi ya Magonjwa ya a ngono kwa sababu mama akibeba mimba na magonjwa hayo mimba inaweza kutoka kwa hiyo Magonjwa haya kama yapo yatibiwe mara moja.
6. Pia mama anapaswa kupima wingi wa damu, group la damu, RH factor, maambukizi ya virus vya ukimwi, sukari, mkojo, antibodies na mambo mengine yote mawili na mama akikutwa na shida yoyote anaambiwa cha kufanya na akiona kubwa yuko salama anaweza kubeba mimba na mtoto natumaini atakuwa salama. Kwa hiyo akina Mama kabla ya kubeba mimba mnapaswa kufanya hivyo ili kupata watoto wenye afya njema.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 web hosting 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Mbinu za kupunguza Kichefuchefu
Point hii inahusu zaidi mbinu za kupunguza Kichefuchefu hasa kwa wagonjwa na watumiaji wa madawa mbalimbali yanayoweza kusababisha kichefuchefu.
Soma Zaidi...Aina mbalimbali za mimba kutoka.
Post hii inahusu zaidi aina mbalimbali za mimba kutoka, hizi ni jinsi mimba inavyoonyesha dalili za kutoka na nyingine zinaweza kuonyesha dalili Ila kwa sababu ya huduma mbalimbali za kwanza hizo mimba zinaweza kudhibiiwa na mtoto akazaliwa.
Soma Zaidi...Madhara ya fangasi ukeni
Maambukizi ya fangasi katika sehemu za Siri za mwanamke husababishwa na fangasi wanaoitwa CANDIDA ALBICANS pia maambukizi haya hujulikana kama YEAST INFECTION. Pia hupatikana katika midomo, mpira wa kupitisha chakula,kibofu Cha mkojo ,uume na uke.
Soma Zaidi...Fahamu dawa ya tetracycline katika kupambana na bakteria
Post hii inahusu zaidi dawa ya tetracycline katika kupambana na bakteria,ni mojawapo ya antibiotics au anti bacteria ambayo upambana na bakteria kama tutakavyoona hapo mbeleni.
Soma Zaidi...Malengo ya huduma za uzazi kwa akina Mama.
Posti huu inahusu zaidi malengo ya huduma za uzazi kwa akina Mama, ni huduma muhimu ambazo zimetolewa kwa akina Mama ili kuweza kuepuka hatari mbalimbali zinazowakumba akina Mama wakati wa ujauzito, kujifu na malezi ya watoto chini ya miaka mitano.
Soma Zaidi...je maumivu ya nyonga na tumbo la chini ni dalili ya mimba?
Nina swali langu:-je maumivu ya nyonga na tumbo la chini ni dalili ya mimba?
Soma Zaidi...