Madhara ya sindano za kuzuia mimba kwa vijana.
Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kwa sababu ya matumizi ya sindano za kuzuia mimba kwa vijana ambao hawajafikilia mpango wa kuanza kujifungua watoto.
Madhara ya sindano za kuzuia mimba kwa vijana au wasichana ambao hawana mpango wa kuanza kujifungua.
1. Kwanza kabisa tunapaswa kufahamu maana ya uzazi wa mpango ni njia inayotumiwa na wenza Ili kupata idadi ya watoto wanaowahitaji au kuwapatia nafasi kutoka kwa mtoto mmoja kwenda kwa mwingine ila Kuna wasichana ambao hawana mpango wa kuanza kujifungua karibuni ila wanatumia njia ya uzazi wa mpango kwa mda mrefu na Kuna madhara yake kama ifuatavyo.
2. Kubadilika kwa hedhi.
Kwanza kabisa kama msichana anatumia siku tatu wakati wa hedhi anaweza kuanza kutumia siku tano ,sita Saba na kuendelea hali inayosababisha upungufu wa damu mwilini au pengine damu inakuwa ni nzito au nyepesi kuliko kawaida kwa sababu ya matumizi ya sindano kwa mda mrefu.
3. Maumivu ya kichwa ya mara Kwa mara.
Kwa sababu ya kuwepo au kubadilika kwa homoni usababisha maumivu ya kichwa ya mara Kwa mara au kwa sababu ya kutokwa na damu nyingi nayo usababisha maumivu ya kichwa ya mara Kwa mara.
4. Kuwepo kwa kizungu zungu.
Kwa kawaida kwa sababu ya kutumia dawa za sindano usababisha kuongezeka kwa homoni au kubadilika kwa mwili kwa hali isiyo ya kawaida au kitendo cha kupungua kwa damu mwilini nacho usababisha kuwepo kwa kizungu zungu kwa akina dada.
5. Kuwepo kwa kichefuchefu.
Hali hii utokea kwa sababu ya kuongezeka kwa homoni nyingine kutoka kwenye sindano na Ile hali ya kuvurugika kwa mfumo wa hali ya mwili kwa sababu ya sindano.
6. Kuwepo kwa uzito usio wa kawaida.
Kwa wakati mwingine kunakuwepo na uzito usio wa kawaida kwa sababu ya sindano na meongezeko wa homoni.
7. Kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi.
Kwa sababu ya sindano za kila mwezi na kuharibu mfuko mzima wa mwili usababisha kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi.
8. Kwa hiyo dalili hizi si kwa akina dada tu zinaweza kutokea hata kwa baadhi ya akina Mama kwa hiyo tunaenda kuwataarifu akina dada kusubiri wakati wao ufike ndo wajiingize kwenye matumizi ya uzazi wa mpango.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Simulizi za Hadithi Audio 👉2 kitabu cha Simulizi 👉3 Kitau cha Fiqh 👉4 web hosting 👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉6 ai web app
Post zinazofanana:
Namna ya kufunga kitovu cha mtoto.
Posti hii inahusu zaidi njia au namna ya kufunga kitovu cha mtoto mara tu anapozaliwa, kwa kawaida tunafahamu kwamba ili mtoto aweze kuishi akiwa tumboni anategemea sana kula na kufanya shughuli zake kwa kupitia kwenye plasenta kwa hiyo mtoto akizaliwa tu
Soma Zaidi...Vyanzo vya mwanamke kushindwa kupata ujauzito
Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya mwanamke kushindwa kupata ujauzito, kwa sababu kuna sababu nyingi ambazo Usababisha mwanamke kushindwa kupata ujauzito kama tutakavyoona hapo mbeleni
Soma Zaidi...Faida na hasara za Kufunga kizazi kwa Wanaume
Posti hii inazungumzia Faida, hasara, na madhara ya Kufunga kizazi kwa Wanaume.
Soma Zaidi...Utaratibu wa chakula kwa Mama mjamzito.
Post huu inahusu zaidi utaratibu wa chakula kwa Mama mjamzito, ni chakula anachopaswa kutumia na ambavyo hapaswi kutumia kwa Mama mjamzito mzito, kwa sababu Mama mjamzito anapaswa kuwa makini katika matumizi ya chakula ili kuweza kuongeza vitu muhimu mwil
Soma Zaidi...Hiv n kweli majivu hutoa mimb ya siku moja hadi wiki moja
Inashangaza sana, wakati wengine wanahangaika kutafutavijauzito kwa gharama yoyote ile, kuna wengine wanataka kutoa ujauzito kwa gharama yeyote ile. Unadhani njia za kienyeji sa kutoa mimba ni salama?
Soma Zaidi...Sifa za siku za kupata mimba
Somo hili linakwenda kukueleza baadhi ya sifa za siku za kupata mimba
Soma Zaidi...