Posti hii inahusu zaidi madhara ambayo yanaweza kutokea kwa sababu ya matumizi ya sindano za kuzuia mimba kwa vijana ambao hawajafikilia mpango wa kuanza kujifungua watoto.
1. Kwanza kabisa tunapaswa kufahamu maana ya uzazi wa mpango ni njia inayotumiwa na wenza Ili kupata idadi ya watoto wanaowahitaji au kuwapatia nafasi kutoka kwa mtoto mmoja kwenda kwa mwingine ila Kuna wasichana ambao hawana mpango wa kuanza kujifungua karibuni ila wanatumia njia ya uzazi wa mpango kwa mda mrefu na Kuna madhara yake kama ifuatavyo.
2. Kubadilika kwa hedhi.
Kwanza kabisa kama msichana anatumia siku tatu wakati wa hedhi anaweza kuanza kutumia siku tano ,sita Saba na kuendelea hali inayosababisha upungufu wa damu mwilini au pengine damu inakuwa ni nzito au nyepesi kuliko kawaida kwa sababu ya matumizi ya sindano kwa mda mrefu.
3. Maumivu ya kichwa ya mara Kwa mara.
Kwa sababu ya kuwepo au kubadilika kwa homoni usababisha maumivu ya kichwa ya mara Kwa mara au kwa sababu ya kutokwa na damu nyingi nayo usababisha maumivu ya kichwa ya mara Kwa mara.
4. Kuwepo kwa kizungu zungu.
Kwa kawaida kwa sababu ya kutumia dawa za sindano usababisha kuongezeka kwa homoni au kubadilika kwa mwili kwa hali isiyo ya kawaida au kitendo cha kupungua kwa damu mwilini nacho usababisha kuwepo kwa kizungu zungu kwa akina dada.
5. Kuwepo kwa kichefuchefu.
Hali hii utokea kwa sababu ya kuongezeka kwa homoni nyingine kutoka kwenye sindano na Ile hali ya kuvurugika kwa mfumo wa hali ya mwili kwa sababu ya sindano.
6. Kuwepo kwa uzito usio wa kawaida.
Kwa wakati mwingine kunakuwepo na uzito usio wa kawaida kwa sababu ya sindano na meongezeko wa homoni.
7. Kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi.
Kwa sababu ya sindano za kila mwezi na kuharibu mfuko mzima wa mwili usababisha kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi.
8. Kwa hiyo dalili hizi si kwa akina dada tu zinaweza kutokea hata kwa baadhi ya akina Mama kwa hiyo tunaenda kuwataarifu akina dada kusubiri wakati wao ufike ndo wajiingize kwenye matumizi ya uzazi wa mpango.
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.
Download NowJe umeipenda post hii ?
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za mwanzo za ujauzito katika wiki ya kwanza
Soma Zaidi...Tezi dume hii ni tezi inayopatikana katika katika mfumo wa uzazi wa mwanaume Ila hujulikana kama PROSTATE GLAND. pia hukua karibu na kibofu Cha mkojo na mirija ya mkojo hutumika kuzalisha majimaji (simen) yanayobeba mbegu hivyo bas mk
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za mimba kuanzia siku ya 7 Hadi ya 14
Soma Zaidi...dalili za mimba zinaweza kuwa na mkanganyiko kwani zinafanana na shida nyingine za kiafya. Hali hii utaigunduwa endapo utakuwa na dalili za mimba lakini kila ukipima hakuna mimba.
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia kuhusiana na huduma kwa mama wajawazito na waliojifungua.
Soma Zaidi...ukiwa na ujauzito unaweza kuona mabadiliko mengi katika mwili wako yakiwemo kutokwa na majimaji. je majimaji haya yana dalili gani kwenye ujauzito?
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi sababu za kutoshika mimba kwa mwanamke, kuna kipindi ambacho mwanamke hushindwa kushika mimba kuna sababu mbalimbali mojawapo ni kama zifuatazo
Soma Zaidi...Unaweza kupitiliza siku zako za hedhi kwa sababu nyingi. Post hii itakueleza ni kwa nini umechelewa kupata siku zako.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi mambo ya kuzingatia iwapo mimba imetoka mambo haya yanaweza yakawahusu akina Mama wenyewe, familia na jamii kwa ujumla.
Soma Zaidi...