Dalili za tezi dume na sababu za kutokea kwa tezi dume.

dalili za ugonjwa wa tezi dume, na sababu za kutokea kwa tezi dume, maana ya tezi dume na athari zake

Dalili za tezi dume na sababu za kutokea kwa tezi dume.

TEZI DUME SIO BUSHA, ZIJUWE DALILI ZA TEZI DUME



Watu wengi wamekuwa wakidhania kuwa tezi dume ni busha ama ngiri maji kwa jina jinngine. Hapana hii sio sahihi kabisa. Mpenzi msomaji tambuwa kuwa tezi dume sio busha na haifananni kabisa na busha. Tezi dume isipotibiwa kwa haraka inaweza kuwa hatari sana kwani ina maumivu makali sana. Sasa nini hasa hii tezi dume?. katika makala hii nitakwenda kukupa mwangaza kuhusu tezi dume., dalili za tezi dume na athari za tezi dume kwa afya ako.


Nini maana ya tezi dume
Tezi hii kitaalamu hufahamika kama prostate gland. Hii ni tezi inayopatikana katika mfumo wa uzazi wa kiume. Tezi hii inapatikana jirani na kibofu cha mkojo na mirija ya mkojo. Tezi hii ina kazi ya kuzalisha majimaji ambayo hubeba mbegu za kiume. Majimaji haya ndio yale anayotoa mwanaume anapofikia kilele. Hivyo tezi hii ni muhimu sana katika mfumo wa kizazi wa mwanaume. Tezi hii si kubwa saana inapata sentimita zisizozidi 5. lakini tezi hii hukuwa kadiri umri unavyoenda.


Kwa ufupi wa maneno ni kuwa tezi dume ipo zini ya kibofu karibu na shingo ya kibofu. Na imezunguka mrija unaotoa mkojo kutoka kwenye kibofu kuja nje (urethra). hivyo mkojo unapotoka kwenye kipofu hipitia katikati kwenye tezi dume ukiwa kwenye mrija wa urethra. Urethra ndio mrija unaotoa mkojo kutoka kwenye kibofu.


Vipi ugonjwa wa tezi dume hutokea?
Kama ulivyojifunza hapo juu mkojo ukiwa kwenye mrija hupita katikati ya tezi tume. Sasa tezi hii ina kawaida ya kukuwa kadiri mtu anavyopata umri zaidi. Hivyo basi kadiri tezi hii inapoongezeka ukubwa ndivyo inavyoanza kuminya mirija ya kupitisha mkojo na hatimaye huanza tatizo la ugonjwa wa tezi dume. Tatizo hili kitaalamu hufahamika kama Benign Prostatic Hyperplasia (BPH).


Nini sababu za kutokea kwa tezi duma?
Kama ilivyokwisha kutajwa hapo juu, tezi hii hukuwa kadiri mtu anavyokuwa. Kwa baadhi ya watu inapokuwa huwa kubwa kiasi cha kuanza kuminya mirija ya mkojo na kuleta shida kwenye mfumo wa mkojo. Tafiti mbalimbali zinaonyesha kuwa miongoni mwa mambo yanayohatarisha uwezekano wa kupata ugonjwa huu ni haya yafuatayo:-



1.Umri, kikawaida tezi dume huwapata watu wenye umri kuanzia miaka 40. ni mara chache sana kuwapata walio chini ya umri huo. Pia tezi dume kwa kiasi kikubwa huwapata walio kati ya miaka sitini na kuendelea. Hususan robo tatu ni wale walio na miaka kuanzia 60,na nusu yao ni wale walio na miaka kuanzia 80.



2.Tatizo la tezi dume pia huweza kurithiwa. Yaani kama baba yako ana tezi dume ama yeyote katika damu yako hapo mwanzo alikuwa na tezi dume, hivyo upo uwezekana na wewe kurithi tatizo hili.



3.Pia inaonakana kuwa baadhi ya rangi huathiriwa sana na tatizo la tezi dume. Tafiti zinaonesha kuwa watu walio katika bara la Asia si sana kupatwa na tezi dume kuliko watu weusi na wazungu. Hata hivyo kwa watu weusi upo uwezekano wa kupatwa na tatizo hili katika umri mdogo kuliko wengine.



4.Maradhi, tafiti zinaonyesha kuwa kuna baadhi ya maradhi huweza kupelekea kupatwa na tatizo la tezi dume. Kwa mfano watu wenye maradhi ya sukari, na maradhi ya moyo wapo hatarini kupatwa na tezi dume ukilinganisha na watu wengine.
5.Staili za maisha. Tafiti pia zinaonyesha kuwa watu wenye kiribatumbo na wasiofanya mazoei wapo hatarini kupatwa na tatizo la tezi dume.


Ni zipi dalili za ugonjwa wa tezi dume?
Dalili za tezi dume zinaweza kuwa kali ama hafifu kutoka mtu hadi mtu. Ukali wa dalili hizi hautegemei ukubwa wa tezi. Inaweza kuwa tezi ni kubwa lakini dalili zisiwe kali. Miongoni mwa dalili za tezi dume ni:-



1.Kukojoa mara kwa mara, ama kuhisi kukojoa mara kwa mara
2.Kukojoa mara kwa mara wakati wa usiku
3.Kupatwa na uzgumu kutoa mkojo
4.Mchirizi wa mkojo kuwa dhaifu
5.Mkojo kukatakata unapofika karibu a mwisho
6.Kujichafua wakati wa kukojoa
7.Kushindwa kumaliza mkojo kabisa.
8.Damu kwenye mkojo
9.Kushindwa kukojoa kabisa.
10.Kupata mkojo mchache sana


Kuwa na dalili tajwa hapo juu pekee hakuwezi kukupa uhakika kuwa una tatizo la tezi dume. Kwani dalili tajwa hapo juu zinaweza kuambatananna shida nyingine za kiafya kwa mfano:-
1.Maambukizi ya UTI
2.Kuvimba kwa tezi
3.Kupunguwa ukubwa wa mrija wa mkojo
4.Kuwepo na vijiwe kwenye kibofu
5.Kuwa na shida kwenye mfumo wa neva ambazo hudhibiti ufanyaji kazi wa kibofu
6.Kuwa na saratani
7.Kama upasuaji katika kibofu haukufanyika sawa.


Ni zipi athari za tezi dume kama haitawahi kutibiwa?
Tezi dume ni kama maradhi mengine, inatibika bila wasi. Hata hivyo endapo matibabu yatachelewa athari zifuatazo zinaweza kupatikana:-
1.Kushindwa kabisa kukojoa
2.Kupatwa na maambukizi ya UTI
3.Kupatwa na vijiwe kwenye kibofu
4.Uharibifu wa kibofu unaweza kutokea
5.Figo inaweza kuharibika


Mwisho
Mwisho napenda kumaliza kwa kusema kuwa tatizo la tezi dume linatibika bila wasi. Zipo dawa za hospitali mgonjwa anaweza kupewa. Kamatatizo lake ni kubwa zaidi anaweza kufanyiwa upasuaji. Usisite kutembeleabongoclass.com kwa makala nyingine za aya




Download kitabu cha Afya na Magonjwa
bofya hapa



                   


Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 5083

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Simulizi za Hadithi Audio    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Sababu za kuharibika kwa ujauzito na dalili zake

Dalili za kuharibika kwa ujauzito na dalili za kuharibika kwa ujauzo

Soma Zaidi...
Kwa mjamzito kuumia wakati wa tendo la ndoa tatizo linaweza kuwa ni nini?

Je unaweza kunielezaKwa mjamzito kuumia wakati wa tendo la ndoa tatizo linaweza kuwa ni nini?

Soma Zaidi...
Mabadiliko ya via vya uzazi kwa Mama mjamzito.

Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye via vya uzazi kwa wajawazito, tunajua kuwa Mama akibeba mimba tu kuna mabadiliko utokea katika sehemu mbalimbali za mwili.

Soma Zaidi...
Sababu za kutokea uvimbe kwenye kizazi.

Posti hii inahusu zaidi sababu za kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi,kwa kawaida tumesikia akina mama wengi wanalalamika kuhusu kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi na wengine hawajui sababu zake kwa hiyo sababu zifuatazo ni za kuwepo kwa uvimbe kwenye kizazi.

Soma Zaidi...
Yajue mazoezi ya kegel

Posti inahusu zaidi mazoezi ya kegel, ni mazoezi ambayo ufanywa na watu wengi na sehemu yoyote yanaweza kufanywa kama vile chumbani, sebuleni, uwanjani na sehemu yoyote ile na kwa watu tofauti.

Soma Zaidi...
CHANGAMOTO ZA UJAUZITO, NA DALILI ZAKE NA NAMNA YA KUKABILIANA NAZO

Utawezaje kukabiliana na changamoto za ujauzito, je ni zipi changamoto hizo. Hapa nitakujuza.

Soma Zaidi...
Dalili za mimba yenye uvimbe

Mimba ya tumbo - pia inajulikana kama hydatidiform mole - ni ugumu usiyo na kansa (benign) ambayo hutokea kwenye uterasi. Mimba ya molar huanza wakati yai linaporutubishwa, lakini badala ya mimba ya kawaida, yenye uwezo wa kutokea, plasenta hukua na kuwa

Soma Zaidi...
faida za tendo ka ndoa wakati wa ujauzito

Kufanya tendo la ndoa wakati wa ujauzito kina faida nyingi kwa mama na mtoto. Miongni mwa faida hizo ni kuimarisha mfumo wa kinga wa mama, kumuondolea stress na ukuajinmzuri wa mimba

Soma Zaidi...
Jinsi ya kuacha kupiga punyeto.

Post hii inakwenda kukupa njia za kukusaidia kuacha punyeto.

Soma Zaidi...