Dalili za tezi dume na sababu za kutokea kwa tezi dume.

dalili za ugonjwa wa tezi dume, na sababu za kutokea kwa tezi dume, maana ya tezi dume na athari zake

Dalili za tezi dume na sababu za kutokea kwa tezi dume.

TEZI DUME SIO BUSHA, ZIJUWE DALILI ZA TEZI DUME



Watu wengi wamekuwa wakidhania kuwa tezi dume ni busha ama ngiri maji kwa jina jinngine. Hapana hii sio sahihi kabisa. Mpenzi msomaji tambuwa kuwa tezi dume sio busha na haifananni kabisa na busha. Tezi dume isipotibiwa kwa haraka inaweza kuwa hatari sana kwani ina maumivu makali sana. Sasa nini hasa hii tezi dume?. katika makala hii nitakwenda kukupa mwangaza kuhusu tezi dume., dalili za tezi dume na athari za tezi dume kwa afya ako.


Nini maana ya tezi dume
Tezi hii kitaalamu hufahamika kama prostate gland. Hii ni tezi inayopatikana katika mfumo wa uzazi wa kiume. Tezi hii inapatikana jirani na kibofu cha mkojo na mirija ya mkojo. Tezi hii ina kazi ya kuzalisha majimaji ambayo hubeba mbegu za kiume. Majimaji haya ndio yale anayotoa mwanaume anapofikia kilele. Hivyo tezi hii ni muhimu sana katika mfumo wa kizazi wa mwanaume. Tezi hii si kubwa saana inapata sentimita zisizozidi 5. lakini tezi hii hukuwa kadiri umri unavyoenda.


Kwa ufupi wa maneno ni kuwa tezi dume ipo zini ya kibofu karibu na shingo ya kibofu. Na imezunguka mrija unaotoa mkojo kutoka kwenye kibofu kuja nje (urethra). hivyo mkojo unapotoka kwenye kipofu hipitia katikati kwenye tezi dume ukiwa kwenye mrija wa urethra. Urethra ndio mrija unaotoa mkojo kutoka kwenye kibofu.


Vipi ugonjwa wa tezi dume hutokea?
Kama ulivyojifunza hapo juu mkojo ukiwa kwenye mrija hupita katikati ya tezi tume. Sasa tezi hii ina kawaida ya kukuwa kadiri mtu anavyopata umri zaidi. Hivyo basi kadiri tezi hii inapoongezeka ukubwa ndivyo inavyoanza kuminya mirija ya kupitisha mkojo na hatimaye huanza tatizo la ugonjwa wa tezi dume. Tatizo hili kitaalamu hufahamika kama Benign Prostatic Hyperplasia (BPH).


Nini sababu za kutokea kwa tezi duma?
Kama ilivyokwisha kutajwa hapo juu, tezi hii hukuwa kadiri mtu anavyokuwa. Kwa baadhi ya watu inapokuwa huwa kubwa kiasi cha kuanza kuminya mirija ya mkojo na kuleta shida kwenye mfumo wa mkojo. Tafiti mbalimbali zinaonyesha kuwa miongoni mwa mambo yanayohatarisha uwezekano wa kupata ugonjwa huu ni haya yafuatayo:-



1.Umri, kikawaida tezi dume huwapata watu wenye umri kuanzia miaka 40. ni mara chache sana kuwapata walio chini ya umri huo. Pia tezi dume kwa kiasi kikubwa huwapata walio kati ya miaka sitini na kuendelea. Hususan robo tatu ni wale walio na miaka kuanzia 60,na nusu yao ni wale walio na miaka kuanzia 80.



2.Tatizo la tezi dume pia huweza kurithiwa. Yaani kama baba yako ana tezi dume ama yeyote katika damu yako hapo mwanzo alikuwa na tezi dume, hivyo upo uwezekana na wewe kurithi tatizo hili.



3.Pia inaonakana kuwa baadhi ya rangi huathiriwa sana na tatizo la tezi dume. Tafiti zinaonesha kuwa watu walio katika bara la Asia si sana kupatwa na tezi dume kuliko watu weusi na wazungu. Hata hivyo kwa watu weusi upo uwezekano wa kupatwa na tatizo hili katika umri mdogo kuliko wengine.



4.Maradhi, tafiti zinaonyesha kuwa kuna baadhi ya maradhi huweza kupelekea kupatwa na tatizo la tezi dume. Kwa mfano watu wenye maradhi ya sukari, na maradhi ya moyo wapo hatarini kupatwa na tezi dume ukilinganisha na watu wengine.
5.Staili za maisha. Tafiti pia zinaonyesha kuwa watu wenye kiribatumbo na wasiofanya mazoei wapo hatarini kupatwa na tatizo la tezi dume.


Ni zipi dalili za ugonjwa wa tezi dume?
Dalili za tezi dume zinaweza kuwa kali ama hafifu kutoka mtu hadi mtu. Ukali wa dalili hizi hautegemei ukubwa wa tezi. Inaweza kuwa tezi ni kubwa lakini dalili zisiwe kali. Miongoni mwa dalili za tezi dume ni:-



1.Kukojoa mara kwa mara, ama kuhisi kukojoa mara kwa mara
2.Kukojoa mara kwa mara wakati wa usiku
3.Kupatwa na uzgumu kutoa mkojo
4.Mchirizi wa mkojo kuwa dhaifu
5.Mkojo kukatakata unapofika karibu a mwisho
6.Kujichafua wakati wa kukojoa
7.Kushindwa kumaliza mkojo kabisa.
8.Damu kwenye mkojo
9.Kushindwa kukojoa kabisa.
10.Kupata mkojo mchache sana


Kuwa na dalili tajwa hapo juu pekee hakuwezi kukupa uhakika kuwa una tatizo la tezi dume. Kwani dalili tajwa hapo juu zinaweza kuambatananna shida nyingine za kiafya kwa mfano:-
1.Maambukizi ya UTI
2.Kuvimba kwa tezi
3.Kupunguwa ukubwa wa mrija wa mkojo
4.Kuwepo na vijiwe kwenye kibofu
5.Kuwa na shida kwenye mfumo wa neva ambazo hudhibiti ufanyaji kazi wa kibofu
6.Kuwa na saratani
7.Kama upasuaji katika kibofu haukufanyika sawa.


Ni zipi athari za tezi dume kama haitawahi kutibiwa?
Tezi dume ni kama maradhi mengine, inatibika bila wasi. Hata hivyo endapo matibabu yatachelewa athari zifuatazo zinaweza kupatikana:-
1.Kushindwa kabisa kukojoa
2.Kupatwa na maambukizi ya UTI
3.Kupatwa na vijiwe kwenye kibofu
4.Uharibifu wa kibofu unaweza kutokea
5.Figo inaweza kuharibika


Mwisho
Mwisho napenda kumaliza kwa kusema kuwa tatizo la tezi dume linatibika bila wasi. Zipo dawa za hospitali mgonjwa anaweza kupewa. Kamatatizo lake ni kubwa zaidi anaweza kufanyiwa upasuaji. Usisite kutembeleabongoclass.com kwa makala nyingine za aya




Download kitabu cha Afya na Magonjwa
bofya hapa



                   


Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Uzazi Main: Afya File: Download PDF Views 8533

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 web hosting    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Simulizi za Hadithi Audio   

Post zinazofanana:

Nimetoka kufanya tendo la ndoa ghafla tumbo likaanza kukaza upande wa kushoto na kutoka maji yenye uzito wa kawaida kama ute mengi je hii itakuwa ni nini

Maumivu yavtumbo huwenda yakachanganya sana, Keane yanahusianana sababu nyingi sana. Kina baadhi ya watu hupata na maumivu ya tumbo wakati wa tendo la ndoa ama punde tu baada ya kumaliza.

Soma Zaidi...
Umuhimu wa maji yaliyomo kwenye mfuko wa mtoto akiwa tumboni mwa mama

Post hii inahusu zaidi umuhimu wa maji yaliyomo kwenye mfuko wa mtoto akiwa tumboni. Ni maji ambayo kwa kitaalamu huitwa (Amniotic fluid)

Soma Zaidi...
Dalili za kupasuka kondo la nyuma (placenta)

Posti hii inazungumzia kuhusiana na Kupasuka kwa kondo la nyuma (plasenta) (abruptio placentae) ni tatizo lisilo la kawaida lakini kubwa la ujauzito.Kondo la nyuma (Placenta) ni muundo ambao hukua ndani ya uterasi wakati wa ujauzito ili kumlisha mtoto ana

Soma Zaidi...
Maambukizi kwenye kitovu cha mtoto.

Posti hii inahusu zaidi Maambukizi kwenye kitovu cha mtoto, ni Maambukizi ambayo yanaweza kutokea kwenye kitovu cha mtoto pale ambapo mtoto amezaliwa inawezekana ni kwa sababu ya hali ya mtoto au huduma kuanzia kwa wakunga na wale wanaotumia mtoto.

Soma Zaidi...
Mama mjamzito anaruhusiwa kushiriki tendo la ndoa?

Mama mjamzito anaruhusiwa kushiriki tendo la ndoa mpaka siku ya kujifungua Kama mume wake pamoja na yeye akiwa Hana maambukizi ya zinaa na Kama akiona dalili zozote zile za hatari ndio hataruhusiwa kushiriki tendo la ndoa.

Soma Zaidi...
Je bado unasumbuliwa na nguvu za kiume?

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kuondoa tatizo la nguvu za kiume

Soma Zaidi...
Njia za uzazi wa mpango kwa watu wenye Ukimwi

Posti hii inahusu zaidi njia za uzazi wa mpango kwa watu waliopata maambukizi ya Virusi vya Ukimwi.

Soma Zaidi...
Uzazi wa mpango kwa njia ya kumwaga manii nje.

Posti hii inahusu zaidi uzazi wa mpango kwa njia ya kumwaga shahawa nje, hii ni njia mojawapo kati ya njia za uzazi wa mpango ambapo mwanaume humwaga nje mbegu ili asimpatie Mama mimba.

Soma Zaidi...
NAMNA YA KUITAMBUA SIKU HATARI YA KUPATA MIMBA (UJAUZITO)

SIKU YA KUPATA UJAUZITO Mimba hutokea pindi mbegu ya kiume (sperm) inapokutana na yai la mwanamke (ova) na kuungana kwa pamoja kutengeneza selli moja iitwayo zygote.

Soma Zaidi...
Ni zipi njia za kutatua tatizo la nguvu za kiume

Somo hili linakwenda kukuletea njia za kutatua tatizo la nguvu za kiume

Soma Zaidi...