DALILI ZA UGONJWA WA MALARIA, (homa,uchovu, kutapika, kichefuchefu, maumivu ya kichwa n.k)
DALILI ZA MALARIA
Dalili za malaria huenda pia zikafungamana na maradhi mengine, lakini endapo zikikusanyika pamoja kwa asilimia kubwa vitakuwa vinaonyesha uwepo wa malaria. Kumbuka hizi ni dalili tu, lakini ni vyema kupima ili kuwa na uhakika zaidi kabla ya kumeza dawwa.
Homa, homa ni kupanda kwa joto mwilini. Kikawaida homa ni dalili za maradhi mengi sanaila leo nitakueleza homa ya malaria ilivyo. Kikawaida hima ya malaria inaweza kuambatana na mambo kadhaa wa kadhaa. Mambo hayo ni kama
Kuhisi baridi, kutetemeka na kutaka kuotea jua ama moto. Haijalishi ni saa ngapi iwe mchana ama usiku lakini mgonjwa atahisi baridi kali sana. Na inaweza kumsababishia hali ya kutetemeka viungo ama taya za mdomo wake kugongana kwa baridi. Hivyo endapo homa itaungana na hali hii huenda ni malaria. Lakini haitishi, inaweza pia kuambatana na japo hili hap chini:-
Maumivu ya kichwa, uchovu na maumivu ya misuli pamoja na viungio. Endapo homa ya mgojwa itaambatana na baridi, kisha ikafuatiwa na maumivu ya kichwa, maumivu haya yanaambatana na misuli kuuma pamoja na viungio. Mgonjwa anahisi katikati ya akutano ya viungio kama kuna vuta. Halli hizi zikikusanyika kwa pamoja huashiria malaria.
Mvurugiko wa tumbo unaopelekea kichefuchefu, ama kuharisha, ama kutapika ama vyote kwa pamoja. Mgonjwa anaweza kupata hali moja kati ya hizi ama akawa nazo zote. Mgonjwa anaweza kutapika maji ama chakula alichokula ama anaweza kutapika ile tunayoita nyongo. Hali hizi zinaweza kumpelekea mgonjwa akachoka sana. Tofauti na kuchoka huku lakini hatakuwa na hamu ya kula, na hata ladha ya chakula inabadilika na kuwa kichungu.
Uchovu, kukosa hamu ya kula, maumivu ya viungo, kuchanganyikiwa, maumivu ya kichwa, kutapika ama kuharishah. Hizi ni katika dalili za malaria.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 ai web app 👉2 Dua za Mitume na Manabii 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
Uchunguzi wa kuharisha damu na tiba yake
Posti hii inahusu zaidi uchunguzi wa kuharisha damu na Tiba yake, ni Ugonjwa ambao unaowashambulia sana watoto hasa wenye chini ya umri wa miaka mitano, kwa hiyo huoaugonjwa tunaweza kuutambua na kutibu kwa njia zifuatazo.
Soma Zaidi...Njia za jumla za kujikinga na magonjwa mbalimbali
Posti hii inahusu zaidi njia mbalimbali za kujikinga na magonjwa, kwa kawaida tunajua wazi kuwa magonjwa yapo na yanasambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na mengine hayasambai yanaweza kumpata mtu mmoja akapona au magonjwa mengine si ya kupona
Soma Zaidi...Virusi vya Homa ya Ini (Hepatitis B): Dalili na chanjo.
Homa ya ini aina ya B (Hepatitis B) ni maambukizi makubwa ya virusi yanayoathiri ini. Virusi hivi vinaweza kusababisha ugonjwa wa papo hapo (wa muda mfupi) au sugu (wa maisha yote). Maambukizi sugu ya Hepatitis B yanaweza kusababisha uharibifu mkubwa wa ini, ikiwemo makovu (cirrhosis), saratani ya ini, na kushindwa kwa ini kufanya kazi. Makala haya yanakupa uelewa wa dalili zake na umuhimu wa chanjo kama njia kuu ya kujikinga.
Soma Zaidi...Sababu za Maambukizi kwenye mifupa.
Post hii inahusu zaidi Maambukizi kwenye mifupa ambayo kwa kitaalamu huitwa Osteomyelitis, ni Maambukizi ambayo hutokea kwenye mifupa kwa sababu mbalimbali ambazo usababisha ugonjwa huu.
Soma Zaidi...Jinsi ya Kumsaidia Mtoto Mwenye Kikohozi
Kikohozi ni njia ya asili ya mwili kujisafisha, lakini kwa mtoto, inaweza kuwa chanzo cha usumbufu mkubwa na wasiwasi kwa wazazi. Post hii inatoa mbinu salama na za nyumbani za kumsaidia mtoto kupata nafuu, huku ikielekeza dalili za hatari zinazohitaji msaada wa kitabibu haraka.
Soma Zaidi...Mimba kuharibika (Miscarriage): Sababu na dalili zake.
Mimba kuharibika ni kupotea kwa ujauzito kabla ya wiki ya 20 ya ujauzito. Hali hii ni jambo linaloweza kuleta huzuni kubwa kwa familia. Ingawa inaweza kutokea ghafla, ni muhimu kuelewa kuwa mara nyingi husababishwa na sababu za kibiolojia zisizo chini ya uwezo wa mama. Makala hii inaelezea sababu za kawaida, dalili za tahadhari, na hatua za kuchukua baada ya kupitia hali hii.
Soma Zaidi...