picha

Sababu za Maambukizi kwenye mifupa.

Post hii inahusu zaidi Maambukizi kwenye mifupa ambayo kwa kitaalamu huitwa Osteomyelitis, ni Maambukizi ambayo hutokea kwenye mifupa kwa sababu mbalimbali ambazo usababisha ugonjwa huu.

Sababu za Maambukizi kwenye mifupa.

Kwanza kabisa Maambukizi kwenye mifupa yanaweza kuwa ya mda mfupi au pengine yanakuwa ya mda mrefu, Maambukizi haya ushambulia hasa sehemu za mikono, miguu na sehemu za kwenye kiuno ambapo mtu uhisi sana maumivu na pengine ikitokea mgonjwa akapatiwa matibabu mapema anaweza kupona na kuendelea kwenye hali yake ya kawaida, kwa hiyo iwapo mtu akasikia maumivu yasiyo ya kawaida kwenye mikono , miguu na kiuno anapaswa kuwaona wataalamu wa afya kwa matibabu zaidi.

 

1. Maambukizi haya usababishwa na bakteria, bakteria hao kwa kitaalamu huitwa staphylococcus Aureus na aina nyingine ya bakteria ambao nao kwa kitaalamu huitwa group B streptococcus, bakteria hao upitia sehemu mbalimbali za mwili na kuingia kwenye mifupa na kusababisha madhara makubwa. Kwa sababu ya kuwepo kwa Maambukizi haya yanayosababishwa na bakteria dawa mbalimbali utumika kutibu maambukizi haya, Ili mradi mgonjwa anapaswa kuwahi hospitali ili kupata matibabu mapema.

 

2. Pia ugonjwa huu usababishwa na Maambukizi kutoka sehemu mbalimbali za mwili kama vile Maambukizi kwenye mfumo wa hewa, Maambukizi kwenye sehemu ya ndani ya sikio, tonsis ambazo ni kali  kuoza kwa meno  haya Maambukizi yakikaa mwilini na usababisha na mifupa kupata Maambukizi kwa sababu bakteria hao waliopo kwenye sehemu nyingine za mwili wanaweza pia kusambaza na kushambulia mifupa na kusababisha ugonjwa huu. Kwa hiyo tunapaswa kutibu Maambukizi yoyote kwenye mwili ili kuepuka kuwepo kwa madhara mengine.

 

Kuwepo kwa aina yeyote ya uwazi kwenye mifupa.kitendo cha kuwepo kwa uwazi wowote kwenye mifupa usababisha Maambukizi kwenye mifupa, kwa mfano kuwepo kwa kidonda kilicho wazi, kuvunjika ambapo wadudu wanaweza kupita  na kuharibu mfupa

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2322

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game     👉2 web hosting     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 Simulizi za Hadithi Audio     👉5 Dua za Mitume na Manabii     👉6 Kitau cha Fiqh    

Post zinazofanana:

Ujuwevmv ugonjwa Nimonia na dalili zake

Nimonia ni Hali ya kuvimba pafu inayoathiri hasa vifuko vya hewa viitwavyo Alveoli, husababishwa na Maambukizi ya virusi

Soma Zaidi...
Dalili za tezi dume ambayo hazijashuka (cryptorchidism)

Tezi dume ambayo haijashuka si ya kawaida kwa ujumla, lakini ni ya kawaida kwa wavulana waliozaliwa kabla ya wakati.na muda mwingine zikipanda tumboni huwa hazishuki kabisa kwenye korodani.

Soma Zaidi...
Maambukizi ya njia ya mkojo kwa wanawake

​Maambukizi ya Njia ya Mkojo (UTI) ni moja kati ya changamoto kubwa za kiafya zinazowasumbua wanawake wengi kote ulimwenguni. Makala haya yanajadili kwa kina vyanzo vya maambukizi haya, dalili zake, sababu zinazowafanya wanawake kuwa katika hatari zaidi, mbinu za kujikinga, na ufafanuzi wa ukweli wa kisayansi dhidi ya dhana potofu zilizopo kwenye jamii.

Soma Zaidi...
Magonjwa ya kuambukiza

Magonjwa ya kuambukiza: Ni yale yanayoweza kuambukizwa kutoka kwa mtu mmoja hadi kwa mwingine au kutoka kwa wanyama kwenda kwa mtu Mlipuko tukio lililoenea la ugonjwa katika jamii kwa wakati fulani ambao huonekana kama kesi mpya kwa kiwango ambacho kinazi

Soma Zaidi...
Dalili za vidonda vya tumbo

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu dalili za vidonda vya tumbo

Soma Zaidi...
Dalili za moyo kushindwa kufanya kazi (heart failure)

post inaonyesha dalili mbalimbali za Kushindwa kwa moyo, wakati mwingine hujulikana kama kutofaulu kwa moyo, hutokea wakati misuli ya moyo wako haisukuma damu kama inavyopaswa. Hali fulani, kama vile ateri nyembamba katika moyo wako (Ugonjwa wa ateri y

Soma Zaidi...