Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)
mbinu walizotumia Makafiri wa Kiqureish katika kuupinga Uislamu Makkah.
- Maqureish wa Makkah walitumia kila mbinu kuhakikisha kuwa ujumbe wa Uislamu haufiki na kukubalika katika jamii yao, miongoni ni hizi zifuatazo;
- Makafiri walimdhihaki Mtume (s.a.w) na waumini wachache kwa
kumuita majina mabaya kama; mwendawazimu, mtunga mashiri,
aliyepagawa na mashetani, mchawi, n.k.
- Pamoja na kusimangwa huko Mtume (s.a.w) na waislamu hawakukata
tamaa, waliendelea kuutangaza Uislamu katika jamii yote.
- Wakuu wa Maquraish walimuagiza Abu Talib amkataze Muhammad
(mwanae) kuendelea kuutangaza Uislamu kwa kumbadilishia mtoto
mwingine la sivyo watamshambulia yeye na Muhammad (s.a.w).
- Mbinu hii haikufanikiwa badala yake Abu Talib alimuunga mkono
Mtume (s.a.w) kwa kazi yake baada ya kujua msimamo wake.
- Maquraish walitumia diplomasia kwa kumtaka Mtume (s.a.w) aache
kazi ya kuutangaza Uislamu kwa kumpa kati ya vitu vifuatavyo;
utajiri, mwanamke mzuri, madaraka au yote kama akitaka.
- Mtume (s.a.w) aliwakatalia vyote hivyo kwa kumsomea aya za Qur’an
(41:1-37) mjumbe aliyetumwa kazi hiyo, Utbah bin Rabi’ah.
- Maqureish walimletea Mtume (s.a.w) pendekezo kuwa washirikiane
katika ibada kwa awamu, mwaka mmoja wamuabudu Mungu mmoja
kwa pamoja na mwaka unaofuatia waabudu miungu yao pamoja pia.
- Hapo ndipo iliposhuka suratul-Kafiruun kuvunja pendekezo lao hilo la
kushiki katika ibada na Mtume akawasomea aya za Qur’an kukataa.
Rejea Qur’an (109:1-6) na (10:15).
- Baada ya Maqureish kuona mbinu zote zimefeli, walianza kutumia
nguvu na mabavu kuwatesa, kuwanyonga na kuwaua Waislamu
waliong’ang’ani imani yao kama akina; Bilal bin Rabbah, Sumaiyya,
Ammar bin Yasir na baba yake, n.k.
- Pamoja na mateso na mauaji, waislamu walibakia na msimamo wao
bila kutetereka na kukata tamaa.
- Maquraish kwa kuhofia ujumbe wa Qur’an kuenea kwa watu,
walianza kuzuia watu kwenda kuonana na Mtume (s.a.w) kwa
kuwashawishi kuwa wasisikilize aya za Qur’an kwani ni uchawi,
mashairi ya Muhammad.
- Walizidi kufitinisha kwa kumzuia Mtume (s.a.w) kuswali na
kuwaambia watu kuwa Muhammad anapinga ibada na miungu wenu,
lakini mbinu na ushawishi wao ulifeli pia.
Rejea Qur’an (31:6), (41:26), (10:38), (11:13) na (96:9-19).
- Maquraish walizidi kuongeza mateso kwa waislamu kwa kutenga na
kuwafukuza Makka na kwenda kuishi katika jangwa la Shi’ab miaka
mitatu bila chakula wala mahusiano mengine ya kijamii.
- Mbinu pia ilifeli baada ya baadhi ya Maquiesh kuona huruma kwa
ndugu zao waliotengwa bila sababu za msingi, hivyo wakavunja
mkataba wa kuwatenga.
- Maquish waliazimia kumuua Mtume (s.a.w) na rafiki yake Abubakar
(r.a) walipogundua kuwa waislamu wamehamia mji wa Madinah.
- Mbinu hii pia ilifeli baada ya Allah (s.w) kuwanusu katika pango yeye
na sahibu yake Abubakar (r.a).
Rejea Qur’an (9:40).
Je! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu
Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Download PDF
Share On
Facebook
or
Whatsapp
Imesomwa mara 2332
Sponsored links
π1 kitabu cha Simulizi
π2 Kitabu cha Afya
π3 Madrasa kiganjani
π4 Kitau cha Fiqh
Nabii Isa(a.s) Azungumza Akiwa Mtoto Mchanga
Maryam akamtwaa mwanawe, akaenda naye kwa jamaa zake amembeba. Soma Zaidi...
Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Nabii Daud(a.s)
Kutokana historia ya Nabii Daud (a. Soma Zaidi...
KIKAO CHA KUMFUKUZA MTUME MUHAMMAD KUTOKA MAKKAH (MAKA), KIKAO ALICHOHUDHURIA IBLISI
KIKAO CHAKALIWA KUJADILI HATMA YA MUHAMMAD KATIKA MJI WA MAKAHiki ni kikao kizito hakijapata kutokea toka muhammad katika ji wa maka. Soma Zaidi...
Yunus(a.s) Kulingania Uislamu kwa Watu Wake
Nabii Yunus(a. Soma Zaidi...
vita vya ahzab, sababu ya kutokea vita hivi na mafunzo tunayoyapata
Vita vya Ahzab- Maquraish waliungana na mayahudi, wanafiki na makabila mengine ya waarabu baada ya kuona kuwa wao peke yao hawawezi kuufuta Uislamu. Soma Zaidi...
Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Adam(a.s)
(i) Utukufu wa mtu katika Uislamu hautokani na nasaba, rangi,kabila,utajiri ila uwajibikaji kwa Allah(s. Soma Zaidi...
Khalifa na Uendeshaji wa Dola kwa ujumla, kulinda wasio waislamu na haki zao na mali zao.
Soma Zaidi...
Wapinzani wa Ujumbe wa Nabii Salih(a.s)
Baada ya Nabii Salih(a. Soma Zaidi...
Kuangamia kwa Mtoto na Mke wa Nuhu(a.s)
Tukirejea Qurβan (11:36-48) na (23:26 -29) tunapata maelezo juu ya mchakato wa kuangamizwa makafiri na kuokolewa waumini katika kaumu ya Nabii Nuhu(a. Soma Zaidi...
Mtume amezaliwa mwaka gani?
Na tumemuusia mwanaadamu afanye wema kwa wazazi wake. Soma Zaidi...
Hali za bara arab zama za jahiliya karne ya 6 kabla ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad
7. Soma Zaidi...
Msimamo wa Nabii Hud(a.s) Dhidi ya Makafiri wa Kaumu Yake
Pamoja na kwamba alipingwa na nguvu za Dola ya makafiri wa kaumu yake, Mtume Hud(a. Soma Zaidi...