Mbinu walizotumia makafiri wa kiqureish katika kuupinga uislamu makkah
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)
mbinu walizotumia Makafiri wa Kiqureish katika kuupinga Uislamu Makkah.
- Maqureish wa Makkah walitumia kila mbinu kuhakikisha kuwa ujumbe wa Uislamu haufiki na kukubalika katika jamii yao, miongoni ni hizi zifuatazo;
- Kumkatisha tamaa Mtume (s.a.w) na wafuasi wake.
- Makafiri walimdhihaki Mtume (s.a.w) na waumini wachache kwa
kumuita majina mabaya kama; mwendawazimu, mtunga mashiri,
aliyepagawa na mashetani, mchawi, n.k.
- Pamoja na kusimangwa huko Mtume (s.a.w) na waislamu hawakukata
tamaa, waliendelea kuutangaza Uislamu katika jamii yote.
- Mbinu ya Vitisho na Kumkataza Mtume (s.a.w) kuulingania Uislamu kwa kumtumia Ami yake, Abu Talib.
- Wakuu wa Maquraish walimuagiza Abu Talib amkataze Muhammad
(mwanae) kuendelea kuutangaza Uislamu kwa kumbadilishia mtoto
mwingine la sivyo watamshambulia yeye na Muhammad (s.a.w).
- Mbinu hii haikufanikiwa badala yake Abu Talib alimuunga mkono
Mtume (s.a.w) kwa kazi yake baada ya kujua msimamo wake.
- Mbinu ya Kumhonga na kumrubuni Mtume (s.a.w).
- Maquraish walitumia diplomasia kwa kumtaka Mtume (s.a.w) aache
kazi ya kuutangaza Uislamu kwa kumpa kati ya vitu vifuatavyo;
utajiri, mwanamke mzuri, madaraka au yote kama akitaka.
- Mtume (s.a.w) aliwakatalia vyote hivyo kwa kumsomea aya za Qur’an
(41:1-37) mjumbe aliyetumwa kazi hiyo, Utbah bin Rabi’ah.
- Mbinu ya kutaka kumlaghai Mtume (s.a.w).
- Maqureish walimletea Mtume (s.a.w) pendekezo kuwa washirikiane
katika ibada kwa awamu, mwaka mmoja wamuabudu Mungu mmoja
kwa pamoja na mwaka unaofuatia waabudu miungu yao pamoja pia.
- Hapo ndipo iliposhuka suratul-Kafiruun kuvunja pendekezo lao hilo la
kushiki katika ibada na Mtume akawasomea aya za Qur’an kukataa.
Rejea Qur’an (109:1-6) na (10:15).
- Mbinu ya Kuwatesa na kuwaua Waislamu.
- Baada ya Maqureish kuona mbinu zote zimefeli, walianza kutumia
nguvu na mabavu kuwatesa, kuwanyonga na kuwaua Waislamu
waliong’ang’ani imani yao kama akina; Bilal bin Rabbah, Sumaiyya,
Ammar bin Yasir na baba yake, n.k.
- Pamoja na mateso na mauaji, waislamu walibakia na msimamo wao
bila kutetereka na kukata tamaa.
- Mbinu ya fitina, kuipinga Qur’an na kuzuia watu kukutana na Mtume (s.a.w).
- Maquraish kwa kuhofia ujumbe wa Qur’an kuenea kwa watu,
walianza kuzuia watu kwenda kuonana na Mtume (s.a.w) kwa
kuwashawishi kuwa wasisikilize aya za Qur’an kwani ni uchawi,
mashairi ya Muhammad.
- Walizidi kufitinisha kwa kumzuia Mtume (s.a.w) kuswali na
kuwaambia watu kuwa Muhammad anapinga ibada na miungu wenu,
lakini mbinu na ushawishi wao ulifeli pia.
Rejea Qur’an (31:6), (41:26), (10:38), (11:13) na (96:9-19).
- Mbinu ya kuwatenga na kila huduma ya kijamii.
- Maquraish walizidi kuongeza mateso kwa waislamu kwa kutenga na
kuwafukuza Makka na kwenda kuishi katika jangwa la Shi’ab miaka
mitatu bila chakula wala mahusiano mengine ya kijamii.
- Mbinu pia ilifeli baada ya baadhi ya Maquiesh kuona huruma kwa
ndugu zao waliotengwa bila sababu za msingi, hivyo wakavunja
mkataba wa kuwatenga.
- Mbinu ya kutaka kumuua Mtume (s.a.w).
- Maquish waliazimia kumuua Mtume (s.a.w) na rafiki yake Abubakar
(r.a) walipogundua kuwa waislamu wamehamia mji wa Madinah.
- Mbinu hii pia ilifeli baada ya Allah (s.w) kuwanusu katika pango yeye
na sahibu yake Abubakar (r.a).
Rejea Qur’an (9:40).
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉3 Madrasa kiganjani 👉4 Bongolite - Game zone - Play free game 👉5 Kitau cha Fiqh 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
Ukasha bin Mihsan ni Sahaba aliyechangamkia Fursa
Katika somo hili utakwnda kujifunz anamna nambavyo Sahaba Ukasha alivyochangamkia fursa katika mambo ya heri
Soma Zaidi...Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Zakaria(a.s) na Yahya(a.s)
Kutokana na Historia ya Nabii Zakaria (a.
Soma Zaidi...KIKAO CHA KUMFUKUZA MTUME MUHAMMAD KUTOKA MAKKAH (MAKA), KIKAO ALICHOHUDHURIA IBLISI
KIKAO CHAKALIWA KUJADILI HATMA YA MUHAMMAD KATIKA MJI WA MAKAHiki ni kikao kizito hakijapata kutokea toka muhammad katika ji wa maka.
Soma Zaidi...