Mbinu walizotumia makafiri wa kiqureish katika kuupinga uislamu makkah
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)
mbinu walizotumia Makafiri wa Kiqureish katika kuupinga Uislamu Makkah.
- Maqureish wa Makkah walitumia kila mbinu kuhakikisha kuwa ujumbe wa Uislamu haufiki na kukubalika katika jamii yao, miongoni ni hizi zifuatazo;
- Kumkatisha tamaa Mtume (s.a.w) na wafuasi wake.
- Makafiri walimdhihaki Mtume (s.a.w) na waumini wachache kwa
kumuita majina mabaya kama; mwendawazimu, mtunga mashiri,
aliyepagawa na mashetani, mchawi, n.k.
- Pamoja na kusimangwa huko Mtume (s.a.w) na waislamu hawakukata
tamaa, waliendelea kuutangaza Uislamu katika jamii yote.
- Mbinu ya Vitisho na Kumkataza Mtume (s.a.w) kuulingania Uislamu kwa kumtumia Ami yake, Abu Talib.
- Wakuu wa Maquraish walimuagiza Abu Talib amkataze Muhammad
(mwanae) kuendelea kuutangaza Uislamu kwa kumbadilishia mtoto
mwingine la sivyo watamshambulia yeye na Muhammad (s.a.w).
- Mbinu hii haikufanikiwa badala yake Abu Talib alimuunga mkono
Mtume (s.a.w) kwa kazi yake baada ya kujua msimamo wake.
- Mbinu ya Kumhonga na kumrubuni Mtume (s.a.w).
- Maquraish walitumia diplomasia kwa kumtaka Mtume (s.a.w) aache
kazi ya kuutangaza Uislamu kwa kumpa kati ya vitu vifuatavyo;
utajiri, mwanamke mzuri, madaraka au yote kama akitaka.
- Mtume (s.a.w) aliwakatalia vyote hivyo kwa kumsomea aya za Qur’an
(41:1-37) mjumbe aliyetumwa kazi hiyo, Utbah bin Rabi’ah.
- Mbinu ya kutaka kumlaghai Mtume (s.a.w).
- Maqureish walimletea Mtume (s.a.w) pendekezo kuwa washirikiane
katika ibada kwa awamu, mwaka mmoja wamuabudu Mungu mmoja
kwa pamoja na mwaka unaofuatia waabudu miungu yao pamoja pia.
- Hapo ndipo iliposhuka suratul-Kafiruun kuvunja pendekezo lao hilo la
kushiki katika ibada na Mtume akawasomea aya za Qur’an kukataa.
Rejea Qur’an (109:1-6) na (10:15).
- Mbinu ya Kuwatesa na kuwaua Waislamu.
- Baada ya Maqureish kuona mbinu zote zimefeli, walianza kutumia
nguvu na mabavu kuwatesa, kuwanyonga na kuwaua Waislamu
waliong’ang’ani imani yao kama akina; Bilal bin Rabbah, Sumaiyya,
Ammar bin Yasir na baba yake, n.k.
- Pamoja na mateso na mauaji, waislamu walibakia na msimamo wao
bila kutetereka na kukata tamaa.
- Mbinu ya fitina, kuipinga Qur’an na kuzuia watu kukutana na Mtume (s.a.w).
- Maquraish kwa kuhofia ujumbe wa Qur’an kuenea kwa watu,
walianza kuzuia watu kwenda kuonana na Mtume (s.a.w) kwa
kuwashawishi kuwa wasisikilize aya za Qur’an kwani ni uchawi,
mashairi ya Muhammad.
- Walizidi kufitinisha kwa kumzuia Mtume (s.a.w) kuswali na
kuwaambia watu kuwa Muhammad anapinga ibada na miungu wenu,
lakini mbinu na ushawishi wao ulifeli pia.
Rejea Qur’an (31:6), (41:26), (10:38), (11:13) na (96:9-19).
- Mbinu ya kuwatenga na kila huduma ya kijamii.
- Maquraish walizidi kuongeza mateso kwa waislamu kwa kutenga na
kuwafukuza Makka na kwenda kuishi katika jangwa la Shi’ab miaka
mitatu bila chakula wala mahusiano mengine ya kijamii.
- Mbinu pia ilifeli baada ya baadhi ya Maquiesh kuona huruma kwa
ndugu zao waliotengwa bila sababu za msingi, hivyo wakavunja
mkataba wa kuwatenga.
- Mbinu ya kutaka kumuua Mtume (s.a.w).
- Maquish waliazimia kumuua Mtume (s.a.w) na rafiki yake Abubakar
(r.a) walipogundua kuwa waislamu wamehamia mji wa Madinah.
- Mbinu hii pia ilifeli baada ya Allah (s.w) kuwanusu katika pango yeye
na sahibu yake Abubakar (r.a).
Rejea Qur’an (9:40).
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉2 web hosting 👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉4 Madrasa kiganjani 👉5 Kitau cha Fiqh 👉6 Bongolite - Game zone - Play free game
Post zinazofanana:
Mbinu walizotumia Makafiri wa Kiqureish katika kuupinga Uislamu Makkah.
Mbinu walizotumia Makafiri wa Kiqureish katika kuupinga Uislamu Makkah.
Soma Zaidi...Yusufu Aokotwa na Kuuzwa nchini Misri
Huko nyuma wapita njia walikisogelea kisima kwa lengo la kuteka maji.
Soma Zaidi...Sifa au vigezo vya dini sahihi
Dini sahihi anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...