Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)
mbinu walizotumia Makafiri wa Kiqureish katika kuupinga Uislamu Makkah.
- Maqureish wa Makkah walitumia kila mbinu kuhakikisha kuwa ujumbe wa Uislamu haufiki na kukubalika katika jamii yao, miongoni ni hizi zifuatazo;
- Makafiri walimdhihaki Mtume (s.a.w) na waumini wachache kwa
kumuita majina mabaya kama; mwendawazimu, mtunga mashiri,
aliyepagawa na mashetani, mchawi, n.k.
- Pamoja na kusimangwa huko Mtume (s.a.w) na waislamu hawakukata
tamaa, waliendelea kuutangaza Uislamu katika jamii yote.
- Wakuu wa Maquraish walimuagiza Abu Talib amkataze Muhammad
(mwanae) kuendelea kuutangaza Uislamu kwa kumbadilishia mtoto
mwingine la sivyo watamshambulia yeye na Muhammad (s.a.w).
- Mbinu hii haikufanikiwa badala yake Abu Talib alimuunga mkono
Mtume (s.a.w) kwa kazi yake baada ya kujua msimamo wake.
- Maquraish walitumia diplomasia kwa kumtaka Mtume (s.a.w) aache
kazi ya kuutangaza Uislamu kwa kumpa kati ya vitu vifuatavyo;
utajiri, mwanamke mzuri, madaraka au yote kama akitaka.
- Mtume (s.a.w) aliwakatalia vyote hivyo kwa kumsomea aya za Qur’an
(41:1-37) mjumbe aliyetumwa kazi hiyo, Utbah bin Rabi’ah.
- Maqureish walimletea Mtume (s.a.w) pendekezo kuwa washirikiane
katika ibada kwa awamu, mwaka mmoja wamuabudu Mungu mmoja
kwa pamoja na mwaka unaofuatia waabudu miungu yao pamoja pia.
- Hapo ndipo iliposhuka suratul-Kafiruun kuvunja pendekezo lao hilo la
kushiki katika ibada na Mtume akawasomea aya za Qur’an kukataa.
Rejea Qur’an (109:1-6) na (10:15).
- Baada ya Maqureish kuona mbinu zote zimefeli, walianza kutumia
nguvu na mabavu kuwatesa, kuwanyonga na kuwaua Waislamu
waliong’ang’ani imani yao kama akina; Bilal bin Rabbah, Sumaiyya,
Ammar bin Yasir na baba yake, n.k.
- Pamoja na mateso na mauaji, waislamu walibakia na msimamo wao
bila kutetereka na kukata tamaa.
- Maquraish kwa kuhofia ujumbe wa Qur’an kuenea kwa watu,
walianza kuzuia watu kwenda kuonana na Mtume (s.a.w) kwa
kuwashawishi kuwa wasisikilize aya za Qur’an kwani ni uchawi,
mashairi ya Muhammad.
- Walizidi kufitinisha kwa kumzuia Mtume (s.a.w) kuswali na
kuwaambia watu kuwa Muhammad anapinga ibada na miungu wenu,
lakini mbinu na ushawishi wao ulifeli pia.
Rejea Qur’an (31:6), (41:26), (10:38), (11:13) na (96:9-19).
- Maquraish walizidi kuongeza mateso kwa waislamu kwa kutenga na
kuwafukuza Makka na kwenda kuishi katika jangwa la Shi’ab miaka
mitatu bila chakula wala mahusiano mengine ya kijamii.
- Mbinu pia ilifeli baada ya baadhi ya Maquiesh kuona huruma kwa
ndugu zao waliotengwa bila sababu za msingi, hivyo wakavunja
mkataba wa kuwatenga.
- Maquish waliazimia kumuua Mtume (s.a.w) na rafiki yake Abubakar
(r.a) walipogundua kuwa waislamu wamehamia mji wa Madinah.
- Mbinu hii pia ilifeli baada ya Allah (s.w) kuwanusu katika pango yeye
na sahibu yake Abubakar (r.a).
Rejea Qur’an (9:40).
Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiw ana App yetu. Bofya liln hapo chini kuweza ku download
Download NowJe! umeipenda hii post?
Ndio Hapana Save post
Rajabu
Tarehe 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sira
Main: Post
File: Download PDF
Share On
Facebook
or
Whatsapp
Views 2858
Sponsored links
π1
Kitabu cha Afya
π2
kitabu cha Simulizi
π3
Madrasa kiganjani
π4
Kitau cha Fiqh
π5
Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)
π6
Simulizi za Hadithi Audio
Sababu ya uislamu kuwa ndiyo dini sahihi pekee
Dini anayostahiki kufuata mwanadamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
Kupigwa vita Uislamu Tanganyika na Afrika Mashariki
Soma Zaidi...
HISTORIA YA MTUME AL-YASAβA(A.S)
Mtume Alyasaβa(a. Soma Zaidi...
Mafunzo yatokanayo na vita vya uhudi
Dola ya uislamu madinah (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
Uendeshaji na Kupanuka kwa Dola ya Kiislamu Kipindi cha Makhalifa Waongofu
Soma Zaidi...
Hija ya kuaga kwa mtume, na hutuba ya mwisho aliyotowa mtume katika hija
Mwaka mmoja baada ya msafara wa Tabuuk Bara Arab zima ilikuwa chini ya Dola ya Kiislamu. Soma Zaidi...
tarekh 5
KUZALIWA KWA MTUME (S. Soma Zaidi...
Uanzishwaji wa Makundi mbalimbali ya Harakati za Kuhuisha Uislamu Ulimwenguni
8. Soma Zaidi...
Malezi ya mtume
Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu) Soma Zaidi...
Historia ya uislamu wakati wa Makhalifa wanne: Abubakar, Umar, Uthman na Ally
Soma Zaidi...