Kiapo ya Mtume Ayub na utekelezwaji wake

Mkewe Ayyuub(a.

Kiapo ya Mtume Ayub na utekelezwaji wake

Nabii Ayyuub(a.s) Kutekeleza Kiapo Chake


Mkewe Ayyuub(a.s) alikuwa naye ni mama mcha-Mungu mwenye subira. Alimuuguza mumewe kwa kipindi kirefu kiasi hicho katika hali ngumu bila ya kuchoka. Lakini inasemekana siku moja aliteleza na kutamka maneno ambayo yalimchukiza Nabii Ayyuub(a.s) kwa kuwa yalikuwa yanamtoa katika imani ya Allah(s.w). Inasemekana mkewe aliteleza na kusema, β€œHivi huu ugonjwa utaendelea mpaka lini?” Nabii Ayyuub(a.s) alimkemea mkewe juu ya kauli yake hiyo na kumuahidi kuwa akipona atamuadhibu kwa kumcharaza bakora mia.



Baada ya Nabii Ayyuub(a.s) kupona, Allah(s.w) alimuelekeza namna yakutekeleza kiapo cha kumuadhibu mkewe aliyemfanyia ihsani na kuvumilia shida kiasi kile, kwa maelekezo ya Allah(s.w) hakupaswa kumcharaza bakora mia, bali aliagizwa achukue vijiti mia avifunge pamoja kisha ampige navyo mara moja kama tunavyojifunza katika aya ifuatayo:




β€œNa shika kicha cha vijiti tu mkononi mwako, (si fimbo); kisha mpige kwacho (mkeo kwa kiapo ulichoapa kuwa utampiga kwa mabaya aliyoyafanya), wala usivunje kiapo.” Bila shaka tulimkuta ni mwenye subira, mja mwema; kwa hakika alikuwa mnyenyekevu sana. (38:44)



                   

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sira Main: Dini File: Download PDF Views 892

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
πŸ‘‰1 kitabu cha Simulizi    πŸ‘‰2 Madrasa kiganjani    πŸ‘‰3 Kitau cha Fiqh    πŸ‘‰4 Simulizi za Hadithi Audio    πŸ‘‰5 Kitabu cha Afya    πŸ‘‰6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Historia ya Firaun, Qarun na Hamana

Karun na Hamana waliishi zama za Mtume Musa(a.

Soma Zaidi...
NI UPI MKATABA WA AL-FUDHUL NA ASILI YAKE, ATHARI ZAKE NA WALOHUSIKA

MKATABA WA AL-FUDHULBaada ya vita hivi viongozi wa pande mbili hizi waliamuwa wakae chini na wakubaliane kuweka kanun i na utaratibu utakaozuia kutotokea uonevu kama huuu tena.

Soma Zaidi...
Mafunzo Yatokanayo na Historia ya Adam(a.s)

(i) Utukufu wa mtu katika Uislamu hautokani na nasaba, rangi,kabila,utajiri ila uwajibikaji kwa Allah(s.

Soma Zaidi...
Kuandaliwa kwa Muhammad kabla ya kupewa utume

Bara arabu zama za jahiliyyah (EDK form 2 dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Tukio la kupasuliwa kifua Mtume Muhammad S.A.W

Sura na historia ya Mtume Muhammad S.A.W, sehemu ya 7

Soma Zaidi...