Elimu kuhusu HIV na UKIMWI
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu elimu ya kuhusu HIV na UKIMWI
ELIMU YA KUHUSU HIV NA UKIMWI
Ni nini maana ya Ukimwi?
UKIMWI ni ufupisho wa maneno “upungufu wa kinga mwilini” ni hali sugu, inayoweza kutishia maisha inayosababishwa na virusi vya Ukimwi (VVU). Kwa kuharibu mfumo wako wa kinga, VVU huingilia uwezo wa mwili wako kupambana na viumbe vinavyosababisha magonjwa. Viumbe hivyo ni kama bakteria, virusi, protozoa, fangasi na vinginevyo.
Nini maana ya Virusi Vya Ukimwi (VVU)?
VVU ni ufupisho wa maneno Virusi Vya Ukimwi, ni virusi vinavyosababisha upungufu wa kinga mwilini. Hudhoofisha mwili uwezo wake kujilinda dhidi ya vijidudu vya maradhi. Neon hili kwa lugha ya kiingereza hufupishwa kama HIV.
VVU ni maambukizo ya zinaa. Yanayoweza pia kuenezwa kwa kuongezewa damu iliyoambukizwa au kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto wakati wa ujauzito, wakati wa kujifungua au kunyonyesha. Inaweza kuchukua miaka mimngi huwenda 5 mpaka 10 kabla ya VVU kudhoofisha kinga yako ya mwili hadi kufikia ukimwi.
Je ipo tiba ya VVU na UKIMWI?
Hakuna tiba ya VVU / UKIMWI, lakini kuna dawa ambazo zinaweza kupunguza kasi ya ukuaji wa magonjwa na uharibifu wa kinga ya mwili. Dawa hizi zimepunguza vifo vya UKIMWI katika mataifa mengi yaliyoendelea. Lakini VVU inaendelea kupunguza idadi ya watu barani Afrika, Haiti na sehemu za Asia. Dawa hizi mimkusanyiko wa dawa nyingi kwa pamoja hufahamika kama ARV yaani Ant-Retrovirus na matibabu yake hufahamika kama ART yaani Ant-Retroval Therapy. Dawa hizi piazimegawanyika katika makundi mengi kama NRTIs, NNRTs, Protease inhibitors na nyinginezo kibao.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 Kitabu cha Afya 👉3 ai web app 👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉5 Bongolite - Game zone - Play free game 👉6 Madrasa kiganjani
Post zinazofanana:
ninatatizo la miguu kuuma nimepima wanasema seli nyeupe za damu ipo chini Sana sasa nauliza dawa hizi za vitamin k na sindano vinaweza nisaidia?
Upungufu wa damu ni tatizo la kiafya, lakini kupunguwa seli nyeupe za damu ni tatizo zaidi, nikwa sabaabu seli hizi ndizo ambazo hupambana na wadudu shambulizi wanapoingia mwilini.
Soma Zaidi...Sababu za maumivu ya tumbo kwa chini uapande wa kushoto
Zijuwe sababu kuu zinazokufanya ukahisi maumivu makali ya tumbo kwa chini upande wa kushoto
Soma Zaidi...Vitu vinavyochochea kuwepo kwa Ugonjwa wa ukimwi.
Posti hii inahusu zaidi vitu ambavyo vinasababisha kuongezeka kwa Ukimwi kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na baada ya watu kujua Ugonjwa huu na matokeo ila bado ugonjwa unazidi kuongezeka.
Soma Zaidi...Dalili za kuvunjika kwa nyonga
Kuvunjika kwa nyonga ni jeraha kubwa, na matatizo ambayo yanaweza kuhatarisha maisha. Hatari ya kupasuka kwa nyonga huongezeka na umri.
Soma Zaidi...Dalili za ugonjwa wa uvimbe na mashambulizi ya bacteria kwenye korodani
Posti hii inaonyesha dalili,Sababu,na namna ya kujikinga na ugonjwa wa uvimbe na mashambulizi ya bacteria kwenye korodani ambao kitaalamu hujulikana Kama orchitis.
Soma Zaidi...