picha

Elimu kuhusu HIV na UKIMWI

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu elimu ya kuhusu HIV na UKIMWI

ELIMU YA KUHUSU HIV NA UKIMWI

 

Ni nini maana ya Ukimwi?

UKIMWI ni ufupisho wa maneno “upungufu wa kinga mwilini” ni hali sugu, inayoweza kutishia maisha inayosababishwa na virusi vya Ukimwi (VVU). Kwa kuharibu mfumo wako wa kinga, VVU huingilia uwezo wa mwili wako kupambana na viumbe vinavyosababisha magonjwa. Viumbe hivyo ni kama bakteria, virusi, protozoa, fangasi na vinginevyo.

 

 

Nini maana ya Virusi Vya Ukimwi (VVU)?

VVU ni ufupisho wa maneno Virusi Vya Ukimwi, ni virusi vinavyosababisha upungufu wa kinga mwilini. Hudhoofisha mwili uwezo wake kujilinda dhidi ya vijidudu vya maradhi. Neon hili kwa lugha ya kiingereza hufupishwa kama HIV.

 

 

VVU ni maambukizo ya zinaa. Yanayoweza pia kuenezwa kwa kuongezewa damu iliyoambukizwa au kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto wakati wa ujauzito, wakati wa kujifungua au kunyonyesha. Inaweza kuchukua miaka mimngi huwenda 5 mpaka 10 kabla ya VVU kudhoofisha kinga yako ya mwili hadi kufikia ukimwi.

 

Je ipo tiba ya VVU na UKIMWI?

Hakuna tiba ya VVU / UKIMWI, lakini kuna dawa ambazo zinaweza kupunguza kasi ya ukuaji wa magonjwa na uharibifu wa kinga ya mwili. Dawa hizi zimepunguza vifo vya UKIMWI katika mataifa mengi yaliyoendelea. Lakini VVU inaendelea kupunguza idadi ya watu barani Afrika, Haiti na sehemu za Asia. Dawa hizi mimkusanyiko wa dawa nyingi kwa pamoja hufahamika kama ARV yaani Ant-Retrovirus na matibabu yake hufahamika kama ART yaani Ant-Retroval Therapy. Dawa hizi piazimegawanyika katika makundi mengi kama NRTIs, NNRTs, Protease inhibitors na nyinginezo kibao.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 3409

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     πŸ‘‰2 ai web app     πŸ‘‰3 Simulizi za Hadithi Audio     πŸ‘‰4 Madrasa kiganjani     πŸ‘‰5 Kitau cha Fiqh     πŸ‘‰6 Kitabu cha Afya    

Post zinazofanana:

Ugonjwa wa degedege na dalili zake

Ugonjwa wa degedege ni ugonjwa unaowapata sana watoto chini ya miaka mitano ingawa na watu wazima wanapatwa na ugonjwa huo

Soma Zaidi...
Dalili za Saratani ya utumbo mdogo.

Posti hii inaonyesha ishara na dalili za Saratani ya utumbo mdogo

Soma Zaidi...
Dalili za mimba ya wiki mbili unazopaswa kujua

​Post hii inaangazia kile kinachotokea mwilini mwako katika wiki ya pili ya ujauzito. Ingawa wiki ya pili mara nyingi huchukuliwa kama kipindi ambacho mwili unajiandaa kuachilia yai, tutaangazia ishara za mwanzo kabisa za utungaji wa mimba, jinsi ya kuzitambua, na hatua za kuchukua ili kuhakikisha afya njema.

Soma Zaidi...
Dalili za Mimba Changa Wiki ya Kwanza

​Wiki ya kwanza ya ujauzito mara nyingi ni kipindi ambacho mwili huanza mabadiliko ya siri ya homoni. Post hii inatoa mwongozo kuhusu dalili ambazo mwanamke anaweza kuzihisi, ikizingatia ukweli wa kibaolojia na umuhimu wa utambuzi sahihi katika hatua hii ya awali.

Soma Zaidi...
Daliliza shinikizo la Chini la damu.

Shinikizo la chini la damu (hypotension) litaonekana kuwa jambo la kujitahidi. Hata hivyo, kwa watu wengi, shinikizo la chini la damu linaweza kusababisha dalili za Kizunguzungu na kuzirai. Katika hali mbaya, shinikizo la chini la damu linawez

Soma Zaidi...
Zifahmu Dalili za homa ya ini Kali ya pombe.

Posti hii inaonyesha dalili na Mambo Hatari yanayosababisha homa ya ini Kali ya pombe.

Soma Zaidi...