picha

Vitu vinavyochochea kuwepo kwa Ugonjwa wa ukimwi.

Posti hii inahusu zaidi vitu ambavyo vinasababisha kuongezeka kwa Ukimwi kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na baada ya watu kujua Ugonjwa huu na matokeo ila bado ugonjwa unazidi kuongezeka.

Mambo yanayosababisha kuongezeka kwa Ugonjwa wa Ukimwi.

1. Kwanza kabisa kitu kikubwa ni watu kutokuwa wazi kuhusu maisha yao.

Kwa sababu watu wengi wanakuwa ni waathirika na wana wapenzi wengi wanaendelea kujamiiana na watu wengine ambao hawana Ugonjwa hali ambayo inafanya kuendelea kuwepo kwa Ugonjwa huu na kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa hiyo uaminifu na uwazi ni lazima.

 

2.Watu wengine kutojali afya zao 

Hali hii inatokea pale ambapo mtu anakuwa anasafiri akifika kituoni yuko radhi kulala na kahaba anayeuza mwili wake bila kutumia kinga ili mradi atulize hamu yake, kwa hiyo hali ya namna hiyo usababisha kusambaa kwa ugonjwa wa ukimwi kila siku na kuwepo kwa Maambukizi mapya.

 

3. Mila na desturi za jamii.

Kuna baadhi ya mila na desturi ambazo Usababisha kuenea kwa Maambukizi ya Ugonjwa wa Ukimwi, mila hizo ni pamoja na kuridhishwa mke au mme wa marehemu aliyefariki kwa Ugonjwa wa Ukimwi na pia yule aliyeridhishwa utakuta naye ana wapenzi wengine na wapenzi wana wapenzi wengine hali ambayo Usababisha kusambaa kwa ugonjwa wa ukimwi kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.

 

4.umaskini katika jamii.

Umaskini pia nao unasababisha kuwepo kwa ongezeko la Ugonjwa wa Ukimwi kwa sababu unaweza kukuta familia moja wanatumia wembe mmoja, pini na vitu vyote vya ncha kali vinatumiwa na pia kama kuna mgonjwa ambaye yuko katika hatua ya nne ya Maambukizi wanahudumia kwa kutumia mikono bila kujikinga.

 

5. Pia kwa upande wa umaskini unakuta tajiri analala na watoto wa shule na wengine ambao hawasomi kwa lengo la kuwapatia hela kidogo ya kununua matumizi yao ya kawaida na watoto wanakuwa tayari kufanya hivyo ili wapate mahitaji yao yanayokosa kwenye familia zao

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 1953

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Tafasiri ya Riyadh Swalihina     πŸ‘‰2 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     πŸ‘‰3 ai web app     πŸ‘‰4 Bongolite - Game zone - Play free game     πŸ‘‰5 kitabu cha Simulizi     πŸ‘‰6 Kitabu cha Afya    

Post zinazofanana:

AFYA NA MAGONJWA

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
Jinsi ya kujenga afya ya akili katika ulimwengu wa sasa.

​Katika ulimwengu wa kidijitali na wenye kasi kubwa, afya ya akili imekuwa rasilimali muhimu zaidi kwa binadamu. Makala haya yanachunguza mbinu za kisayansi na kivitendo za kujenga ustahimilivu wa kiakili, kudhibiti mfadhaiko wa teknolojia, na kukuza usawaziko wa maisha. Kupitia mwongozo huu, utajifunza jinsi ya kuweka mipaka, kuboresha mahusiano, na kutumia mazoea ya kujijali (self-care) ili kudumisha utulivu wa ndani katikati ya changamoto za kisasa.

Soma Zaidi...
Makundi yaliyo katika hatari ya kupata Ugonjwa wa ngiri.

Posti hii inahusu zaidi makundi ambayo yapo katika hatari ya kupata ugonjwa wa ngiri, ni hatari kwa sababu tunajua kuwa ngiri utokea kwa sababu ya kuta au tishu zinazoshikilia viungo fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwepo kwa uwazi na kufanya viun

Soma Zaidi...
Sababu za Kichwa Kuuma Mara kwa Mara

​Kichwa kuuma mara kwa mara ni changamoto inayomfanya mtu kushindwa kutekeleza majukumu yake ya kila siku kwa ufanisi. Makala hii inaangazia sababu mbalimbali za maumivu ya kichwa ya mara kwa mara, jinsi ya kuyatofautisha, na wakati mwafaka wa kutafuta msaada wa kitaalamu

Soma Zaidi...
Makundi ya watu walio katika hatari ya kupata Ugonjwa wa Ukimwi

Posti hii inahusu zaidi watu walio katika hatari ya kupata Maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi,ni kutokana na kazi zao pamoja na mazingira yao kwa hiyo wako kwenye hatari ya kupata Ugonjwa wa ukimwi.

Soma Zaidi...
Fangasi wanaojulikana kama Blastomyces

Fangasi wanaojulikana kama Blastomyces, hawa ni fangasi wanaosababisha maradhi yajulikanayo kama blastomycosis.

Soma Zaidi...