Posti hii inahusu zaidi vitu ambavyo vinasababisha kuongezeka kwa Ukimwi kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na baada ya watu kujua Ugonjwa huu na matokeo ila bado ugonjwa unazidi kuongezeka.
1. Kwanza kabisa kitu kikubwa ni watu kutokuwa wazi kuhusu maisha yao.
Kwa sababu watu wengi wanakuwa ni waathirika na wana wapenzi wengi wanaendelea kujamiiana na watu wengine ambao hawana Ugonjwa hali ambayo inafanya kuendelea kuwepo kwa Ugonjwa huu na kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa hiyo uaminifu na uwazi ni lazima.
2.Watu wengine kutojali afya zao
Hali hii inatokea pale ambapo mtu anakuwa anasafiri akifika kituoni yuko radhi kulala na kahaba anayeuza mwili wake bila kutumia kinga ili mradi atulize hamu yake, kwa hiyo hali ya namna hiyo usababisha kusambaa kwa ugonjwa wa ukimwi kila siku na kuwepo kwa Maambukizi mapya.
3. Mila na desturi za jamii.
Kuna baadhi ya mila na desturi ambazo Usababisha kuenea kwa Maambukizi ya Ugonjwa wa Ukimwi, mila hizo ni pamoja na kuridhishwa mke au mme wa marehemu aliyefariki kwa Ugonjwa wa Ukimwi na pia yule aliyeridhishwa utakuta naye ana wapenzi wengine na wapenzi wana wapenzi wengine hali ambayo Usababisha kusambaa kwa ugonjwa wa ukimwi kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.
4.umaskini katika jamii.
Umaskini pia nao unasababisha kuwepo kwa ongezeko la Ugonjwa wa Ukimwi kwa sababu unaweza kukuta familia moja wanatumia wembe mmoja, pini na vitu vyote vya ncha kali vinatumiwa na pia kama kuna mgonjwa ambaye yuko katika hatua ya nne ya Maambukizi wanahudumia kwa kutumia mikono bila kujikinga.
5. Pia kwa upande wa umaskini unakuta tajiri analala na watoto wa shule na wengine ambao hawasomi kwa lengo la kuwapatia hela kidogo ya kununua matumizi yao ya kawaida na watoto wanakuwa tayari kufanya hivyo ili wapate mahitaji yao yanayokosa kwenye familia zao
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
maambukizi ya kawaida ya zinaa (STI), Hujulikana Kama Chlamydia. Huenda usijue una Ugonjwa huu kwa sababu watu wengi hawapati dalili au ishara, kama vile maumivu ya sehemu za siri na kutokwa na uchafu kutoka kwa uke au uume. Maambukizi haya huathiri
Soma Zaidi...Posti hii inahusu dalili za figo.figo husawazisha maji mwilini pamoja na kuchuja mkojo.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi tatizo la kushindwa kushuka kwa makende kutoka kwenye tumbo kwenda kwenye skolatumu(scrotum).
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi namna ya kuwasaidia Watu wale ambao wana Maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo.
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu elimu ya kuhusu HIV na UKIMWI
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi Magonjwa ya kuambukiza, ni magonjwa ambayo yanaweza kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na kuweza kusababisha madhara yale yale kwa mtu aliyeambukizwa au anayeambukiza kwa hiyo Maambukizi yanaweza kuwa ya moja kwa moja au yasi
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi maumivu ya kiuno na dalili zake, ni maumivu ambayo utokea kwenye kiuno na kusababisha madhara mbalimbali katika mwili,
Soma Zaidi...