Vitu vinavyochochea kuwepo kwa Ugonjwa wa ukimwi.

Posti hii inahusu zaidi vitu ambavyo vinasababisha kuongezeka kwa Ukimwi kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na baada ya watu kujua Ugonjwa huu na matokeo ila bado ugonjwa unazidi kuongezeka.

Mambo yanayosababisha kuongezeka kwa Ugonjwa wa Ukimwi.

1. Kwanza kabisa kitu kikubwa ni watu kutokuwa wazi kuhusu maisha yao.

Kwa sababu watu wengi wanakuwa ni waathirika na wana wapenzi wengi wanaendelea kujamiiana na watu wengine ambao hawana Ugonjwa hali ambayo inafanya kuendelea kuwepo kwa Ugonjwa huu na kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa hiyo uaminifu na uwazi ni lazima.

 

2.Watu wengine kutojali afya zao 

Hali hii inatokea pale ambapo mtu anakuwa anasafiri akifika kituoni yuko radhi kulala na kahaba anayeuza mwili wake bila kutumia kinga ili mradi atulize hamu yake, kwa hiyo hali ya namna hiyo usababisha kusambaa kwa ugonjwa wa ukimwi kila siku na kuwepo kwa Maambukizi mapya.

 

3. Mila na desturi za jamii.

Kuna baadhi ya mila na desturi ambazo Usababisha kuenea kwa Maambukizi ya Ugonjwa wa Ukimwi, mila hizo ni pamoja na kuridhishwa mke au mme wa marehemu aliyefariki kwa Ugonjwa wa Ukimwi na pia yule aliyeridhishwa utakuta naye ana wapenzi wengine na wapenzi wana wapenzi wengine hali ambayo Usababisha kusambaa kwa ugonjwa wa ukimwi kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.

 

4.umaskini katika jamii.

Umaskini pia nao unasababisha kuwepo kwa ongezeko la Ugonjwa wa Ukimwi kwa sababu unaweza kukuta familia moja wanatumia wembe mmoja, pini na vitu vyote vya ncha kali vinatumiwa na pia kama kuna mgonjwa ambaye yuko katika hatua ya nne ya Maambukizi wanahudumia kwa kutumia mikono bila kujikinga.

 

5. Pia kwa upande wa umaskini unakuta tajiri analala na watoto wa shule na wengine ambao hawasomi kwa lengo la kuwapatia hela kidogo ya kununua matumizi yao ya kawaida na watoto wanakuwa tayari kufanya hivyo ili wapate mahitaji yao yanayokosa kwenye familia zao

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: magonjwa Main: Afya File: Download PDF Views 1604

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Bongolite - Game zone - Play free game    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Maambukizi ya Kawaida ya zinaa (Chlamydia)

maambukizi ya kawaida ya zinaa (STI), Hujulikana Kama Chlamydia. Huenda usijue una Ugonjwa huu kwa sababu watu wengi hawapati dalili au ishara, kama vile maumivu ya sehemu za siri na kutokwa na uchafu kutoka kwa uke au uume. Maambukizi haya huathiri

Soma Zaidi...
Dalili za madhara ya figo

Posti hii inahusu dalili za figo.figo husawazisha maji mwilini pamoja na kuchuja mkojo.

Soma Zaidi...
KISUKARI

Pata elimu juu ya afya hapa ukiwa na vitabu vyetu bila ya malipo yoyote

Soma Zaidi...
Zijue sababu za kushindwa kushuka kwa makende (testicle))

Posti hii inahusu zaidi tatizo la kushindwa kushuka kwa makende kutoka kwenye tumbo kwenda kwenye skolatumu(scrotum).

Soma Zaidi...
Huduma kwa wenye Maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo

Posti hii inahusu zaidi namna ya kuwasaidia Watu wale ambao wana Maambukizi kwenye tumbo na utumbo mdogo.

Soma Zaidi...
Elimu kuhusu HIV na UKIMWI

Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu elimu ya kuhusu HIV na UKIMWI

Soma Zaidi...
Magonjwa ya kuambukiza.

Posti hii inahusu zaidi Magonjwa ya kuambukiza, ni magonjwa ambayo yanaweza kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na kuweza kusababisha madhara yale yale kwa mtu aliyeambukizwa au anayeambukiza kwa hiyo Maambukizi yanaweza kuwa ya moja kwa moja au yasi

Soma Zaidi...
Maumivu ya kiuno na dalili zake

Posti hii inahusu zaidi maumivu ya kiuno na dalili zake, ni maumivu ambayo utokea kwenye kiuno na kusababisha madhara mbalimbali katika mwili,

Soma Zaidi...