Vitu vinavyochochea kuwepo kwa Ugonjwa wa ukimwi.
Posti hii inahusu zaidi vitu ambavyo vinasababisha kuongezeka kwa Ukimwi kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na baada ya watu kujua Ugonjwa huu na matokeo ila bado ugonjwa unazidi kuongezeka.
Mambo yanayosababisha kuongezeka kwa Ugonjwa wa Ukimwi.
1. Kwanza kabisa kitu kikubwa ni watu kutokuwa wazi kuhusu maisha yao.
Kwa sababu watu wengi wanakuwa ni waathirika na wana wapenzi wengi wanaendelea kujamiiana na watu wengine ambao hawana Ugonjwa hali ambayo inafanya kuendelea kuwepo kwa Ugonjwa huu na kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa hiyo uaminifu na uwazi ni lazima.
2.Watu wengine kutojali afya zao
Hali hii inatokea pale ambapo mtu anakuwa anasafiri akifika kituoni yuko radhi kulala na kahaba anayeuza mwili wake bila kutumia kinga ili mradi atulize hamu yake, kwa hiyo hali ya namna hiyo usababisha kusambaa kwa ugonjwa wa ukimwi kila siku na kuwepo kwa Maambukizi mapya.
3. Mila na desturi za jamii.
Kuna baadhi ya mila na desturi ambazo Usababisha kuenea kwa Maambukizi ya Ugonjwa wa Ukimwi, mila hizo ni pamoja na kuridhishwa mke au mme wa marehemu aliyefariki kwa Ugonjwa wa Ukimwi na pia yule aliyeridhishwa utakuta naye ana wapenzi wengine na wapenzi wana wapenzi wengine hali ambayo Usababisha kusambaa kwa ugonjwa wa ukimwi kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.
4.umaskini katika jamii.
Umaskini pia nao unasababisha kuwepo kwa ongezeko la Ugonjwa wa Ukimwi kwa sababu unaweza kukuta familia moja wanatumia wembe mmoja, pini na vitu vyote vya ncha kali vinatumiwa na pia kama kuna mgonjwa ambaye yuko katika hatua ya nne ya Maambukizi wanahudumia kwa kutumia mikono bila kujikinga.
5. Pia kwa upande wa umaskini unakuta tajiri analala na watoto wa shule na wengine ambao hawasomi kwa lengo la kuwapatia hela kidogo ya kununua matumizi yao ya kawaida na watoto wanakuwa tayari kufanya hivyo ili wapate mahitaji yao yanayokosa kwenye familia zao
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Madrasa kiganjani 👉2 web hosting 👉3 Bongolite - Game zone - Play free game 👉4 ai web app 👉5 Kitabu cha Afya 👉6 Kitau cha Fiqh
Post zinazofanana:
Kikohozi kikavu: Chanzo chake na dawa za asili za kutibu.
Kikohozi kikavu ni tatizo linaloathiri mfumo wa upumuaji bila kuzalisha makohozi, mara nyingi likisababishwa na mzio (allergies), maambukizi ya virusi, au asidi ya tumbo kupanda kooni (GERD). Makala haya ya kina yanachambua vyanzo vikuu vya kitaalamu vya changamoto hii na kuorodhesha tiba 6 za asili zilizothibitishwa kisayansi kama vile asali, tangawizi, na binzari. Pia, utajifunza ishara hatari zinazohitaji uononaji wa daktari na ukweli wa kimatibabu kuhusu kikohozi kupitia sehemu ya "Je, Wajua?".
Soma Zaidi...Jinsi ya kutambua mimba kwa vipimo vya kawaida vya mkojo.
Kujitambua mimba mapema ni hatua muhimu katika kuanza safari ya uzazi salama. Makala haya yanaelezea misingi ya kisayansi ya vipimo vya mkojo vya nyumbani (Pregnancy Test Strips/Sticks), njia sahihi ya kuvitumia, muda mwafaka wa kupima, na jinsi ya kusoma matokeo ili kupata usahihi wa hali ya juu.
Soma Zaidi...Dalili za kifua kikuu kwa watoto.
Posti hii inahusu zaidi dalili za kifua kikuu kwa watoto,ni Dalili ambazo ujitokeza kwa watoto pindi wanapopata Maambukizi ya kifua kikuu.
Soma Zaidi...Homa ya manjano kwa watoto wachanga: Nini kifanyike?
Homa ya manjano ni hali ya kawaida kwa watoto wachanga ambapo ngozi na sehemu nyeupe ya macho hubadilika na kuwa na rangi ya manjano. Hali hii hutokea pale kiwango cha bilirubin—kemikali ya manjano inayotokana na kuvunjika kwa seli nyekundu za damu—kinapokuwa kikubwa mwilini kuliko uwezo wa ini la mtoto kuiondoa. Ingawa mara nyingi si hatari, ni muhimu kuifuatilia kwa karibu ili kuzuia madhara kwa mfumo wa neva wa mtoto.
Soma Zaidi...Dalili za maumivu ya uti wa Mgongo
Posti hii inahusu zaidi dalili za uti wa mgongo ni dalili ambazo ujitokeza kwa mtu Mwenye tatizo la uti wa Mgongo.
Soma Zaidi...Kazi ya mwanasaikolojia na daktari wa magonjwa ya akili.
Unapokutana na changamoto za afya ya akili, ni rahisi kuchanganyikiwa kuhusu ni nani unayepaswa kumuona kati ya mwanasaikolojia na daktari wa magonjwa ya akili. Ingawa wote wanasaidia kuboresha afya ya akili, taaluma zao, mifumo yao ya mafunzo, na mbinu zao za matibabu ni tofauti kabisa. Makala haya yanachambua majukumu ya kila mmoja ili ujue wapi pa kupata msaada sahihi.
Soma Zaidi...