Posti hii inahusu zaidi vitu ambavyo vinasababisha kuongezeka kwa Ukimwi kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine na baada ya watu kujua Ugonjwa huu na matokeo ila bado ugonjwa unazidi kuongezeka.
1. Kwanza kabisa kitu kikubwa ni watu kutokuwa wazi kuhusu maisha yao.
Kwa sababu watu wengi wanakuwa ni waathirika na wana wapenzi wengi wanaendelea kujamiiana na watu wengine ambao hawana Ugonjwa hali ambayo inafanya kuendelea kuwepo kwa Ugonjwa huu na kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa hiyo uaminifu na uwazi ni lazima.
2.Watu wengine kutojali afya zao
Hali hii inatokea pale ambapo mtu anakuwa anasafiri akifika kituoni yuko radhi kulala na kahaba anayeuza mwili wake bila kutumia kinga ili mradi atulize hamu yake, kwa hiyo hali ya namna hiyo usababisha kusambaa kwa ugonjwa wa ukimwi kila siku na kuwepo kwa Maambukizi mapya.
3. Mila na desturi za jamii.
Kuna baadhi ya mila na desturi ambazo Usababisha kuenea kwa Maambukizi ya Ugonjwa wa Ukimwi, mila hizo ni pamoja na kuridhishwa mke au mme wa marehemu aliyefariki kwa Ugonjwa wa Ukimwi na pia yule aliyeridhishwa utakuta naye ana wapenzi wengine na wapenzi wana wapenzi wengine hali ambayo Usababisha kusambaa kwa ugonjwa wa ukimwi kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine.
4.umaskini katika jamii.
Umaskini pia nao unasababisha kuwepo kwa ongezeko la Ugonjwa wa Ukimwi kwa sababu unaweza kukuta familia moja wanatumia wembe mmoja, pini na vitu vyote vya ncha kali vinatumiwa na pia kama kuna mgonjwa ambaye yuko katika hatua ya nne ya Maambukizi wanahudumia kwa kutumia mikono bila kujikinga.
5. Pia kwa upande wa umaskini unakuta tajiri analala na watoto wa shule na wengine ambao hawasomi kwa lengo la kuwapatia hela kidogo ya kununua matumizi yao ya kawaida na watoto wanakuwa tayari kufanya hivyo ili wapate mahitaji yao yanayokosa kwenye familia zao
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu Tina ya vidonda vya tumbo na dawa zake
Soma Zaidi...Somo hili linakwenda kukueleza kuhusu njia za kupambana na fangasi
Soma Zaidi...Posti hii inazungumzia kuhusiana na maumivu ya shingo na ndani yake kunasababu zinazopelekea shingo kupata maumivu.
Soma Zaidi...Posti hii inaonyesha mambo mbalimbali yanayoweza kusababisha Ugonjwa wa kifua kikuu kwa watoto chini ya miaka mitano.
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi namna ya magonjwa ya koo yanavyosambaa, magonjwa haya usambaa kutoka sehemu Moja kwenda nyingine kwa njia tofauti kama ifuayavyo
Soma Zaidi...Post hii inahusu magonjwa yasiyo ya kuambukizwa,haya ni magonjwa ambayo hayawezi kusambaa kutoka kwa mtu mmoja kwenda mwingine
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi sababu za moyo kutanuka, Kuna kipindi ambapo moyo utoka kwenye hali yake ya kawaida na kutanuka hali ambayo usababisha madhara kwa mwenye tatizo hilo, ila Kuna sababu ambazo usababisha moyo kutanuka kama tutakavyoona.
Soma Zaidi...Je unasumbuliwa na tatizo la kukosa nguvu, kuchoka ama kuhisi viungi vinelegea. Endelea na post hii.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi namna ya kuwasaidia mtoto akiwa na ugonjwa wa UTI.
Soma Zaidi...