picha

Hatua za Maambukizi ya ugonjwa wa ukimwi.

Posti hii inahusu zaidi hatua mbalimbali za Ugonjwa wa Ukimwi, kawaida Ugonjwa huu huwa na hatua kuu nne ila kila hatua huwa na sifa zake kwa hiyo tunapaswa kujua hatua za Ugonjwa huu na kujaribu kuzuia maambukizi yasisambae kabisa.

Hatua za Ugonjwa wa Ukimwi.

1. Kadri ya sheria za Shirika la afya duniani limejaribu kuweka Dalili hizi nne kufuatana na Dalili anazozionyesha mtu. Kuna hatua ya kwanza kwenye hatua hii hakuna Dalili yoyote ambayo inaweza kujitokeza , mtu anakuwa kawaida na anafanya shughuli zake za kawaida bila shida yoyote yaani kwa ujumla hawezi kujua mpaka apime ndipo anapoweza kugundua kwamba ana Maambukizi.

 

2. Hatua ya tatu. Hii nayo ni Dalili ambayo kunakuwepo nadalili fulani kwa mgonjwa mfano uzito kupungua kwa asilimia kumi, mgonjwa anaanza kuwa na ma upele kwenye midomo na kwenye sehemu za siri, kuwepo kwa magonjwa ya mafua ya mara kwa mara na hayaponi na Magonjwa mengi mengi ushambulia mtu kwenye kipindi hiki ,kwa hiyo Mgonjwa baada ya kuona dalili kama hizi anapaswa kuwahi hospitali au sehemu yoyote akapime.

 

3. Hatua ya tatu ni ile uzito unashuka sana kuliko kawaida na pia mgonjwa anakuwa anaharisha sana, na homa ambazo hazikatiki, yaani homa za mara kwa mara,na kwa kipindi hiki mgonjwa huwa na fungusi za kwenye mdomo, kifua kikuu uwepo kwa mgonjwa, kunakuwepo pia kwa Maambukizi ya bakteria kwa wingi, katika kipindi hiki wagonjwa wengi wanakuwa wamelala kitandani.

 

4.Hatua ya nne na ya mwisho.

Kwenye hatua hii virusi vinakuwepo kwenye mwili mzima na mtu hudhoofika sana, kunakuwepo na matatizo kwenye Upumuaji, kuharisha kwa wingi, mgonjwa kwa mara nyingine anakuwa amelala kitandani, kwa upande wa mgonwa wanapaswa kumpeleka hospitali ili akapime mapema.

 

5. Kwa hiyo baada ya kutambua hatua hizi watu wanapaswa kujua Dalili, Ugonjwa unavyosambaa na kuweza kujiwekea msimamo na malengo ya kweli.

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: magonjwa Main: Post File: Download PDF Views 2411

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
πŸ‘‰1 Bongolite - Game zone - Play free game     πŸ‘‰2 ai web app     πŸ‘‰3 Simulizi za Hadithi Audio     πŸ‘‰4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)     πŸ‘‰5 Kitabu cha Afya     πŸ‘‰6 Dua za Mitume na Manabii    

Post zinazofanana:

Homa ya matone (Mumps): Dalili na tiba yake.

Homa ya matone, inayojulikana kama Mumps, ni maambukizi ya virusi yanayoathiri tezi zinazozalisha mate (salivary glands), hasa tezi zilizopo pande zote mbili za shavu (tezi za parotidi). Ugonjwa huu huambukiza kwa urahisi kupitia matone ya maji yanayotoka unapopiga chafya, kukohoa, au kuzungumza. Ingawa kwa sasa ni nadra kutokana na chanjo, bado inaweza kuwapata watu ambao hawajapata chanjo hiyo. Makala haya yanakupa uelewa wa dalili zake na jinsi ya kutoa huduma ya kwanza.

Soma Zaidi...
Fahamu aina mbalimbali za Magonjwa nyemelezi ya moyo

Posti hii inahusu zaidi aina mbalimbali za Magonjwa ya moyo,kwa kawaida tunajua wazi kuwa kuna moyo mmoja lakini moyo huo unaweza kushambuliwa na magonjwa kwa kila aina kwa mfano kuna Maambukizi kwenye mishipa ya moyo,au kubadilika kwa mapigo ya moyo na m

Soma Zaidi...
Vyakula Muhimu kwa Mama Mjamzito

Ujauzito ni kipindi cha kipekee kinachohitaji uangalizi maalum wa lishe. Makala hii inaangazia vyakula muhimu ambavyo kila mama mjamzito anapaswa kuzingatia ili kuhakikisha afya yake na ukuaji bora wa mtoto aliyepo tumboni.

Soma Zaidi...
Dalili za miguu kufa ganzi

Posti hii inahusu zaidi dalili mbalimbali ambazo Uweza kujitokeza na kuona kwamba ni Dalili za miguu kufa ganzi, pengine utokea kwa watu wote na pengine huwa ni kwa ghafla

Soma Zaidi...
Dalili za Minyoo kwa Watoto

​Minyoo ni tatizo la kawaida kwa watoto ambalo linaweza kuathiri ukuaji na afya zao kwa ujumla. Makala haya yataeleza dalili za kawaida za maambukizi ya minyoo, ukweli muhimu kuhusu tiba yake, na umuhimu wa usafi katika kuzuia tatizo hili.

Soma Zaidi...