Uwepo wa asidi nyingi mwilini
Posti hii inahusu zaidi tatizo la kuwepo kwa asidi nyingi mwilini hali uwasumbua watu wengi na kufikia kiasi cha kusababisha madhara mengine mawilini ikiwamo pamoja na kansa ya koo, ili kujua kama una wingi wa asildi mwilini unapaswa kujua dalili kama ifu
Dalili za asidi nyingi mwilini.
1. Dalili ya kwanza ni kupata vipele kwenye koo.
Kwa kawaida watu wenye asidi nyingi huwa na vidonda kwenye koo vidonda hivyo vinaweza kutibika na kupona lakini tatizo la asidi kama halijashughulikiwa vidonda ujirudia mara kwa mara na pia kama mtu anapata vidonda vya mara kwa mara kooni ni vizuri kuangalia tatizo la asidi mwilini.
2. Kuhisi kama kuna kitu kinababa kooni.
Kwa wakati mwingine unaweza kuona unabanwa kooni au kama kuna kitu kinakuniga jaribu kuwaona wataalamu wa afya ili kuweza kuweza kuangalia tatizo la asidi mwilini.
3. Kuhisi chakula kinarejea mdomoni.
Kuna wakati mwingine unaweza kuwa unakula na ukameza ila ukahisi labda chakula kinataka kurudi ila hauna kichefuchefu na inawezekana kabisa kuwa na Dalili za kuwepo kwa asidi mwilini.
4. Kupata kiungulia mara kwa mara.
Kuna wakati mwingine unaweza kupata kiungulia hata kama umemaliza mda mrefu,na ukatumia madawa mbalimbali na mengi bila kupata nafuu yoyote kwa hiyo unapaswa kuangalia kiwango cha asidi mwilini.
5. Kuna kipindi tumbo linajaa sana gesi na wakati mwingine linaambatana na kunguruma, hali inayosababisha pengine mtu kukosa hata hamu ya kula , kwa hiyo ni vizuri kabisa kugundua tatizo ni lipi.
6. Kuna wakati mwingine kifua kinabana sana na kuambatana na maumivu kwa mgonjwa, utakuta matibabu mengi yanakuwa katika kutibu kifua na hakuna nafuu yoyote ila tatizo unakuta ni kujaa kwa gesi kwenye mwili.
7. Tumbo kuwaka moto.
Kuna wakati mwingine tumbo linawaka moto kama mgonjwa wa vidonda vya tumbo na pengine matibabu ya vidonda vya tumbo ufanyika kwa mda mrefu bila msaada wowote ila baadae unakuta ni kuwepo kwa asidi mwilini.
8. Tunapaswa kujua kuwa tatizo hili lipi na lina dalili kama Magonjwa mengine hasa hasa kama vidonda vya tumbo na pia kifua, ikitokea matibabu yanafanyika na hakuna matokeo yoyote ya kupona ni vizuri kabisa kupima na kuangalia kama kuna kiwango kikubwa cha asidi mwilini.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Kitabu cha Afya 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 ai web app 👉4 Kitau cha Fiqh 👉5 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w) 👉6 kitabu cha Simulizi
Post zinazofanana:
Dalili za ugonjwa wa herpes simplex au vipele kwenye midomo na sehemu za siri
Posti hii inahusu zaidi dalili za ugonjwa wa wa vipele kwenye midomo na sehemu za siri ambao kwa kitaalamu huitwa herpes zoster. Kwa hiyo ili kugundua kubwa mtu ana Ugonjwa huu Dalili kama hizi zifuatazo zinaweza kutokea kwa mgonjwa.
Soma Zaidi...Fangasi wanaojulikana kama Blastomyces
Fangasi wanaojulikana kama Blastomyces, hawa ni fangasi wanaosababisha maradhi yajulikanayo kama blastomycosis.
Soma Zaidi...Dalili za saratani ya ini
Posti hii inahusu zaidi dalili za saratani ya ini, ni baadhi ya Dalili ambazo zinaweza kujitokeza na kuona kwamba mtu fulani ana saratani ya ini.
Soma Zaidi...Namna ya kugundua mtu mwenye kaswende.
Post hii inahusu zaidi njia za kumgundua mgonjwa wa kaswende, njia hizi utumika baada ya kuongea na mgonjwa kuhusu maisha yake hasa kujamiiana na watu mbalimbali.
Soma Zaidi...Kivimba kwa utando wa pua
post hii inazungumzia kuhusiana na kuvimba kwa utando wa pua unaoonyeshwa na mchanganyiko wa dalili zifuatazo: Kupiga chafya Msongamano wa pua Muwasho wa kiwambo cha sikio Kuwasha kwa pua na koromeo Uvimbe huu hutokea ikiwa mashambulizi ya kupiga chafya,
Soma Zaidi...Matatizo ya mapigo ya moyo
posti hii inazungumzia kuhusiana na matatizo ya mapigo ya moyo.Mapigo ya moyo ni hisia za kuwa na moyo wa haraka, unaodunda. Mapigo ya moyo yanaweza kuchochewa na mafadhaiko, mazoezi, dawa au, mara chache, hali ya kiafya. Ingawa mapigo ya moyo yanaweza k
Soma Zaidi...