Mabaka yanayowasha chini ya matiti.
Posti hii inahusu zaidi mabaka yanayowasha chini ya matiti, ni ugonjwa ambao uwapata wanawake walio wengi na wengine hawajapata jibu Sababu zake ni zipi na pengine uchukua hatua za kutumia miti shamba wakidai juwa hospitalini nugonjwa huu hautibiwa, ila n
Tatizo la mabaka yanayowasha chini ya matiti.
1. Tatizo hili kwa kawaida linaweza kumpata mwana mke yeyote yule hasa hasa uwapata wanawake walio wanene , wanawake wenye Ugonjwa wa kisukari, wanawake wenye matiti makubwa, wanawake wanaofanya mazoezi sana na pia wale wenye pilika pilika nyingi.
2.Ugonjwa huu utokea pale ambapo kuna misuguano kutoka sehemu mbili za matiti zinazoangaliana , baada ya sehemu hizo kubwa na msuguano kwa sababu ya shughuli mbalimbali au wakati wa mazoezi na hewa kwenye sehemu hiyo uwa kidogo hali ambayo Usababisha kuwepo kwa michubuko.
3.Kwa sababu ya michubuko ambayo huwa kwenye sehemu za matiti Usababisha wadudu kama vile bakteria na virusi kuweza kuingia kwenye michubuko hiyo kwa hiyo mama anaanza kuwasha na kujikuna hali ambayo Usababisha michubuka chini ya matiti.
4. Na kwa wakati mwingine kama kuna unyevunyevu kwenye matiti ukachanganyikana na wadudu hao hali inaweza kwa ngumu zaidi na kusababisha kujikuna sana , tatizo hili huwa kubwa zaidi hasa kwa wanawake wale wanaoshinda kwenye shughuli za kutumia nguvu na hawaogi hali huwa ngumu kwa sababu unaweza kukuta matiti yamechubuka sana.
5. Kwa hiyo baada ya kujua tatizo hili wanawake wote hasa kama ni wanene au wembamba ni vizuri kusafisha kwenye sehemu za matiti kwa maji safi na sabuni ili kuepuka na tatizo hili kwa sababu chanzo hiki ni kutofanya usafi na pia wanawake wenye Ugonjwa wa kisukari wawe makini sana kwa sababu walipatwa na tatizo hili ni vigumu kupona haraka kama wale wasio juwa na kisukari.
6.Pia ikumbukwe kwamba kwa akina Mama wanaopiga mazoezi kila siku au kufanya kazi zenye nguvu kama vile kulima kwa mda mrefu wanapaswa kuiga kila siku walau kwa mara moja na kunywa maji mengi ili kuepuka tatizo hili la kuwashwa kwenye matiti.
7.Pia kama imetokea mtu akapata na Ugonjwa huu anapaswa kutumia dawa kutegemea na kisababishi kama waliosababisha ni bakteria Mgonjwa anapaswa kutumia dawa ambazo ni antibiotics kama vile benzathine penicillin, erythromycin, oral penicillin kwa ajili ya kuondoa Maambukizi.
8.Pia Mgonjwa anaweza kutumia dawa iwapo kisababishi ni fungusi anaweza kutumia dawa zinazotibu fungasi kama vile cream zinazotibu fungasi na pia katika matumizi ya dawa hizi hazipaswi kutumiwa kiholela zinatumiwa kwa ushauri wa wataalamu wa afya kwa sababu mtu unaweza kutumia dawa huku una Ugonjwa mwingine hali ambayo inaweza kusababisha matatizo mengine makubwa.
9. Vile vile kwa wale wenye imani potofu juu ya ugonjwa huu waache kwa sababu watu baada ya kupata tatizo kama hili hawakubali kwenda hospitalini na kuanza kutumia miti shamba ambayo uchukua mda mrefu kutibu tatizo na tatizo linaendelea kuongezeka kila siku hali ikiwa mbaya ndipo wanakumbuka hospitali na unakuta wadudu wanakuwa wameingia mpaka ndani na kusababisha madhara makubwa.
10.Kwa hiyo akina Mama huu ni ugonjwa wa kawaida tu na unatibika ukipata tatizo nenda moja kwa moja hospitali ili uweze kupata matibabu kwa sababu Ugonjwa huu umewapa eatu wengi wametibiwa na wamepona na wanaendelea vizuri na maisha.
Umeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 Dua za Mitume na Manabii 👉2 Madrasa kiganjani 👉3 ai web app 👉4 web hosting 👉5 Simulizi za Hadithi Audio 👉6 Tafasiri ya Riyadh Swalihina
Post zinazofanana:
Habari Mimi ni mjamzito was miezi Tisa sasa nimeanza kutokwa na maji kidogo kidogo ukeni bila uchungu na no mimba yangu ya kwanza he Kuna shida?
Ujauzito husababisha mabadiliko mengi mwilini, ikiwepo ongezeko la Majimaji ukeni ifikapo tarehe za kukaribia kujifunguwa. Majimaji haya ni muhimu kwa afya ya mtoto aliye tumboni.
Soma Zaidi...Sababu za kuongezeka uzito wa wajawazito.
Posti hii inahusu zaidi sababu za kuongezeka uzito kwa wajawazito, Mara nyingi Mama akibeba mimba uongezeka uzito kutoka wiki ya Kwanza mpaka wiki ya mwisho ya kujifungua.
Soma Zaidi...Nguzo kuu za umama katika umri wa kupata watoto na kulea watoto
Posti hii inahusu zaidi nguzo kuu za umama katika umri wa kujifungua na kulea watoto, ni kipindi ambacho mama anakuwa analea watoto kwa kawaida kadri ya makadirio kipindi hiki uanza kati ya miaka kumi na mitano mpaka arobaini kwa walio wengi na kinaweza k
Soma Zaidi...Fahamu sifa za Ute wa siku za kupata mimba yaani ovulation day
Posti hii inahusu zaidi sifa za Ute wa ovulation, ni Ute ambao utokea siku za ovulation yaani siku ambazo ni tayari kwa kubeba mimba, yaani siku za upevishaji wa yai.
Soma Zaidi...Vyanzo vya mwanamke kushindwa kupata ujauzito
Posti hii inahusu zaidi vyanzo vya mwanamke kushindwa kupata ujauzito, kwa sababu kuna sababu nyingi ambazo Usababisha mwanamke kushindwa kupata ujauzito kama tutakavyoona hapo mbeleni
Soma Zaidi...Mabadiliko kwenye mfumo wa chakula kwa wajawazito.
Posti hii inahusu zaidi mabadiliko kwenye mfumo wa chakula kwa wajawazito, ni mabadiliko ambayo utokea kwa wajawazito hasa kwenye mfumo wa chakula.
Soma Zaidi...