Mabaka yanayowasha chini ya matiti.
Posti hii inahusu zaidi mabaka yanayowasha chini ya matiti, ni ugonjwa ambao uwapata wanawake walio wengi na wengine hawajapata jibu Sababu zake ni zipi na pengine uchukua hatua za kutumia miti shamba wakidai juwa hospitalini nugonjwa huu hautibiwa, ila n
Tatizo la mabaka yanayowasha chini ya matiti.
1. Tatizo hili kwa kawaida linaweza kumpata mwana mke yeyote yule hasa hasa uwapata wanawake walio wanene , wanawake wenye Ugonjwa wa kisukari, wanawake wenye matiti makubwa, wanawake wanaofanya mazoezi sana na pia wale wenye pilika pilika nyingi.
2.Ugonjwa huu utokea pale ambapo kuna misuguano kutoka sehemu mbili za matiti zinazoangaliana , baada ya sehemu hizo kubwa na msuguano kwa sababu ya shughuli mbalimbali au wakati wa mazoezi na hewa kwenye sehemu hiyo uwa kidogo hali ambayo Usababisha kuwepo kwa michubuko.
3.Kwa sababu ya michubuko ambayo huwa kwenye sehemu za matiti Usababisha wadudu kama vile bakteria na virusi kuweza kuingia kwenye michubuko hiyo kwa hiyo mama anaanza kuwasha na kujikuna hali ambayo Usababisha michubuka chini ya matiti.
4. Na kwa wakati mwingine kama kuna unyevunyevu kwenye matiti ukachanganyikana na wadudu hao hali inaweza kwa ngumu zaidi na kusababisha kujikuna sana , tatizo hili huwa kubwa zaidi hasa kwa wanawake wale wanaoshinda kwenye shughuli za kutumia nguvu na hawaogi hali huwa ngumu kwa sababu unaweza kukuta matiti yamechubuka sana.
5. Kwa hiyo baada ya kujua tatizo hili wanawake wote hasa kama ni wanene au wembamba ni vizuri kusafisha kwenye sehemu za matiti kwa maji safi na sabuni ili kuepuka na tatizo hili kwa sababu chanzo hiki ni kutofanya usafi na pia wanawake wenye Ugonjwa wa kisukari wawe makini sana kwa sababu walipatwa na tatizo hili ni vigumu kupona haraka kama wale wasio juwa na kisukari.
6.Pia ikumbukwe kwamba kwa akina Mama wanaopiga mazoezi kila siku au kufanya kazi zenye nguvu kama vile kulima kwa mda mrefu wanapaswa kuiga kila siku walau kwa mara moja na kunywa maji mengi ili kuepuka tatizo hili la kuwashwa kwenye matiti.
7.Pia kama imetokea mtu akapata na Ugonjwa huu anapaswa kutumia dawa kutegemea na kisababishi kama waliosababisha ni bakteria Mgonjwa anapaswa kutumia dawa ambazo ni antibiotics kama vile benzathine penicillin, erythromycin, oral penicillin kwa ajili ya kuondoa Maambukizi.
8.Pia Mgonjwa anaweza kutumia dawa iwapo kisababishi ni fungusi anaweza kutumia dawa zinazotibu fungasi kama vile cream zinazotibu fungasi na pia katika matumizi ya dawa hizi hazipaswi kutumiwa kiholela zinatumiwa kwa ushauri wa wataalamu wa afya kwa sababu mtu unaweza kutumia dawa huku una Ugonjwa mwingine hali ambayo inaweza kusababisha matatizo mengine makubwa.
9. Vile vile kwa wale wenye imani potofu juu ya ugonjwa huu waache kwa sababu watu baada ya kupata tatizo kama hili hawakubali kwenda hospitalini na kuanza kutumia miti shamba ambayo uchukua mda mrefu kutibu tatizo na tatizo linaendelea kuongezeka kila siku hali ikiwa mbaya ndipo wanakumbuka hospitali na unakuta wadudu wanakuwa wameingia mpaka ndani na kusababisha madhara makubwa.
10.Kwa hiyo akina Mama huu ni ugonjwa wa kawaida tu na unatibika ukipata tatizo nenda moja kwa moja hospitali ili uweze kupata matibabu kwa sababu Ugonjwa huu umewapa eatu wengi wametibiwa na wamepona na wanaendelea vizuri na maisha.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Share On:
👉1 web hosting 👉2 ai web app 👉3 Tafasiri ya Riyadh Swalihina 👉4 kitabu cha Simulizi 👉5 Madrasa kiganjani 👉6 Simulizi za Hadithi Audio
Post zinazofanana:
Je siku sahihi yakufanya tendo la ndoa niipi ukipata siku zake za hatari?
Swali langu ni hili doktaJe siku sahihi yakufanya tendo la ndoa niipi ukipata siku zake za hatari?
Soma Zaidi...Sababu za maumivu ya tumbo baada ya tendo la ndoa
Utajifunza sababua zinazopelekea kuhisi maumivu makali ya tumbo baada ya kumaliza tendo la ndoa
Soma Zaidi...NAMNA YA KUITAMBUA SIKU HATARI YA KUPATA MIMBA (UJAUZITO)
SIKU YA KUPATA UJAUZITO Mimba hutokea pindi mbegu ya kiume (sperm) inapokutana na yai la mwanamke (ova) na kuungana kwa pamoja kutengeneza selli moja iitwayo zygote.
Soma Zaidi...Dalili za kuharibika kwa mimba
Katika post hii utajifunza ishara na dalili ninazoonyesha kuwa mimba ipo hatarini kutoka ama inaweza kuwa imeshatoka.
Soma Zaidi...Fahamu dawa ya tetracycline katika kupambana na bakteria
Post hii inahusu zaidi dawa ya tetracycline katika kupambana na bakteria,ni mojawapo ya antibiotics au anti bacteria ambayo upambana na bakteria kama tutakavyoona hapo mbeleni.
Soma Zaidi...