Posti hii inahusu zaidi mabaka yanayowasha chini ya matiti, ni ugonjwa ambao uwapata wanawake walio wengi na wengine hawajapata jibu Sababu zake ni zipi na pengine uchukua hatua za kutumia miti shamba wakidai juwa hospitalini nugonjwa huu hautibiwa, ila n
Tatizo la mabaka yanayowasha chini ya matiti.
1. Tatizo hili kwa kawaida linaweza kumpata mwana mke yeyote yule hasa hasa uwapata wanawake walio wanene , wanawake wenye Ugonjwa wa kisukari, wanawake wenye matiti makubwa, wanawake wanaofanya mazoezi sana na pia wale wenye pilika pilika nyingi.
2.Ugonjwa huu utokea pale ambapo kuna misuguano kutoka sehemu mbili za matiti zinazoangaliana , baada ya sehemu hizo kubwa na msuguano kwa sababu ya shughuli mbalimbali au wakati wa mazoezi na hewa kwenye sehemu hiyo uwa kidogo hali ambayo Usababisha kuwepo kwa michubuko.
3.Kwa sababu ya michubuko ambayo huwa kwenye sehemu za matiti Usababisha wadudu kama vile bakteria na virusi kuweza kuingia kwenye michubuko hiyo kwa hiyo mama anaanza kuwasha na kujikuna hali ambayo Usababisha michubuka chini ya matiti.
4. Na kwa wakati mwingine kama kuna unyevunyevu kwenye matiti ukachanganyikana na wadudu hao hali inaweza kwa ngumu zaidi na kusababisha kujikuna sana , tatizo hili huwa kubwa zaidi hasa kwa wanawake wale wanaoshinda kwenye shughuli za kutumia nguvu na hawaogi hali huwa ngumu kwa sababu unaweza kukuta matiti yamechubuka sana.
5. Kwa hiyo baada ya kujua tatizo hili wanawake wote hasa kama ni wanene au wembamba ni vizuri kusafisha kwenye sehemu za matiti kwa maji safi na sabuni ili kuepuka na tatizo hili kwa sababu chanzo hiki ni kutofanya usafi na pia wanawake wenye Ugonjwa wa kisukari wawe makini sana kwa sababu walipatwa na tatizo hili ni vigumu kupona haraka kama wale wasio juwa na kisukari.
6.Pia ikumbukwe kwamba kwa akina Mama wanaopiga mazoezi kila siku au kufanya kazi zenye nguvu kama vile kulima kwa mda mrefu wanapaswa kuiga kila siku walau kwa mara moja na kunywa maji mengi ili kuepuka tatizo hili la kuwashwa kwenye matiti.
7.Pia kama imetokea mtu akapata na Ugonjwa huu anapaswa kutumia dawa kutegemea na kisababishi kama waliosababisha ni bakteria Mgonjwa anapaswa kutumia dawa ambazo ni antibiotics kama vile benzathine penicillin, erythromycin, oral penicillin kwa ajili ya kuondoa Maambukizi.
8.Pia Mgonjwa anaweza kutumia dawa iwapo kisababishi ni fungusi anaweza kutumia dawa zinazotibu fungasi kama vile cream zinazotibu fungasi na pia katika matumizi ya dawa hizi hazipaswi kutumiwa kiholela zinatumiwa kwa ushauri wa wataalamu wa afya kwa sababu mtu unaweza kutumia dawa huku una Ugonjwa mwingine hali ambayo inaweza kusababisha matatizo mengine makubwa.
9. Vile vile kwa wale wenye imani potofu juu ya ugonjwa huu waache kwa sababu watu baada ya kupata tatizo kama hili hawakubali kwenda hospitalini na kuanza kutumia miti shamba ambayo uchukua mda mrefu kutibu tatizo na tatizo linaendelea kuongezeka kila siku hali ikiwa mbaya ndipo wanakumbuka hospitali na unakuta wadudu wanakuwa wameingia mpaka ndani na kusababisha madhara makubwa.
10.Kwa hiyo akina Mama huu ni ugonjwa wa kawaida tu na unatibika ukipata tatizo nenda moja kwa moja hospitali ili uweze kupata matibabu kwa sababu Ugonjwa huu umewapa eatu wengi wametibiwa na wamepona na wanaendelea vizuri na maisha.
Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetuUmeionaje Makala hii.. ?
Posti hii inahusu zaidi namna ya kuepuka fangasi za ukeni, ni njia ambazo usaidia kuepuka madhara ya fangasi za ukeni.
Soma Zaidi...Matatizo yahusianayo na nguvu za kume na kukosa hamu ya tendo la ndoa kwahuweza kuchangiwa sana na mpangilio mbovu wa vyakula pamoja na saikolojia ya mtu.
Soma Zaidi...Mapacha walioungana ni watoto wawili wanaozaliwa wakiwa wameunganishwa kimwili. Mapacha walioungana hukua wakati kiinitete cha mapema kinapojitenga na kuunda watu wawili. Ingawa fetusi mbili zitakua kutoka kwa kiinitete hiki, zitabaki zimeunganishwa mar
Soma Zaidi...Unaweza kutaka kujuwa je naweza kupata dalili za mimba baada ya siku nne toka ujauzito kutungwa? ama baada ya siku nne toka kushiriki tendo la ndoa. Makala hii itakwenda kujibu maswali haya na mengineyo.
Soma Zaidi...Je kichwa cha uume wako kinawasha, na je kinatoa majimaji kwenye njia ya mkojo, una muda ganinavtatizo hili. Na je ulishiriki ngono zembe siku za hivi karibuni?
Soma Zaidi...Posti hii inahusu zaidi Dalili ambazo anaweza kuzipata mwenye Ugonjwa wa tezi dume, sio Dalili zote mtu anaweza kuzipata kwa sababu dalili kama hizi zinaweza kujitokeza hata kwa magonjwa mengine.
Soma Zaidi...Makala hii itakwenda kukufundisha dalili za kujifunguwa, hatuwa za kujifunguwa na kuzalisha, pia utajifunza mabo muhimu kabla na wakatii wa kujifungua.
Soma Zaidi...Jifunze muda ambao mjamzito hatatkiwa kishiriki tendo la ndoa. je kuna madhara kwa mjamzito kushiriki tendo la ndoa.
Soma Zaidi...Post hii inahusu zaidi sababu mbalimbali za mtoto kuzaliwa akiwa na uzito mkubwa, mara nyingi tatizo hili uwakumba akina mama mbalimbali ambapo mtoto uzaliwa akiwa na uzito mkubwa
Soma Zaidi...Ni vyakula gani anapasa kula mjamzito, na utaratibu mzima wa lishe kwa wajawazito
Soma Zaidi...