TAKBIRA YA KWANZA, DUA BAADA YA TAKBIRA YA KUHIRIMIA SWALA NA KUSOMA ALHAMDU (SURAT AL-FATIHA KWENYE SWALA

2.

TAKBIRA YA KWANZA, DUA BAADA YA TAKBIRA YA KUHIRIMIA SWALA NA KUSOMA ALHAMDU (SURAT AL-FATIHA KWENYE SWALA

2. Kusoma Dua ya Kufungulia Swala
Kusoma dua ya kufungulia swala ni sunnah. Katika Hadithi ya Bukhari na Muslim iliyosimuliwa na Abu Hurairah (r.a), baada ya kuhirimia swala Mtume (s.a.w) alikuwa akileta dua ifuatayo: โ€œwajahtu wajhi lilladhi fatwaras-samaawat wal-ardha hanifam-muslima wamaa ana minal-mushrikina. Inna swalatiy wanusukii, wamah-haya, wamaamatiy, lillahi rabil-alamiina laa sharikalahu wabidhalika umirtu wa-ana minal-muslimina.โ€โ€œNimeuelekeza uso wangu kwa yule aliyeziumba mbingu na ardhi. Nimeacha dini za upotovu. Mimi si miongoni mwa washirikina. Hakika swala yangu (na ibada zangu zote) na uzima wangu na kufa kwangu (yote) ni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, bwana (Rabbi) wa walimwengu wote. Hana mshirika wake. Na haya ndio niliyoamrishwa na mimi ni wa kwanza walio jisalimisha kikamilifu kwa Mwenyezi Mungu. (6:79, 162-163)

3. Kupiga Audhu Billah Kabla ya kuanza kusoma Qur-an ni amri ya Allah (s.w) kujikinga na sheitwani kama inavyodhihirika katika aya ifuatayo: 109 โ€œNa ukitaka kusoma Qur-an piga Audhu billah (jikinge) kwa Allah (akulinde) na Sheitwani aliyefukuzwa (kwenye Rehema). (16:98) Hivyo tuanze kusoma Qur-an kwa kusema โ€œAโ€™udhu-billahi minash-shaytwanir- Rajiimโ€ Najikinga kwa Allah na sheitwan aliyefukuzwa-kwenye Rehma yako

4. Kusoma Suratul-Fatiha Kusoma Suratul-Fatihah ni nguzo ya tatu ya swala na ndio nguzo kubwa ya swala. Tunasoma suratul-Fatiha kama ifuatavyo:- Bismillahir Rahmaanir Rahiim (1) Alhamdu liLLahi rabbil-โ€™Aalamiin (2). Rrahmaanir Rahiim (3) Maaliki yaumiddiin (4) Iyyaakana โ€˜abudu waiyyaaka nastaโ€˜iin (5) Ih dinasw-swiraatwal mustaqiim (6) Swiraatwa lladhiina an โ€˜amta โ€˜alaihim; ghairil maghdhuubi โ€˜alaihim wala dhw-dhwaaliin (7)

Tafsri:
(1) Kwa jina la Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema na mwenye kurehemu: (2) Shukrani zote anastahiki Mwenyezi Mungu, Mola wa Walimwengu wote: (3) Mwingi wa Rehema mwenye kurehemu (4) Mwenye kumiliki siku ya malipo: (5) Wewe tu ndiye tunayekuabudu, na wewe tu ndiye tunaye kuomba msaada: (6) Tuongoze njia iliyonyooka: (7) Njia ya wale uliowaneemesha; siyo (ya wale ) waliokasirikiwa, wala ya wale waliopotea
5. Kusoma Qur-an baada ya Suratul-Fatiha Katika rakaa ya kwanza na ya pili ni Sunnah baada ya kusoma Suratul-Fatiha kuleta Surah au aya nyingine za Qur-an:


                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Download App yetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Fiqh Main: Dini File: Download PDF Views 2148

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
๐Ÿ‘‰1 Simulizi za Hadithi Audio    ๐Ÿ‘‰2 Kitau cha Fiqh    ๐Ÿ‘‰3 Kitabu cha Afya    ๐Ÿ‘‰4 Madrasa kiganjani    ๐Ÿ‘‰5 kitabu cha Simulizi    ๐Ÿ‘‰6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Taratibu za kumuona mchumba katika uislamu

Hspa utajifunza taratibu za kuonana na mchumba katika uislamu.

Soma Zaidi...
Funga za Sunnah na umuhimu wake

Nguzo za uislamu (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
NAMNA YA KUCHINJA KATIKA UISLAMU

ุนูŽู†ู’ ุฃูŽุจููŠ ูŠูŽุนู’ู„ูŽู‰ ุดูŽุฏูŽู‘ุงุฏู ุจู’ู†ู ุฃูŽูˆู’ุณู ุฑูŽุถููŠูŽ ุงู„ู„ู‡ู ุนูŽู†ู’ู‡ู ุนูŽู†ู’ ุฑูŽุณููˆู„ู ุงู„ู„ูŽู‘ู‡ู ุตู„ู‰ ุงู„ู„ู‡ ุนู„ูŠู‡ ูˆ ุณู„ู… ู‚ูŽุงู„ูŽ: "ุฅู†ูŽู‘ ุงู„ู„ูŽู‘ู‡ูŽ ูƒูŽุชูŽุจูŽ ุงู„ู’ุฅูุญ...

Soma Zaidi...
NI KWA NINI TUNASWALI?, NI UPI UMUHIMU WA KUSWALI NA NI ZIPI FADHILA ZA KUSWALI

Umuhimu wa KusimamishaSwala Kwa mujibu wa Hadith ya Ibn Umar (r.

Soma Zaidi...
MAMBO YANAYOBATILISHA (HARIBU) SWALA YAKO

Lugha ya Swala Lugha ya swala,kuanzia kwenye Takbira ya kuhirimia Swala mpaka kumalizia swala kwa Salaam, ni Kiarabu.

Soma Zaidi...
Kujitwaharisha kutokana na najisi

Post hii itakufundisha namna ya kutwaharisha Najisi.

Soma Zaidi...
JIFUNZE FIQH

Fahamu darsa mbalimbali za fiqh kama swala, twahara, zaka pamoja na funga. Zijuwe sharti za swala, funga na zaka.

Soma Zaidi...
Jinsi ya kukaa itiqaf na taratibu zake

Hapa utajifunza kuhusu taratibu za ibada ya itiqaf yaani kukaa msikitini kwa ajili ya ibada.

Soma Zaidi...