mitume

Labda itaulizwa: Kwanini Mtume Muhammad (s.

Kwa nini Mtume Muhammad awe ni wa ulimwengu mzima?


Labda itaulizwa: Kwanini Mtume Muhammad (s.a.w) awe Mtume wa walimwengu wote? Ama kuhusu suali hili, hapana jibu lolote lililotolewa katika Qur-an wala katika hadithi za Mtume (s.a.w). Hivyo ni Allah (s.w) pekee anayejua ni kwanini alimleta kwa ulimwengu mzima.


Lakini tunaweza kutumia akili zetu finyu tukajaribu kuona hikima iliyopo kwa Mtume (s.a.w) kuwa Mtume wa ulimwengu mzima jambo ambalo halikuwezekana kwa Mitume waliotangulia. Hapo awali, kabla ya Mtume (s.a.w), Mitume walikuwa wakitokea kwa kila nchi au kila taifa.


Sababu ya msingi tunayoweza kuona kirahisi ni kwamba katika wakati huo wa historia njia za usafiri na mawasiliano yalikuwa finyu sana kwa kiasi ambacho mawasiliano kati ya watu na nchi moja na nyingine yalikosekana kabisa.


Kila nchi au ukanda wa jiografia ulikuwa ni ulimwengu wa peke yake. Katika hali hii ilikuwa ni vigumu mno kuwa na Mtume mmoja kwa ulimwengu wote. Ndio tunakuta kila nchi au kila ukanda wa jiografia ukatumiwa Mtume wake.
Sote tunashuhudia kuwa katika umma huu wa mwisho wa Mtume Muhammad (s.a.w) pamekuwa na maendeleo makubwa sana ya mawasiliano kiasi kwamba dunia inakuwa kama kijiji. Suala la “Globalization” (utandawazi) kwa Waislamu sijambo geni


Tunafahamishwa katika Qur-an kuwa umma huu wa Mtume Muhammad (s.a.w) ni umma mmoja na unawajibika kuufanya Uislamu utawale ulimwengu mzima.
Kutokana na hoja hizi tatu itaonekana wazi ni kwanini hakuna haja ya Mtume mwingine baada ya Muhammad (s.a.w). Na ndivyo Allah (s.w) anavyotufahamisha katika Qur-an kuwa yeyeMuhammad (s.a.w) ni “Khataman-Nabiyyina” - yaani mwisho wa Mitu me:Muhammad si baba wa yeyote katika wanaume wenu, bali yeye ni Mtume wa Allah na mwisho wa Mitume na Allah ni mjuzi wa kila kitu. (33:40)Na Mtume Muhammad (s.a.w) mwenyewe pia anasema:
Palikuwa na Mitume waliowaongoza Banii Israil katika njia sahihi.


Kila Mtume alipokufa, alifuatiwa na Mtume mwingine. Lakini hapana Mtume atakayekuja baada yangu. Kazi hii (ya kuufundisha Uislamu na kuusimamisha) inaweza kufanywa na makhalifa (viongozi wa Kiislamu). (Bukhari).
Na katika Hadithi nyengine Mtume (s.a.w) amesema: “Uhusiano wangu na (msururu mrefu) wa Mitume unaweza kueleweka vizuri kwa mfano wa nyumba nzuri ya kifalme. Nyumba hii ikawa imejengwa vizuri sana na ikawa inapendeza lakini pakawa na nafasi moja iliyobakia. Watu wakawa wanaizungumza nyumba hii nzuri na wakawa wanauliza kwa mshangao.Kwanini hii sehemu isiwe imejazwa! Nimejaza pengo hili na ni Mtume wa mwisho”. (Bukhari).




                   


Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 530

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 kitabu cha Simulizi    👉3 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉4 Madrasa kiganjani    👉5 Bongolite - Game zone - Play free game    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Himizo la kuwasamehe waliotukosea

“Na wasiape wale wakarimu na wenye wasaa miongoni mwenu, kujizuia kuwasaidia jamaa zao, maskini na wale waliohama kwa ajili ya Dini ya Allah; na wasamehe na waachilie mbali (wapuuze yaliyopita).

Soma Zaidi...
NGUZO ZA IMANI

Tunajifunza katika Qur-an na hadithi sahihi kuwa Imani ya Kiislamu imejengwa juu ya nguzo sita zifuatazo:1 Kumuamini Allah (s.

Soma Zaidi...
Sifa za wanafiki zilizotajwa katika surat al-Baqarah

Na katika watu, wako (wanafiki) wasemao: "Tumemwamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho"; na hali ya kuwa wao si wenye kuamini.

Soma Zaidi...
Udhaifu wa mtazamo wa makafiri juu ya dini dhidi ya mtazamo wa uislamu

Somo Hili linaeleza kuhusu mtazamo wa uislamu juu ya dini (EDK form2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Elimu yenye manufaa

Elimu yenye manufaa Ni ipi? (EDK form 1:elimu yenye manufaa)

Soma Zaidi...
Sifa za waumini zilizotajwa katika surat Al-Anfal (8:2-4) na Al-Hujurat

"Hakika wanaoamini kweli ni wale ambao anapotajwa Allah nyoyo zao hujaa khofu; na wanaposomewa aya zake huwazidishia imani na wanamtegemea Mola wao tu basi.

Soma Zaidi...