mitume

Labda itaulizwa: Kwanini Mtume Muhammad (s.

Kwa nini Mtume Muhammad awe ni wa ulimwengu mzima?


Labda itaulizwa: Kwanini Mtume Muhammad (s.a.w) awe Mtume wa walimwengu wote? Ama kuhusu suali hili, hapana jibu lolote lililotolewa katika Qur-an wala katika hadithi za Mtume (s.a.w). Hivyo ni Allah (s.w) pekee anayejua ni kwanini alimleta kwa ulimwengu mzima.


Lakini tunaweza kutumia akili zetu finyu tukajaribu kuona hikima iliyopo kwa Mtume (s.a.w) kuwa Mtume wa ulimwengu mzima jambo ambalo halikuwezekana kwa Mitume waliotangulia. Hapo awali, kabla ya Mtume (s.a.w), Mitume walikuwa wakitokea kwa kila nchi au kila taifa.


Sababu ya msingi tunayoweza kuona kirahisi ni kwamba katika wakati huo wa historia njia za usafiri na mawasiliano yalikuwa finyu sana kwa kiasi ambacho mawasiliano kati ya watu na nchi moja na nyingine yalikosekana kabisa.


Kila nchi au ukanda wa jiografia ulikuwa ni ulimwengu wa peke yake. Katika hali hii ilikuwa ni vigumu mno kuwa na Mtume mmoja kwa ulimwengu wote. Ndio tunakuta kila nchi au kila ukanda wa jiografia ukatumiwa Mtume wake.
Sote tunashuhudia kuwa katika umma huu wa mwisho wa Mtume Muhammad (s.a.w) pamekuwa na maendeleo makubwa sana ya mawasiliano kiasi kwamba dunia inakuwa kama kijiji. Suala la “Globalization” (utandawazi) kwa Waislamu sijambo geni


Tunafahamishwa katika Qur-an kuwa umma huu wa Mtume Muhammad (s.a.w) ni umma mmoja na unawajibika kuufanya Uislamu utawale ulimwengu mzima.
Kutokana na hoja hizi tatu itaonekana wazi ni kwanini hakuna haja ya Mtume mwingine baada ya Muhammad (s.a.w). Na ndivyo Allah (s.w) anavyotufahamisha katika Qur-an kuwa yeyeMuhammad (s.a.w) ni “Khataman-Nabiyyina” - yaani mwisho wa Mitu me:Muhammad si baba wa yeyote katika wanaume wenu, bali yeye ni Mtume wa Allah na mwisho wa Mitume na Allah ni mjuzi wa kila kitu. (33:40)Na Mtume Muhammad (s.a.w) mwenyewe pia anasema:
Palikuwa na Mitume waliowaongoza Banii Israil katika njia sahihi.


Kila Mtume alipokufa, alifuatiwa na Mtume mwingine. Lakini hapana Mtume atakayekuja baada yangu. Kazi hii (ya kuufundisha Uislamu na kuusimamisha) inaweza kufanywa na makhalifa (viongozi wa Kiislamu). (Bukhari).
Na katika Hadithi nyengine Mtume (s.a.w) amesema: “Uhusiano wangu na (msururu mrefu) wa Mitume unaweza kueleweka vizuri kwa mfano wa nyumba nzuri ya kifalme. Nyumba hii ikawa imejengwa vizuri sana na ikawa inapendeza lakini pakawa na nafasi moja iliyobakia. Watu wakawa wanaizungumza nyumba hii nzuri na wakawa wanauliza kwa mshangao.Kwanini hii sehemu isiwe imejazwa! Nimejaza pengo hili na ni Mtume wa mwisho”. (Bukhari).




                   


Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass

Nyuma Endelea


Je umeipenda post hii ?

Ndio            Hapana            Save post
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 450

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Simulizi za Hadithi Audio    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Kitabu cha Afya    👉4 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉5 kitabu cha Simulizi    👉6 Kitau cha Fiqh   

Post zinazofanana:

Muhtasari wa sifa za waumini

Lengo tarajiwa la Muhtasari huu ni kutuwezesha kuzibaini fika sifa za Waumini zilizoainishwa katika Qur'an, kisha kujipamba nazo ili tuwe waja wema watakaorehemewa na kuridhiwa na Allah (s.

Soma Zaidi...
Nini chanzo cha elimu zote na ujuzi wote

Ninichanzo cha Elimu? (EDK form 1 Dhanaya Elimu)

Soma Zaidi...
Kina Cha uovu wa shirk

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
KUAMINI MITUME WA ALLAH (S.W)

Mtu hawi Muumini wa kweli mpaka awe na yakini juu ya Mitume wa Allah (s.

Soma Zaidi...
Kujiepusha na kufuata mambo kwa kibubusa

Waislamu wanakatazwa kufanya na kufuata mambo kwa kibubusa (kwa mkumbo) bila ya kuwa na ujuzi unaostahiki.

Soma Zaidi...
Mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu

Mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu Ni upi? (EDK form 1: mgawanyo wa elimu usiokubalika katika uislamu)

Soma Zaidi...
Tofauti kati ya Quran na vitabu vingine vya mwenyezi Mungu

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mgawanyiko wa Elimu kwa mtazamo wa kikafiri

Kwa mtazamo wa kikafiri elimu imegawanyika katika makundi mawili ambayo ni Elimu ya dunia na Elimu ya akhera.

Soma Zaidi...
Sifa za Wanafiki zilizotajwa katika surat Hashir

Huwaoni wale wanafiki wanawaambia ndugu zao walio makafiri miongoni mwa watu waliopewa Kitabu (kabla yenu) Mayahudi (Wanawaambia): "Kama mkitolewa, (mkifukuzwa hapa) tutaondoka pamoja nanyi, wala hat utamtii yoyote kabisa juu yenu.

Soma Zaidi...