mitume

mitume

Labda itaulizwa: Kwanini Mtume Muhammad (s.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Kwa nini Mtume Muhammad awe ni wa ulimwengu mzima?


Labda itaulizwa: Kwanini Mtume Muhammad (s.a.w) awe Mtume wa walimwengu wote? Ama kuhusu suali hili, hapana jibu lolote lililotolewa katika Qur-an wala katika hadithi za Mtume (s.a.w). Hivyo ni Allah (s.w) pekee anayejua ni kwanini alimleta kwa ulimwengu mzima.


Lakini tunaweza kutumia akili zetu finyu tukajaribu kuona hikima iliyopo kwa Mtume (s.a.w) kuwa Mtume wa ulimwengu mzima jambo ambalo halikuwezekana kwa Mitume waliotangulia. Hapo awali, kabla ya Mtume (s.a.w), Mitume walikuwa wakitokea kwa kila nchi au kila taifa.


Sababu ya msingi tunayoweza kuona kirahisi ni kwamba katika wakati huo wa historia njia za usafiri na mawasiliano yalikuwa finyu sana kwa kiasi ambacho mawasiliano kati ya watu na nchi moja na nyingine yalikosekana kabisa.


Kila nchi au ukanda wa jiografia ulikuwa ni ulimwengu wa peke yake. Katika hali hii ilikuwa ni vigumu mno kuwa na Mtume mmoja kwa ulimwengu wote. Ndio tunakuta kila nchi au kila ukanda wa jiografia ukatumiwa Mtume wake.
Sote tunashuhudia kuwa katika umma huu wa mwisho wa Mtume Muhammad (s.a.w) pamekuwa na maendeleo makubwa sana ya mawasiliano kiasi kwamba dunia inakuwa kama kijiji. Suala la “Globalization” (utandawazi) kwa Waislamu sijambo geni


Tunafahamishwa katika Qur-an kuwa umma huu wa Mtume Muhammad (s.a.w) ni umma mmoja na unawajibika kuufanya Uislamu utawale ulimwengu mzima.
Kutokana na hoja hizi tatu itaonekana wazi ni kwanini hakuna haja ya Mtume mwingine baada ya Muhammad (s.a.w). Na ndivyo Allah (s.w) anavyotufahamisha katika Qur-an kuwa yeyeMuhammad (s.a.w) ni “Khataman-Nabiyyina” - yaani mwisho wa Mitu me:Muhammad si baba wa yeyote katika wanaume wenu, bali yeye ni Mtume wa Allah na mwisho wa Mitume na Allah ni mjuzi wa kila kitu. (33:40)Na Mtume Muhammad (s.a.w) mwenyewe pia anasema:
Palikuwa na Mitume waliowaongoza Banii Israil katika njia sahihi.


Kila Mtume alipokufa, alifuatiwa na Mtume mwingine. Lakini hapana Mtume atakayekuja baada yangu. Kazi hii (ya kuufundisha Uislamu na kuusimamisha) inaweza kufanywa na makhalifa (viongozi wa Kiislamu). (Bukhari).
Na katika Hadithi nyengine Mtume (s.a.w) amesema: “Uhusiano wangu na (msururu mrefu) wa Mitume unaweza kueleweka vizuri kwa mfano wa nyumba nzuri ya kifalme. Nyumba hii ikawa imejengwa vizuri sana na ikawa inapendeza lakini pakawa na nafasi moja iliyobakia. Watu wakawa wanaizungumza nyumba hii nzuri na wakawa wanauliza kwa mshangao.Kwanini hii sehemu isiwe imejazwa! Nimejaza pengo hili na ni Mtume wa mwisho”. (Bukhari).




                   


Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 561

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Madrasa kiganjani    👉3 Kitau cha Fiqh    👉4 Bongolite - Game zone - Play free game    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 kitabu cha Simulizi   

Post zinazofanana:

Lengo la kuumbwa Mwanadamu ni lipi?
Lengo la kuumbwa Mwanadamu ni lipi?

Kwenye kipengele hichi tutajifunza lengo la kuumbwa mwaanadamuengo la kuumbwa ulimwengu na viumbe vilivyomo.

Soma Zaidi...
SHIRK
SHIRK

Jifunze tawhid yaani kumpwekesha Allah subhaanah wata'aala

Soma Zaidi...
Kumuamini malaika wa mwenyezi Mungu
Kumuamini malaika wa mwenyezi Mungu

Nguzo za Imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
NGUZO ZA IMANI
NGUZO ZA IMANI

Tunajifunza katika Qur-an na hadithi sahihi kuwa Imani ya Kiislamu imejengwa juu ya nguzo sita zifuatazo:1 Kumuamini Allah (s.

Soma Zaidi...
Kina Cha uovu wa shirk
Kina Cha uovu wa shirk

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Shirk na aina zake
Shirk na aina zake

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Neema za Allah(s.w) Juu ya Bani Israil
Neema za Allah(s.w) Juu ya Bani Israil

Katika Qur'an tunakumbushwa neema mbali mbali walizotunukiwa Bani Israil (Mayahudi) na Mola wao ili kuwawezesha kusimamisha Ufalme wa Allah(s.

Soma Zaidi...
Haki za kielimu za mwanamke katika uislamu
Haki za kielimu za mwanamke katika uislamu

Haki ya ElimuKatika Uislamu kujielimisha ni faradhi inayowahusu Waislamu wote, wanaume na wanawake: "Soma kwa jina ?

Soma Zaidi...
Uchambuzi wa Neema Alizopewa Nabii Sulaiman(a.s)
Uchambuzi wa Neema Alizopewa Nabii Sulaiman(a.s)

(i) Kutiishiwa Upepo Qur'an inatufahamisha kuwa Nabii Sulaiman alitiishiwa upepo akaweza kuutumia apendavyo kwa amri yake.

Soma Zaidi...