kuwa na kauli njema, na faida zake katika jamii

kuwa na kauli njema, na faida zake katika jamii

11.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

kuwa na kauli njema, na faida zake katika jamii

11. Kuwa na Kauli Njema


Muislamu anatakiwa kila mara azungumze mambo ya maana na ya kheri. Ulimi utumike kusema ukweli, kuamrisha mema, kukataza maovu, kuwashauri wengine juu ya mambo ya kheri, kupatanisha waliogombana, kumsabihi Allah, kutoa elimu yenye kunufaisha watu na katika mazungumzo mengine ya kheri.


“Na ni nani asemaye kauli bora kuliko (yule) aitaye (watu) kwa Allah na (mwenyewe) akafanya vitendo vizuri na kusema (kwa maneno yake na vitendo vyake): “Hakika mimi ni miongoni mw a Waislamu ”. (41:33).
Allah (s.w) anatuamrisha kusema maneno mazuri katika aya ifu atayo:

“Na waambie waja wangu waseme daima maneno yaliyo mazuri. Maana Shetani huchochea ugomvi baina yao. Hakika shetani kwa wanaadamu ni adui aliye dhahiri”. (17:53)
Hivyo Muislamu hana budi kuzungumza na watu kwa maneno mazuri ya heshima. Maneno mazuri ya heshima yanajenga na kuzidisha upendo kati ya watu. Maneno mazuri ya heshima ni ngao ya kumzuilia shetani asiingilie kati na kuleta migongano na kutoelewana. Ni katika msingi huu tunaamrishwa tuulinganie Uislamu kwa hekima na kwa mawaidha mazuri:

“Walinganie (watu) katika njia ya Mola wako kwa hekima na mawaidha m em a, na ujadiliane nao kw a namna iliyo bora. Hakika Mola w ako ndiye anayemjua aliyepotea katika njia yake naye ndiye anayewajua walioongoka ”. (16:125).
Kauli njema ni yenye kumuongoza mja kwenda Peponi na kauli mbaya humuongoza mja kwenda Motoni kama tunavyojifunza katika Hadithi zifuatazo:
Sahl bin Sa ’d(r.a) ameeleza kuwa Mtume wa Allah amesema: “Atakayeweza kuchunga kilichopo kati kati ya taya zake (ulimi) na kilichopo katikati ya miguu yake miwili (utupu) ninaw eza kumhakikishia Pepo.” (Bukhari).

Abu Hurairah(r.a) amesimulia kuwa Mtume wa Allah amesema: “Mja atatamka neno lenye kumfurahisha Allah bila ya kuona uzito wake, bado Allah (s.w) humlipa malipo makubwa kutokana na neno hilo. Na mja atatamka neno lenye kumuudhi Allah bila ya kuona uzito wake, na bado linakuw a ndio mw anzo w a kumuingiza Motoni. (Bukhari).



                   

Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sunnah Main: Dini File: Download PDF Views 1424

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

Masharti ya kukubaliwa kwa dua
Masharti ya kukubaliwa kwa dua

Post hii itakwenda kukugundisha masharti yanayofungamana na kukubaliwa kwa dua.

Soma Zaidi...
Dua sehemu 03
Dua sehemu 03

Zijuwe njia ambazo Allah hujibu Dua yako. Tambua kama umejibiwa dua yako au bodo, soma darsa za dua hapa.

Soma Zaidi...
Dua sehemu ya 04
Dua sehemu ya 04

Soma dua mbalimbali za kila siku ambazo unatakiwa uzijuwe. Dua 120 ambazo muislamu anatakiwa kuzijua

Soma Zaidi...
MAANA YA HADITHI SUNNAH
MAANA YA HADITHI SUNNAH

Maana ya SunnahKilugha: Neno sunnah katika lugha ya Kiarabu lina maana ya mwenendo au mila.

Soma Zaidi...
 hadithi ya 8
hadithi ya 8

عَنْ ابْنِ عُمَرَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا، أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه و سلم قَالَ: "أُمِرْتُ أَنْ أُقَاتِلَ النَّاسَ حَتَّى ?...

Soma Zaidi...