picha

Jinsi ya kuzuru makaburi na dua unazotakiwa kuzisoma ukiwa makaburini.

Posti hii inakwenda kukufundisha maneno unayotakiwa kuyasema unapozuru makaburi.

UTARATIBU NA DUA YA KUZURU MAKABURI

Kuzuru makaburi ni katika matendo ya sunah yaani unapata thawabu kwa kwenda klizuru kaburi. Ni katika matendo yanayotukumbusha kifo. Hata mtume allikuwa akienda kuzuru makaburi mara kadhaa. Hata mwishoni mwa siku za mwisho za uhai wake alikwenda kuzuru makaburi na kuwaaga waliokufa na kuwaombea dua.



Hapo mwanzo wanawake walikatazwa kuzuru makaburi kwa maneno ya Mtume aliposema “wamelaaniwa wanawake wenye kuzuru makaburi”. lakini baadaye mtume akawaruhusu wanawake kuzuru makaburi. Kwa ufupi ibada hii ni kwa waislamu wote na haina siku maalumu ama wakati maalumu. Kwani Mtume alikuwa anakwenda kuzuru makaburi hadi wakati wa usiku.



Kuzuru makaburi sio lakima uwe na udhu. Unaweza kuzuru hata ukiwa hupo twahara. Ukifika kwanza unaanza kusalimia (kutoa salamu) kisha unaomba dua pia ukiwa makaburini unaweza kulimia ama kusafishai kaburi ama makaburi. Ama kujazia udongo haya yote sio ya lazima. Kisha utaomba dua



Dua ya kuzuru kaburi
لسَّلامُ عَلَـيْكُمْ أَهْلَ الدِّيارِ مِنَ المؤْمِنيـنَ وَالْمُسْلِمينَ، وَإِنّا إِنْ شاءَ اللهُ بِكُـمْ لاحِقُـونَ، (وَيَرْحَمُ اللَّهُ الْمُسْتَقْدِمِينَ مِنَّا وَالْمُسْتَأْخِرِينَ) أَسْـاَلُ اللهَ لَنَـا وَلَكُـمْ العَـافِيَةَ.

Assalaamu ’alaykum ahlad-diyaar minal Mu-uminiyna wal Muslimiyn, wainnaa In Shaa Allaahu bikum laahiquwn. (Wa yarhamu-Allaahu al-mustaqdimiyna minnaa wal musta-akhiriyna). As-alu-Allaaha lanaa walakumul-’aafiyah
 

Amani ishuke juu yenu watu wa nyumba za Waumini na Waislamu, nasi apendapo Allaah tutakutana nanyi (Na Allaah Awarehemu wa mwanzo na wa mwisho). Namuomba Allaah Atupe sisi nanyi Al-’Aafiyah
al-hidaayah.com
 

Mwenye kuzuru makaburi anaruhusiwa kwenda akiwa peke yake ama akiwa na wenzie. Halikadhalika hakuna mavazi ya rangi maalumu wakati wa kuzuru ama kuzika. Hakuna haja ya kunyoa nywele wana kuandaa vyakula. Hairuusiwi kuyataja mabaya ya aliuyefariki ama kukaa juu ya kaburi. Pia hairuhusiwi kuzungumza mabo maovu maeneo ya makaburi.
 

Kwa hakika kuzuru makaburi ni ibada inayotaka utulivu wa nafsi. Kwani inatakikana moyo upate mawaidha kutokana na kutembelea kaburi. Mwenye kuzuru kaburi apate athari ya kuyaogopa mauti ili apate kufanya maandalizi.

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu
Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

       
Author: Rajabu image Tarehe: 2024-05-10 14:53:23 Topic: Sunnah Main: Post File: Download PDF Views 4055

Share On:

Share follows: 0 | Unique share links followed: 0
Sponsored links
👉1 Dua za Mitume na Manabii     👉2 Kitabu cha Afya     👉3 Madrasa kiganjani     👉4 kitabu cha Simulizi     👉5 Kitau cha Fiqh     👉6 Simulizi za Hadithi Audio    

Post zinazofanana:

DUA ZA KUONDOA WASIWASI

DUA ZA KUONDOA MAUMIVU MWILINI Katika uislamu Allah amejaalia dawa katika kufuata sunnah.

Soma Zaidi...
Nafasi ya Elimu na wenye elimu katika Uislamu

Nafasi ya elimu na mwenye elimu katika uislamu inaonkana katika maeneo yafuatayo: Kwanza, Elimu ndio takrima ya kwanza aliyokirimiwa mwanaadamu na Mola wake.

Soma Zaidi...
DUA YA MUUMINI NA DUA YA KAFIRI

DUA YA KAFIRI NA DUA YA MUUMINI.

Soma Zaidi...
Je! inajuzu wanawake kuzuru makaburi?

As salaam alaykum warahmatullah wabarakatuh, nauliza inajuzu wanawake kuzuru makaburi?

Soma Zaidi...
KUINGIA KWA WAGENI

Download kitabu Hiki Bofya hapa KUINGIA KWA WAGENI Amina na Sadie walimuonea huruma wakamuomba Zubeid amruhusu abakie.

Soma Zaidi...