kuwa na ikhlas

Ikhlas ni kufanya kila jambo jema kwa ajili ya Allah (s.

kuwa na ikhlas

  1. KUWA NA IKHLAS

Ikhlas ni kufanya kila jambo jema kwa ajili ya Allah (s.w) tu. Yaani kutoa huduma na mali kwa watu wanaohitajia msaada bila ya kutaraji malipo yoyote kutoka kwao ila kutoka kwa Allah (s.w) tu. Kwa mfano kumlisha na kumvisha fukara, maskini au yatima bila ya kutarajia hata kupata shukurani (ahsante) kutoka kwake ila tu kwa kutegemea malipo kutoka kwa Allah (s.w) ni kitendo cha Ikhlas. Wale wanaotoa misaada



kwa wanaohitajia kwa Ikhlas, wamesifiwa na Allah (s.w) katika Qur-an:



“Na huwalisha chakula maskini na yatima na wafungwa na hali yakuwa wenyewe wanakipenda (chakula hicho. Husema nyoyoni mwao wanapowapa chakula hicho): Tunakulisheni kwa ajili ya kutaka radhi ya Mw enyezi Mungu (tu). Hatutaki kw enu m alipo w ala shukurani. Hakika sisi tunamuogopa Mola wetu hiyo siku yenye shida na taabu.”

(76:8-1 0).



“Na amchaye (Mwenyezi Mungu) ataepushwa nao (huo moto uwakao kwa nguvu). Ambaye hutoa mali yake kwa ajili ya kujitakasa na hali ya kuwa hakuna yeyote anayemfanyia ihsani ili awe anamlipa. Isipokuwa (anafanya haya) kwa kutaka radhi ya Mola wake Mtukufu. Basi atapata la kumridhisha.” (92:1 7-21).

Si katika kutoa tu mali, bali lolote lile analolifanya Muislamu wa kweli hana budi kulifanya kwa nia ya kupata radhi ya Allah (s.w). Utendaji wa Mwanaadamu uliofanywa kwa Ikhlas ndio tu utakaomuwezesha kuwajibika vilivyo kwa wanaadamu wenzake na kwa Mola wake Mtukufu.

Ili kujikumbusha mara kwa mara kufanya mambo yetu kwa Ikhlas, ni Sunnah kila tunapoanza swala kabla ya kusoma Suratul-Fatiha tu seme:

“Ninauelekeza uso wangu kwa yule aliyeziumba mbingu na ardhi, hali ya kuwa nimewacha dini za upotofu mimi (nimejisalimisha ni Muislamu na ) si miongoni mwa washirikina. (6:79)



Hakika swala yangu, na ibada zangu (zote nyingine) na uzima wangu na kufa kwangu ni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, Bwana wa walimwengu wote. Hana mshirika wake na kwa haya ndiyo niliyoamrishwa,na mimi ni wa kwanza wa waliojisalimisha. (6:162-163)



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sunnah Main: Dini File: Download PDF Views 1743

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Kitabu cha Afya    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Dua za Mitume na Manabii    👉4 Tafasiri ya Riyadh Swalihina    👉5 Kitau cha Fiqh    👉6 Bongolite - Game zone - Play free game   

Post zinazofanana:

NAFASI YA SUNNAH KATIKA UISLAMU

Nafasi ya Sunnah katika UislamuMtume Muhammad (s.

Soma Zaidi...
Dua Sehemu ya 01

Zijue fadhila za kuomba dua, tambua umuhimu na mahimizo juu ya kuomba dua?

Soma Zaidi...
Dua sehemu 03

Zijuwe njia ambazo Allah hujibu Dua yako. Tambua kama umejibiwa dua yako au bodo, soma darsa za dua hapa.

Soma Zaidi...
MAANA YA HADITHI SUNNAH

Maana ya SunnahKilugha: Neno sunnah katika lugha ya Kiarabu lina maana ya mwenendo au mila.

Soma Zaidi...
Dua ya kuingia nyumbani

Hii ni Dua inayisomwa unapoingia nyumbani

Soma Zaidi...
Namna ambazo Allah hujibu dua ya mwenye kuomba.

Post hii inakwenda kukufundisha namna ama staili ambazo Allah hujibu dua za watu.

Soma Zaidi...
NYAKATI AMBAZO DUA HUJIBIWA

NYAKATI AMBAZO DUA HUJUBIWA.

Soma Zaidi...
Maana ya dua na fadhila zake

Dua ni moja ya Ibada ambazo tunatakiwa kuziganya kila siku. Kuna fadhila nyingi sana za kuomba dua. Post hiibitakwenda kukujuza fadhila za kuomba dua.

Soma Zaidi...