kuwa na ikhlas

Ikhlas ni kufanya kila jambo jema kwa ajili ya Allah (s.

kuwa na ikhlas

  1. KUWA NA IKHLAS

Ikhlas ni kufanya kila jambo jema kwa ajili ya Allah (s.w) tu. Yaani kutoa huduma na mali kwa watu wanaohitajia msaada bila ya kutaraji malipo yoyote kutoka kwao ila kutoka kwa Allah (s.w) tu. Kwa mfano kumlisha na kumvisha fukara, maskini au yatima bila ya kutarajia hata kupata shukurani (ahsante) kutoka kwake ila tu kwa kutegemea malipo kutoka kwa Allah (s.w) ni kitendo cha Ikhlas. Wale wanaotoa misaada



kwa wanaohitajia kwa Ikhlas, wamesifiwa na Allah (s.w) katika Qur-an:



“Na huwalisha chakula maskini na yatima na wafungwa na hali yakuwa wenyewe wanakipenda (chakula hicho. Husema nyoyoni mwao wanapowapa chakula hicho): Tunakulisheni kwa ajili ya kutaka radhi ya Mw enyezi Mungu (tu). Hatutaki kw enu m alipo w ala shukurani. Hakika sisi tunamuogopa Mola wetu hiyo siku yenye shida na taabu.”

(76:8-1 0).



“Na amchaye (Mwenyezi Mungu) ataepushwa nao (huo moto uwakao kwa nguvu). Ambaye hutoa mali yake kwa ajili ya kujitakasa na hali ya kuwa hakuna yeyote anayemfanyia ihsani ili awe anamlipa. Isipokuwa (anafanya haya) kwa kutaka radhi ya Mola wake Mtukufu. Basi atapata la kumridhisha.” (92:1 7-21).

Si katika kutoa tu mali, bali lolote lile analolifanya Muislamu wa kweli hana budi kulifanya kwa nia ya kupata radhi ya Allah (s.w). Utendaji wa Mwanaadamu uliofanywa kwa Ikhlas ndio tu utakaomuwezesha kuwajibika vilivyo kwa wanaadamu wenzake na kwa Mola wake Mtukufu.

Ili kujikumbusha mara kwa mara kufanya mambo yetu kwa Ikhlas, ni Sunnah kila tunapoanza swala kabla ya kusoma Suratul-Fatiha tu seme:

“Ninauelekeza uso wangu kwa yule aliyeziumba mbingu na ardhi, hali ya kuwa nimewacha dini za upotofu mimi (nimejisalimisha ni Muislamu na ) si miongoni mwa washirikina. (6:79)



Hakika swala yangu, na ibada zangu (zote nyingine) na uzima wangu na kufa kwangu ni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, Bwana wa walimwengu wote. Hana mshirika wake na kwa haya ndiyo niliyoamrishwa,na mimi ni wa kwanza wa waliojisalimisha. (6:162-163)



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sunnah Main: Dini File: Download PDF Views 2171

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 kitabu cha Simulizi    👉2 Kitau cha Fiqh    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 Kitabu cha Afya    👉5 Dua za Mitume na Manabii    👉6 Madrasa kiganjani   

Post zinazofanana:

DUA ZA KUONDOA WASIWASI

DUA ZA KUONDOA MAUMIVU MWILINI Katika uislamu Allah amejaalia dawa katika kufuata sunnah.

Soma Zaidi...
Fadhila za udhu yaani faida za udhu

Katika makala hii utajifunza faida za kuwa na udhu

Soma Zaidi...
Historia ya uandishi wa Hadithi, na ni kwa nini wakati wa Mtunme hakukuwa na uandishibmkubwa wa hadithi

Hapa utakwendabkuijuwabhistoria ya uandishi wa hadithi. Pia utaijuwa sababu iliyopelekea uandishi wa hadithi kuwa mdogo .

Soma Zaidi...
DUA ZENYE MANENO HAYA HUJIBIWA

SIFA ZA (MANENO NA MATAMSHI YA) DUA YENYE KUJIBIWA.

Soma Zaidi...
DUA ZA WAKATI WA SHIDA

DUA ZA WAKATI WA SHIDA 1.

Soma Zaidi...
NAMNA AMBAZO DUA HUJIBIWA

NAMNA AMBAYO ALLAH HUJIBU DUA.

Soma Zaidi...
MAANA YA HADITHI SUNNAH

Maana ya SunnahKilugha: Neno sunnah katika lugha ya Kiarabu lina maana ya mwenendo au mila.

Soma Zaidi...
Dua za kuomba wakati unapokuwa na maumivu kwenye mwili

Posti hii inakwenda kukufundisha dua za kuomba wakati wa kuwa na maumivu kwenye mwili wako.

Soma Zaidi...
AINA ZA HADITHI

Aina za HadithKuna aina kuu mbili za Hadith- (a) Hadith Nabawiyyi.

Soma Zaidi...
Al-Arbauwn An-Nawawiyyah hadithi ya 6: ubainifu wa halali na haramu

Post hii inakwenda kukupa tahadhari juu ya mambo ya halali na mambo ya haramu.

Soma Zaidi...