kuwa na ikhlas

Ikhlas ni kufanya kila jambo jema kwa ajili ya Allah (s.

kuwa na ikhlas

  1. KUWA NA IKHLAS

Ikhlas ni kufanya kila jambo jema kwa ajili ya Allah (s.w) tu. Yaani kutoa huduma na mali kwa watu wanaohitajia msaada bila ya kutaraji malipo yoyote kutoka kwao ila kutoka kwa Allah (s.w) tu. Kwa mfano kumlisha na kumvisha fukara, maskini au yatima bila ya kutarajia hata kupata shukurani (ahsante) kutoka kwake ila tu kwa kutegemea malipo kutoka kwa Allah (s.w) ni kitendo cha Ikhlas. Wale wanaotoa misaada



kwa wanaohitajia kwa Ikhlas, wamesifiwa na Allah (s.w) katika Qur-an:



“Na huwalisha chakula maskini na yatima na wafungwa na hali yakuwa wenyewe wanakipenda (chakula hicho. Husema nyoyoni mwao wanapowapa chakula hicho): Tunakulisheni kwa ajili ya kutaka radhi ya Mw enyezi Mungu (tu). Hatutaki kw enu m alipo w ala shukurani. Hakika sisi tunamuogopa Mola wetu hiyo siku yenye shida na taabu.”

(76:8-1 0).



“Na amchaye (Mwenyezi Mungu) ataepushwa nao (huo moto uwakao kwa nguvu). Ambaye hutoa mali yake kwa ajili ya kujitakasa na hali ya kuwa hakuna yeyote anayemfanyia ihsani ili awe anamlipa. Isipokuwa (anafanya haya) kwa kutaka radhi ya Mola wake Mtukufu. Basi atapata la kumridhisha.” (92:1 7-21).

Si katika kutoa tu mali, bali lolote lile analolifanya Muislamu wa kweli hana budi kulifanya kwa nia ya kupata radhi ya Allah (s.w). Utendaji wa Mwanaadamu uliofanywa kwa Ikhlas ndio tu utakaomuwezesha kuwajibika vilivyo kwa wanaadamu wenzake na kwa Mola wake Mtukufu.

Ili kujikumbusha mara kwa mara kufanya mambo yetu kwa Ikhlas, ni Sunnah kila tunapoanza swala kabla ya kusoma Suratul-Fatiha tu seme:

“Ninauelekeza uso wangu kwa yule aliyeziumba mbingu na ardhi, hali ya kuwa nimewacha dini za upotofu mimi (nimejisalimisha ni Muislamu na ) si miongoni mwa washirikina. (6:79)



Hakika swala yangu, na ibada zangu (zote nyingine) na uzima wangu na kufa kwangu ni kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, Bwana wa walimwengu wote. Hana mshirika wake na kwa haya ndiyo niliyoamrishwa,na mimi ni wa kwanza wa waliojisalimisha. (6:162-163)



                   

Jiunge nasi WhatsApp kupata update zetu

Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Sunnah Main: Dini File: Download PDF Views 1536

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)    👉2 Bongolite - Game zone - Play free game    👉3 Simulizi za Hadithi Audio    👉4 kitabu cha Simulizi    👉5 Madrasa kiganjani    👉6 Kitabu cha Afya   

Post zinazofanana:

Maswali juu ya Sunnah na hadithi

Sunnah na hadithi (EDK form 3: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
AINA ZA HADITHI

Aina za HadithKuna aina kuu mbili za Hadith- (a) Hadith Nabawiyyi.

Soma Zaidi...
Masharti ya kukubaliwa kwa dua

Post hii itakwenda kukugundisha masharti yanayofungamana na kukubaliwa kwa dua.

Soma Zaidi...
HALI AMBAZO MTU AKIOMBA DUA HUJIBIWA

HALI AMBAZO MTU AKIOMBA DUA ITAJIBIWA.

Soma Zaidi...
DUA YA MUUMINI NA DUA YA KAFIRI

DUA YA KAFIRI NA DUA YA MUUMINI.

Soma Zaidi...
Utofauti wa dua ya kafiri na dua ya muislamu katika kujibiwa

Posti hii inakwenda kukufundisha ni kwa nini dua ya kafiri inawwza kujibiwa wakati ya muumini haijibiwi.

Soma Zaidi...
Hukumu ya kukusanyika kwenye dua na umuhimu wa dua ya watu wengi

Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu umuhimu wa kukusanyika katika kuomba dua.

Soma Zaidi...
NAMNA AMBAZO DUA HUJIBIWA

NAMNA AMBAYO ALLAH HUJIBU DUA.

Soma Zaidi...