Kujiepusha na Shirk

Kujiepusha na Shirk

Shirki ni kitendo chochote cha kukipa kiumbe nafasi ya Allah (s.

Jiunge nasi WhatsApp
Upate Update zetu

Kujiepusha na Shirk

(b) Kujiepusha na Shirk



Shirki ni kitendo chochote cha kukipa kiumbe nafasi ya Allah (s.w) katika dhati yake, Sifa zake, Mamlaka yake na Hukumu zake.
Allah (s.w) aliyemuumba binaadamu na viumbe vyote vilivyo mzunguka kwa lengo, ndiye mwenye Haki na Uwezo pekee wa kumuwekea mwanaadamu mwongozo wa maisha utakao muwezesha kuishi kwa furaha na amani katika maisha ya hapa duniani na maisha ya baadaye huko akhera.


Yeyote yule katika viumbe atakayechukua au kupewa nafasi ya Allah (s.w) katika kutoa kanuni, sheria na mwongozo wa maisha ya binaadamu katika jamii, atakuwa amechukua au amepewa mamlaka ambayo hana uwezo nayo na kwa vyovyote vile atakuwa ameitumbukiza jamii katika Kiza cha Khofu na Huzuni kinachosababishwa na dhuluma za aina mbalimbali. Allah (s.w) analiweka hili wazi katika aya zifuatazo:


"Hakuna kulazimishwa (mtu kuingia) katika dini. Uongofu umekwisha pambanuka na upotofu. Basi anayemkataa shetani na akamwamini Mwenyezi Mungu, bila shaka yeye ameshika kishiko chenye nguvu kisichokuwa na kuvunjika. Na Mwenyezi Mungu ni mwenye kusikia mwenye kujua.."



"Mwenyezi Mungu ni mlinzi wa wale walioamini. Huwatoa katika giza na kuwaingiza katika nuru. Lakini waliokufuru, walinzi wao ni matwaghuti. Huwatoa katika nuru na kuwaingiza katika giza. Hao ndio watu wa Motoni, humo watakaa milele." (2:256-25 7).



Hivyo kwa mnasaba wa maelezo haya na aya tulizozirejea, tunajifunza kuwa chanzo cha dhuluma zote anazofanyiwa binaadamu na binaadamu mwenziwe zimetokana na kumshirikisha Allah (s.w) ama katika Dhati yake, Sifa zake, Mamlaka yake au katika Hukumu zake.




                   


Download Post hii hapa

Download App Yetu

Jifunze zaidi, na wasiliana nasi ukiwa na App yetu. Bofya link hapo chini kuweza kuipakua.

Download Now Bongoclass Zoezi la Maswali

Nyuma Endelea


Umeionaje Makala hii.. ?

Nzuri            Mbaya            Save
Author: Rajabu image Tarehe: 1970-01-01 03:33:44 Topic: Tawhid Main: Dini File: Download PDF Views 1363

Share On:

Facebook WhatsApp
Sponsored links
👉1 Bongolite - Game zone - Play free game    👉2 Simulizi za Hadithi Audio    👉3 Madrasa kiganjani    👉4 Kitau cha Fiqh    👉5 Kitabu cha Afya    👉6 Sira ya Mtume Muhammad (s.a.w)   

Post zinazofanana:

Shirk na aina zake
Shirk na aina zake

Nguzo za imani (EDK form 2: dhana ya elimu ya uislamu)

Soma Zaidi...
Mgawanyo sahihi wa elimu kwa mtazamo wa uislamu
Mgawanyo sahihi wa elimu kwa mtazamo wa uislamu

Ni upi mgawanyo sahihi wa elimu katika uislamu? Nini naana ya elimu ya muongizo. Je elimu ya mazingiravmaana yakeni nini. Ni upi utofauti wa elimu ya muongozo na elimu ya mazingira?

Soma Zaidi...
Kujiepusha na kufuata mambo kwa kibubusa
Kujiepusha na kufuata mambo kwa kibubusa

Waislamu wanakatazwa kufanya na kufuata mambo kwa kibubusa (kwa mkumbo) bila ya kuwa na ujuzi unaostahiki.

Soma Zaidi...
Nafasi ya Elimu katika uislamu
Nafasi ya Elimu katika uislamu

Elimu imepewa kipaumbele kikubwa kwenye uislamu. Post hii inakwenda kukufundisha kuhusu nafasi ya Elimu katika uislamu.

Soma Zaidi...
Nguzo za imani
Nguzo za imani

Zifuatazo ni nguzo za imani (EDK form 2: elimu ya dini ya kiislamu)

Soma Zaidi...
KUAMINI VITABU VYA ALLAH (S.W)
KUAMINI VITABU VYA ALLAH (S.W)

Mtu hawi Muumini wa kweli mpaka awe na yakini juu ya vitabu vya Allah (s.

Soma Zaidi...
Nini chanzo cha elimu zote na ujuzi wote
Nini chanzo cha elimu zote na ujuzi wote

Ninichanzo cha Elimu? (EDK form 1 Dhanaya Elimu)

Soma Zaidi...
Maana ya uislamu.
Maana ya uislamu.

Kwenye kipengele hichi titajifunza maana ya uislamu,na maana nyingine tofauti.

Soma Zaidi...