Shirki ni kitendo chochote cha kukipa kiumbe nafasi ya Allah (s.
Shirki ni kitendo chochote cha kukipa kiumbe nafasi ya Allah (s.w) katika dhati yake, Sifa zake, Mamlaka yake na Hukumu zake.
Allah (s.w) aliyemuumba binaadamu na viumbe vyote vilivyo mzunguka kwa lengo, ndiye mwenye Haki na Uwezo pekee wa kumuwekea mwanaadamu mwongozo wa maisha utakao muwezesha kuishi kwa furaha na amani katika maisha ya hapa duniani na maisha ya baadaye huko akhera.
Yeyote yule katika viumbe atakayechukua au kupewa nafasi ya Allah (s.w) katika kutoa kanuni, sheria na mwongozo wa maisha ya binaadamu katika jamii, atakuwa amechukua au amepewa mamlaka ambayo hana uwezo nayo na kwa vyovyote vile atakuwa ameitumbukiza jamii katika Kiza cha Khofu na Huzuni kinachosababishwa na dhuluma za aina mbalimbali. Allah (s.w) analiweka hili wazi katika aya zifuatazo:
"Hakuna kulazimishwa (mtu kuingia) katika dini. Uongofu umekwisha pambanuka na upotofu. Basi anayemkataa shetani na akamwamini Mwenyezi Mungu, bila shaka yeye ameshika kishiko chenye nguvu kisichokuwa na kuvunjika. Na Mwenyezi Mungu ni mwenye kusikia mwenye kujua.."
"Mwenyezi Mungu ni mlinzi wa wale walioamini. Huwatoa katika giza na kuwaingiza katika nuru. Lakini waliokufuru, walinzi wao ni matwaghuti. Huwatoa katika nuru na kuwaingiza katika giza. Hao ndio watu wa Motoni, humo watakaa milele." (2:256-25 7).
Hivyo kwa mnasaba wa maelezo haya na aya tulizozirejea, tunajifunza kuwa chanzo cha dhuluma zote anazofanyiwa binaadamu na binaadamu mwenziwe zimetokana na kumshirikisha Allah (s.w) ama katika Dhati yake, Sifa zake, Mamlaka yake au katika Hukumu zake.
Umeionaje Makala hii.. ?
Uislamu unaitazama dini katika nyanja zote za maisha ya mwanadamu. Hii ni tofauti na mtazamo wa kikafiri juu ya dini.
Soma Zaidi...Kuwa ni kwa nini mwanadamu hawezi kuishi bila ya dini kutokana na umbile la mwanadamu.
Soma Zaidi...โKatika kuumbwa mbingu na ardhi na mfuatano wa usiku na mchana,ziko alama (hoja) za kuonyesha kuwepo Allah (s.
Soma Zaidi...Dhana ya faradh kwa muislamu (EDK form 2:dhana ya elimu ya uislamu)
Soma Zaidi...Kwenye kipengele hichi tutajifunza makundi ya dini za watu. Na makundi hayo ni matatu.
Soma Zaidi...Njia ambazo Allah hutumia kuwasiliana na wanadamu nakuwafundisha elimu mbalimbali. (Edk form 1 dhana ya Elimu)
Soma Zaidi...Waumini wanawajibika kuwatunzia mayatima mali zao na kuwakabidhi wanapofikia baleghe yao baada ya kuwajaribu na kuthibitisha kuwa wanao uwezo wa kutunza mali zao - Rejea Qur-an (4:5-6).
Soma Zaidi...ุนููู ุฃูุจูู ููุฑูููุฑูุฉู ุฑูุถููู ุงูููู ุนููููู ุฃูููู ุฑูุณูููู ุงูููููู ุตูู ุงููู ุนููู ู ุณูู ููุงูู: "ู ููู ููุงูู ููุคูู ููู ุจูุงููููููู ููุงููููููู ู...
Soma Zaidi...